Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,655
- 593
January Makamba, Serukamba wapewe rungu!
wamesaini petition ya Zito?
January Makamba, Serukamba wapewe rungu!
Mkuu Kimbunga, kuna mtu kaiba ID yako nini? Maana siku zite Kimbunga ni mtetezi wa uchafu wa Magamba humu!!Hivi kama Mawaziri wanane wanajiuzulu hii haina maana kwamba serikali imefika kikomo? Ina maana wanane wote hawajui wanalolitenda ama ni wabadhirifu. Je wanaowasimamia wao hawana share yao katika uzembe huu?
Haya mambo yanachanganya.
Kwa hali ya uchumi ulivyo hivi sasa wakiondoka hao nchi ita-collapse kwa kuitisha uchaguzi mkuu tena!JK na Pinda ndio waondoke otherwise ni kubadili chupa tu wakati mvinyo ni ule ule.
HATIMAYE mawaziri saba kati ya nane wakiwemo wanaokabiliwa na tuhuma za ubadhirifu, wamekubali kuandika barua za kujiuzulu wenyewe kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kukinusuru Chama cha Mapinduzi (CCM).
Habari za kuaminika kutoka mjini Dodoma zimesema kuwa mawazirihao, walilazimishwa kujiuzulu katika kikao cha dharura kilichokuwa chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kilichofanyika mara tu baada ya kumalizika kwa kikao chaBunge.
Taarifa zimewataja waliokubali kujiuzulu kuwa ni pamoja na Waziriwa Viwanda na Biashara, Cyril Chami;
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika;
Waziri wa Uchukuzi Omari Nundu; na Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda.
Wengine wanaodaiwa kujiuzulu ni:
Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja;
Naibu Waziri wa Afya, Lucy Nkya;
na Naibu Waziri wa Viwanda, Lazaro Nyarandu.
Hata hivyo, Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye alishambuliwa vikali kwa kuitwa kinara wa ufujaji, hakuwepo katika kikao hicho kwa madai kuwa yuko nje ya nchi, anasubiriwa aungane na wenzake kuachia ngazi.
Kujiuzulu kwa mawaziri hao kumekuja baada ya kuzuka kwa mjadala mzito ndani ya Bunge kwa siku mbili mfululizo kuhusiana na tuhuma za ufujaji wa kutisha wa fedha za umma, kiasi chakusababisha kuwepo kwaazimio la kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
january makamba apewe nishati na madini bcoz jamaa anamachungu na gharama kubwa za umeme.
wamesaini petition ya Zito?
Afu hv huyu mama mavifaranga hana sehem aliyo iba kweli! Hembu makamanda tafuteni muanze nae kwanza coz ni tatizo