Mawaziri 6 sasa mikononi mwa TAKUKURU!

Mawaziri 6 sasa mikononi mwa TAKUKURU!

- Ni kwa sababu tunalia lia sana bila vitendo na kusubiri wengine na kuanza kuwatukana tu, lakini matendo hakuna! Tumedai waondoke wameondoka, sasa tudai Sheria maneno mengi off course ndicho watwala wanachokitaka kwenye maneno haya mengi watapitisha agenda zao na kubadili subject, kama wanavyojaribu sana kwa kukomalia Mbowe aeme majina by kesho media nzima itakuwa kwenye hiyo ishu, huku la mawaziri na Sheria hakuna!

- Haya tunayataka wenyewe, kwa sababu ni very clear kwamba Rais aemwaondoa kwa sababu ya CAG, sasa kwa nini tusidaai aende mbele zaidi? No wengi tunafurahia kuwaona wapo nje tu as if watapanda dala dala na sisi hata siku moja, never!

William.

Tumepiga kelele sawa. Matokeo yamekuwa si 100 per, wengi tulitegemea Rais angesimamia dhana ya uwajibikaji fully, aidha wote waliokuwa implicated katika ripoti ya CAG wavuliwe madaraka pending further investigation au wenyewe wangejiudhuru lakini naona kama Rais kafunika kombe mwanaharam apite.
Madai yako ya sheria kuchukua mkondo hayaleti maana kama tuhuma nzima hazikuchukuliwa kwa uzito stahiki tokea mwanzo.
Mimi naona kelele zetu ziendelee kupigwa kuhusu hii scam nzima. Sheria ichukue nafasi kuanzia wale waliochaguliwa tena na waliotolewa....
 
Niliipenda sana katuni ya Kipanya
Takukuru ni mwewe au tai wa msituni anayesubiri mzoga wa fisi au simba ajipatie ulaji
Hiyo takukuru wakati mapesa yanaliwa tena mengine taarifa zinatoka kila siku kwenye vyombo vya habari kwa nini isichukue hatua mpaka isubiri watu wapige kelele ndo iamke
Wakurugenzi wangapi ambao wanatuhumumiwa kuwa halmashauri zao zimeoza kwa ulaji ila Takukuru iko kimya au inasubiri mzoga kutoka kwa CAG
Hizi nazo ni mbwembwe maana file litapelekwa Takukuru na taarifa kibao likirudishwa kwa DPP linakaa mwaka bila kufanyiwa kazi
Eti mpaka DPP ajiridhishe kuwa kuna ushahidi wa kutosha
Sioni jipya hapo sana sana ni kiinimacho cha kesi kuendeshwa miaka kadhaa na then mahakama inawaachia kwa kukosa ushahidi wa kutosheleza kuwatia hatiani
 
Mimi naona kwa sisi waTanzania bahati sijui niseme nzuri au mbaya! Mungu katupa uwezo wa kusahau saana, tena wakati mwingine hata mambo ya msingi kabisa.

Watanzania tunapenda saana hearsay, na tunaamini saana hearsay! Kuuzwa kwa wanyama waziri aliyepita Mwangunga ndio alihusika huyu dogo Maige hayumo! Report ya CAG inawaingiza mawaziri wapya kwenye mikasa mikuuukuu, Prof. Maghembe hayumo kwennye kashfa ya awali ya pembejeo, ni Wassira n.k.

Kama GT hebu tuwe tunatunza kumbukumbu ya vitu vinavyo tokea kwenye taifa letu, la si hivyo tutaishia kuumiza watu wasio stahili.
 
Watanzania tunapenda saana hearsay, na tunaamini saana hearsay! Kuuzwa kwa wanyama waziri aliyepita Mwangunga ndio alihusika huyu dogo Maige hayumo! Report ya CAG inawaingiza mawaziri wapya kwenye mikasa mikuuukuu, Prof. Maghembe hayumo kwennye kashfa ya awali ya pembejeo, ni Wassira n.k.

Kama GT hebu tuwe tunatunza kumbukumbu ya vitu vinavyo tokea kwenye taifa letu, la si hivyo tutaishia kuumiza watu wasio stahili.
Umetumwa!!??......
 
TAKUKURU imepewa jukumu la kuwasafisha wala si vinginevyo.
 
