Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Naomba nisipingane na asili ambayo inalandana hata mitazamo ya kiimani kwamba ALIYE NACHO HUONGEZEWA! Kuna uwezekano mkubwa mabepari walijifunzia huku.
Matukio haya mawili ni ya ma rais wetu wastaafu ambao kupitia kwao weekend iliyopita walisababisha mijadala mipana mitandaoni
1. TUKIO LA KWANZA
Aliyekuwa rais wa pili wa Tanzania baada ya uhuru wa Tanganyika mzee Ali Hassan Mwinyi alizindua kitabu cha maisha yake..! Hili si tukio la dharura ni tukio lililoandaliwa kwa muda mrefu na kwa kuzingatia protokali mgeni rasmi si mwingine bali ni rais aliyeko madarakani.
Mipango ya Mungu si ya mwanadamu hivyo inawezekana kabisa aliyekuwa kaandaliwa kuwa mgeni rasmi kwenye tukio hili kubwa ni aliyekuwa rais wa awamu ya tano hayati Pombe John Magufuli na inawezekana kabisa na zawadi ya mgeni rasmi kwenda kwa mhusika ilikuwa imeshaandaliwa!
Kudra za Mwenyezi Mungu zikamuangukia aliyekuwa makamu wa rais kuwa rais kamili wa Tanzania baada ya kifo cha maradhi cha mtangulizi wake. Na huyu ndio kawa mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa kitabu cha mzee Mwinyi.
Kilicholeta mjadala ni ukarimu wa zawadi aliyotunukiwa na rais Samia Hassan Suluhu..zawadi ya gari la kifahari la bei ghali aina ya Mercedes Benz linalofikia kiasi cha Tsh milion 250 kabla ya usafiri na usajili na kodi.
Lawama zimeenda kwa mama kwa matumizi mabaya ya pesa za wananchi. Lakini pengine si kosa lake inawezekana kabisa ni kitu kilichokuwa kimeshapangwa kitambo.
Wengine wamesema sababu iliyotolewa haikidhi ama angetafutiwa walau gari la bei ndogo zaidi... Ama la angepewa zawadi nyingine... Waswahel wanasema usimuingilie aliyepewa kapewa! Mzee mwinyi hana shida ya chochote ana kila kitu cha kimaisha katika level ya kibinadamu. Zawadi aliyopewa ni bakshish tu. Aliye nacho huongezewa! Tafakuri yangu kwenye hili tukio ni kile kitendo cha mzee Mwinyi kugoma kupokea zawadi ile! (Tetesi) Pengine kaona ni kufuru sasa tena ukizingatia huu ni mwezi wa toba kwa imani yake!
2. TUKIO LA PILI
Mzee Jakaya Kikwete rais mstaafu wa awamu ya nne kukabidhiwa nyumba aliyojengewa na serikali. Hii ni kwa marais wote wastaafu wamefanyiwa hivyo! Kwa picha tu za nje si nyumba ya kitoto bali ni jumba kubwa la kifahari.
Hili nalo si tukio la dharura ni tukio lililokuwa limepangwa kitambo na kwa muktadha uleule mgeni rasmi angekuwa JPM kama angekuwa hai!
Tafakuri yangu kwenye hili! Hivi ni kweli kabisa JK anashida na nyumba? Tena lijumba kubwa kama lile? Lakini tukirejea kwenye ile kanuni ya asili ya aliyenacho huongezewa basi kauli inakata na mjadala unaisha.
JK pia ana kitabu cha maisha yake. Sina kumbukumbu kama alishakizindua na katika hafla ile alipewa zawadi gani na mgeni rasmi!
Mzee Mwinyi kwa tetesi ni kwamba kaikataa zawadi nzuri ya gari la kifahari .. Sina hakika kama atakapokabidhiwa jumba lake la kifahari nalo atalikataa. Nasema sina hakika.
Viongozi wakuu wa nchi ni viongozi ambao hulelewa na serikali zao mpaka kifo. Na kwa viongozi wetu wa Afrika huingia madarakani wakiwa watupu na kutoka wakiwa na ukwasi wa kutisha wao na ndugu zao na familia zao. Lakini bado katika kulelewa huko na ukwasi huo bado huongezewa bakshish ya hiki na kile
Yaani ni kama vile wananyang'anya kile kidogo ambacho kingewasaidia wanyonge fukara na maskini wa Taifa hili. Na hawajali ama macho yao yamejaa upofu kuyaona haya. Ni kilevi cha madaraka na kupata hupofusha mpaka weledi wetu.
