Itakuwa ni ya siri hakuna ajuae nani ni nani. Ilishafanywa kitu kama hii duniani wafatiliaji wa mambo wananielewa nazungumzia nini.
Mheshimiwa ni vyema kuangalia mambo ya duniani lakini unapotaka kuyaleta hapa kwetu ni vyema ukaangalia mazingira yetu, utamaduni wetu na aina ya watu tulio nao kwenye vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo ndiyo hasa vinatarajiwa kufanya haya unayopendekeza.
Kama vyombo vyote vya ulinzi na usalama na hata mahakama vimetekwa na hili wimbi la ufisadi ni wapi utawapata watu watakaofanya hayo unayoyasema bila kurubuniwa na mafisadi au bila siri za hicho wanachofanya kujulikana na walengwa kabla ya kutekelezwa?
Mimi nachukulia wazo lako kama jibu rahisi mno kwenye swali linalohitaji tafakuri ya kina ili kupata suluhu.