Mauaji ya wabeba mkaa maarufu 'booster'

Mauaji ya wabeba mkaa maarufu 'booster'

Police hawana ujuzi wa kumkamata mharifu na kumfikisha mahakamani ili apate adhabu kiutaratibu na sheria

Police kujichukulia sheria mkonnoni ni vita ya kimbari
 
Kwa hali hiyo hatuna haja ya kua na jeshi la polisi, ukimkaba mtu ili ujipatie chochote ukale na familia yako sawa tu! Kila uhalifu ufanyike ilimradi unajitafutia ukale na familia yako ruksa, nchi itapendeza kama Haiti.
Kuna siku tukio baya litakupata wewe au mtu wako wa karibu ndiyo utajua maana ya polisi kufuata sheria. Sisi binadamu siyo maroboti yasio na uwezo wa kufikiri. Hakuna anayesema uhalifu uachiwe bali sheria zifuatwe. olisi hawako ili kuua raia wahalifu bali wako ili kuhakikisha kila mtu anafuata sheria.
 
Tuendelee kujenga tabia hii ambayo itatufanya na sisi tuwe violence national, police hawaruhusiwi kutumia deadly force, unless maisha ya raia au ya kwake yakiwa hatarini, police state in the making, kulalama humu hakusaidii chochote ni push back ndio lugha hawa kenges watakayo isikia

Serikali inauza na kugawa maliasili kwa wageni pasipo kuzingatia sheria
Negative, inatumia sheria hizo hizo ndio, ila wanatumia udhaifu na mianya kwenye sheria kujinufaisha
 
Kheri ya wanaume kuliko wanawake, na huko kwenu hali ni hihii mkaa ni marufuku bila kibali.
Viongozi wanapogawa raslimali za taifa letu wako juu ya sheria? Muuza mkaa maskini anayetafuta ugali wa watoto anauawa na kiongozi anayeuza raslimali ili anunue saa ya sh milioni mia moja yupi anastahili kuuawa.
 
Kwa hiyo Mkaa unathamani kuliko uhai wa MTU??Kwani wangewakamata na kuwapiga faini waongeze pato la taifa na la familia,,,kuliko kupoteza nguvu kazi ya taifa
 
Hao maliasili wanamjua kwamba Kessy ni mbavu wangechelewa angewamaliza yeye ....Poleni ndugu jamaa na marafiki wa Kessy na Tobby.......Msiba upo kwake Kibaha Loliondo(Kessy) na Kwa Mathias(Tobby).
 
Wana jamvi habarini za wakati huu.

Jana majira ya saa sita usiku kuna mauaji yametokea yaliyosababishwa na watu wa maliasili.

Tukio hilo limetokea Mkoa wa Pwani, wilaya ya Kibaha (V), tarafa ya Ruvu, Kata ya Kwala, kijiji cha Kwala! ambapo watu wa kubeba mkaa maarufu kama booster wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wa maliasili walipokuwa wakisafirisha mkaa majira ya usiku na kupita maeneo walipokuwa wameweka mtego maliasili.

Watu hao walipigwa risasi na mmoja wao akapoteza maisha hapo hapo, mwingine alifariki akiwa anapelekwa hospital leo saa sita mchana mara baada ya askari wa mlandizi kufika eneo la tukio, mtu huyo mmoja alishindwa kupata msaada wa kwanza kwa muda wa masaa zaidi ya 12 sababu kuu ikiwa ni zuio kutoka kwa watu wa maliasili huku akizidi kupoteza damu nyingi zaidi.

Maoni yangu

Hawa watu ni watafutaji kama watafutaji wengine, wameacha familia zao wakienda kutafuta maisha katika kipindi hiki kigumu tunachopitia watanzania wengi,

Hivyo basi, ni vyema maliasili kuongozwa na utu wakati wa kufanya kazi zenu, silaha ya moto itumike pale penye ulazima tena baada ya kuchukua precautions kama sheria inavyotaka.

Wanajukwaa tupaze sauti ili haki intendeke kwa ndugu wa marehemu, uchunguzi katika hili ninmuhimu sana, maana mauaji yamekuwa yakichukuliwa kama kawaida na hawa wanaojiita watu wa maliasili.
Heri wafe hao wachache ili iwe fundisho kuliko majanga ya mazingira yatakayo athiri watu wengi huko mbeleni.
 
Wana jamvi habarini za wakati huu.

Jana majira ya saa sita usiku kuna mauaji yametokea yaliyosababishwa na watu wa maliasili.

Tukio hilo limetokea Mkoa wa Pwani, wilaya ya Kibaha (V), tarafa ya Ruvu, Kata ya Kwala, kijiji cha Kwala! ambapo watu wa kubeba mkaa maarufu kama booster wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wa maliasili walipokuwa wakisafirisha mkaa majira ya usiku na kupita maeneo walipokuwa wameweka mtego maliasili.

Watu hao walipigwa risasi na mmoja wao akapoteza maisha hapo hapo, mwingine alifariki akiwa anapelekwa hospital leo saa sita mchana mara baada ya askari wa mlandizi kufika eneo la tukio, mtu huyo mmoja alishindwa kupata msaada wa kwanza kwa muda wa masaa zaidi ya 12 sababu kuu ikiwa ni zuio kutoka kwa watu wa maliasili huku akizidi kupoteza damu nyingi zaidi.