Matukio haya mawili ni ya ma rais wetu wastaafu ambao kupitia kwao weekend iliyopita walisababisha mijadala mipana mitandaoni
1. TUKIO LA KWANZA
Aliyekuwa rais wa pili wa Tanzania baada ya uhuru wa Tanganyika mzee Ali Hassan Mwinyi alizindua kitabu cha maisha yake..! Hili si tukio la dharura ni tukio lililoandaliwa kwa muda mrefu na kwa kuzingatia protokali mgeni rasmi si mwingine bali ni rais aliyeko madarakani.
Mipango ya Mungu si ya mwanadamu hivyo inawezekana kabisa aliyekuwa kaandaliwa kuwa mgeni rasmi kwenye tukio hili kubwa ni aliyekuwa rais wa awamu ya tano hayati Pombe John Magufuli na inawezekana kabisa na zawadi ya mgeni rasmi kwenda kwa mhusika ilikuwa imeshaandaliwa!
Kudra za Mwenyezi Mungu zikamuangukia aliyekuwa makamu wa rais kuwa rais kamili wa Tanzania baada ya kifo cha maradhi cha mtangulizi wake. Na huyu ndio kawa mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa kitabu cha mzee Mwinyi.
Kilicholeta mjadala ni ukarimu wa zawadi aliyotunukiwa na rais Samia Hassan Suluhu..zawadi ya gari la kifahari la bei ghali aina ya Mercedes Benz linalofikia kiasi cha Tsh milion 250 kabla ya usafiri na usajili na kodi.
Lawama zimeenda kwa mama kwa matumizi mabaya ya pesa za wananchi. Lakini pengine si kosa lake inawezekana kabisa ni kitu kilichokuwa kimeshapangwa kitambo.
Wengine wamesema sababu iliyotolewa haikidhi ama angetafutiwa walau gari la bei ndogo zaidi... Ama la angepewa zawadi nyingine... Waswahel wanasema usimuingilie aliyepewa kapewa! Mzee mwinyi hana shida ya chochote ana kila kitu cha kimaisha katika level ya kibinadamu. Zawadi aliyopewa ni bakshish tu. Aliye nacho huongezewa! Tafakuri yangu kwenye hili tukio ni kile kitendo cha mzee Mwinyi kugoma kupokea zawadi ile! (Tetesi) Pengine kaona ni kufuru sasa tena ukizingatia huu ni mwezi wa toba kwa imani yake!
2. TUKIO LA PILI
Mzee Jakaya Kikwete rais mstaafu wa awamu ya nne kukabidhiwa nyumba aliyojengewa na serikali. Hii ni kwa marais wote wastaafu wamefanyiwa hivyo! Kwa picha tu za nje si nyumba ya kitoto bali ni jumba kubwa la kifahari.
Hili nalo si tukio la dharura ni tukio lililokuwa limepangwa kitambo na kwa muktadha uleule mgeni rasmi angekuwa JPM kama angekuwa hai!
Tafakuri yangu kwenye hili! Hivi ni kweli kabisa JK anashida na nyumba? Tena lijumba kubwa kama lile? Lakini tukirejea kwenye ile kanuni ya asili ya aliyenacho huongezewa basi kauli inakata na mjadala unaisha.
JK pia ana kitabu cha maisha yake. Sina kumbukumbu kama alishakizindua na katika hafla ile alipewa zawadi gani na mgeni rasmi!
Mzee Mwinyi kwa tetesi ni kwamba kaikataa zawadi nzuri ya gari la kifahari .. Sina hakika kama atakapokabidhiwa jumba lake la kifahari nalo atalikataa. Nasema sina hakika.
Viongozi wakuu wa nchi ni viongozi ambao hulelewa na serikali zao mpaka kifo. Na kwa viongozi wetu wa Afrika huingia madarakani wakiwa watupu na kutoka wakiwa na ukwasi wa kutisha wao na ndugu zao na familia zao. Lakini bado katika kulelewa huko na ukwasi huo bado huongezewa bakshish ya hiki na kile
Yaani ni kama vile wananyang'anya kile kidogo ambacho kingewasaidia wanyonge fukara na maskini wa Taifa hili. Na hawajali ama macho yao yamejaa upofu kuyaona haya. Ni kilevi cha madaraka na kupata hupofusha mpaka weledi wetu.