Mazishi ya Prof. Jwan Mwaikusa

Mkuu De Novo, mwenyewe nimejaribu kufikiria na kuanza kuamini kuwa Tanzania is no longer safe!

Mwili wa marehemu sasa unapelekwa makaburini na jeneza lilibebwa na walimu wa sheria tu wakiwa wamevalia majoho yao.

Kaburi lipo jirani na nyumbani, limeshajengwa na kunakshiwa na vigae (marumaru)

tell that to Sokoine, Kombe, Kolimba, etc....zote ni political assassinations! Mkuu...usicheza na politics na power. Its a dangerous game, hasa kwa wale wanaojaribu kuondoa status quo...

Professor Mwaikusa RIP.
 
Pasco amekwama sehemu lakini updates ziko kama ifuatavyo:

Heshima za mwisho zimeisha toka Nkrumah Hall, na msafara wa kuelekea nyumbani kwa marehemu Sala Sala uliongozwa na pikipiki ya Traffic.

Mwili wa marehemu kwa sasa upo nyumbani ukisubiri taratibu za kifamilia

yaani wanamuua na PIKIPIKI WANAMPATIA JAMANI HII NCHI IMELAANIKA KWELI??KWELI
DUH POLEN WAFIWA SOON UTASIKIA WATU WANATANGAZIWA ULAJI WA TUME YA KUCHUNGUZA KIFO CHA PROF..WAFIWA MSIKUBALI HILI AMEENDA MWACHEN BABA WA WATU ALALE SALAMA....
 
hotuba ya rais siku ya kuchaguliwa dodoma namnukuu

ndugu zanguni napenda uwaambia na kuwaonya wale woote walio mstari wambele kulitenganisha taifa hili kwa njia moja ama nyingine hakika ntadili nao...nawaambia kweli waulizeni waliojaribu wako wapi sasa..nasema hili nikiwatahadharisha ndugu zangu kama kitu nikisema no hata uende mahakamani,,uende sijui haki za binadamu itabaki no tu..usijaribu kutafuta umaarufu kwenye seriakli yangu ukaja kujutia milele namnkuu.....waliona rekodi wamsome vizuri mh sana...dk wetu naona kaamua kuanza na maprof...

Mungu amlaze pema peponi
 
Prof Kanywani naye yupo, na mhe. Diwani Kippi Warioba (ambaye ametangaza nia jimbo la Kawe) yupo pia
 
Mazishi tayari, yanawekwa mashada sasa. Serikali imewakilishwa na Prof. Mark Mwandosya (mwakilishi wa rais)
 
Thanks Invisible...
Macho msibani huku vidole kwenye ketpad ya simu (Computer????) yako
 
Invisible uko msibani au inaoneshwa kwenye luninga?Asante kwa kutuhabarisha tuliko mtaani kwenye mizunguko..
 
I wonder kama kweli Kabudi alienda msibani au alienda kuzuga....(usinitafsiri vibaya) kuna baadhi ya watu ningependa sana kujua kama wamekwenda lakini majina yao hayajatajwa, i hope hawakuwepo...
 
hotuba ya rais siku ya kuchaguliwa dodoma namnukuu

ndugu zanguni napenda uwaambia na kuwaonya wale woote walio mstari wambele kulitenganisha taifa hili kwa njia moja ama nyingine hakika ntadili nao...nawaambia kweli waulizeni waliojaribu wako wapi sasa..nasema hili nikiwatahadharisha ndugu zangu kama kitu nikisema no hata uende mahakamani,,uende sijui haki za binadamu itabaki no tu..usijaribu kutafuta umaarufu kwenye seriakli yangu ukaja kujutia milele namnkuu.....waliona rekodi wamsome vizuri mh sana...dk wetu naona kaamua kuanza na maprof...

Mungu amlaze pema peponi

Hii kauli inaniumiza sana. Maneno haya hayakupaswa kusemwa na Rais wa nchi inayoendeshwa kwa misingi ya democrasia na sheria. Maana ilivyokaa ni dhahiri kwamba miaka hii mitano itakuwa ni ya kuua kila atakayejaribu kupinga au kukosoa utawala wake. Lakini Mungu anajua, maana hakuna muuaji hata mmoja ambaye hatakufa au akifa atazikwa angani. Their days are underway! Sina ushahidi wowote kwamba serikali imeshiriki katika kifo cha prof Jwani, but kama ni kweli kuna viongozi wa serikali ambao wanawaua wenzao ili kujipatia ulaji zaidi, naamini Mungu hatawaacha.

Alikuwepo Mfalme Nebukadneza aliyejiona yupo juu ya kila kitu, aliwategemea waganga na wachawi wamtabirie uelekeo wa uongozi wake na ndoto zake, kama CCM na Kikwete wanavyomtegemea Sheik Yahya, lakini mwisho wa siku alikula nyasi na kukaa porini na kunyeshewa na mvua kwa vipindi saba. Kila mtu atalipwa sawasawa na matendo yake. Nyie tuueni tu, lakini siku ya siku tutakuwa wote kaburini na tutaoza sawasawa kati ya aliyeua na kuuawa.
Laiti binadamu angekuwa anatambua kinachokuja mbele yake hata dk moja ya baadaye, angejitahidi kila wakati kutenda mema na kuwapenda na kuwalinda wenzake. Lakini kwa kuwa hajui, matokeo yake yanakuwa ndo kama hayo. Unaua tu, wewe unajua utaishi hadi lini? Inatia uchungu sana. Ndiyo maana kwenye signature yangu nasema binadamu ni kiumbe mjinga kuwashinda viumbe wote waliowahi kuishi duniani milele ne milele. Wakati wanyama wengine wanaofanana huungana kujilinda na mnyama tofauti na wao, binadamu wanauana wao kwa wao. wanatengeneza silaha nzitonzito kwa ajili ya kuulia binadamu wenzao. Ni kiumbe wa ajabu kabisa binadamu.
Lakini nawaambieni watanzania wenzangu Mungu wetu ni mwaminifu, kama hii kazi ya kumwaga damu zisizo na hatia inafanywa na CCM (ninasema kama inafanywa na CCM), basi miaka mitano hii haitaisha. Najua hamtaniamini kwa kuwa mnamwamini zaidi sheik Yahya, lakini mtaamini yatakapotokea. Najua mtaitafuta hii post hapo yatakapokuwa yamejiri.
 
hotuba ya rais siku ya kuchaguliwa dodoma namnukuu

ndugu zanguni napenda uwaambia na kuwaonya wale woote walio mstari wambele kulitenganisha taifa hili kwa njia moja ama nyingine hakika ntadili nao...nawaambia kweli waulizeni waliojaribu wako wapi sasa..nasema hili nikiwatahadharisha ndugu zangu kama kitu nikisema no hata uende mahakamani,,uende sijui haki za binadamu itabaki no tu..usijaribu kutafuta umaarufu kwenye seriakli yangu ukaja kujutia milele namnkuu.....waliona rekodi wamsome vizuri mh sana...dk wetu naona kaamua kuanza na maprof...

Mungu amlaze pema peponi
Ni kweli sijawahi kusikia mtu kafungwa kisiasa ktk vipindi vya miaka mitano ya VASCO... ila tumeshuhudia assassinations za ajabu ajabu kwa kisingizio cha majambazi, ajali n.k. Hivyo nadhani Vasco ametuma ujumbe kwa wana JF kuwa mnapokosoa mjue siku rungu litawashukia. Tuombe MUNGU awaline akina invisible maana bila hivyo ishu itakuwa ishu.
Maneno ya Rais yanapaswa kuchujwa na kuhifadhiwa kama kumbukumbu kwa vizazi vijavyo. Tena LHRC wanapaswa kuipeleka segment ya hutuba hii The Hague ili waone dhamira iliyopo kwenye mistari ya mpewa dhamana.....
 
Mkuu Robot thanx kwa updates za msibani.
vp mmeupload picha to jamii photo ili tuone pilika za huko?
 
Kama kuua ataua nchi nzima aimalize. Kwa nini awaue kimya kimya kama anavyofanya Kagame? ili kuonyesha umwamba anaotangaza aweke firing squad na ku shoot wote tunaomsema na haki za binadamu hawatamsema. Kwa nini awaue kwa siri?

Tena nina hakika yule wa pili aliuawa kwa kuwa alimuona muuaji na kumtambua.

Mungu wetu atalipiza sawa sawa na walivyotenda na watapata mapigo makubwa wao na familia zao.
 
Pasco amekwama sehemu lakini updates ziko
Asante Invisible, wanabodi poleni, nilikwama mahali, na sio vibaya tukisaidiana ili kesho nisikwame tena.
Kwa kawaida hutumia Nokia E90 kupost JF na Backbery Storm 9500 kulog JF 24/7 kwa sababu mtandao wa blacbery internet ni bure.

Baada ta technology kupanda, nikaachana na E90 na kutumia N97. Leo from no where Blackbery just went black screen hivyo niliona inadim tuu. Na hiki ki N97 ni kimeo, log in kwa JF hakikubali, wala ukipost kitu hakiendi.

Kama kuna yoyote mwenye N Series naomba anijulishe anafanya nini kupost JF.
Blackbery storm najua zina kichaa, matatizo ni hayo tuu.
Asante tena Invisible.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom