Mawaziri 6 sasa mikononi mwa TAKUKURU!

Mawaziri 6 sasa mikononi mwa TAKUKURU!

Kaka William, kama kumbukumbu zangu ziko sawa nakumbuka uliwahi kuulizwa hapa kama ungeunga mkono mapinduzi dhidi ya mawaziri watuhumiwa ukasema unataka legal facts.

Do u really need facts besides a professional auditor's report?

- Hoja yangu ni wananchi tulilie mawaziri waende kwenye Sheria, nini maoni yako on that? FULLSTOP!

William.
 
Hili ni changa la macho kwa Watanzania. TAKUKURU hawana lolote ni chombo cha propaganda katika kuficha upuuzi unaofanywa na serikali na kulinda maslahi binafsi ya viongozi na chama tawala
 
- Zamani kilikuwa ni cheo cha Waziri wa Usalama wa Taifa, well mimi ni binadam kama wengine ninaheshimu sana utumishi wa Waziri Mwandosya, ningempa the same position ili kumpa nafasi ya kuendelea kutibiwa na Taifa.

William.

William u deserve like umejibu vizuri kabisa....Mbali ya matibabu lakini kuna issue ya Siasa za Mbeya.

Mytake: Kuwe na Medical Scheme kwa watu kama Prof kuliko kumpa cheo ambacho mnajua kabisa kuwa hakina kazi
 
Hivi wewe Wiliam ni mwanasiasa? Au ni mwigiza siasa? Mbona kijana una propaganda dhaifu sana? Ni mdogo wa umri lakini mawazo yako yamezeeka na uwezekano wa kuyakarabati ni mgumu. Sijui iweje, ili uje umbadili ubunge nduguyo Kibajaji a.k.a Livingstone Lusinde wa Mtera! Tofauti ni ndogo sana, itumie vizuri elimu yako ya darasani na kutembea kwako katika siasa uzifanyazo. Vinginevyo watu watakupotezea! Soma alama za nyakati kijana, nenda na mapigo ya sasa hivi. 2015 is not far.
 
- Nothing to do na ishu at hand, the ishu hapa ni wananchi tuamue kuililia Serikali mawaziri waende kwenye Sheria, what is your point on that? au unataka Zitto ndio apigane peke yake?

- Hayo mengine ni kelele za mlango! keep them to yourself! ha! ha! ha! ha!

William.

Ndugu toa mbinu zipi wananchi waililie serikali ili mawaziri waende kwenye sheria. bado unatumia hizo lugha za ccm, zisizo na ujumbe kamilifu natekelezi (propoganda), Zitto akiraise hoja mbungeni maana yake ni onbehalf ya wananchi,kama pressure ilivyokuwa kwa waziri mkuu awajibike. Au unataka wananchi wote waende bungeni? kama ni maandamano waachie wapinzani wako cdm. TOA MBINU IPI WANANCHI WAILILIE SERIKALI??

Hizo kelele za mlango mtazisikia tu mtake msitake, hayo matabaka yaliyojengeka ndo kelele za milango hizo kitaeleweka tu, ha ha! ha! ha!
 
- Umeonyesha tu uwezo wako finyu wa kufikiri unapoanzia na kuishia, Mwandosya ni Kiongozi wa juu sana wa Taifa na kwa muda mrefu sana, sasa unasema nini wakifikia mahali wanaugua wakiwa kwenye power dawa ni kuwatupa?

- Halafu tizama your contradictions, unasema hutaki Mwandosya atibiwe halafu unarudia tena kwamba ni afadhali atibiwe na hela zetu walipa kodi, pure confusion unataka nini na hutaki nini bro?

William.

William,

Kwa hiyo unataka kutuambia kwa kuwa Mwandosya ni kiongozi wa juu nchi hii, wananchi inabidi wabebe mzigo wa kumutibia hata kama hana utendaji kwa kuwatumikia! Huu si ni wizi tu, kwamaba "wenzetu" hawatupwi mpaka wafie kazini!!

Na kwanini wananchi tufikie hatua ya kulia lia tu eti hadi serikali itusikilize? I have a lot of reservations kwa ujio wako bongo!! Wewe ni uzao wa mfumo huu mchafu tulionao, huwezi hata siku moja kuupinga au hata kuhitaji uondolewe, maana u mmoja wa beneficiaries!! Mchongo wa EALA umedunda, labda jipange kwa Mahanga!!!

Tatizo la nchi hii si watendaji, bali MFUMO......ambao CCM itakufa nao!!
 
Hapa ndo linapokuja suala kutafuta ushahidi uliofichwa na mtafutaji mwenyewe sawa na mwizi kujaribu kijiibia mwenyewe.Hakuna kitu hapo na tusipotezeane muda na hela za kutafuta magazeti
 
Wale mawaziri waliofikishwa mahakamani miaka ya nyuma akina yona na mramba mpaka leo kesi zao ziko mahakamani hawajahukumiwa... hawa wengine wako wengi mno na nina uhakika itachukua miaka 10 mpaka kesi zao kukamilika, tutazidi kupoteza hela za walipa kodi kuendesha hizi kesi alafu mwisho wa siku watapatikana hawana hatia....waste of money and waste of time

Na kuna wengine wako kwenye hizi kashfa na bado ni mawaziri..mheshimiwa hajawatimua wote so hao aliowabakiza tuwafanyeje!!??

