Matamko ya (baadhi) waislam (Dar na Mwanza)

Matamko ya (baadhi) waislam (Dar na Mwanza)

Status
Not open for further replies.
Kwa nini na nyie waislam msiwe na MOU yenu na serikali??

Usidhani Waislam wanatatizizo na MoU ya wakiristo na serikali ila wana tatizo jinsi MoU hiyo ilivyosainiwa "kwa mlango wa nyuma" bila ya public kuwa aware.

Hivi unadhani Serikali wangewapa waislam mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC kwa siri ingekuwaje? Maaskofu na Mapadri si wangeitusi Serikali na Waislam.

Tumeshuhudia mambo mengi ya kejeli juu ya Uislam lakini Waislam wamekuwa na "subra" na uvumilivu.
 
Hi Mdanganyika, Big up!

Nimeifurahia sana thread yako. Hakika imetulia. Naona US imekubadilisha mtazamo mazee.Tunataka WAISLAMU wenye mtazamo kama wewe na si hawa vihiyo kina Ponda na pamoja na Masheikh wote waliotamka hili TAMKO LA UBABAISHAJI.

Mimi nimeshawahi kusema kwenye forum hii kuwa WAISLAMU WANANG'ANG'ANIA KUSOMA KIARABU KWENYE MADRAS BADALA YA KUSOMESHWA KISWAHILI AU KIINGEREZA KWENYE SHULE ZA KAWAIDA ILI WAPATE ELIMU DUNIA ITAKAYOWAPANUA UPEO WAO WA KUFIKIRI.

Nimeshasema QURAN siyo lazima isomeke KIARABU wakti wote. KIARABU si lugha ya Mbinguni. Waislamu wanatakiwa wakatae UKOLONI MAMBOLEO WA KIARABU kuwa Quran ikitafsiriwa kwa LUGHA NYINGINE itapotoshwa. Hii si kweli. Kitu ninachokiona ni kuwa kuna Waislamu wanahofia kuwa ZIPO AYA ZIKITAFSIRIWA KATIKA NATIVE LANGUAGE zinaweza kuwafumbua macho na kuushtukia Uislamu maana kwenye Quran kumejaa AYA ZENYE KUTILIWA MASHAKA!Do you remember the SATANIC VERSES?

Ignorance kills, kasumba eti kwa sababu umekaa marekani!!! Ngoja nikutoe ujinga na ubaguzi kidogo, Tafsiri ya Quran ipo ya Kiswahili na Kiingereza! Usiwe mvivu wa kutafuta elimu na kutegemea JF..
 
Walioanzisha upendeleo huu wa misamaha ya kodi, ruzuku n.k walijua exactly this is what will happen in the future. Wakati watakapo kuwa wamepiga hatua kubwa mno kiasi hata kufikika hawafikiki..wamejaa kwenye idara zote za serikali, wana idadi kubwa ya shule na vyo vikuu, wana vitua vya afya na hospitali bora kabisa na wana wana taaluma bora na wengi mno.

Ila dhulma kamwe haijengi na malipo ni hapa hapa duniani, lazima kizazi kimojawapo kitakuja pata haki za waliodhukumiwa wazazi wao. Wewe huwezi kukata watu kodo za serikali na kwenda kuimarisha makanisa na taasisi zake. Tunaamini kama Mungu wetu ji Mungu wa haki na yeye ndio mlipaji wa yote juu ya dhula zote. Tuna Yaqiin atatusaidia tu!
Ma'ssalaam.
Shkh Yahya

Ulijifunza kuandika kweli darasa la kwanza?maana hata keyboard kwako kiama mkuu...
 
Na wewe pia hujasoma tamko, umekurupuka na prejudices zenu mlizofundishwa kanisani..lipi ambalo si kweli katika tamko..

Tamko halina mwanzo mie naona kila kitu pamoja, nimesoma mistali miwili nikaona pumba, sikuendelea...wape watu waliedit linaweza vutia lkn sio kustahimili wasomaji...UPUPU MTUPU
 
Topica said:
Originally Posted by Topical
Action follows, sawa tu na tamko la maaskofu ok?
]
Kwa heshima na taadhima naomba ubandike tamko la maaskofu kama la waislamu lilivyobandikwa


Mhhhhhhhhhhh bandiko lao liko shallow mkuu, usilinganishe na la MAASKOFU lililoenda school
 
Muslim university badala ya kuwa kitovu cha elimu kwa waislam mnaitumia kwa propaganda za kutaka kuandamana kumuunga mkono mhalifu wa kivita Al Bashir na kuwafagilia Al Shabaab mnadhani mtaondokana na ujinga kweli? Thubutu, mtaendelea kulalamika hadi siku tutakaypgawana nchi. Nyie waarabu wanawapa zawadi za tende na halua, wenzenu wazungu wanawapa zawadi za vitabu na computer, je mtaoka kweli?

Another crap!! Prejudices....una bomoa zaidi badala ya kujenga Taifa hili...Mchango wako ni wa chuki na hauna maendeleo katika nchi yetu!!!
 
Another crap!! Prejudices....una bomoa zaidi badala ya kujenga Taifa hili...Mchango wako ni wa chuki na hauna maendeleo katika nchi yetu!!!

Hoja zinakwepwa mkuu ili kupoteza maudhui yanayozungumzwa usipoteze muda kujibizana na wapotoshaji.
 
Anzisheni zenu sio kuchapana makofi.Moslems ur disorganised,unfocused and departed,simply on cheap thinking. so after this tamko, mnasubiri remix ya maaskofu,shame on u

Na maaskofu hawatatoa remix tuone mtadesa wapi! Shame on u!
 
natamani hizo hospitali za waikristo(bugando,kcmc) zirudi kipravate ili ziendeshwe kwa gharama kubwa tuone hayo mabusha mtayatibu wapi.ruzuku kwenye hizi hospitals ni kwasababu govt haina hospitals zakutosha ikiziacha ziendeshwe kibinafsi wallah wananchi twafaaaaaa

Una tatizo la msingi wewe.Kwani ni asilimia ngapi ya waislamu wanatibiwa ktk hospitali hizo? Je una habari kuwa gharama za matibabu ktk hospitali hizo ziko juu sana huwezi jua kama kuna ruzuku inayotoka serikalini?Nenda TMJ kwa mfano isiyopata ruzuku za serikali linganisha gharama zake kama hutakuta TMJ ni nafuu sana kuliko hizo za kanisa.
Hata hivyo suala la huduma kama za matibabu ni wajibu wa serikali.Tatizo ni kwamaba serikali imekasimu wajibu wake kwa makanisa na unakuta hata viongozi wakristu badala ya kujenga nchi wanajenga dini yao.Mimi nataka kodi yangu serikali iitumie kutoa huduma kama za hospitali kwa raia wote na ifanye yenyewe kazi hiyo sio kodi yangu kwenda kwenye taasis za kanisa halafu wakati huo hou eti serikali inalishukuru kanisa kwa kuisaidi ktaka huduma.Nani anamsaidia nani? Kila mwezi nakatwa kodi kubwa kwenye mshahara wangu pia nalipia kodi zingine mabalimbali sipendi kabisa ziende kanisani.Hii sio haki na ni ufisadi namaba moja.
 
Ndugu Waislamu haya mnayoyajua sasa ya MOU ni madogo.Nina ushahidi ngoja niufanyie scanning ntautoa,unaoonesha kuwa makanisa yameiba mali nyingi sana tz kuanzia ukoloni hadi leo.Wana viwanja vya ndege karibu sehemu zote zenye madini na kenye mali asili zetu ambapo siku zote wao huruka na mali nyingi na huwa ndege zao hazikaguliwi.Sijui ile kesi ya yule Padri wa kinaijeria aliyekamatwa Arusha anatorosha madini iliishia wapi? Kwa kulindana kwao kuna uwezekano mkubwa kesi ilishafutwa zamani.Zamani nilikuwa nashanagaa unamkuta Padri mzungu yuko swekeni ndani kabisa porini lakini unajiuliza hivi kweli huyu yuko huku kwa sababu ya dini tu? Kumbe ni maagent wa wizi kwa mabwanyeye wa ulaya wantuibia kwa jina la dini.Maskini tz yetu,hata wakristu wazalendo haya hawayajui.Mimi sitaki kujeneralise ninaamini na ninajua kuwa kuna wakristu wazalendo wanaopenda nchi bila unafiki wowote,wanochukia dhulma za aina zote bila kujali kafanya au kafanyiwa nani,lakini wengi wao hawawezi kujitokeza hadaharani kusema kwani viongozi wao huwa hawapingwi wanaogopa kutengwa.
 
Ndugu Waislamu haya mnayoyajua sasa ya MOU ni madogo.Nina ushahidi ngoja niufanyie scanning ntautoa,unaoonesha kuwa makanisa yameiba mali nyingi sana tz kuanzia ukoloni hadi leo.Wana viwanja vya ndege karibu sehemu zote zenye madini na kenye mali asili zetu ambapo siku zote wao huruka na mali nyingi na huwa ndege zao hazikaguliwi.Sijui ile kesi ya yule Padri wa kinaijeria aliyekamatwa Arusha anatorosha madini iliishia wapi? Kwa kulindana kwao kuna uwezekano mkubwa kesi ilishafutwa zamani.Zamani nilikuwa nashanagaa unamkuta Padri mzungu yuko swekeni ndani kabisa porini lakini unajiuliza hivi kweli huyu yuko huku kwa sababu ya dini tu? Kumbe ni maagent wa wizi kwa mabwanyeye wa ulaya wantuibia kwa jina la dini.Maskini tz yetu,hata wakristu wazalendo haya hawayajui.Mimi sitaki kujeneralise ninaamini na ninajua kuwa kuna wakristu wazalendo wanaopenda nchi bila unafiki wowote,wanochukia dhulma za aina zote bila kujali kafanya au kafanyiwa nani,lakini wengi wao hawawezi kujitokeza hadaharani kusema kwani viongozi wao huwa hawapingwi wanaogopa kutengwa.

Weka na ainisha na uizi walioufanya waarabu ili muende ngoma droo, maana nao waliwakoloni mababu zetu, kuwatesa, kuwaibia, na kuwauza utumwani, na kuwaua.
 
Usibadilishe mada, topic iliyopo ni kwa waislam kutumiwa kama toilet paper bado wana mategemeo ambayo Kikwete hawezi yatimiza, walidanganywa watulie hadi baada ya uchaguzi sasa wameanza kushituka kuona miezi inapita, Kikwete naye baada ya kuona hawezi timiza anatapatapa na kuutupa mpira kwenye udini kiwe kama kisingizio cha kushindwa kwake.

Sasa kumbe we ulitaka Waislam wafanyeje.Waislam wana subira na ndio maana hii inayoitwa amani nchini kama sio subira yao isngekuwepo.Jaalia hali ya Waislmu na ubaguzi na dhulma walizofanyiwa tangia mkoloni hadi tz huru ingekuwa ni wakristu unadhani hii inayoitwa amani ingekuwepo?Wakristu mafanikio madogo ya waislam huwa yanawauma sana sembuse leo hii waislam wawe ndo wenye vyuo vikuu zaidi ya 20,hospitali kibao na juu ya yote serikali ndio inaytoa pesa zake kuwezesha taasisi hizo hali ingekuwaje?

Wakati wa kampeni wakristu waliju kwa kiasi kikubwa kuwa waislamu ni vigumu kumpa kura Padri na walikuwa wanatwambia kuwa sisi waislamu kura zetu tutazigawana kwa Lipumba na jk lakini sisi tukawa wajanja tukasema hatuzigawani na kwa ujumla wetu tumuwezeshe jk arudi madarakani kwani kuna mambo fulani anayafanya yanyoelekea kuwakomboa wananch wote bila ubaguzi.kwa mfano shule za kata,zahanati kila kata nk.Hii inatoa fursa kwa kila mtz kusoma na kupata matibabu bila kutegemea taasisi teule za wakristu na hizi ni sabau ojawapo ya maaskofu kumchukia jk.
 
Mkuu Topical, nadhani kuna kitu watoa mada wanakosea kidogo. Jamani maisha magumu mbona yanatugonga wote waislamu kwa wakristo na tusokuwa na dini? umeme ukikatika..unakatika nyumba za waislamu tuu? umaskini wa kutupwa ni kwa waislamu tuu? Wakuu mnahitaji kujipanga kwa upya Hizi hoja zenu hazina mashiko kabisa. Sasa hivi Raisi ni muislam, Makamu wa Rais, Jaji Mkuu, IGP nk! Sasa hamuoni kwamba hoja zenu zimekosea timing? BASI KAMA MNAWEZA WAITENI HAO VIONGOZI AMBAO NI WAUMINI wenzenu muwape msimamo wenu.

Harafu niwaulize....kama mnasema mnadhurumiwa waislamu...mbona hamsemi hivyo kwenye sanduku la kura? Kwa nini wote msingempigia kura Lipumba? (Maana JK ni muislamu ila ni uzao wa mtakatifu Nyerere kwenye CCM!).

I strongly believe all moslems dont share this kind of nonsense! Mbona kuna waislamu wako so successful ndani na nje ya nchi..na wamefanya hivo on merit? Watu kama mnaendekeza ujinga..msitake kutugombanisha watanzania. Mnalalamikia shule za wakristo..jamani..kuna Muislamu alishabaguliwa kwa kunyimwa nafasi ya shule kwenye shule ya hao "maaskofu"? Kama yupo..ajitokeze hapa..kesi yake tutaigharimia mahakamani.....Naamini..waliotoa hili tamko ni ma-opportunist tuu....na wanataka kutumia migongo ya watu kujinufaisha..siwatofautishi na wakristo ambao wametuibia kodi zetu. Kuna waislamu wanahangaika kujitafutia mkate wa kila siku kama wengine hapa....sema tuu nyingi mnataka mlete vuguvugu na machafuko hapa...muweze kuonekana wa maana huko Saudia na kwingineko... HATUDANGANYIKI! HUU WARAKA NI WAJINGA WACHACHE WANAOJIITA WAISLAMU NDO WANATAKA KUTUGHILIBU!

Muislam habaguliwi kwenye shule za masista lakini mkriso akienda shule za kiislam hijabu lazima! Hutaki chapa lapa!
 
Weka na ainisha na uizi walioufanya waarabu ili muende ngoma droo, maana nao waliwakoloni mababu zetu, kuwatesa, kuwaibia, na kuwauza utumwani, na kuwaua.

Inawezekana waarabu walifanya hayo unayoseam japo kuwa mengine ni propaganda.Kama walifanya ndio maana tuilipigania na hatimae tujitawale tuondokane na dhulma za wageni wote wawe waarabu au wazungu.Lakini bahati mbaya wazungu waliendelea kutuibia hata baada ya kujitawla kwa kutumia mgong wa kanisa.
Suala la waarabu kuwauwa babu zetu ni propganda ya wakristu ili kujidai eti kubalansi baina ya maovu yaliyofanywa na waarabu na wazungu. waarabu wengi waliokuja huku hawakuwa na sababu za kupeleka watumwa kwao kwa sababu hawakuwa na kazi za kuwatumikisha,hawakuwa na viwanda hata ardhi yao haifai kwa kilimo,ndio maana wengi wao waliokuja huku waliseto kabisa wakachanganyikana na wenyeji.Hadi sasa tunaishi nao hata uswahilini.Mfano mzuri ni wa Sultani aliyehamishia hata makazi yake Zanzibar.Lakini hilo halipo kwa wazungu wao wlikuwa wanakwiba na kuhamishia kwao,tulipowafukuza waliondoka jumla hatunao kama raia isipokuwa wamissoinari waliobakia kuendeleza wizi kama nilivyoutaja
 
Inawezekana waarabu walifanya hayo unayoseam japo kuwa mengine ni propaganda.Kama walifanya ndio maana tuilipigania na hatimae tujitawale tuondokane na dhulma za wageni wote wawe waarabu au wazungu.Lakini bahati mbaya wazungu waliendelea kutuibia hata baada ya kujitawla kwa kutumia mgong wa kanisa.
Suala la waarabu kuwauwa babu zetu ni propganda ya wakristu ili kujidai eti kubalansi baina ya maovu yaliyofanywa na waarabu na wazungu. waarabu wengi waliokuja huku hawakuwa na sababu za kupeleka watumwa kwao kwa sababu hawakuwa na kazi za kuwatumikisha,hawakuwa na viwanda hata ardhi yao haifai kwa kilimo,ndio maana wengi wao waliokuja huku waliseto kabisa wakachanganyikana na wenyeji.Hadi sasa tunaishi nao hata uswahilini.Mfano mzuri ni wa Sultani aliyehamishia hata makazi yake Zanzibar.Lakini hilo halipo kwa wazungu wao wlikuwa wanakwiba na kuhamishia kwao,tulipowafukuza waliondoka jumla hatunao kama raia isipokuwa wamissoinari waliobakia kuendeleza wizi kama nilivyoutaja

Kwanini kila anapoguswa mwarabu ni propaganda ? Unajua hata mtu objective akitaka kukusikiza ataona tu unatawaliwa na bigotry na ana loose interest very fast.
 
Muislam habaguliwi kwenye shule za masista lakini mkriso akienda shule za kiislam hijabu lazima! Hutaki chapa lapa!

Sikujua kama waislam wakienda kwenye shule za wakristu wanaruhusiwa kuvaa hijabu! nijuavyo mimi huwa hawruhusiwi,ni lazima wavae vimini ambalo ndo vazi rasmi la wakristu hutaki chapa lapa!
Uovu mwingine wanaofanyiwa waislamu ktk shule za kanisa ni kulazimishwa kusali kikristu,huo zi ubaguzi?
 
Sikujua kama waislam wakienda kwenye shule za wakristu wanaruhusiwa kuvaa hijabu! nijuavyo mimi huwa hawruhusiwi,ni lazima wavae vimini ambalo ndo vazi rasmi la wakristu hutaki chapa lapa!
Uovu mwingine wanaofanyiwa waislamu ktk shule za kanisa ni kulazimishwa kusali kikristu,huo zi ubaguzi?

Shule zipi? Hao waislamu wako wa kufikirika wakati wanaomba kuingia kwene hizo shule za Kikristu hawakujua kwamba wanaingia shule za kikristu?
 
Shule zipi? Hao waislamu wako wa kufikirika wakati wanaomba kuingia kwene hizo shule za Kikristu hawakujua kwamba wanaingia shule za kikristu?

Naona hasira zinakufanya hadi unakurupuka tu. Soma vizuri thread halafu ndoe upayuke.Mi nilimjibu yule aliyedai kuwa waislamu hawabaguliwi kwenye shule za wakristu lakini wakristu hulazimishwa kuvaa hijabu kwenye shule za waislam. Bora swali lako ungelielekeza kwake huyo aliyesema wakristu hulazimishwa kuvaa hijab kwenye shule za waislam
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom