Matumizi ya Magufuli, tuyajadili

Matumizi ya Magufuli, tuyajadili

mimi naona angeachana na madaraja yasiyo na tija hasa lile la coco ambalo naona kama anasa na urembo. Sioni element za kumsaidia masikini kwenye huu mradi.

Kwanza nchi lazima ikue holistically sio dsm tu. Priority ingekuwa ni kuunganisha mikoa yote na wilaya zote kwa rami.Hapo kutahamasisha maendeleo ya kweli.
Ahame na serikali yake yote pamoja na Ikulu wahamie dodoma.

Badala ya barabara SITA za Dar Challinze, Ingetengenezwa reli na treni express DSM moro, ninauhakika asilimia zaidi ya 40 ya wakazi wa dsm wangehamia Moro.
sina uhakika ila naona hizo barabara sita zitasababisha bottleneck effect.
Hiyo dar chalinze ni muhimu sana, na si kwa ajili ya abiria pekee, ukisema aweke rell si mbaya, ikiwepo pia, hata station had I bagamoyo kupitia Tegeta, ikiwepo rell nitakuwa poa sana, na hii pia iwe njia sita.
 
sawa hata angeamua kufanya hayo pia ungekuja hapa na wazo tofauti na hayo ,sijui unatakaje mkuu ili nafsi yako iridhike,ifike hatua wandugu tuone kuwa kuna haja ya kuacha kwanza yafanyike alafu ndiyo tuje na mapendekezo,kuliko hii ya kujifanya kila mtu anamaono
Yule wa UKAWA alisema kuwa akipewa nchi ataiweka rehani gesi ili apate fedha ya kusomesha watu kuanzia shule ya msingi mpaka chuo kikuu!. Alipozidi kubanwa na maswali ya msingi, akasema eti anaonewa. JPM haonewi bali anafanya kazi.Kukosoa ni kitu rahisi lakini kufanya kazi wakati unapopewa nafasi ni kitu kigumu sana.
 
Hivi mnaolaumu humu JF mnafanyakazi taasisi gani nchi hii tuone ufanisi wenu?
 
Kwa sasa tumuunge mkono huyu Mheshimiwa, mambo mengi yalitakiwa yawe yamefanyika miaka mingi lakini wenzie walizingatia Zaidi kujinufaisha binafsi.

Kuna hii wodi ya Muhimbili aliyosema imelala tokea Enzi za Mzee Mwinyi, badala ya kuanza kujenga jengo jipya inabidi ahangaike na hivyo viporo.

Ni kumwombea Mungu tu ili aiweke Tanzania kwenye ramani.
 
Kiongozi, The Boss nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Ni lazima serikali iwe na vipaumbele vyake kwa muda wa miaka mitano ijayo ili kujipambanua kuwa serikali ya awamu ya tano imefanya mambo fulani ya maana. Ni muhimu sana. Lakini hivyo vipaumbele ulivyoainisha hapo sio vya awamu ya tano; Kigamboni, Mwanza, Coco Beach, rapid transport na Ubungo....haya yamekuwa aired tangu phase ya kwanza ya JK..so huo ni muendelezo wa plans zilizokuwepo.
Umegusia swala la express electric trains, ni wazo zuri sana. Lakini kabla hujasemea swala la express trains, say from Dar-Moro, which i do support, hujaangalia maandalizi ya umeme ambao hata hatuna. Huwezi kuwa na electric trams, trains na hata hizo subways trains kama huna umeme unaoeleweka. Maandalizi ya electric trams & trains yanahitaji thorough investment in reliable sources of electricity, sio huu umeme unaokatika kila baada ya masaa mawili. I, for once support the BRT projects, japo naamini ubadhirifu mkubwa sana ulifanyika. Let's wait and see huu mradi uanze kazi, kama utaleta mapungufu tutaona. Niliona same project ilifanywa na nchi ya Peru, na iliwasaidia sana kupunguza foleni za barabara kuu za majiji.
 