Rais wetu kapangua mawaziri, Mkuu wa Polisi nae kapangua safu yake ya makamanda wa polisi...Je Nani atapangua safu ya mahakimu/Majaji wanaoendesha kesi zetu za hapa nchini? maana huko mahakamani nako kunanuka rushwa na ufisadi nani atafanya hivyo na ni lini tutegemee hilo bwana Malecela??!!

Mkuu nadhani umemaliza kila kitu. Nchi yetu ni hodari kwa kugungua wizi wa fedha za umma, lakini ni vivu sana kuwaadhibu. Ninakuhakikishia kuwa kauli ya rais ya upepo utapita ilikuwa na maana nzito ndani yake, na sidhani kama kweli alikuwa na nia ya kubadilisha baraza la mawaziri, alishinikizwa kiasi.
Siamini kama mahakama, Takukuru na hata serikali yenyewe ina uwezo wa kuwashughulikia watu hao. Zitapigwa porojo hadi upepo utapita.
 
- Umeonyesha tu uwezo wako finyu wa kufikiri unapoanzia na kuishia, Mwandosya ni Kiongozi wa juu sana wa Taifa na kwa muda mrefu sana, sasa unasema nini wakifikia mahali wanaugua wakiwa kwenye power dawa ni kuwatupa?

- Halafu tizama your contradictions, unasema hutaki Mwandosya atibiwe halafu unarudia tena kwamba ni afadhali atibiwe na hela zetu walipa kodi, pure confusion unataka nini na hutaki nini bro?

William.

Mkuu your line of argument in this matter is a little bit questionable. I do not believe that appointing him to head the ministry without portfolio, or a ministry which is not there, is a way to go about it. I do not believe that JK cares much about his health, i would believe that it is much safer to have him in the cabinet that to let him go. He will be more dangerous being out of cabinet than being within it. Kumwacha mgonjwa toka kwenye baraza la mawaziri si kumtupa serikali inaweza kuwa na mechanism nyingine za kugharamia matibabu yake kama ikitaka. All in all tunachochukia zaidi baadhi ya wananchi ni uozo serikalini, that is bigger picture. Uozo huo unaendelea kuthibitishwa kila kukicha.
 
- Kuja upande wa pili ni lazima nipaamini huko, so far bado sijafikia hilo kutokana na kujua mengi sana yanayoendelea within na hizi siasa, lakini mimi nimesema hivi na wakati wote kwamba siwezi hata siku moja kukosa kuweka wazi msimamo wangu on any ishus hapa bongo, kwenye hili la mawaziri ninasema sasa tumewaondoa kwenye nafasi kwa sababu ya kuamini sio wasafi, basi wakasafishwe na Sheria!

- Upande wa pili bado sijaamini kwamba huku niliko kumeshindwa, siku nitakapoaamini hivyo utaniona nikiwa wa kwanza kuja huko, sio sasa!

William.

Kwa kweli mkuu unastahili "admiration". Kama kweli bado una imani na utawala wa CCM "kama ulivyo" kwamba unafanya kazi ya maana nchini basi imani yako ni ya aina yake. Labda hali halisi anayokumbana nayo Mtanzania wa kawaida asiye na usuhuba na nyezo za dola huijui kabisa. Yaani unaamini kabisa kwamba hayo mabadiliko ya baraza la mawaziri ni hatua makini iliyofanywa ili kusafisha serikali ya CCM? Kwamba hao walioondolewa ni "wabovu wachache" waliokuwa "wakicheza peke yao" kuharibu "umakini na taswira safi" ya serikali ya CCM? Kwamba ni haki kwao kufikishwa mahakamani kwa "madhambi yao binafsi"?

Kwa vile unaonekana ni mtu makini sana naomba nikupe ushauri huu: kama unaipenda CCM kiasi hicho basi ongoza harakati nzito kabisa za kuipindua "establishment ya kimafia" iliyojijenga ndani yake kwa miongo kadhaa sasa na kukirejesha chama kwa wananchi. Nakuhakikishia hakuna dawa kwa CCM hii na serikali zake nje ya hizi mbili: chama kufa au mfumo wake mzima kupinduliwa kikamilifu. Sina imani na uwezekano wa mapinduzi ya ndani; lakini jaribu!
 
Mkuu your line of argument in this matter is a little bit questionable. I do not believe that appointing him to head the ministry without portfolio, or a ministry which is not there, is a way to go about it. I do not believe that JK cares much about his health, i would believe that it is much safer to have him in the cabinet that to let him go. He will be more dangerous being out of cabinet than being within it. Kumwacha mgonjwa toka kwenye baraza la mawaziri si kumtupa serikali inaweza kuwa na mechanism nyingine za kugharamia matibabu yake kama ikitaka. All in all tunachochukia zaidi baadhi ya wananchi ni uozo serikalini, that is bigger picture. Uozo huo unaendelea kuthibitishwa kila kukicha.

- Thank you, I rest my case!

William.
 
Back
Top Bottom