Matamko ya (baadhi) waislam (Dar na Mwanza)

Matamko ya (baadhi) waislam (Dar na Mwanza)

Status
Not open for further replies.
nikiacha miaka mitano iliyopita ya utawala wa JK..... takribani miezi kadhaa tumeona jinsi vugu vugu la uchaguzi liilvyoacha mengi ya kujifunza , kujiuliza na, kutafakari na kujutia kama sio na kujipongeza pia.... ila kubwa ni hili la DINI kutanza kuchukua kasi katika swala zima la siasa na uongozi/utendaji mzima wa serikali....

Kikubwa ninachotaka kusema hapa ni jinsi gani watu walivyoamua kukaa chini ya kivuli cha udini ilimradi waungwe mkono na watu wa aina flani kwa MSLAHI YAO BINAFSI... kwa heshima kubwa na adabu niliyonayo kwa waislam na kwa kuwa nina wajali na kuwaheshim kama watu wangu ninaoishi katika yao... nasikitika kuwaambia kuwa WAO NDIO WATAKUWA WA KWANZA KUWARUSHIA MAWE VIONGOZI/WANACHAMA WA CCM 2015 bila kujali dini zao. pengine kabla hata ya 2015

ninasema hivi kwasababu CCM wameona kwa kutumia udhaifu (no offence) ya baadhi ya waislam katika kuchanganua mambo ya kijamii na kisiasa na kulowea kwao katika dini yao pasipo kutazama na kuisoma dunia inayowazunguka bac ccm wameamua kuwatumia kama MTI..... wakitatumia watakavyo wakati wa shida zao... wanawatumia kama kivuli cha uovu wao... kwa kuwagombanisha na raia wenzao.. huku wao wakiwa chanzo cha mafarakano yao....

kwanza napenda kuwaambia waislam kuwa Amin Amin nawaambia kuwa yote mliyohaidiwa kama yanahusisha jamii yoyote ambayo sio waislam bac hayatatekelezeka kwa 100% au yasitekelezwe kabisa ikiwa hazikufuatwa njia za haki... kwa kuwa kumbuka hiyo serikali iliyowaahidi au hao viongozi ina watendaji ambao nao ni sehem ya jamii...

ubabe au fitina zozote zinaziofanywa na CCM kwa kuwatumia ninyi kumbuka zitawaathiri pia ninyi kwa mlango wa nyuma kwani wao wanajua kuwa hawana ubavu wa kusimama mbele na kuwanyoshee watu vidole ss wanachofanya wanatumia DINI..

KWA NINI CCM hawawatumii wakristo.(kama kun a wanaotumika ni very few percent)

jibu ni rahisi CCM haiwatumii wakristo katika propaganda na conspiracy zake ni kwasabbau mafundisho ya kikristo yamelenga kumjenga mkristo kiroho na kimwili..... (sifahamu kwa waislam so siwezi kuelezea)

kiroho - ni kwa misingi ya imani na kumjua mungu na sheria zake na kuishi kwa mujibu wa amri zake

kimwili - ni kujua mahitaji yako halali ya kimwili na mazingira yanayokuzunguka.. na kuhakikisha hayaingiliani au hayaharibu maisha yako ya kiroho.. na ili uweze kujua mazingira yanayokuzunguaka inabidi uface tabia zake na vyote vilivyomo.. ss kwa hali hii mkristo analishwa chakula cha roho na pia analishwa chakula cha mwili...

mungu aliumba viumbe vyote akavipa pumzi na (UTASHI) utashi ni zaidi ya ufahamu huitaji kujua vifungu flani vya biblia au quran ili ujue kuwa jambo flani ni jema au baya.. kwa utashi wako tu utajua.. ss unapochanganya maamuzi ambayo yanamuliwa kwa utashi ukayapeleka kiimani, trust me u make things even worse... kwasababu iman its very complicated things na... cc wakristo tunaamini kuwa iman ni kitu chenye effect kubwa ukiweza kumtawala mtu kiiman bac kamwe itakuwa ngumu huyo mtu kukugeuka... ndio maana kibwetere aliweza choma watu moto kwani alishika iman.. na hata yesu alisema ukiwa na iman utaweza kuhamisha mlima alijaribu kuonyesha nguvu ya iman...

sasa CCM wanajua kuwa kuna baahdi ya waislam hawana utashi wa kuweza kuchanganua mambo na kuwa ile hali ya ushabiki aliyoijenga huku yeye akiamini ni iman bac wanakubali na kufanya lolote wakiamini wanafanya kwa ajili ya uislam...

Ndio hao wailsam wako kishabiki... coz kama ni kwa iman huwezi taka kitu flani kifanyike na muilsam ili kiwe halali ikiwa mungu alisema heshimuni mamlaka iliyowekwa na ninyi wenye mkakubali kuwa na serikali isiyo na dini iweje uingize swala la dini kwenye uongozi na kumbuka viongozi wenu hawateuliwi mnawachagua ingekuwa mko kiiman mngesimami misingi inayohakikisha serikali yenu haivunji haki yenu yoyote ya misingi yenu ya dini na pia misingi yenu haiathiri iman zingine kwani tunachangamana...

ila ss CCM itawatumia kwa kivuli chenu kama mti jua likishazama na giza kuingia bac itakata huo mti na kuufanya kuni ya kuokea moto ili ajikinge na baridi la usiku... na hapo ndipo mtakapo kuwa wa kwanza kuwarushia mawe...

NB: atakapo ondoka kikwete amin nawaambia CCM yeyote watakayemsimamisha akiwa muislam nawaahidi hata yafanya yale mnayoyataka ya dini yenu kwasababu hicho chama kiko mikonononi kwa mafisadi na lugha pekee wanayoielewa ni pesa na mali... kama walivyomuweka JK ... Jk anaahidi anayo ahidi hadharani na sirini ila anajua utekelezaji wake inategemea mafisadi wamelipokeaje..

ss aina hiyo ya chama na watu wake itawasaidia vp kwenye dini yenu huku mkizidi kuweka gape na watu mnaoishia nao na kupanga foleni za maji mitaani huku watoto wenu wakisoma chini ya miti na kukaa kwenye udongo ..lakini mmegeuka maadui kwasababu tu wao hawaelekei kwenye nyumba ile mnayoenda ninyi kuabudu bali wanaenda ya kwao... wanakaoimba na kushanbgilia kwa sauti.

tafakari.. sio mzuri wa kuandika Article ila naamini walau nusu ya ujumbe utakuwa umeeleweka
 
Hao wanatafuta plau na ubwabwa, hawakuwa na la zaidi ila kujipendekeza kwa JK
 
Well said

Ewe rais jk uliechakachua kura zetu,watie kolokoloni hawa wapuuzi wanaokaa na kuandika ujinga. Hawa wanaonekana walimu wazuri,kwa nini wasiende kufundisha wanao wakajua dhuluma na jinsi ya kuikemea wanaishia kumili gazeti na redio ili walisumbue taifa? Wanamkataa nyerere baadae wanamnukuu kama dira yao,ivi wanajielewa kweli?wasije wakawa ni freemasons waliokuja kutugawa Tanzania. Huku mtaani,mh.jk nakuhakikishia kuwa sie tumeshikama ,si muislam wala mkiristo anayefikiria ujinga huo wa waraka! Napenda kukuambia kuwa sie bado kwa ujumla tunatafuta jinsi ya kukunyoosha kwa kukwapua kura zetu,kwa kujilipa IPTL,DOWANS,na EPA. Wala ilo la udini ni lako na kikundi kiduchu waliosikia ukitangaza udini bungeni. Mkuu segerea haijajaa usiogope kuwatunza wachochezi wote kama mzee Mwinyi alivofanya. Siwezi kujibu ujinga wa waraka wao,mi nakushauri wewe tu na watanzania wote wanadai ivo ispokuwa magaidi wachache waliziingilia dini zetu. Sisi waislam na wakristo milele tutaikosoa serikali ata ikiongoza na Osama ibn Laden,ata iongozwe na shetani,ata iongoze na makanisa,ata iongozwe na misikiti. Kamwe hatutaacha rasilimali zetu zichezewe!
 
Sasa kaka kama dini ya kiislamu haiendeshwi kwa katiba na inaendeshwa kwa mafunzo ya kitabu kitukufu Quraan, kwa nini waslamu wanaishupalia serikari ianzishe mahakama ya KADHI? badala ya waislamu kuanzisha wenyewe kwa utaratibu ulio ainishwa kwenye Quraan tukufu? kwanini waislamu wanaishupalia serikari imtambue kadhi mkuu kikatiba? yaani nyie watu mnanichekesha sana................haha haha!

Sasa JK aneyehujumiwa na maaskofu nae anakubali BAKWATA iliyowekwa na wakatoliki na serikari kuendelea kuhujumu uislamu, inamaana JK, GHALIB BILAL, MAKAMBA, NAHODHA, MKULO, CHANDE, MWEMA, MWINYI MKUBWA NA MDOGO,sheni, id seif wote hawa ni waislamu wenye mamlaka na nafasi kubwa za kutetea uislamu na mamlaka ya kuondoa hizo hujuma na hizo conspiracy sasa kwanini wasisaidie uislamu na kutumia mamlaka yao kuondoa hizo hujuma kwa waislamu?


Hebu soma hapa ujue historia ya BAKWATA halafu somo la Mahakama ya kadhi litafuata usirukie kutembea wakati hujatamaa bado.
Mkutano wa Iringa ulipitisha katiba ya jumuiya mpya ya Waislam, katiba ambayo ilikuwa sawasawa na katiba ya TANU. Hivi ndivyo BAKWATA ilivyoundwa. BAKWATA ikamchagua Saleh Masasi, Muislam tajiri na ambae alikuwa kama mwenyekiti wa mkutano ule kuwa Mwenyekiti wa Taifa na Adam Nasibu akawa Katibu Msaidizi. Nafasi zote za juu katika BAKWATA kama ilivyotegemewa zilichukuliwa na kundi la Adam Nasibu, kundi ambalo toka mwanzo lilikuwa likidai kuvunjwa kwa EAMWS. Uongozi wa BAKWATA uliomba serikali itambue jumuiya hiyo mara moja na ipige marufuku EAMWS kama jumuiya isiyo halali na mali zake zizuiwe. BAKWATA ilitoa maazimio kadha lakini azimio namba nne ndilo hasa linafaa kuelezwa. Azimio hilo liliomba serikali, TANU na ASP kuwatazama na kufanya uchunguzi wa kina kwa viongozi wote wa EAMWS, hasa Rais, Makamo wa Rais, Katibu wao na baadhi ya viongozi wa mikoa na wilaya ambao wana chuki na hii jumuiya mpya.[1] Uongozi wa BAKWATA katika ushindi wao hawakutaka salama na mawaelewano na Waislam wenzao katika EAMWS wala kuwaonea huruma kama Uislam unavyofundisha, bali ulitaka chama na serikali uwaandame, hasa wale waliokuwa viongozi.
Baada ya kuundwa BAKWATA, ili kuondoa wasiwasi na kuwarudishia imani Waislam, Katibu wa Tume ya Waislam, Mussa Kwikima alitoa taarifa iliyosema:
Hakuna anaeweza kutishia kuwepo kwa EAMWS isipokuwa wanachama wake, sheria na serikali, lakini si watu binafsi…hata ikiwa mikoa yote kumi na saba ikijitoa haitamaananisha kuwa jumiya imekufa kwa kuwa kuwepo kwake hakutokani na kuwepo kwa mikoa hiyo kama wanachama isipokuwa kuwepo kwa wanachama wake, Waislam.[2]
Wakati ilipotoka taarifa hii BAKWATA ilikuwa bado haijaandikishwa rasmi na Msajili wa Vyama. Kisheria ilikuwa haiwezekani kwa kundi la Adam Nasibu kuunda jumiya mpya iliyokuwa na malengo sawa na jumuiya ambayo tayari ishaandikishwa. Kwa muda wa siku tatu BAKWATA na EAMWS zikawepo kwa wakati mmoja. Ilionekana kama kwamba EAMWS itashinda vitimbi vya serikali na vya kundi la Adam Nasibu.
Tarehe 19 Desemba, 1968 serikali kama vile imegutushwa na taarifa ya Kwikima, iliipa BAKWATA Cerificate of Exemption na kuifungia EAMWS.[3] Waziri wa Mambo ya Ndani Said Ali Maswanya kwa niaba ya serikali alitoa taarifa fupi:
Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kuamriwa na Rais anatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[4]
Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Julus Nyerere, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao. Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo hilo.
Viongozi wa EAMWS waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS. Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama. Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza. Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali ya Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam. Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA. Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe. Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu. BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa. Hivi ndivyo halikadhalika moto wa Waislam uliowashwa kwa kupatikana kwa uhuru waliopigania hadi ukapatikana ulivyokufa. Moto huu ulikuja ukawaka tena, lakini hiki ni kisa kingine. Insha Allah Mwenyezi Mungu akipenda tutakuja kukieleza.
Huu ndiyo ukawa mwisho wa kile kilichokuwa kikijulikana kama mgogoro wa Waislam ulivyomalizika. Mgogoro ambao ulianza pale mwalimu wa shule ya msingi asiyefahamika na yeyote alipofanya maandamano katika mitaa ya Bukoba akimuunga mkono Julius Nyerere na Azimio lake la Arusha na ukaishia kwa mwalimu huyu akiwa na nafasi juu katika jumuiya ya Kiislam ambayo ilikuwa ikichukiza machoni mwa Waislam. Mwalimu huyu ambae sasa amekuwa Makamu Katibu Mkuu wa BAKWATA alianza kazi yake kwa kuwashutua Waislam. Katika mkutano wa waandishi wa habari Adam Nasibu aliiomba TANU na ASP kujikinga na watu wanaohujumu umoja wa nchi kupitia dini. Akaendelea na kusema kuwa BAKWATA ni sawa na Baraza la Kikristo la Tanzania. [5] Kwa kuwa Waislam walinyimwa fursa ya kujadili “mgogoro’ hivi sasa kilichobaki na dhana tu, kuwa nini kingelitokea endapo wangeliruhusiwa kufanya mkutano ule ulioitishwa na EAMWS. Waislam wa Bukoba ambao ilitaarifiwa kuwa walifanya maandamano kuunga mkono Azimio la Arusha hawakutayarisha maandamano ya kuunga mkono BAKWATA. Dar es Salaam na katika miji mingi ya Tanzania, neno BAKWATA halina tofauti na tusi. Kumuita Muislam kuwa yeye ni mwanachama wa BAKWATA ni sawa na kumuita Mkristo mfuasi wa Yuda Iscariot, aliyemsaliti Yesu kwa vipande thelathini vya fedha.
Mjumbe mmoja wa Tume ya Waislam inastahili kuelezwa habari zake – Mussa Kwikima. Mussa Kwikima mwaka 1968 alikuwa ameteuliwa kuwa jaji na Rais Nyerere. Yeye ndiye hasa alikuwa nguvu kuu katika tume ya Waislam. Wakati alipojitolea kuisaidia tume katika kupambana na kundi la Adam Nasibu, Waikela alimuonya kuhusu hatari ambayo itamkabili yeye mwenyewe binafsi na kazi yake. Kwikima alijibu kuwa umoja wa Waislam ni muhimu kuliko maslahi yake binafsi. Ilipoundwa BAKWATA na hapo kuwa ndiyo mwisho wa ‘mgogoro’, Kwikima alihamishwa kutoka Dar es Salaam na kupelekwa Mwanza kama Hakimu Mkazai na Rais Nyerere akamvua madaraka ya ujaji wake. [6]
Kilichobakia baada ya kuvunjika kwa EAMWS ilikuwa ni kujaribu kuiweka BAKWATA katika mikoa kama jumuiya inayowakilisha Waislam wote wa Tanzania Bara. Mwaka mzima wa 1969 Adam Nasibu na kamati ya watu wanne walitembea katika mikoa wakiahidi msaada wa fedha kwa katibu yeyote wa zamani wa EAMWS ambae atashirikiana na BAKWATA makao makuu kuisaidia kufungua ofisi katika mkoa wake. Waislam waliipuuza BAKWATA.
Tabora ambayo haikujitoa katika EAMWS, serikali iliwaruhusu Adam Nasibu na kikundi chake kufanya mkutano wa hadhara. Kabla Adam Nasibu hajahutubia Waislam, Maulid Kivuruga mmoja wa wakongwe wa African Association na muasisi wa TANU Tabora, alipanda jukwaani kwa niaba ya Waislam wa Tabora na kuweka sharti kuwa Waislam watakuwa tayari kumsikiliza Adam Nasibu endapo Waikela mjumbe wa Tume ya Waislam iliyokuwa ikitafuta sulhu na yeye ataruhusiwa na serikali kuwahutubia Waislam ili aeleze upande wa pili wa kisa kile. Kivuruga alisema kuwa Waislam wanaomba sharti hili likubaliwe kwa sababu katika Uislam panapotokea mgogoro basi mpatanishi ni lazima asikilize pande zote mbili. Sharti hili lilikataliwa na BAKWATA na serikali. Palepale mbele ya waheshimiwa wa serikali na viongozi wa BAKWATA, Waislam wakaanza kuzomea huku wakitawanyika wakipiga takbir na wengine wakiitikia Allahu Akbar.
Siku chache baada ya tukio hili Waikela aliitwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai kusailiwa kwa nini anaipinga BAKWATA. Wakiwa ndani ya chumba cha Tabora Hotel, Geoffrey Sawaya, Mkrugenzi wa C.I.D, alimpiga maswali Waikela na kutaka kujua kwa nini yeye hayuko tayari kushirikiana na serikali kuipa nguvu na kuieneza BAKWATA. Sawaya akatoa hongo ya shilingi elfu arobaini kwa Waikela ili asaidie kuimarisha BAKWATA. Waikela kama istizai alimuuliza Sawaya kama fedha zile zilikuwa zimetoka bait mal. Waikela alikataa kupokea hongo ile. Sawaya akamtisha lakini Waikela hakutishika. Waikela aliwekwa ndani ya chumba kile akiulizwa maswali kwa kiasi cha saa nne na kisha akaamrishwa kuweka sahihi yake katika makaratasi fulani. Hili alilifanya. Waikela hakufuatwa tena na serikali. Ingawa kulikuwepo na juhudi za chinichini za kuipinga BAKWATA, juhudi hizi hazikushinda kwa kuwa BAKWATA iliweza kufungua matawi yake nchi nzima pamoja na Tabora. Wapo baadhi ya viongozi ambao hawakuweza kuhimili vishawishi vya kupokea ile hongo ya serikali na kwa ajili hii walishirikiana na serikali hivyo kuwezesha ofisi za BAKWATA kufunguliwa, hata kama zipo pale kwa jina tu. Kuangushwa kwa EAMWS kulisababishwa na watu watatu ambao wao ndiyo walikuwa mstari wa mbele kabisa – Adam Nasibu, Sheikh Kassim Juma na Abdallah Chaurembo[7] – na njama hii ikaungwa mkono na Rashid Kawawa na Abeid Amani Karume. Mkono wa Julius Nyerere na Kanisa Katoliki katika njama hii haukuonekana kabisa kama ilivyo kawaida katika njama zote za kupiga vita Uislam na Waislam Tanzania. [8]
Uchambuzi Kuhusu Dhulma

[1] Angalia Kiwanuka, uk.85. Vilevile Proceedings of the Iringa Conference 12th – 15th December,1968 katika Maktaba ya Chama cha Mapinduzi, Dodoma. Vilevile The Standard, 18th December, 1968.

[2] The Standard,18th December, 1968.

[3] The Standard, 20th December 1968.

[4] Ibid.

[5] Tewa, ibid. Vilevile angalia The Standard, 20thDecember 1968.

[6] Kiwanuka, uk. 86. Habari nyingine kuhusu Mussa Kwikima zimepatikana katika mazungumzo na yeye mwenyewe Kwikima pamoja na maelezo kutoka kwa Bilali Rehani Waikela. Katika mabadiliko makubwa na bishara Mussa Kwikima ndiye alisimama mahakamani kumtetea Sheikh Kassim Juma wakati aliposhtakiwa kwa ‘kuwachonganisha Waislam na serekali’. Sheikh Kassim Juma alikuwa akimpiga vita Kwikima wakati akiwa katibu wa Tume ya Waislam chini ya EAMWS, Kwikima alipokuwa akitafuta sulhu baina ya pande mbili.

[7] Pamoja na watu hawa watatu wengine waliokuwa katika mpango ule walikuwa: Omari Muhaji, Juma Jambia, Juma Swedi

[8] Baada ya miaka mingi ya Waislam kuisusia BAKWATA ikafika mahali ikawa inashindwa hata kufanya mikutamo ya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wakatiba yake. Kwa hali kama hiyo ilikuwa kwa Msajili wa Vyama kuivunja. Serikali ilipooona imekabiliwa na hali hiyo ikachukua jukumu la kutayarisha mkutano ili kuihuisha BAKWATA. Tarehe 28 Aprili 1993 Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamo Waziri Mkuu Augustine Mrema aliitisha mkutano kati ya Waislam na Wakristo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam. Mkutano ulikuwa hauna agenda. Kanisa lilipeleka ujumbe wa hali ya juu kabisa. Waislam hawakutokea isipokuwa BAKWATA. Katika mkutano ule Mrema alieleza kuwa uchaguzi katika BAKWATA umechelewa sana kwa kukosa faedha.Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake. Halikadhalika Mrema alisaidia kukusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya uchaguzi wa BAKWATA. Mkutano ulifanyika Dodoma tarehe 10th -12th Mei. Badala ya kufanya uchaguzi BAKWATA ilirekebisha katiba yake ili iweze kumpa ruhusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA haki ya kufukuza na kumweka katika uongozi au kumtoa mtu yeyote bila ya kipingamizi.
 
dears,

ifahamike wazi kabisa, serikali ya ccm haiko tayari kufanya mabadiliko ambayo wa tanzania tunayahitaji kwa sasa, kati ya mabadiliko hayo ni suala la kuundwa kwa katiba mpya, kuanzishwa kwa tume huru ya uchaguzi, kutokuilipa kampuni ya kitapeli ya dowans jumla ya ths 94 bilions na mambo mengi ambayao mnawezakunikumbusha.

Inatupasa tuwe makini sana na mwenendo wa mambo yanayotokea hivi sasa ambayo ukifikirisha sana ubongo wako unaweza kuya relate na njama chafu za serkali ya ccm kutaka kuyazima,kuyadhoofisha na kuyapotezea kabisa madai ya watanzania tulio wengi ambayo nimejaribu kuyaorodhesha hapo juu.

tamko la waislam:

katika hali ya kushangaza, kusikitisha,kufedhehesha na kukatisha tamaa ni tamko la viongozi wa dini ya kiislam ambayo ukuyachunguza na ukafikirisha ubongo kidogo utagundua kuwa yana mkono wa ccm.

Sina haja ya kujadili tamko lao la kuwajibu maaskofu kwa sababu tumeshalijadili sana.
Tamko walilotoa juzi nita summarize baadhi ya mambo waliyoyasema:



Hiki ni kiashirio tosha kuwa serikali ya ccm haitaki katiba mpya,inachofanya ni kuwachochea ndugu zetu waislam waone kuwa kudai haki zao (sijui ni zipi kwa kweli) ni bora zaid kabla ya kudai katiba mpya, eti waislam hawako huru ilhal rais,makamu wa rais,katibu mkuu wa chama n.k ni waislam,naomba tuchukue fursa hii kwa wale wenye mapenzi mema na nchi yetu,kuwaelimisha ndugu zetu wasiingizwe kwenye mkumbo ambao unafanywa na viongozi wao bila kujijua kwa hila za ccm.


Hii ni trick ya ccm kujaribu kupoteza malengo yetu wapenda mabailiko kwa kupoteza hoja amabazo kimsingi zinichachafya ccm na serlikali yake, wanataka kutupoteza tusijadili dowans, tusijadili mauaji waliyoyafanya arusha, tusijadili katiba mpya, tusihoji nia na uwezo wa muungwana katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi kama alivyodokeza edward hoseah.

Sisi wapenda mabadiliko hatutyumbishwa na haya na mapambano yataendelea kama kawaida, waislam ni watu wastaraabu, ni marafiki zetu, tumesoma nao,ni wa tanzania wenzetu, ni majirani zetu, wengine tumeoa huko.

Regardless, the strugle shall continue "matola's signature"

nawaza kwa sauti tu, hivi somalia pale ni dini gani? Na hapo zenji nnani kiongozi au mbunge mkristu? Kama tatizo ni uislam au ukristu pakistan na tunisia kunani au ni wakristu wale? Nafikiri ifike wakati tuanze kutumia akili zetu hata kama tunazo kiduchu zitatusaidia angalau kujua pumba na mchele.
 
Angalia kati ukristo na uislam upi ulitangulia.....



Ukristo ni dini mpya Tanzania kwa kuwa uliingizwa katika karne ya kumi na nane na wamisionari. Kanisa na Mwafrika Mkristo ni matokeo ya ukoloni. Kwa ajili hii basi historia ya Kanisa katika Afrika ni ile ya kuhirikiana na kuwa tiifu kwa serikali ya kikoloni.See Family Mirror, Second Issue, November 1994, uk. 6. D.B. Barret, Frontier Situations for Evangilisation in Africa, Nairobi, 1976. Africa South of the Sahara, Europa Publication, London, No. 20, 1991, uk. 1027.
Utafiti wa kuaminika kidogo ni ule uliofanywa na Dar es Salaam University Muslim Trustee (DUMT), Angalia ‘The Position of Muslims and Islam in Tanzania', katika Al Haq International, (Karachi) September/October 1992.

Chini ya
ukoloni, taratibu Kanisa likaweza kujenga uhusiano maalum kati yake na serikali pamoja na Mkristo Mwafrika ambae imemuelimisha katika shule zake. Mwafrika Mkristo akawa ananufaika na mfumo wa kikoloni.

Uislam umekuwepo Afrika ya Mashariki toka karne ya nane. Hata hivyo wana-historia wameghitilafiana kuhusu ni lini hasa Uislam uliingia. A.A. Ahmed akinukuu mswada ambao haujachapishwa wa Muhammad B. Sharif Al-Baidh, Stages in East African History, anasema kuwa, ‘Uislam uliingia wakati wa Khalifa ‘Abd al Malik bin Marwan, katika mwaka wa 702/80H. Al-Baidh anasema Uislam uliletwa Afrika ya Mashariki na kundi la Waomani, miongoni mwao wakiwemo waungwana wawili Sa'id na Sulaiman. Sa'id inasemekana alikuja Lamu na Sulaiman alikwenda Mombasa'. [1] Lakini wanahistoria wengi wazalendo wanaamini kuwa Uislam ulifika Afrika ya Mashariki wakati wa uhai wa Bwana Mtume (SAW), hata kabla haja hajiri kwenda Madina. Pamoja na Uislam ikazuka lugha ya Kiswahili, lugha ianyozungumzwa Afrika ya Mashariki na ya Kati na utamaduni wa Kiswahili ambao unanasibishwa na Uislam. Nembo ya Muislam katika Afrika ya Mashariki na Kati ni kuikubali lugha ya Kiswahili kama lugha yake ya asili.
Theluthi mbili ya Waislam wote wa Afrika ya Mashariki wanaishi Tanzania [2] ambayo ndiyo nchi yenye watu wengi kuliko zote katika Afrika ya Mashariki, yaani Kenya, Uganda na Tanzania. Hii ni pamoja na Zanzibar – nchi ya Kiislam yenye Waislam takriban asilimia tisini na tisa na kuna wakati ilikuwa ndiyo kitovu cha maarifa ya Kiislam katika Afrika ya Mashariki na Kati. Kutokana na sensa ya mwaka 1957, kwa kila Waislam watatu walikuwepo Wakristo wawili. Kwa wakati ule hii ilionyesha kuwa Tanganyika ilikuwa na Waislam wengi katika nchi zote Kusini ya Ikweta. Lakini katika sensa ya kwanza mwaka 1967 baada ya uhuru jumla ya Wakristo Tanzania Bara ilikuwa asilimia thelathini na mbili na Waislam asilimia thelathini na Wapagani asilimia thelathini na saba. Sensa hii inaonyesha kuwa Wapagani ndiyo walio wengi Tanzania. Sensa hii ya mwaka 1967 haikueleza kwa nini katika kipindi cha miaka kumi kwa ghafla Waislam wamepungua nchini au kwa nini ghafla Wapagani wameongozeka katika nchi ya waumini.

[1]
A.A. Ahmed, ‘Lamu's Sacred Meadows', Fountain, April-June, 1995 Vol. 2 No. 10, p.30.

[2]
August H. Nimtz Jr, Islam and Politics in East Africa, University of Minneapolis, 1980, p.11.


 
Lawama nyingine waliitupia serikali kwa kuacha Kanisa liendeshe nchi kwa kuachia Kanisa kuwa na Hospitali nyingi, vyuo vingi, na shule nyingi kitu ambacho vitu hivyo walidai kama vingemilikIwa na serikali kanisa lisingekuwa na nguvu. Kutokana mafanikio haya ya kanisa washehe hao (waliokuwa studio za Iman Radio) walikubaliana kwa pamoja kuwa njia pekee ya kufanya ni kuhamasishana kwa sasa na kudai wapewe eneo lao wajitawale ili kuepuka uonevu wa kutawaliwa na kanisa.



Nani kawaambia waislamu kuwa wakristo wanachangiwa na serikali kuleta maendeleo, wafahamu kuwa wakristo wanajitoa kuchangia hospital,shule na vyuo, hawaitegemei serikali. Hoja hapa si wao kupewa eneo lao bali wajitoe kuleta maendeleo kwa waislam na sio kubwabwaja(domo domo tupu) hao viongozi wao wamenunuliwa kwa njaa zao, kikwete hawezi kuwanunua maaskofu kwani hawana njaa.



 
Jamani

Mke wangu ni Muislam.........sasa yachafuko haya ya Kidini yakitokea NIMWACHE.
 
Exactly, tegemeo lao la mwisho ambalo litawafanya waanze kurusha mawe ni pale ahadi ya kuanzishwa Mahakama ya kadhi na OIC itakapoyeyuka wait and see.
 
Dears,

Ifahamike wazi kabisa, serikali ya CCM haiko tayari kufanya mabadiliko ambayo wa Tanzania tunayahitaji kwa Sasa, kati ya Mabadiliko hayo ni Suala la Kuundwa kwa Katiba mpya, Kuanzishwa kwa Tume huru ya Uchaguzi, kutokuilipa Kampuni ya Kitapeli ya Dowans jumla ya THS 94 Bilions na mambo mengi ambayao mnawezakunikumbusha.

Inatupasa tuwe makini sana na mwenendo wa mambo yanayotokea hivi sasa ambayo ukifikirisha sana ubongo wako unaweza kuya relate na njama chafu za serkali ya CCM kutaka kuyazima,kuyadhoofisha na kuyapotezea kabisa madai ya Watanzania tulio wengi ambayo nimejaribu kuyaorodhesha hapo juu.

Tamko la waislam:

Katika hali ya kushangaza, kusikitisha,kufedhehesha na kukatisha tamaa ni tamko la viongozi wa dini ya Kiislam ambayo ukuyachunguza na ukafikirisha ubongo kidogo utagundua kuwa yana Mkono wa CCM.

Sina haja ya kujadili tamko lao la kuwajibu Maaskofu kwa sababu tumeshalijadili sana.
Tamko walilotoa juzi nita summarize baadhi ya mambo waliyoyasema:



Hiki ni kiashirio tosha kuwa Serikali ya CCM haitaki katiba mpya,inachofanya ni kuwachochea ndugu zetu waislam waone kuwa kudai haki zao (Sijui ni zipi kwa kweli) ni bora zaid kabla ya kudai katiba mpya, eti waislam hawako huru ilhal Rais,Makamu wa Rais,Katibu Mkuu wa chama n.k ni Waislam,naomba tuchukue fursa hii kwa wale wenye mapenzi mema na nchi yetu,kuwaelimisha Ndugu zetu wasiingizwe kwenye Mkumbo ambao unafanywa na Viongozi wao bila kujijua kwa hila za CCM.


Hii ni trick ya CCM kujaribu kupoteza malengo yetu wapenda mabailiko kwa kupoteza hoja amabazo kimsingi zinichachafya CCM na serlikali yake, wanataka kutupoteza tusijadili DOWANS, tusijadili Mauaji waliyoyafanya Arusha, Tusijadili Katiba Mpya, tusihoji nia na uwezo wa Muungwana katika vita Dhidi ya Rushwa na ufisadi kama alivyodokeza Edward Hoseah.

Sisi Wapenda mabadiliko hatutyumbishwa na haya na Mapambano yataendelea kama kawaida, Waislam ni watu wastaraabu, ni marafiki zetu, tumesoma nao,ni Wa Tanzania wenzetu, ni majirani zetu, wengine tumeoa huko.

Regardless, the strugle shall continue "Matola's Signature"

Muungwana Bramo umenena ukweli mtupu, Tanzania yetu ni ya wote bila kujali Mwislamu wala Mkristo, tumezaliwa omoja, shule tumesoma pamoja, wote ni majilani, tumeoleana ni wajomba wakwe shangazi na binamu. Nani anabisha kama hana nasaba na wote wawe Waislamu au Wakristo. Tanzania yetu hii sote ni ndugu, huyo aliyeishiwa mitaji ya kisiasa sasa anataka kutusambalatisha tumeisha gundua hila zake; toto lala mama cheja.
Sasa nasema hatudanganyiki, kuibiwa mchana kweupe; DOWANS,RICHIMOND,EPA; hapo hatuna simile, hakuna cha Ushehe wala Upadiri wizi ni wizi hatutarudi nyuma kupambana nao, wote kwa pamoja maana mtumbwi ni mmoja ukizama twafa wote pia. Ukola TZ umezidi wanatafuta pa kushika, tuwapelekee moto wajue kabisa hatujalala, mbwa akibweka sana hata mwizi sugu huwa akimbia watu wasimkute. Tugangamale wote katika hili ni ndugu moja bila kujali dini yako. Mafisadi ama zao au zetu, tumechoka kuibiwa tena hadharani!!!!!!!!!!!!!!!