CAG kazi yako safi sana, wanaweza kufikishwa mahakamani kwa mchezo ule ule wa kuigiza kama kina yona, mramba, jeetu patel n.k, pole kwake rajab maranda kwani aliingizwa kwenye mtandao usiokuwa wa kwake, ndio maana kesi yake kwisha chap chap na mvua juu
 
hakuna lolote, labda yy jk ajipeleke mahakamani kwanza ! Mbona bado kaweka walaji wengine kulinda maslahi yake ktk sekta flan flan ? Katibu mkuu km yule komba alimpa zawadi ya ubalozi uganda baada ya kufanikisha kuuza wale wanyama sasa kama kweli yy hausiki basi amtimue yule haraka na kumrudisha ajibu mashtaka !

What about jahiro ? Blandina nyoni anajulikana tangu zamani, hao akina mapunjo wanajulikana madili yao na yy mwenyewe tangu wakiwa wizara kibao mpaka alipmvuta ikulu, na then kumpeleka viwanda na biashara ambako yy ni mmoja wa hao wenye makampuni feki na jk anajua siku nyingi.

Wtf, mnampa sifa kuwa yy ndiyo aliamua report ijadiliwe, kwani hii ni report ya cag ya kwanza ? Ni upinzani ndiyo umesababisha haya yote na baadhi ya wabunge wa ccm baada ya kufuatilia wakagundua ni kweli wenzao wanakomba bila huruma na jk anajua na kuhusika thru mtandao plus rz1. Mbona yule ded aliyetafuna mahela akiwa bagamoyo, rafiki yake mkubwa ndiyo kampa u rc arusha ?

So wewe acha hizi sifa hewa unless sasa unavizia nafasi iliyobaki ya kuteuliwa ubunge !! Vp anakuja lini kufungua tawi lako la ccm...lol

issue hapa ni kuingia street na kuanza kuwashughulikia wabongo tuache usingizi. Tangu enzi majimaji nchi hii haijaishiwa watu wabaya ila wazuri ndio wanaoondoka. Sasa ili vita ya majimaji ya mwaka 1905-07 iwe na maana basi tuanze kuwafurusha watawala hawa walafi wa mali yetu sote. Nafikiri kinjekitile ndiye mzalendo ambaye hakuhitaji kuingia darasani ili awe mzalendo. Sasa tujipime uzalendo wetu uko wapi. Je hatuoni uchungu hawa walafi kuendelea kuitafuna nchi yetu bila huruma kupitia kwenye madaraka tuliyowakabidhi wenyewe. Nimegundua ndio maana jk. Aliamua fomu yake ipelekwe kwa wadhamini.na mwanae kwani ndiye anayeifaidi nchi jamani tuko wapi leo?
. Sasa wale wadhamini sijui wanapata nini au ndo waliachwa solemba wakambulia mavumbi ya msafara wa r1.
 
Wakuu JF heshima mbele sana,

- Well, kitendo cha Rais kuwabadili mawaziri waliokuwa wakituhumiwa kuhusika na upotevu wa hela za wananchi na ripoti ya CAG, kina maana moja tu kwamba hata na yeye ameridhika kwamba kuna ukweli au FACTS katika tuhuma walizokuwa wakituhumiwa nazo, ninasema great second day kwa Taifa, kwanza ilikuwa kuweka ripoti wazi to the public na kuruhusu mjadala wa public!

- Sasa ifike mahali pa kufanya kweli, yaani Watuhumiwa wote kufikishwa kwenye mkondo wa Sheria, haki itakua imetendeka na sio otherwise, kwanza haki kwao mawaziri maana wanahitaji kuwa wasafi mbele ya public na pili Serikali kulinda heshima yake kwamba sasa ipo serious, ama sivyo kuitoa ripoti ya CAG to the public itakuwa ni kazi ya bure, I mean mawaziri na viongozi wetu wakijua kwamba madhara ya kuiba ni kujiuzulu tu na kuachiwa ukale mihela ya wananchi tutakua tunajenga taifa la kusadikika, na itakuwa kazi kubwa kumpitisha Rais wa CCM 2015!

