Matumizi ya Magufuli, tuyajadili

Matumizi ya Magufuli, tuyajadili

sawa hata angeamua kufanya hayo pia ungekuja hapa na wazo tofauti na hayo ,sijui unatakaje mkuu ili nafsi yako iridhike,ifike hatua wandugu tuone kuwa kuna haja ya kuacha kwanza yafanyike alafu ndiyo tuje na mapendekezo,kuliko hii ya kujifanya kila mtu anamaono
Acha kufunga watu midomo, tuko watanzania more than 45 mill , wote hawa wana akili na mawazo chanya, ndiyo maana mashule,vyuo vinaimarishwa ili wasome na kuelimika na hatimaye wawe na mchango kwenye ujenzi wa nchi yao.
Kujenga nchi si kazi ndogo ya kufanywa tuu na rais na baraza lake, ndiyo maana juzi umemsikia JPM akilisifia gazeti la Jamhuri kwa sababu lingekuwa limefungwa mdomo kama wewe unavyohamasisha hapa, basi waziri mkuu asingepata pa kuanzia. Kumbuka rais ni binadamu kama wewe hivyo hawezi kufanya na kujua kila kitu halafu wengine woooote tuwe tumekaa na kusifia tuu.
 
Allmost ku'run taifa lenye Wapumbaf wengi ni rahisi mno icpokua soon we kiongoz pia utajulikana tu kua lipi ulisemalo lina Maslahi kijamii kiMtazamo muelekeo wake uko wap,na hapo ndpo inafkia mahala uta amini"Magufuli ni wakukurupuka"
 
Maguuli ni mtu wa papara hana popote anapo refer si mpango wa taifa wala wa maendeleo yeye anaropoka ropoka akiona watu mzuka unampanda basi anasema chochote anasahau wananchi wanasikia na rekodi wanaweka
 
The Boss , kwanza si sahihi kusema kwa kuwa rail project ya Ethiopia imechukua 500ml $ basi na ya Dar itachukua hivyo hivyo, pili hiyo reli si jawabu au mbadala wa ya barabara Dar - Chalinze, hii barabara ni lazima ijengwe kupunguza msongamano na ajali.

Vile vile hiyo reli si jawabu ya daraja la Kigamboni, inaonekana unawachukulia wakazi wa Kigamboni kama mateso ya Pantoni ni haki yao vile kwa kuwa hii si mara ya kwanza wewe kuelezea daraja la Kigamboni halina umuhimu.

Cha mwisho na cha muhimu, wewe huna jema kwa Magu hilo lipo wazi kwa hiyo hizi ni baadhi tu ya chuki zako binafsi, wewe ni wa kupuuzwa, kwa sababu hata angeanza kwa kujenga hiyo Metro Dar ungekuja kulalamika huyu Magu kwa nini kaanzia Dar na si Arusha au kwingine, nyie ni wakupuuzwa na hadi ikifika 2020 baadhi ya vijana wenu watakuwa #LGBT activists
 
- Daraja la kigamboni bilioni 200
- Daraja la furahisha mwanza bilioni 200 (nakaribisha masahisho)
- Daraja la Coco Beach-bilioni 200 zimetengwa
- Barabara ya Dar-Chalinze-zaidi ya trilioni 1.3(dollar milioni 500)
- Mabasi yaendayo kasi -zaidi ya bilioni 200
- Flyover ya Ubungo bilioni 100

Iwapo serikali ingeamua kujenga treni za umeme badala ya mabasi yaendayo kasi ingetumia dollar milion 430 kwa km 32...yaani karibu Dar yote ingekuwa unapanda treni dakika 10 uko popote pale hata Kigamboni treni ingefika kupitia Mbagala.

Hii ni link ya Ethiopia inaelezea gharama za treni hizo na tayari wenzetu wanatumia..

Ethiopia gets first sub-Saharan Africa metro - CNN.com


Na kama hizo bilioni zingetumika kujenga vyuo vikuu UDOM gharama zake ilikuwa kiasi cha bilioni 25.
mikurupuko
 
Kujadili trend kwa three data point ni kupoteza muda. mpeni muda angalau tuwe na miezi 6 hadi 12 ndio tujadili trend.
Binafsi naichukia hii Lugha ya tuwape Muda CCM iko madarakani tangu UHURU muda wa vipi sasa wanaotaka tuwape
 
