Mauaji ya wabeba mkaa maarufu 'booster'

Mauaji ya wabeba mkaa maarufu 'booster'

Mvua zisiponyesha, mabwawa yakose maji Umeme uwe wa mgao mnailaumu serikali. Maji yakipungua huko Mto Ruvu ambao ndio unalisha Dar mnailaumu serikali..

Tukubali kufata tu sheria, mapori tengefu yasiyoruhusiwa kuvunwa miti yaachwe..
Mbona hata kuvuna mkaa kwenye maeneo mengine inaruhusiwa? Tatizo ni baadhi ya watu hawataki kwenda ofisi za maliasili kupata leseni na kulipia ushuru ili serikali ipate mapato yake. Misitu na mapori ni ya Watanzania wote sasa kama wewe Juma na John mnataka kwenda kuvuna mkaa basi kateni leseni, mlipe ushuru na muonyeshwe wapi muende kuvuna mkaa. Mkilipa ushuru ina maana watanzania wengine pia watafaidika na mapato ya Misitu yao. Msipolipa ushuru ina maana mnafaidika nyie tuu peke yenu wakati misitu ni ya wananchi wote.
 
Mbona hata kuvuna mkaa kwenye maeneo mengine inaruhusiwa? Tatizo ni baadhi ya watu hawataki kwenda ofisi za maliasili kupata leseni na kulipia ushuru ili serikali ipate mapato yake. Misitu na mapori ni ya Watanzania wote sasa kama wewe Juma na John mnataka kwenda kuvuna mkaa basi kateni leseni, mlipe ushuru na muonyeshwe wapi muende kuvuna mkaa. Mkilipa ushuru ina maana watanzania wengine pia watafaidika na mapato ya Misitu yao. Msipolipa ushuru ina maana mnafaidika nyie tuu peke yenu wakati misitu ni ya wananchi wote.
Sawa mkuu ila utaratibu huu unafanya kazi?au tunaandika humu kutokea kwenye comfort zones zetu?,sheria zingekua zinafutwa nchini usingeshughudia hizi petrol stations zikimea kama uyoga, why sheria ziwe kwa lower class tu?,why police wa mali asili atumie deadly weapon kwa raia?
 
Una shida ya akuli? Kuna watu wezi na wanaiba n a kuuza maliasuli na bado wako ofisini. Je kwanini wasiwakamate
Mtu aliyeko ofisini na akawa anaiba huyo ni mwizi tuu kama wezi wengine, hana tofauti na traffic anayepokea rushwa barabarani, hakimu anayepokea rushwa mahakamani, daktari au nesi wanaopokea rushwa hospitalini, mwendesha pikipiki iliyobeba mkaa ambao haujalipiwa ushuru, muuzaji wa sukari anayeuza kilo sh 5000 na wengine wengi, mifano ni mingi sana. Kama tunataka wavunaji wa mkaa wasilipie ushuru serikalini basi tukae kimya na kwenye maeneo mengine pia. Ila mimi siungi mkono kabisa mhalifu kuuwawa kwa sababu kwenye sheria ya Misitu Na. 14 ya Mwaka 2002 pamoja na kanuni zake, hakuna hata kifungu kimoja kinachowapa nguvu maafisa misitu kuuwa mtu aliyekutwa na kosa.
 
Ndugu yangu unadanganya mchana kweupe? Wewe ni mmoja wa hao askari wauaji? Tanzania mara ngapi tumeona cold blooded killings za polisi kwa wahalifu wasio tishio au hata kwa raia wema? Ni mara ngapi tumeona askari wanaua raia wema ili wachukuwe mali au fedha walizonazo? Kama hili tukio limeripotiwa tofauti, hebu wewe tuambie ilikuwaje?
kwahiyo kwa mujibu wa maelezo yako,askari waliua wauza mkaa ili wachukue mkaa!!!!
 
Ndiyo. Ni sawa na nyumbu kadhaa wanachaguliwa miongoni mwa nyumbu kuwa simamieni wenzenu wawe wananiletea watt wenu namkula damu na nyama. Ila chui yeye amekaa akatulia. Cheki tusivyo na uelewa hata kidogo yaani nyumbu wangekuwa na akili kidogo tu Simba asingedhubutu kuwala na kuwamaliza kabisa
Anae uza mkaa na anaeuza wanyama sijui yupi mwizi hapa.. wa kupigwa risasi
 
Mheshimiwa waziri anayehusika tunaomba ushughulike na hili...

Askari Maliasili wana wajibu wa kulinda maliasili zetu kwa kutumia sheria na sio risasi...
 
Askari kuua wamekosea sana wanastahili kushtakiwa

Ila pia kumbukeni misitu inaisha jamani Tanzania

Tabianchi Tanzania kwa kiwango kikubwa na shughuli za mkaa

Serkali ingepunguza gharama za gesi ili hata sisi wa chini tuweze kumudu
Kila mwaka eneo la misitu inayopotea kwa kufyekwa na kuharibiwa ni hekta 400,000 na ushee. Tanzania ina misitu na mapori (Forests and Woodlands) yenye ukubwa wa hekta milioni 48.1 hii maana yake ni kwamba tukiendelea na hii kasi ya ufyekaji misitu niliyosema kizazi chetu kitakachokuja baada ya miaka 120 ijayo kitakuta jangwa tupu. Kugeuza nchi kuwa jangwa maana yake ni kwamba kutakuwa hakuna kilimo tena maana mvua hakuna, vyanzo vya maji hakuna tena, wanyama kwenye mbuga za wanyama hakuna tena, mabadiliko ya tabia nchi, ambayo kwa sasa yanabipu tuu ndiyo kipindi itakuwa yamejenga kibanda. Kiufupi tutakuwa tumeuwa maisha ya vizazi vyetu sisi sote hapa kwa sababu kila mtu hapa ana uzao wake ataacha. Imagine mababu zetu na wakoloni kama wangekuwa wabinafsi na kuanza kuharibu misitu yetu kama sisi je tungekuta hali gani? Tujitafakari wajameni.
 
Askari wa maliasili na wale wa wanyama pori ni wanyama kuliko wanyama halisi. Bora ukutane na simba na mamba kuliko kukutana na askari hao porini na mbugani. Ni washenzi, wanadhani kila mtu ni jangili, wanamfanyia unyama hata akijieleza yeye si jangili au mharibu misitu
 
Back
Top Bottom