Maoni yangu

Hawa watu ni watafutaji kama watafutaji wengine, wameacha familia zao wakienda kutafuta maisha katika kipindi hiki kigumu tunachopitia watanzania wengi,

Hivyo basi, ni vyema maliasili kuongozwa na utu wakati wa kufanya kazi zenu, silaha ya moto itumike pale penye ulazima tena baada ya kuchukua precautions kama sheria inavyotaka.

Wanajukwaa tupaze sauti ili haki intendeke kwa ndugu wa marehemu, uchunguzi katika hili ninmuhimu sana, maana mauaji yamekuwa yakichukuliwa kama kawaida na hawa wanaojiita watu wa maliasili.
Katiba mpya muhimu, itakayomuwajibisha yeyote anayezembea kulinda utu wa MTz!
 
Hao watu wa maliasili wanasahau kuwa, Nchi yetu ina watu masikini sana hivyo kuna mambo yanahitaji busara ya hali ya juu kuyashuhulikia.
KIMSINGI Sio sawa kupiga mtu risasi huku ukijua kabisa kuwa amebeba gunia la mkaa au niseme Maliasili walienda pale kusubiria mtu/watu (boda boda) waliobeba gunia za mkaa kwenye pikipiki zao.
Na hata kama kulitokea changamoto/vurugu wakati wa kuwakamata, nafikiri ingetosha kuwaacha wakimbie na gunia zao za mkaa na wao kujipanga upya.
Suluhisho:
ELIMU ELIMU ELIMU na ULINZI SHIRIKISHI....ndio suluhisho.......
 
Tuendelee kujenga tabia hii ambayo itatufanya na sisi tuwe violence national, police hawaruhusiwi kutumia deadly force, unless maisha ya raia au ya kwake yakiwa hatarini, police state in the making, kulalama humu hakusaidii chochote ni push back ndio lugha hawa kenges watakayo isikia
Hata watumishi wa maliasili (idara ya Misitu) hawaruhusiwi kabisa kutumia bunduki. Kwenye doria zao labda kama walichukua askari polisi.
 
Na hakuna kinachofanyika mkuu, nimesikitika sana sana , ni huzuni sana kuona maisha ya watu yanachukuliwa kama kuku na mbuzi, ni nchi gani hii so sad
kweli umehuzunika sana hadi umeshindwa kutambua jina la nchi😭😭
 
Kuna mmoja alikutwa kwenye pori akahisiwa muwindaji alimenywa nyayo halafu akaambiwa nenda
 
Kwa Nini hao askari wasiwe bize kulinda hyo misitu isivunwe,wakati mwingine mkaaa unaweza Toka kwenye shamba la mtu .wabunge wa sisi emu hawawezi kututetea wananchi wa Hali ya chini,tunalazimiahana kutumia gesi ambayo hatuimidu gharama zake
Umeongea vizuri sana, zamani mabwana miti walikuwepo karibu kila kijiji au kata kwenye Wilaya zenye misitu mikubwa. Baadae watumishi walivyo punguzwa maliasili wakawa hawana tena uwezo wa kutembelea misitu na mapori ili kukagua na kudhibiti uvunaji wa miti, mbao na mkaaa. Ndiyo wakaja na staili ya kuweka check points badala ya kwenda huko msituni. Suluhu kubwa ya uvunaji wa mkaa itapatikana ikiwa matumizi ya gesi mijini, kwenye miji midogo mpaka vijijini yataongezeka. Na ili matumizi ya gesi yaongezeke ni lazima gesi ishushwe bei, kwa serikali kuweka ruzuku ili walau mitungi midogo iuzwe chini ya elfu kumi na mtungi mkubwa walau chini ya elfu 30. Yaani ifikie mahali gesi iwe rahisi kuliko mkaa. Kingine umeme upungue bei ili watu wa uchumi wa kati na wa juu watumie zaidi umeme kwenye kupikia, kuoka vyakula, nk
 
Police hawana ujuzi wa kumkamata mharifu na kumfikisha mahakamani ili apate adhabu kiutaratibu na sheria

Police kujichukulia sheria mkonnoni ni vita ya kimbari

Hao Booster ukizembea wanakuua ,wanatembea Mob na wana silaha za jadi ,huyo aliyeuwa Kessy ni Mbavu Nene alishawahi kumvammia askari akamnyang'anya silaha ,yeye Mbavu ndiyo kiongozi wa MaBOOSTER ,na huyo Tobby ni nyoka wa Kessy......Solution ni kwamba hao maBOOSTER wawe wanakusanya mizigo yao wanakodisha kama Fuso au Scania wanabeba kwa pamoja na kulipia ushuru wa serikali.

Wanapitisha usiku kwa ajili ya kukwepa Kodi.....hao akipiga trip moja hakosi laki na 20 hadi laki unusu faida.
 
Reasoning hawana wakuu
Ni suala la kitaasisi zaidi, siyo kosa la level ya mtumishi. Nikupe mfano kwenye mikoa ya ukanda wa ziwa Tanganyika unakuta wilaya ina misitu yenye ukubwa zaidi ya hekta nusu milioni halafu watumishi wa misitu wako 2 tuu wilaya nzima, niambie wataweza kwenye kwenda kutembelea hiyo misitu kusaka wachoma mkaa na wapasua mbao? Jibu ni hawawezi, sasa wanachofanya ni kuwavizia kwenye njia zao wanapokuwa wanatoka msituni na mzigo ndiyo wanawakamata. Ukikamatwa na magunia ya mkaa kuna aidha wataifishe mkaa au ulipe faini, na pia chombo chaweza kutaifishwa.
 
Back
Top Bottom