Binafsi nisaidieni maswali daraja la Coco beach ni la nn?na kwa faida ya nani?mm nilifikiri bora tungejenga la salender lingetusaidia sana.
 
sawa hata angeamua kufanya hayo pia ungekuja hapa na wazo tofauti na hayo ,sijui unatakaje mkuu ili nafsi yako iridhike,ifike hatua wandugu tuone kuwa kuna haja ya kuacha kwanza yafanyike alafu ndiyo tuje na mapendekezo,kuliko hii ya kujifanya kila mtu anamaono
Watu hawawezi kuacha kwasababu CCM mmeongoza hii Nchi zaidi ya miaka 50nakila mlipoambiwa mkaja na hizo soga kwamba mpewe muda sisi tunasema HAKUNA kupewa muda
 
Ndugu MSEZA MKULU hilo la RELI linaogopeka sana hata sijui kwanini kuna nyakati tulisikia kwamba walikuwa wanataka kujenga Bandari Kavu huko MZENGA kama sikosei na wangejenga RELI yakutoka Bandarini hadi hapo then ingechongwa Barabara kutoka huko hadi Mlandizi kuunganisha NJIA kubwa sasa sijui ikoje Ngoja nimuite ndugu yetu Mag3 huenda akawa nalakutusaidia hasa baada yakujipa Likizo ya siku 100 akimfatilia Magufuli kz zake
 
Kumuelewa Magufuli Na Utawala Wake Kwa UJUMLA Unahitaji Kutulia Na Wala Usiwe Na Papara! Soon Mtamuelewa TU
Inawezekana ikawa kweli unachosema Wewe ndg yetu uliemuelewa hebu saidia na wengine ambao bado hawajaelewa maana hapa nikama Shule
 
awa ndo wabongo bwana....ujuaji mwingi mno
Ujuaji huo wa waBONGO ndio umepelekea Magufuli kutangazwa Mgombea wa CCM na NEC vinginevyo MEMBE na blah blah zake ndio angetangazwa
 
Jamani Rais ana wa shauri wengi sana wenye utaalam kwenye issue iliyopo mezani kwa wakati huo tusijifanye wajuaji sana hapa. Hivi unapoweka train morogoro road alafu sehemu zingine za mji hamna ndio utakuwa umesolve tatizo gani, kwa mji kama dar es salaam tatizo ni msongamano wa magari sio msongamano wa abiria na hicho ndio tunachokishudia sasa hivi mchana daladala nyingi zimepaki au zinatembea hazina watu kabisa lakini foleni Tazara, ubungo chang'ombe ,Magomeni na Morocco ni kubwa sana,nafikiri mngeanza kusoma problem statement na implication of doing nothing kwenye proposal ya hii project ndio mje hapa msifanye watu hawana akili. Nyinyi mnafikiri gharama ni kujenga au kununua train tu, Je gharama za uendeshaji na matengenezo kama wangeamua kujenga mifumo ya reli mnazijua, ACHENI BWANA HIZO ON AIR CALCULATION ZENU ZA AJABU AJABU

Mkuu usifikiri watu na hayo magari wanayojazana barabarani ni sababu ya kero za usafiri wa daladala kwa ujumla ila ikaletwa tren za kasi kama Ethiopia unafikiri nani atahangaika na kupata tabu na gari yake barabarani watu wanafanya mambo kutokana na hali ilivyo, alafu usidhani watu wote wana akili kama zako kuwa wana hesabu za hewani humu ndani kuna watu wenye Elimu zao katika ukadiliaji wa miradi ndio maana ukaona huu uzi umekuja na details kamili ila sababu ya uvivu wako wa kusoma unadhani wamekosea.
 
Mkuu usifikiri watu na hayo magari wanayojazana barabarani ni sababu ya kero za usafiri wa daladala kwa ujumla ila ikaletwa tren za kasi kama Ethiopia unafikiri nani atahangaika na kupata tabu na gari yake barabarani watu wanafanya mambo kutokana na hali ilivyo, alafu usidhani watu wote wana akili kama zako kuwa wana hesabu za hewani humu ndani kuna watu wenye Elimu zao katika ukadiliaji wa miradi ndio maana ukaona huu uzi umekuja na details kamili ila sababu ya uvivu wako wa kusoma unadhani wamekosea.

Sasa hivi kinachoitajika Dar es salaam ni miundo mbinu ya barabarani mizuri kutoka maeneo tofauti ya jiji mimi ninge suggest serikali iache kujenga hivi vi single lane road kwenye populate areas lakini sio train nakuita Rishangles kupanda cha barabara cha dar cha cha line kama kilivyo kuwa planed kwa sababu hicho kupanda kina tumika na magari kutoka mikoani karibu 20 ya TZ. Tuambiane ukweli hapa haya mambo ya nahitaji decision matrix kuamua sio kujumulisha na kutoa tu, swali la kwanza na la pili mtihani wa darasa la saba
 
Kwanini wajenge treni za umeme dar badala ya kuboresha huduma za afya kwa kununua vifaa tiba vya kutosha katika hospitali zote nchini!
 
Huyu mzee anaangalia upande mmoja wa shilling na hii itasumbua tu
 
Back
Top Bottom