pakaywatek
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 4,710
- 6,372
Huyu hashauriki kumbuka juzi washauri wake walimwambia usiende akagomaNi nani washauri wake?
Huyu hashauriki kumbuka juzi washauri wake walimwambia usiende akagomaNi nani washauri wake?
Vile ndio alivyo MAGUFULI mzee ulikuwa masomo ni ulaya nini ndio umerudiMimi kiongozi akiwa anaongea anafoka huwa namtoa thamani sana
najiuliza hajawahi kumuona Clinton au Obama akiongea?
hafuatilii rekodi zao?
au anafikiri hata USA hakuna ufisadi?
Ktk vitu vilivyonifanya nimshushe point Magufuli ni tabia yake yakulalama hovyo!!!
Ameshika nafasi sasa aonyeshe anaweza kuliko kuendelea kupiga kelele tumefikishwa hapa na watubwachache ambao hatutajii na hachukui hatua dhidi yao...
Visionary leader halalamiki!! Huchukua matatizo kama changamoto na kuzifanyia kazi...
Ktk vitu ambavyo Magufuli hana na vitamgharimu ni kukosa intelligence...
Viongozi wanahitaji kuwa na maarifa sana ili kuwaongoza watu wao waende wapi...
Lkn huyu bwana ameonesha zaidi uwezo Wa kusimamia kuliko kuongoza!!!
Huu mfumo Wa one man army ni mbaya na hauna tija ktk dunia hii ya Leo...
Anasema Darisaramu ndiyo kira kitu, sasa kwa sababu wao (wakuu) wanakaa darisaramu ndiyo maana wameona waujenge mji wao.
The Boss hayo mapato yanayopatikana ni kwa ajili ya kuijenga darisaramu yao wanayoishi.
Jamaa still ana upeo mdogo sana, nilimshangaa alivyokuwa anasifia kujenga daraja la coco beach to aghakhan[emoji15] [emoji15] [emoji15].
Barabara sita Chalinze-Dar, yaani barabara kuu inayoisambaa from Dar to mikoa mingi TZ na nje ya nchi unajisifu leo kwa three lane. Magu acha utani bana.
Raila ni best yako, nenda hapo Kenya tu ukaangalie ile Thika highway kisha kurudi hapa kichwa kitafunguka coz nikikwambia uende SA utasema huko ni kwa wazungu.
Kwa maelezo ya jana ina maana waziri wa miundu mbinu ni yeye
aliepo hana mamlaka ya kupanga chochote
Mbona mie hujaniita? Kama upo town ile lunch iwe kesho....
Naunga mkono hoja!Daraja la kigamboni bilioni 200
daraja la furahisha mwanza bilioni 200 (nakaribisha masahisho)
daraja la coco beach-bilioni 200 zimetengwa
barabara ya dar-chalinze-zaidi ya trilioni 1.3(dollar milioni 500)
mabasi yaendayo kasi -zaidi ya bilioni 200
flyover ya ubungo bilioni 100
Iwapo serikali ingeamua kujenga treni za umeme
badala ya mabasi yaendayo kasi ingetumia dollar milion 430
kwa km 32...yaani karibu Dar yote ingekuwa unapanda treni dakika 10
uko popote pale hata kigamboni treni ingefika kupitia Mbagala..
hii ni link ya Ethiopia inaelezea gharama za treni hizo na tayari wenzetu wanatumia..
Ethiopia gets first sub-Saharan Africa metro - CNN.com
na kama hizo bilioni zingetumika kujenga vyuo vikuu
UDOM gharama zake ilikuwa kiasi cha bilioni 25....
Hatujawahi kuwa na vipaumbele Tanzania.
Atleast hata Nyerere alianzisha viwanda wakati ule wakati mambo yalikuwa tight.
Mamacita.........hmmm.....
Vipaumbele tumekuwa navyo vya kutosha ktk kipindi cha miaka 15 iliyopita.Hatujawahi kuwa na vipaumbele Tanzania.
Atleast hata Nyerere alianzisha viwanda wakati ule wakati mambo yalikuwa tight.
Napata shida sana kila nikimtafakari Magu,
Hakika haelewi nini anakitaka na nini hataki
Gazeti lilitoa taarifa ambayo wao tayari walikua nayo mezani. Sio kwamba walifanyia kazi taarifa za Gazeti.Kama hadi gazeti tu linawafanya waingie kazini
ni kama vile hawana 'master plan'
so wanaenda na matukio.....
Hawakuwa na masterplan na masuala ya mafuta kabisa nahisi
Sasa mkuu unataka wachangie nini mambo yenyewe ni kama unavyoyaona? Mtu gani akiamka tu anatamka yeye bila kufuata utaratibu? Serikali duniani zingekuwa zinaendeshwa namna hii haki ya nani kusingekalika! Ajirekebishe bwana.Hawa wanaochangia hii thread ni watanzania au wanyarwanda? Too negative
Nilitegemea Jana tuelezwe wamejipanga vipi... Watafanya nini....lini...wapi na kwa njia zipi!!!
Nilitegemea magu aseme vision yangu ni hiii...
Asijidanganye kwa kufoka na kushtukiza akifikiri urais ni uwaziri! Atachoka mwenyewe maana kila kitu kinamhusu!!!
Bado najiuliza hiyo kasi isemwayo ni katika nn?
Bahati mbaya nchini kwetu hatunaga mijadala ya wazi hasa kwa viongozi wetu...
Ingekuwepo tungewaita akina JK watueleze ni vipi ARI MYA.... NGUVU MPYA & KASI MPYA vilikwama...
Coz utafoka na kufukuza watu kazi mpaka lini?