Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,903
- 945
TUTAJENGA SHULE KUMKUMBUKA PROF. DAVID MASAMBA" - WANANCHI MUSOMA VIJIJINI
"Afrika inamfahamu Prof. David Masamba kwa umahiri wake wa lugha ya Kiswahili ni wakati sasa wakufikiria cha kufanya sisi tutajenga shule ambayo itakuwa na jina ambayo ni kumbukumbu ya Profesa na haya ni makubaliano ya wananchi" - Mhe. Prof. Sospeter Muhongo Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini.
Wananchi wa kijiji cha Kurwaki Halmashauri ya wilaya ya Musoma mkoani Mara wamekubalina kuweka alama maalum kama kumbukumbu kwa aliyekuwa mwanazuoni mkongwe wa lugha ya Kiswahili Prof.David Masamba ambaye amefariki dunia nakuzikwa katika kijiji hicho.
Akizungumza katika mazishi ya aliyekuwa mwanazuoni Prof. David Masamba Mbunge wa jimbo la Musoma Vijiji Profesa Muhongo amesema haiwezekana historia ya Prof.Masamba ikapotea kirahisi kwani amefanya mambo mengi katika taifa hili.