Iringa: Mwendesha Bajaj achomwa kisu na mkewe kisa wivu wa mapenzi

Bull Bucka

Member
Oct 5, 2023
34
46
Mwanamke mmoja anayeitwa Fadhila Balama, mkazi wa Kitwiru katika Manispaa na Mkoa wa Iringa, anakabiliwa na tuhuma za kumuua mume wake, Denis Chumbula, kwa kumchoma kitu chenye ncha kali baada ya mzozo kati yao.

Hii ni kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Mtaa, Nazareno Mangw'ata, ambaye amesema tukio hilo lilitokea usiku wa Jumatatu, Novemba 27, 2023.

Mwanamke huyo amekamatwa na Jeshi la Polisi kufuatia tuhuma za kuhusika katika mauaji.

Inaelezwa kuwa familia hiyo imekuwa ikiathiriwa na migogoro mara kwa mara na wawili hao wamekuwa wakipigana mara kadhaa.

asc.JPG




 
Sasa tunakomentije bila taarifa kamili jama. Si ungesubiripo kidogo kisha uimwage yote
 
Hii mikoa ya pande za huko siku hizi sijui imekuaje,,,, ngoja njombe nae aje na lake
 
Back
Top Bottom