Mtakumbuka kuwa wakati ule El akiwa waziri Mkuu, jamani kazi ilikuwa inafanyika. sio wakurugenzi, watendaji wa manispaa, Halmashauri, Kata, mpaka kijiji, kamati za ujenzi wa shule zetu za kata-- n.k. tulishaanza kupata morali ya uwajibikaji na kuondokana na mambo yetu yale ya kufanya kzai kwa mazoea...yote hayo sababu ya ufuatiliaji wa karibu wa Mh. EL. Ameondoka tu,unaona mambo yamezorota, watendaji wa serikali wakapata ahueni kuzembea na wametafuna fedha za umma, ndo haya tunayoyaona kufikishana mahakamani kila kukicha...zile shule zetu za kata zimejengwa mpaka lenta nas wananchi...kumaliziwa na Serikali sijui itakuwa lini?. Namuombea |Mungu amjalie achaguliwe tena kwenda Bungeni na pengine apate nafasi ile au zaidi.