- MHESHIMIWA RAIS, UBARIKIWE KWA KUSIKILIZA MAONI YA WANANCHI, SASA TWENDE MBELE ZAIDI TUFIKE KWENYE SHERIA NA WOTE WENGINE HAO MAKATIBU NA WAKURUGENZI ULIOSEMA KWENYE HOTUBA YAKO KUWA WANAHUSIKA NA WAO PIA UWE MWENDO WA KUELEKEA KWENYE SHERIA!, NI SHERIA TU NDIO INAWEZA KUTUSAFISHA WOTE, SERIKALI NA MAWAZIRI WALIOACHWA!

MUNGU AIBARIKI TANZANIA!



Hakuna kitu hapo TAKUKURU ni bogus. Hawana uwezo huo waache wakamate rushwa za ngono na za Matrafiki barabarani
 
Chukulia mfano wa suala la waziri Maige la kuuza wanyama hai nje ya nchi. Hawa wanyama walibebwa kwenye ndege ya jeshi. Na kama tujuavyo ndege ya jeshi ya taifa lingine haiwezi kuingia nchi nyingine bila kibali cha jeshi la nchi husika. Kwa maana hiyo suala la Maige linatakiwa lifagie watu wengi wakiwemo maofisa wa jeshi waliotoa kibali cha ndege hiyo kutua hapa nchini. Pia tuliambiwa kuwa wanyama hao walisindikizwa na FFU pale KIA tena kwa mitutu ya bunduki, which means maofisa wakuu wa polisi somewhere aidha kwa ngazi ya mkoa au taifa wanahusika. Tutafurahi kuona mtiririko huu unafuatwa katika kuwawajibisha wahusika waliouza wanyama wetu hai nje ya nchi. Naomba kutoa hoja.
 
Gazeti la Mwananchi said:
Baadhi ya tuhuma zilizokuwa zimeibuliwa na CAG kwenye Wizara ya Fedha iliyokuwa chini ya Mkulo ni kuvunja Bodi ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC), ili kuficha tuhuma zake ikiwemo uuzaji wa Kiwanja Na.10 kwa Kampuni ya Mohamed Enterprises (MeTL).

Hii ni mojawapo ya kashfa za Mkulo, Kwahiyo Mohammed Dewji (MB) ambaye ni mmiliki wa MeTL naye anastahili kuwajibishwa kwa rushwa katika kununua kiwanja hiki
 
Wakuu JF heshima mbele sana,

- Well, kitendo cha Rais kuwabadili mawaziri waliokuwa wakituhumiwa kuhusika na upotevu wa hela za wananchi na ripoti ya CAG, kina maana moja tu kwamba hata na yeye ameridhika kwamba kuna ukweli au FACTS katika tuhuma walizokuwa wakituhumiwa nazo, ninasema great second day kwa Taifa, kwanza ilikuwa kuweka ripoti wazi to the public na kuruhusu mjadala wa public!

- Sasa ifike mahali pa kufanya kweli, yaani Watuhumiwa wote kufikishwa kwenye mkondo wa Sheria, haki itakua imetendeka na sio otherwise, kwanza haki kwao mawaziri maana wanahitaji kuwa wasafi mbele ya public na pili Serikali kulinda heshima yake kwamba sasa ipo serious, ama sivyo kuitoa ripoti ya CAG to the public itakuwa ni kazi ya bure, I mean mawaziri na viongozi wetu wakijua kwamba madhara ya kuiba ni kujiuzulu tu na kuachiwa ukale mihela ya wananchi tutakua tunajenga taifa la kusadikika, na itakuwa kazi kubwa kumpitisha Rais wa CCM 2015!

- MHESHIMIWA RAIS, UBARIKIWE KWA KUSIKILIZA MAONI YA WANANCHI, SASA TWENDE MBELE ZAIDI TUFIKE KWENYE SHERIA NA WOTE WENGINE HAO MAKATIBU NA WAKURUGENZI ULIOSEMA KWENYE HOTUBA YAKO KUWA WANAHUSIKA NA WAO PIA UWE MWENDO WA KUELEKEA KWENYE SHERIA!, NI SHERIA TU NDIO INAWEZA KUTUSAFISHA WOTE, SERIKALI NA MAWAZIRI WALIOACHWA!

MUNGU AIBARIKI TANZANIA!



William @DSM CITY!


Nafurahi umerudi hapa..!! Kwanza pole kwa michakato ya kiuchaguzi. Kukosa ubunge si kukosa maoni na maneno ya hekima. Karibu tena ..!!!

Labda tusiende mbali sana.. Unataka kunambia Rais alikuwa hafahamu madudu hayo ya mawaziri wake hadi alipokuja kuamshwa na riport za CAG na wabunge? Mara ngapi wabunge/ wananchi wameupigia kelele ufisadi ndani ya Serikali na hakuna lolote lililo fanyika zaidi ya kupuuzwa.

Rais si lolote na ni mnafiki kwani matatizo ya Tanzania na mawaziri wake ni matatizo ambayo yameshalisumbua Taifa tokea kipindi cha mwisho cha awamu yake ya kwanza.

Kitendo cha kubadirisha mawaziri kwa kipindi hiki si cha kumsifu bali ni kitendo cha kumshangaa na kumpuuza kwani alitakiwa kuyafanya hayo mapema hata kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010.
Tuna kwenda wapi kwa kuongozwa na watu wenye kubebana kwa maslahi binafsi. Tutapiga kelele mwisho wa siku tutakuja kuulizana" Nani mwenye ushahidi? alete"

Kumbuka sentensi " Mwenye kuona ameonewa akimbilie mahakamani"

Watanzania kwasasa tunatakiwa kujipanga na kuona ni jinsi gani tunataka nchi iendeshwe kwa kuanzia chaguzi za mwaka 2015.
Kwa wakati huu nchi imeshaozeshwa na maamuzi ya Rais mengi ni ya kishkaji, Kama member mwingine alivyo sema hapo juu..Kuwashtaki mawaziri na wale wote wenye kuhusika na ubadhilifu wa mali za uma ni kupoteza fedha na muda kwa serikali tuliyo nayo sasa.

Hebu tazama mjinga mwingine wa Kukukuru anakuja na hadithi za kusema anaanza kazi ya kuwahoji waliotajwa kwenye ripoti ya CAG na lipoti zingine. Kama sio kuwafanya Watanzania mahanisi ni nin. Walikuwa wapi siku zote hadi wasubiri ripoti iliyo kamilika, Na vile vile wanataka kuchunguza nini wakati kila kitu tayari kipo kwenye ripoti. Hii nchi hovyo kabisa.
 
Unabembeleza sheria kuchukua mkondo wake! tena kwa kumsifu rais, walikunyima kura kihalali kama akili yenyewe ndio hii.
hii inatokea tanzania pekee

Kuna tofauti kubwa sana kuwa na SHERIA na KUTAFSIRI sheria. Kweli unaweza ukasema kuwa kufuatana na ripoti ya CAG mawaziri fulani wamevunja sheria za nchi lakini hapo hapo mahakama ikatafsiri kuwa hakuna sheria iliyovunjwa!! Hii inawezekana katika nchi kama Tanzania ambapo rushwa imekithiri katika taasisi zote. Katika hali kama hiyo unaweza kusema utawala wa sheria utafanya kazi? Sheria hufanya kazi katika jamii yenye UWAZI,UWAJIBIKAJI UADILIFU na Demokarasia kwa maneno mengine jamii yenye utawala bora ambao hapa kwetu haupo!!
 
Pia tuliambiwa kuwa wanyama hao walisindikizwa na FFU pale KIA tena kwa mitutu ya bunduki, which means maofisa wakuu wa polisi somewhere aidha kwa ngazi ya mkoa au taifa wanahusika. Tutafurahi kuona mtiririko huu unafuatwa katika kuwawajibisha wahusika waliouza wanyama wetu hai nje ya nchi. Naomba kutoa hoja.
Nenda sasa ukaombe askari labda unataka kwa ajili ya kuescort pesa uone watakavyokugandisha, "mara tuna askari wachache leo" mara "kuna tukio wameenda huko" mara njia unayotaka kupita kuna doria......! lol
Utagandishwa mpaka benki zinafungwa.

Lakini hawa wa kusindikiza nyara zetu, defender nzima ilijaaa.

 
- Kuja upande wa pili ni lazima nipaamini huko, so far bado sijafikia hilo kutokana na kujua mengi sana yanayoendelea within na hizi siasa, lakini mimi nimesema hivi na wakati wote kwamba siwezi hata siku moja kukosa kuweka wazi msimamo wangu on any ishus hapa bongo, kwenye hili la mawaziri ninasema sasa tumewaondoa kwenye nafasi kwa sababu ya kuamini sio wasafi, basi wakasafishwe na Sheria!

- Upande wa pili bado sijaamini kwamba huku niliko kumeshindwa, siku nitakapoaamini hivyo utaniona nikiwa wa kwanza kuja huko, sio sasa!

William.

After all the shit you went though when contesting for the seat in the East African Legislature, you still have not found out that CCm is a moribund party? Utakapotaka kutoka it will be too late and your only other option will be to go back to the big Apple and drive those trucks; timing is important in politics. Wazee wako have no future in modern politics it is high time you became your own man not even Nape's crony!!
 
W. J. Malecela wakati wa kina lowassa na wezake ulitueleza mengi tukakuamini ukasifu viongozi wa nchi kwa kaulki zao leo umerudia tena katika hali ile ile utaanza kujiondolea heshima uliyojiwekea nina hakika unaelewa Viongozi wetu wananuka Uongo
 
Haya ni masihala na tambo zilezile za serikali tunazozosikia kila siku. Ripoti ya CAG peke yake haiwezi kuwatia hatiani kwani ni ya ujumla mno. Hata pale ilipo specific haijawa-implicate moja kwa moja kitu ambacho kinawapa mwanya wa ku-save mbele ya sheria. Pili Rais Kikwete na kamati kuu yake alikosea sana au alifanya makusudi kutangaza nia ya kuvunja baraza huku akiwaacha mawaziri kwa takribani wiki mbili wakiingia ofisini na kunyofoa vielelezo vyote vyenye ushahidi kama vile memo n.k. Kitendo hiki cha rais kinatia doa nia thabiti ya kuwachukulia hatua watuhumiwa wote. Mimi hapa naapa hakuna hatua yoyote itakayochukuliwa na kama watafikishwa mahakamani basi itakuwa kiini macho kama kile cha akina Mramba na Yona, kesi zao zimechukua karibia miaka 10 hazijaisha mbona za wengine mwaka mmoja miwili wamehukumiwa? Aibu aibu aibu kwa serikali ya ccm na Kikwete.
 
Iundwe independent elimination squad.

Inachunguza, inahukumu, ina eliminate kila afanyae madudu awe ni waziri au tarishi. Siku anayokuwa eliminated, anawekewa na hukumu yake na ushahidi kamili wa madudu aliyofanya.

Wakifika watano tu! ukimpa mtu hata soda atakataa! wacha "takrima" na "ten percent".

sijui tutafika huko!!
 
william hujui vizuri uchafu wa siasa za ccm au unapenda sana,mpaka chongo unamwita kengeza,kikwete anachofanya ni ucomedy.kawekwa kuwa rais kwa pesa chafu hongo zilizotumika hata kuwapangua akina john malecela,sumaye,salim ahmed salim wote tunajua.sasa kikwete hawezi kukubali sheria iwahukumu hao mawaziri sababu ndani yake na yeye anahusika,tuko pamoja leo,na kesho hutasikia maige nundu ngeleja wala mkulo wakitaifishwa hata bajaji zao.tunataka kubadilisha nguvu ya rais ndio tanzania itabadilika.sababu chini ya chama kinachotawala kwa misingi ya rushwa hakiwezi kuongoza serikari safi.william una safari ndefu kujua uchafu wa ccm yenu.
​andrew@london
 
i am appalled and frustrated that bw malecela, despite being educated and exposed to the outside world, you still bear the rudimentary thinking that we see in our semi literate, feeble minded politicians!!!

yaani tumpe uongozi mwandosya ili atibiwe na nchi!!!!! khaaaa this is the most stupid notion ever, utter nonsense and complete BS!!! kwani hana bima ya afya?? je mababu zetu nao tuwape uongozi ili watibiwe pia na serikali si ndio jamani cz wagonjwa ni wengi.

i have nothing against waziri mwandosya na i would have supported him being treated kwa fedha za kodi yetu but sio kwa namna hii jamani!! utter and complete BS!! na new generation ya CCM kama malecela anasupport!!!! yaani am disappointed , totally.
 
Back
Top Bottom