Mbeya: Ajifungia kwenye nyumba yeye na mkewe kisha kuchoma nyumba moto, kisa wivu wa mapenzi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,982
Mtoto wa marehemu akiwa Hospitalini akiendelea na matibabu.jpg

Mtoto wa marehemu akiwa Hospitalini akiendelea na matibabu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na operesheni, misako na doria katika maeneo mbalimbali ya Mkoa ili kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao. Aidha tumeendelea kupata mafanikio kwa kukamata watuhumiwa wa makosa mbalimbali na kuwafikisha mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin E. Kuzaga amesema Mnamo tarehe 08.03.2023 majira ya saa 04:00 usiku huko maeneo ya Nyigamba, Mtaa wa Itezi, Jijini Mbeya, mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la HAMIS PIUS [41] Dereva, Mkazi wa Nyigamba alifariki dunia kwa kuungua moto baada ya kujifungia ndani ya chumba anacholala na mke wake aitwaye REBELIA MAKOSO [38] Mkazi wa Nyigamba kisha kumwaga mafuta ya Petroli na kuwasha moto.

Wakati wa tukio hilo, mke wa marehemu alipiga kelele kuomba msaada kwa mtoto wake aitwaye MKESHILISI HAMIS [21] ambaye alikuwa chumba kingine ambaye alikwenda kutoa msaada kwa kupiga teke mlango wa chumba na kisha kumuokoa mama yake lakini baba yake alikataa kutoka ndani na kupelekea kuungua hadi kupoteza maisha.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi. Majeruhi ambao ni mke na mtoto wa marehemu wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mji Mdogo wa Mbalizi kutokana na majeraha ya moto waliyoyapata mwilini.
RPC Mbeya.JPG

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin E. Kuzaga

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa jamii kuachana na vitendo vya kujichukulia sheria mkononi. Aidha tunatoa wito kwa jamii kutatua migogoro yao ya kifamilia na ndoa kwa kukaa meza moja ya usuluhishi badala ya kuchukua maamuzi magumu kama hayo.
 
View attachment 2549166
Mtoto wa marehemu akiwa Hospitalini akiendelea na matibabu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na operesheni, misako na doria katika maeneo mbalimbali ya Mkoa ili kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao. Aidha tumeendelea kupata mafanikio kwa kukamata watuhumiwa wa makosa mbalimbali na kuwafikisha mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin E. Kuzaga amesema Mnamo tarehe 08.03.2023 majira ya saa 04:00 usiku huko maeneo ya Nyigamba, Mtaa wa Itezi, Jijini Mbeya, mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la HAMIS PIUS [41] Dereva, Mkazi wa Nyigamba alifariki dunia kwa kuungua moto baada ya kujifungia ndani ya chumba anacholala na mke wake aitwaye REBELIA MAKOSO [38] Mkazi wa Nyigamba kisha kumwaga mafuta ya Petroli na kuwasha moto.

Wakati wa tukio hilo, mke wa marehemu alipiga kelele kuomba msaada kwa mtoto wake aitwaye MKESHILISI HAMIS [21] ambaye alikuwa chumba kingine ambaye alikwenda kutoa msaada kwa kupiga teke mlango wa chumba na kisha kumuokoa mama yake lakini baba yake alikataa kutoka ndani na kupelekea kuungua hadi kupoteza maisha.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi. Majeruhi ambao ni mke na mtoto wa marehemu wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mji Mdogo wa Mbalizi kutokana na majeraha ya moto waliyoyapata mwilini.
View attachment 2549167
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin E. Kuzaga

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa jamii kuachana na vitendo vya kujichukulia sheria mkononi. Aidha tunatoa wito kwa jamii kutatua migogoro yao ya kifamilia na ndoa kwa kukaa meza moja ya usuluhishi badala ya kuchukua maamuzi magumu kama hayo.
KWai haki yake,ila akuna ajuaye mwisho wake
 
Back
Top Bottom