Mawaziri wanane watakiwa kung'oka...!

Mawaziri wanane watakiwa kung'oka...!

DPP alipaswa au sijui kama anafuatilia ubadhirifu huo unaodaiwa kufanywa katika taasisi zinazoongwa na mawaziri hao.. muda wa kesi ukifika utaambiwa kuwa akina DPP hawana ushahidi wa kutosha na mwenye nao awapelekee... wakipelekewa kama alivyofanya msema kweli akina DPP wanapata kigugumizi cha kutojua cha kufanya na kuanza kutafuta visingizio vingine ya kwamba bado tuko kwenye mchakato wa upelelezi, faili bado kukamilika.....na mengineyo mengi....itakuwa kituko sana safari hii kama DPP akisema kwamba hawana ushahi wa kutosha ili hali mambo yamwemwagwa hadharani...inafaa tuwe na kitengo maalumu nje ya mfumo wa sasa cha kuwashitaki viongozi au wanasiasa (kwa makosa ya kisiasa) ambao imedhihilika wazi kwamba wao hawagusiki na mfumo wa sasa wakisha jiudhuru..kama EL... hii yaweza kuwa independent political crime and public adminstrations court..mahakama ya makosa ya kisiasa na uendeshaji wa shughuli za serikali na taasisi zake...
ni hayo kwa leo
 
Kujiuzulu haitoshi, nadhani wapelekwe MAHAKAMANI NA WAFUNGWE!
 
Sidhan kama kuna haja ya naibu kujiuzulu. anaewajibika ni boss wake na ye ni automatic amejiuzulu
 
Sasa ni wakati muafaka kwa JK kuunda baraza dogo la mawaziri atakalolimudu!
 
kama sio JAMBAJAMBA YA CHADEMA ASINGEJIUZULU MTU, big up ZITTO, TUNDU LISSU na wana Chadema kwa ujumla
 
Huyu ndo alitakiwa ajiuzulu kitambo tangu alipoibiwa Na changudoa kule morogoro.
 
Tatizo la CCM ni kushindwa kuwa firm na kuwa wawazi!

kama wanataka kuwafukuza au kuwashinikiza, kwa nini wanafanya behind doors?
Ni kitu gani hicho cha siri ambacho hawataki tukijue?

Si kila itu kimewekwa wazi pale bungeni?

CCM haijifunzi, imechoka.............an old dog!
 
Katibu wa PM anaingia ofisini sasa kuanza jukumu alilofuatiwa nyumbani kuja kulitekeleza hapa usiku huu ili kuandaa Taarifa itakayosomwa asubuhi na mtoto wa mkulima,

Na hiki ndicho kikosi kamili

Mkulo
Mponda
Nkya
Magembe
Nundu
Mkuchika
Chami
Maige
Ngeleja

Mkuu unaweza kuiunga katika ile thread ili kupunguza utitiri wa hizi INFO, Japo ile ya kwanza ilikuwa muhimu kusimama kama uzi unaojitegemea kuepusha usumbufu usio wa lazima kwa watanzania ambao sasa wanafungua JF kujua yanayojiri hapa DODOMA

Hakuna la ziada

ADIOS

Yule mzee wa SMG mbona sioni jina lake hapa? Ngeleja na mwenzake waondoke wote!
 
kwa kweli hii inatia aibu kubwa...hawa watu si kujiudhuru tu..bali wafungwe kabisa ..hata kama mahakama itawatetea..hii nchi tunakwenda wapi????
 
Kinachofata; WANYONGWE hadharani kama wabunge walivyopendekeza
 
Hawa ccm wasituletee mchezo,Vasco dagama anatakiwa kuvunja baraza lote la mawaziri na ateue baraza jipya kabisa bila kuwarudisha hao wazamani hata mmoja kwenye baraza jipya. ni upuuzi mtupu, nchi inafilisiwa mtu tu. wananchi tuwaunge mkono wabunge wetu wanao tutetea.
 
Tumshukuru mungu kwa hao walio jiuzuru kula pesa za wa tz' wa tz tufunge na kuomba ili wakamatwa nakufugwa jela maisha iwefundisho na kwa wengine.

Mkuu Hoho, kwenye mahakama za ccm hili haliwezekani kabisa meza maneno yangu!!!
 
Kwa kuwa mawaziri wote waandamizi wamejiuzuru ni wakati muafaka sasa kwa JK kushauriwa kuunda baraza dogo la mawaziri atakalolimudu. Aidha achague vijana wachapakazi watakaorudisha hadhi ya serikali mbele ya wananchi.

Hakika huu ni wakati murua (Golden chance) kwa JK kurudisha heshima yake!
 
Njia nyeupe kwa bwana Januari Makamba kumrithi Ngeleje!

Tunataka kuondokana na usingizi huu kama wako ndo maana haya yanayotokea yanapata sana nguvu kipindi hiki
Uweke vigezo na sababu za mtu kushika nafasi husika as compared to others sio just kuweka jina tu hapa bila vigezo.

Na diligence ya muhusika katika kufika hapo alipo na kutumikia umma
 
Huyu tumganyeje? Ndo kafanya madudu mengi mpaka sasa kati ya waliowasirisha barua ye hayumo
Tumganyeje= tumfanyeje. Hakuna adhabu inayomfaa huyu Malima zaidi ya kunyongwa publically.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom