Laroi Butata
Member
- Oct 28, 2020
- 91
- 103
Uchaguzi wa rais chama cha wanasheria Tanzania (TLS) unaofanyika jijini Arusha umeshika kasi kukiwa na wagombea watano ila nimeona watu kadhaa wakiwa wamevaa t-shirt nyeupe zikiwa na picha za wagombea tofauti mmojawapo akiwa ni Dr. Hosea na Shehzad Wall.
Sijajua kwa nini wagombea hawa wawili kati wa wote watano wamekuwa na kampeni ya namna hii, nilipokuwa napita maeneo ya Sanawari hapa jijini arusha kuelekea mjini nilipishana na watu waliovaa nguo hizo.
Nilijaribu kuuliza kujua kulikoni ndiposa nikaambiwa hao wawili mmoja ndiye mwenye nafasi na hasa Dk Edward Hose aliyewahi kuwa boss pale Takukuru.
Naambiwa kesho ndiyo kinyang'anyiro cha kupiga kura na kinafanyika hapa arusha kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa AICC.
Nimeuliza na kupata majina ya wagombea wote kama ifuatavyo, Dk Edward Hosea, Albert Msando, Flaviana Charles, Shehzad Wall na Rais wa zamani wa chama hicho, Francis Stolla hawa ndiyo wanaosubiri kudra za wajumbe kesho.
Pichani kushoto ni Dk. Hosea katikati Flaviana Charles na kulia ni Shehzad Wall, nimekosa picha za Albert na Francis.
Kwa kudra za Allah kesho nitawapa kinachojiri kama nitafanikiwa kufika eneo la tukio.
Alamsiki.
UPDATES:
Tayari mshindi wa uchaguzi mkuu wa urais kwa mwaka 2021 ametangazwa ambaye ni dkt. Edward Hosea ambaye amepata jumla ya kura zote 297.
Zaidi, soma: Breaking News: - Dr. Edward Hosea ashinda urais wa Tanganyika law society (TLS) , apata kura 297
Sijajua kwa nini wagombea hawa wawili kati wa wote watano wamekuwa na kampeni ya namna hii, nilipokuwa napita maeneo ya Sanawari hapa jijini arusha kuelekea mjini nilipishana na watu waliovaa nguo hizo.
Nilijaribu kuuliza kujua kulikoni ndiposa nikaambiwa hao wawili mmoja ndiye mwenye nafasi na hasa Dk Edward Hose aliyewahi kuwa boss pale Takukuru.
Naambiwa kesho ndiyo kinyang'anyiro cha kupiga kura na kinafanyika hapa arusha kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa AICC.
Nimeuliza na kupata majina ya wagombea wote kama ifuatavyo, Dk Edward Hosea, Albert Msando, Flaviana Charles, Shehzad Wall na Rais wa zamani wa chama hicho, Francis Stolla hawa ndiyo wanaosubiri kudra za wajumbe kesho.
Pichani kushoto ni Dk. Hosea katikati Flaviana Charles na kulia ni Shehzad Wall, nimekosa picha za Albert na Francis.
Kwa kudra za Allah kesho nitawapa kinachojiri kama nitafanikiwa kufika eneo la tukio.
Alamsiki.
UPDATES:
Tayari mshindi wa uchaguzi mkuu wa urais kwa mwaka 2021 ametangazwa ambaye ni dkt. Edward Hosea ambaye amepata jumla ya kura zote 297.
Zaidi, soma: Breaking News: - Dr. Edward Hosea ashinda urais wa Tanganyika law society (TLS) , apata kura 297