Mauaji ya wabeba mkaa maarufu 'booster'

Mauaji ya wabeba mkaa maarufu 'booster'

Mimi nachoma mkaa nasafairisha na vibali ,hao wanaobeba na pikipiki gunia tatu tatu ni risk sana ,wanawindwa sana na askari wa rostam ,ukikutwa unakula chuma ,huwa wanatoa dakika 15 hadi 20 ila wanakatiwa fungu na kiongozi wa maBOOSTER ,ukichelewa ni kifungo miezi 6.
Ukisema askari wa rostam una maanisha nini mkuu ,kama hutojali nifafanulie kidgo mkuu
 
Hamjui kuna sheria imepitishwa kuwapa watu fulani haki ya kukuua wakijisikia? Yaani anakuua kwa utashi wake kwa mujibu wa sheria. Tulieni mlambe asali nchi imefunguka, demokrasia imetamalaki.
Au ndiyo lile zuio la kukata misitu

Ova
 
Kwa hiyo Mkaa unathamani kuliko uhai wa MTU??Kwani wangewakamata na kuwapiga faini waongeze pato la taifa na la familia,,,kuliko kupoteza nguvu kazi ya taifa
Tatizo bodaboda hawakamatiki jaribu uone, mmesahau wiki mbili zilizopita walichoma moto basi la abiria huko Korogwe, walijichukulia sheria kama kawaida yao.
 
bahati mbaya mtaani matukio huripotiwa tofauti sana.

hawa watu hushambulia askari mara kwa mara kwa mapanga,moja ya case iliyosababisha mambo ya kibiti ni hii.
watu kujiona wana haki sana na hawapaswi kuguswa ktk hilo.

tutakuwa wendawazimu kuamini askari anaweza akaamka tu ameshiba akaanza kurusha risasi kuua watu,halafu tunaendelea na yaliyo kinyume na sheria.
Watu wanafikiri it is OK kuvunja sheria yoyote ya nchi as long as unatafuta kipato. In fact wengi wa wahalifu wa namna hii, wakiwemo na majangili huwa hawako innocent na wanaona ni haki kupambana violently na watumishi wa serkali. Wakiumizwa wao ndio zinakuja hizi one-sided stories zikionesha kuwa wanaonewa.

Ni kweli haipendezi kupoteza maisha kwa kosa kama hilo la kuchoma au kuuza mkaa bila kibali, lakini inawezekana haya yalikuwa mapambano ambapo hata askari angeweza kupoteza maisha.
 
Wana jamvi habarini za wakati huu.

Jana majira ya saa sita usiku kuna mauaji yametokea yaliyosababishwa na watu wa maliasili.

Tukio hilo limetokea Mkoa wa Pwani, wilaya ya Kibaha (V), tarafa ya Ruvu, Kata ya Kwala, kijiji cha Kwala! ambapo watu wa kubeba mkaa maarufu kama booster wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wa maliasili walipokuwa wakisafirisha mkaa majira ya usiku na kupita maeneo walipokuwa wameweka mtego maliasili.

Watu hao walipigwa risasi na mmoja wao akapoteza maisha hapo hapo, mwingine alifariki akiwa anapelekwa hospital leo saa sita mchana mara baada ya askari wa mlandizi kufika eneo la tukio, mtu huyo mmoja alishindwa kupata msaada wa kwanza kwa muda wa masaa zaidi ya 12 sababu kuu ikiwa ni zuio kutoka kwa watu wa maliasili huku akizidi kupoteza damu nyingi zaidi.

Maoni yangu

Hawa watu ni watafutaji kama watafutaji wengine, wameacha familia zao wakienda kutafuta maisha katika kipindi hiki kigumu tunachopitia watanzania wengi,

Hivyo basi, ni vyema maliasili kuongozwa na utu wakati wa kufanya kazi zenu, silaha ya moto itumike pale penye ulazima tena baada ya kuchukua precautions kama sheria inavyotaka.

Wanajukwaa tupaze sauti ili haki intendeke kwa ndugu wa marehemu, uchunguzi katika hili ninmuhimu sana, maana mauaji yamekuwa yakichukuliwa kama kawaida na hawa wanaojiita watu wa maliasili.
Swali la kujiuliza.
Ni mahakama gani ilitoa hukumu ya kifo kwa vijana hao?

Ni sheria gani inawapa mamlaka Maliasili kuua wabeba mkaa?

Kwa sababu hakuna mwanafamilia wa Wambura aliyeaguswa kwenye tukio hili, basi ndo imetoka hiyo
 
Chanika wiki 1 au 2 nyuma kauwawa mmoja pia.
Haya mauaji ni continues.
Nadhani hizi damu kuna watu wananufaika nazo.
Kuna wale watatu huko Pwani walikula chuma miezi kadhaa imepita
 
Kuna siku tukio baya litakupata wewe au mtu wako wa karibu ndiyo utajua maana ya polisi kufuata sheria. Sisi binadamu siyo maroboti yasio na uwezo wa kufikiri. Hakuna anayesema uhalifu uachiwe bali sheria zifuatwe. olisi hawako ili kuua raia wahalifu bali wako ili kuhakikisha kila mtu anafuata sheria.
Mimi binafsi bodaboda alimgonga na kukimbia binti yangu aliyekuwa mbali kabisa na barabara huku wenzake wakishuhudia tukio, hawakumkimbiza mwenzao ili wamkamate, hawakutoa msaada wowote.
 
Viongozi wanapogawa raslimali za taifa letu wako juu ya sheria? Muuza mkaa maskini anayetafuta ugali wa watoto anauawa na kiongozi anayeuza raslimali ili anunue saa ya sh milioni mia moja yupi anastahili kuuawa.
Hii yote it down tu wananchi mmekuwa wapole na waoga kupitiliza. Wanajua hata report ngapi za CAG zitoke hakuna wakuwagusa. Kutwa mnalalamika kwenye mitandao ? Wameshawazoea
 
Wana jamvi habarini za wakati huu.

Jana majira ya saa sita usiku kuna mauaji yametokea yaliyosababishwa na watu wa maliasili.

Tukio hilo limetokea Mkoa wa Pwani, wilaya ya Kibaha (V), tarafa ya Ruvu, Kata ya Kwala, kijiji cha Kwala! ambapo watu wa kubeba mkaa maarufu kama booster wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wa maliasili walipokuwa wakisafirisha mkaa majira ya usiku na kupita maeneo walipokuwa wameweka mtego maliasili.

Watu hao walipigwa risasi na mmoja wao akapoteza maisha hapo hapo, mwingine alifariki akiwa anapelekwa hospital leo saa sita mchana mara baada ya askari wa mlandizi kufika eneo la tukio, mtu huyo mmoja alishindwa kupata msaada wa kwanza kwa muda wa masaa zaidi ya 12 sababu kuu ikiwa ni zuio kutoka kwa watu wa maliasili huku akizidi kupoteza damu nyingi zaidi.

Maoni yangu

Hawa watu ni watafutaji kama watafutaji wengine, wameacha familia zao wakienda kutafuta maisha katika kipindi hiki kigumu tunachopitia watanzania wengi,

Hivyo basi, ni vyema maliasili kuongozwa na utu wakati wa kufanya kazi zenu, silaha ya moto itumike pale penye ulazima tena baada ya kuchukua precautions kama sheria inavyotaka.

Wanajukwaa tupaze sauti ili haki intendeke kwa ndugu wa marehemu, uchunguzi katika hili ninmuhimu sana, maana mauaji yamekuwa yakichukuliwa kama kawaida na hawa wanaojiita watu wa maliasili.
Hapo rostam, February na msoga genge anataka mnunue gesi ambayo Wana hisa nayo Mana anawapenda mno kuwa mkaa na kuni zinaleta Kansa ya mapafu. So wameambiwa waue ili watu waogope kabisa. Wanataka wengi wageukie kwenye gesi yao mkuu.

Yaani mie nashangaa mzungu anachukua maliasili Ila hauwawi Sasa mwenzenu alichukua anauliwa.

Hii Ni Oda imetolewa toka juu.yaaani unakatazwa usikate mtu,mwishowe usilime.hata miti Kama umeipanda inabidi uwaombe ili ukate miti iyo
 
Hata watumishi wa maliasili (idara ya Misitu) hawaruhusiwi kabisa kutumia bunduki. Kwenye doria zao labda kama walichukua askari polisi.
With all my respect kwako mkuu,labda upo nje ya nchi au yanayotokea on the ground huyaoni au unayaona na una pretend huyaoni kwa sababu hayajagusa family yako, T1 kwa wasafiri wa njia hii,kuna vijiji kabla hujafika kijiji cha Duma, always police hawa wa mali asili wanaonekana ndani ya combat zao,gari zao zenye special number plates na AK47 zao, hawa police wanabeba deadly weapons wakiwa kazini, na tuelewe kuwa kuna standard procedures kabla police hajatumia bunduki yake kwa raia, na tuelewe raia/suspect kama anakimbia away from crime scene, HURUHUSIWI KUMPIGA RISASI, SIO THREAT kwa yeyote, mkuu wa usalama wa Taifa anapigwa risasi nyingi tu na kupoteza maisha, reason behind eti alidhaniwa ni jambazi!,ni court of law only inayoamua kuwa huyu ni jambazi au innocent guy
 
Maskini mwenye sare amuua maskini asiye nayo...

Wezi wakubwa wametulia full Ac.. mkaa tuu mmeua watu kwel
Ndiyo. Ni sawa na nyumbu kadhaa wanachaguliwa miongoni mwa nyumbu kuwa simamieni wenzenu wawe wananiletea watt wenu namkula damu na nyama. Ila chui yeye amekaa akatulia. Cheki tusivyo na uelewa hata kidogo yaani nyumbu wangekuwa na akili kidogo tu Simba asingedhubutu kuwala na kuwamaliza kabisa
 
M
Hao Booster ukizembea wanakuua ,wanatembea Mob na wana silaha za jadi ,huyo aliyeuwa Kessy ni Mbavu Nene alishawahi kumvammia askari akamnyang'anya silaha ,yeye Mbavu ndiyo kiongozi wa MaBOOSTER ,na huyo Tobby ni nyoka wa Kessy......Solution ni kwamba hao maBOOSTER wawe wanakusanya mizigo yao wanakodisha kama Fuso au Scania wanabeba kwa pamoja na kulipia ushuru wa serikali.

Wanapitisha usiku kwa ajili ya kukwepa Kodi.....hao akipiga trip moja hakosi laki na 20 hadi laki unusu faida.
Ulipomaliza kuandika comment hii,pale Tunduma OSBP zimeshazungushwa tankers 30,pale Namanga OSBP tankers 40 na pale bandarini container za 40ft zaidi ya 50 zimetoka bila kulipiwa ushuru, ila mkwere huyu aliyekamatwa na 3 bags za charcoal, akasimamishwa akaleta ubishi, piga risasi ua...paaa
 
M
Ulipomaliza kuandika comment hii,pale Tunduma OSBP zimeshazungushwa tankers 30,pale Namanga OSBP tankers 40 na pale bandarini container za 40ft zaidi ya 50 zimetoka bila kulipiwa ushuru, ila mkwere huyu aliyekamatwa na 3 bags za charcoal, akasimamishwa akaleta ubishi, piga risasi ua...paaa

Imeandikwa mwenye nacho ataongezewa na yule asiyenacho hata kidogo atanyang'anywa.
 
Mzungu hawezi kumfanyie whiteman mwenzie ukatiri wa moja kwa moja wa namnaa hii, mtu mweusi mbinafs na ni mtu msahaulifu sana, ndo mana tulitawaliwa kirahis na bado tunashindwa kujiletea maendeleo.
 
Imeandikwa mwenye nacho ataongezewa na yule asiyenacho hata kidogo atanyang'anywa.
Amina mkuu, hili nakubaliana nawe kabisa, royal families Tanzania zitatawala kwa muda mrefu as far as poor of the poorest na middle class hawana uwezo wa push back
 
Back
Top Bottom