Mawaziri wanane watakiwa kung'oka...!

Mawaziri wanane watakiwa kung'oka...!

mwisho wa siku JK anaacha maswali mengi hivi urafiki atauendekeza hadi lini?......maana uteuzi wake kila siku ni noma tu.....

Mkuu, tega sikio uone hao wanaokuja kuziba pengo, ndiyo utashangaa sitegemei jk kama atatafuta nje ya maswahiba zake!
 
Eti wameamua kujiuzuru ili kuinusuru CCM. Maajabu. Chama Cha Makamba HAKINUSURIKI. Wajiuzuru wasijiuzuru CCM HAITAKIWI na Watanzania.
 
kwanini wasimwambie waziri wa mambo ya ndani pia au kwakuwa katoka zanzibar au ndio madudu yake yanakubalika
tumeona raiya wakiuliwa na polisi na yeye kimya au ndio nahoda analipiza ya tarehe 26 2001 kule pemba
Mkuu huyu naye kweli akitakiwa awemo kwa kuwa ameshindwa kulisimami jeshi la polisi. Mauaji ya songea yalitosha kumkaanga.
Malima yeye salama?
 
Eti wameamua kujiuzuru ili kuinusuru CCM. Maajabu. Chama Cha Makamba HAKINUSURIKI. Wajiuzuru wasijiuzuru CCM HAITAKIWI na Watanzania.
CCM bado inapendwa na inahitajiwa sana na watz..na mpaka sasa hamna chama mbdala au chenye nguvu kama CCM. Vyama vyetu vya upinzani ni waganga njaa tu.
 
Ni ukweli ulio wazi hawa wamejiuzuru baada ya kubebwa sana na rais wao JK kwa dhana nzima ya kulindana kwa sababu wanazozijua wenyewe.

Kwa dhambi walizofanya kwa kila mmoja wao watafanywaje na nani atakayewapeleka kwenye mahakama kutoa haki?

Wameua, wameiba, wamedhurumu..........

Mpaka leo wakina Jairo wako wapiiiii........
 
Waziri Mkuu ametikiswa, ujumbe umefika kwa Serikali, hofu imetanda, wamekaa wakazungumza kama wana CCM lakini maamuzi yao hata kama siyo kufukuzana, kuna outcome kidogo, Mawaziri wataongeza msamiati kichwani mwao leo: accountability!!! Tukiwa macho zaidi, tunaweza kufanya mazuri zaidi ya hapa!! Mitandao ya kijamii imefanya kazi kubwa kuwaambia Wabunge wao wasaini fomu ya Zitto....wengi wamefanya, wengine hawakufanya... Ila inawezekana!!!
 
Hivi kama Mawaziri wanane wanajiuzulu hii haina maana kwamba serikali imefika kikomo? Ina maana wanane wote hawajui wanalolitenda ama ni wabadhirifu. Je wanaowasimamia wao hawana share yao katika uzembe huu?
Haya mambo yanachanganya.
 
Hivyo vifungu vya kumpigia waziri mkuu kura ya kutokuwa na imani nae haina exceptions????
Inabidi mabazazi yote yaondolewe kwenye uongozi mapema:shut-mouth:
 
Kweli mitandao ya kijamiii ndo nguzo ya mapinduzi
 
itabidi ccm kama kweli inataka kubaki madarakani warekebishe katiba na kuondoa ukiritimba na kupeana vyeo kwa kujuana na waheshimu wataalamu wenye kujali masilahi ya taifa vinginevyo.......................mwisho wa kiama chao ni sasa.....
 
Wamechelewa sana hao Mabazazi! wafutike kabisa ktk siasa za nchi hii
 
manaibu wa wizara za Nishati na serikali za mitaa wanasubiri nini?......huyu Mwanri na malima......................au wanasubiri watimuliwe?
 
hivi hakuna sheria yeyote ile yakuwa idadi flani ya mawaziri wakijiuzuru kwa pamoja, inabidi baraza zima la mawaziri livunjwe?
 
Tuwekeeni copy ya barua nata moja tu ya sample ya kujiuzulu hapa e.g ya hajj mponda ndo nitaamini.
 
Hongera Zitto, hongera CDM. Hii ni mojawapo ya faida za kuwa na upinzani wenye nguvu!!!

Tiba
 
now we are talking!muda wa kupigapiga porojo wakati wananchi wanazidi kufa kwa kukosa huduma bora na madawa hosp,watoto we2 wanapata elimu duni,rasilimali zetu zinachotwa tu na wenye akili na wapuuzi hao wanoitwa mawaziri na watendaji wengine wanatanua tu....yaani hawa jamaa wanatakiwa kupigwa pingu tu...masuala mengine tukaelezane mahakamani maana kuna watu wanajiona wao na familia zao ndo wenye copyright ya hii nchi!
 
Back
Top Bottom