Umeongelea gharama za tramways za ethiopia huo umeme wa kuziendesha unao? hivi unajua kiasi gani cha umeme kinatumika kuendesha hizo tramways? umeenda na kuandika hadi kiasi cha Km zinawozewa kujengwa kwa fedha chini ya dollar 500 hiyo tramway ikijengwa dar unadhani mji dar imepangika kuaccomodate hiyo mproject au kutakuwa na migarama kibao ya kufidia watu kupisha ujenzi? Hata ethiopia hawakukimbilia tu kwenye ujenzi wa tramway mabarabara yao yako safi mi nimekaa ADDIS ABABA kwa miaka sasa: lakini pia fanya tafiti kuhusu kiasi cha umeme ambacho Ethiopia inategemea kuzalisha siku wa hivi karibuni kwa kifupi huzi wako ni wa kiukawa zaidi hauko kitaalam hata kidogo
Mkuu umemlaumu jamaa kuleta uzi wa kiUKAWA naww umepita mlemle kujadili Hoja kiCCM umeishia kulaumu ilitakiwa uweke uhalisia kama hao waETHIOPIA wamefanyaje wanatumia umeme kiasi gani nk...maana umesema umeishi huko so kuna mengi unayajua hebu Share nasisi uzoefu wako
 
Pengine husomi magazeti. Sehemu kubwa ya pesa hizo ni misaada toka Japan ambayo iko tied na specific projects. TZ inatakiwa kuchangia 10-20% za gharama hizo na hivyo haiwezekani ku-divert pesa hizo kwa kitu kingine.
Hao Dona's unajua watarudishaje pesa zao?
 
- Daraja la kigamboni bilioni 200
- Daraja la furahisha mwanza bilioni 200 (nakaribisha masahisho)
- Daraja la Coco Beach-bilioni 200 zimetengwa
- Barabara ya Dar-Chalinze-zaidi ya trilioni 1.3(dollar milioni 500)
- Mabasi yaendayo kasi -zaidi ya bilioni 200
- Flyover ya Ubungo bilioni 100

Iwapo serikali ingeamua kujenga treni za umeme badala ya mabasi yaendayo kasi ingetumia dollar milion 430 kwa km 32...yaani karibu Dar yote ingekuwa unapanda treni dakika 10 uko popote pale hata Kigamboni treni ingefika kupitia Mbagala.

Hii ni link ya Ethiopia inaelezea gharama za treni hizo na tayari wenzetu wanatumia..

Ethiopia gets first sub-Saharan Africa metro - CNN.com


Na kama hizo bilioni zingetumika kujenga vyuo vikuu UDOM gharama zake ilikuwa kiasi cha bilioni 25.

pesa hizo zingetengwa kwa ajili ya hayo uliyoyataja bado watanzania tungelalamika ,hivyo kwa upande wangu naona mpango huo uendelee bila kikwazo chochote kile
 
- Daraja la Coco Beach-bilioni 200 zimetengwa
Daraja la Busisi kiuchumi ni feasible mara 100 kulinganisha na hili la coco. Yaani ni sawa na kumshawishi mtu kumnunulia perfume ya Calvin-Klein kichupa kidogo kwa sh. 400,000/- wakati mtu huyo huyo hana hata uhakika wa mlo mmoja, uhakika wa pa kulala na nguo zake zina matobo huku akinukia perfume ya malaki!
 
Lowasa was better than Magu
Sababu Magu ndio yupo basi wacha tuendelee tu ila dawa ya Tanzania ilikuwa kuleta mfumo mpyaa
 
sawa hata angeamua kufanya hayo pia ungekuja hapa na wazo tofauti na hayo ,sijui unatakaje mkuu ili nafsi yako iridhike,ifike hatua wandugu tuone kuwa kuna haja ya kuacha kwanza yafanyike alafu ndiyo tuje na mapendekezo,kuliko hii ya kujifanya kila mtu anamaono
Na kwa kuongezea hapo ni kwamba kuongoza nchi si kama mijadala ya humu JF, humu kuna watu hata kuongoza familia zao wameshindwa lakini utakuta kimbele mbele kukosoa, na kama wana mipango mizuri kwanini wasimsaidie magu, kwa tz ilipofikia eti walitaka babu apewe nchi hata bira aibu-sasa ndo wangemponda sana wakati wao ndo wamempa ulaji, wtz ni watu wa ajabu sana, ndo maana hata Raisi alisema tumerogwa na nini?
 
Alipoanza Makusanyo yalikuwa Trilioni 1.3, Mwenzi uliyofuatia yalifika Trilioni 1.5 na yakafika Trilioni 1.0.. Swali la msingi mfuatano huu (trend) una maanisha nini?
Huu mfuatano utashuka mpaka 0.85Trillion then utaanza kupanda taratibu ila kwa uhakika. Asitegemee mapato kuongezeka ilihali huku akipunguza sana matumizi ya kawaida ya Serikali ambayo ndo chachu kuu ya mzunguko wa pesa katika uchumi.
 
Ni nani washauri wake?
Washauri hawana tatizo ila nadhani tatizo liko kwa mshauriwa. Si umesekia mwenyewe anasema kusoma hotuba ya kuandikiwa atakuwa anasoma hotuba isiyo yake hivyo akaiweka kando. Sasa akiboronga mshauri ana kosa gani hapo?
 
Back
Top Bottom