 
Hebu soma hapa ujue historia ya BAKWATA halafu somo la Mahakama ya kadhi litafuata usirukie kutembea wakati hujatamaa bado.
Mkutano wa Iringa ulipitisha katiba ya jumuiya mpya ya Waislam, katiba ambayo ilikuwa sawasawa na katiba ya TANU. Hivi ndivyo BAKWATA ilivyoundwa. BAKWATA ikamchagua Saleh Masasi, Muislam tajiri na ambae alikuwa kama mwenyekiti wa mkutano ule kuwa Mwenyekiti wa Taifa na Adam Nasibu akawa Katibu Msaidizi. Nafasi zote za juu katika BAKWATA kama ilivyotegemewa zilichukuliwa na kundi la Adam Nasibu, kundi ambalo toka mwanzo lilikuwa likidai kuvunjwa kwa EAMWS. Uongozi wa BAKWATA uliomba serikali itambue jumuiya hiyo mara moja na ipige marufuku EAMWS kama jumuiya isiyo halali na mali zake zizuiwe. BAKWATA ilitoa maazimio kadha lakini azimio namba nne ndilo hasa linafaa kuelezwa. Azimio hilo liliomba serikali, TANU na ASP kuwatazama na kufanya uchunguzi wa kina kwa viongozi wote wa EAMWS, hasa Rais, Makamo wa Rais, Katibu wao na baadhi ya viongozi wa mikoa na wilaya ambao wana chuki na hii jumuiya mpya.[1] Uongozi wa BAKWATA katika ushindi wao hawakutaka salama na mawaelewano na Waislam wenzao katika EAMWS wala kuwaonea huruma kama Uislam unavyofundisha, bali ulitaka chama na serikali uwaandame, hasa wale waliokuwa viongozi.
Baada ya kuundwa BAKWATA, ili kuondoa wasiwasi na kuwarudishia imani Waislam, Katibu wa Tume ya Waislam, Mussa Kwikima alitoa taarifa iliyosema:
Hakuna anaeweza kutishia kuwepo kwa EAMWS isipokuwa wanachama wake, sheria na serikali, lakini si watu binafsi…hata ikiwa mikoa yote kumi na saba ikijitoa haitamaananisha kuwa jumiya imekufa kwa kuwa kuwepo kwake hakutokani na kuwepo kwa mikoa hiyo kama wanachama isipokuwa kuwepo kwa wanachama wake, Waislam.[2]
Wakati ilipotoka taarifa hii BAKWATA ilikuwa bado haijaandikishwa rasmi na Msajili wa Vyama. Kisheria ilikuwa haiwezekani kwa kundi la Adam Nasibu kuunda jumiya mpya iliyokuwa na malengo sawa na jumuiya ambayo tayari ishaandikishwa. Kwa muda wa siku tatu BAKWATA na EAMWS zikawepo kwa wakati mmoja. Ilionekana kama kwamba EAMWS itashinda vitimbi vya serikali na vya kundi la Adam Nasibu.
Tarehe 19 Desemba, 1968 serikali kama vile imegutushwa na taarifa ya Kwikima, iliipa BAKWATA Cerificate of Exemption na kuifungia EAMWS.[3] Waziri wa Mambo ya Ndani Said Ali Maswanya kwa niaba ya serikali alitoa taarifa fupi:
Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kuamriwa na Rais anatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[4]
Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Julus Nyerere, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao. Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo hilo.
Viongozi wa EAMWS waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS. Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama. Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza. Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali ya Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam. Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA. Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe. Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu. BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa. Hivi ndivyo halikadhalika moto wa Waislam uliowashwa kwa kupatikana kwa uhuru waliopigania hadi ukapatikana ulivyokufa. Moto huu ulikuja ukawaka tena, lakini hiki ni kisa kingine. Insha Allah Mwenyezi Mungu akipenda tutakuja kukieleza.
Huu ndiyo ukawa mwisho wa kile kilichokuwa kikijulikana kama mgogoro wa Waislam ulivyomalizika. Mgogoro ambao ulianza pale mwalimu wa shule ya msingi asiyefahamika na yeyote alipofanya maandamano katika mitaa ya Bukoba akimuunga mkono Julius Nyerere na Azimio lake la Arusha na ukaishia kwa mwalimu huyu akiwa na nafasi juu katika jumuiya ya Kiislam ambayo ilikuwa ikichukiza machoni mwa Waislam. Mwalimu huyu ambae sasa amekuwa Makamu Katibu Mkuu wa BAKWATA alianza kazi yake kwa kuwashutua Waislam. Katika mkutano wa waandishi wa habari Adam Nasibu aliiomba TANU na ASP kujikinga na watu wanaohujumu umoja wa nchi kupitia dini. Akaendelea na kusema kuwa BAKWATA ni sawa na Baraza la Kikristo la Tanzania. [5] Kwa kuwa Waislam walinyimwa fursa ya kujadili "mgogoro' hivi sasa kilichobaki na dhana tu, kuwa nini kingelitokea endapo wangeliruhusiwa kufanya mkutano ule ulioitishwa na EAMWS. Waislam wa Bukoba ambao ilitaarifiwa kuwa walifanya maandamano kuunga mkono Azimio la Arusha hawakutayarisha maandamano ya kuunga mkono BAKWATA. Dar es Salaam na katika miji mingi ya Tanzania, neno BAKWATA halina tofauti na tusi. Kumuita Muislam kuwa yeye ni mwanachama wa BAKWATA ni sawa na kumuita Mkristo mfuasi wa Yuda Iscariot, aliyemsaliti Yesu kwa vipande thelathini vya fedha.
Mjumbe mmoja wa Tume ya Waislam inastahili kuelezwa habari zake – Mussa Kwikima. Mussa Kwikima mwaka 1968 alikuwa ameteuliwa kuwa jaji na Rais Nyerere. Yeye ndiye hasa alikuwa nguvu kuu katika tume ya Waislam. Wakati alipojitolea kuisaidia tume katika kupambana na kundi la Adam Nasibu, Waikela alimuonya kuhusu hatari ambayo itamkabili yeye mwenyewe binafsi na kazi yake. Kwikima alijibu kuwa umoja wa Waislam ni muhimu kuliko maslahi yake binafsi. Ilipoundwa BAKWATA na hapo kuwa ndiyo mwisho wa ‘mgogoro', Kwikima alihamishwa kutoka Dar es Salaam na kupelekwa Mwanza kama Hakimu Mkazai na Rais Nyerere akamvua madaraka ya ujaji wake. [6]
Kilichobakia baada ya kuvunjika kwa EAMWS ilikuwa ni kujaribu kuiweka BAKWATA katika mikoa kama jumuiya inayowakilisha Waislam wote wa Tanzania Bara. Mwaka mzima wa 1969 Adam Nasibu na kamati ya watu wanne walitembea katika mikoa wakiahidi msaada wa fedha kwa katibu yeyote wa zamani wa EAMWS ambae atashirikiana na BAKWATA makao makuu kuisaidia kufungua ofisi katika mkoa wake. Waislam waliipuuza BAKWATA.
Tabora ambayo haikujitoa katika EAMWS, serikali iliwaruhusu Adam Nasibu na kikundi chake kufanya mkutano wa hadhara. Kabla Adam Nasibu hajahutubia Waislam, Maulid Kivuruga mmoja wa wakongwe wa African Association na muasisi wa TANU Tabora, alipanda jukwaani kwa niaba ya Waislam wa Tabora na kuweka sharti kuwa Waislam watakuwa tayari kumsikiliza Adam Nasibu endapo Waikela mjumbe wa Tume ya Waislam iliyokuwa ikitafuta sulhu na yeye ataruhusiwa na serikali kuwahutubia Waislam ili aeleze upande wa pili wa kisa kile. Kivuruga alisema kuwa Waislam wanaomba sharti hili likubaliwe kwa sababu katika Uislam panapotokea mgogoro basi mpatanishi ni lazima asikilize pande zote mbili. Sharti hili lilikataliwa na BAKWATA na serikali. Palepale mbele ya waheshimiwa wa serikali na viongozi wa BAKWATA, Waislam wakaanza kuzomea huku wakitawanyika wakipiga takbir na wengine wakiitikia Allahu Akbar.
Siku chache baada ya tukio hili Waikela aliitwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai kusailiwa kwa nini anaipinga BAKWATA. Wakiwa ndani ya chumba cha Tabora Hotel, Geoffrey Sawaya, Mkrugenzi wa C.I.D, alimpiga maswali Waikela na kutaka kujua kwa nini yeye hayuko tayari kushirikiana na serikali kuipa nguvu na kuieneza BAKWATA. Sawaya akatoa hongo ya shilingi elfu arobaini kwa Waikela ili asaidie kuimarisha BAKWATA. Waikela kama istizai alimuuliza Sawaya kama fedha zile zilikuwa zimetoka bait mal. Waikela alikataa kupokea hongo ile. Sawaya akamtisha lakini Waikela hakutishika. Waikela aliwekwa ndani ya chumba kile akiulizwa maswali kwa kiasi cha saa nne na kisha akaamrishwa kuweka sahihi yake katika makaratasi fulani. Hili alilifanya. Waikela hakufuatwa tena na serikali. Ingawa kulikuwepo na juhudi za chinichini za kuipinga BAKWATA, juhudi hizi hazikushinda kwa kuwa BAKWATA iliweza kufungua matawi yake nchi nzima pamoja na Tabora. Wapo baadhi ya viongozi ambao hawakuweza kuhimili vishawishi vya kupokea ile hongo ya serikali na kwa ajili hii walishirikiana na serikali hivyo kuwezesha ofisi za BAKWATA kufunguliwa, hata kama zipo pale kwa jina tu. Kuangushwa kwa EAMWS kulisababishwa na watu watatu ambao wao ndiyo walikuwa mstari wa mbele kabisa – Adam Nasibu, Sheikh Kassim Juma na Abdallah Chaurembo[7] – na njama hii ikaungwa mkono na Rashid Kawawa na Abeid Amani Karume. Mkono wa Julius Nyerere na Kanisa Katoliki katika njama hii haukuonekana kabisa kama ilivyo kawaida katika njama zote za kupiga vita Uislam na Waislam Tanzania. [8]
Uchambuzi Kuhusu Dhulma

[1] Angalia Kiwanuka, uk.85. Vilevile Proceedings of the Iringa Conference 12th – 15th December,1968 katika Maktaba ya Chama cha Mapinduzi, Dodoma. Vilevile The Standard, 18th December, 1968.

[2] The Standard,18th December, 1968.

[3] The Standard, 20th December 1968.

[4] Ibid.

[5] Tewa, ibid. Vilevile angalia The Standard, 20thDecember 1968.

[6] Kiwanuka, uk. 86. Habari nyingine kuhusu Mussa Kwikima zimepatikana katika mazungumzo na yeye mwenyewe Kwikima pamoja na maelezo kutoka kwa Bilali Rehani Waikela. Katika mabadiliko makubwa na bishara Mussa Kwikima ndiye alisimama mahakamani kumtetea Sheikh Kassim Juma wakati aliposhtakiwa kwa ‘kuwachonganisha Waislam na serekali'. Sheikh Kassim Juma alikuwa akimpiga vita Kwikima wakati akiwa katibu wa Tume ya Waislam chini ya EAMWS, Kwikima alipokuwa akitafuta sulhu baina ya pande mbili.

[7] Pamoja na watu hawa watatu wengine waliokuwa katika mpango ule walikuwa: Omari Muhaji, Juma Jambia, Juma Swedi

[8] Baada ya miaka mingi ya Waislam kuisusia BAKWATA ikafika mahali ikawa inashindwa hata kufanya mikutamo ya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wakatiba yake. Kwa hali kama hiyo ilikuwa kwa Msajili wa Vyama kuivunja. Serikali ilipooona imekabiliwa na hali hiyo ikachukua jukumu la kutayarisha mkutano ili kuihuisha BAKWATA. Tarehe 28 Aprili 1993 Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamo Waziri Mkuu Augustine Mrema aliitisha mkutano kati ya Waislam na Wakristo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam. Mkutano ulikuwa hauna agenda. Kanisa lilipeleka ujumbe wa hali ya juu kabisa. Waislam hawakutokea isipokuwa BAKWATA. Katika mkutano ule Mrema alieleza kuwa uchaguzi katika BAKWATA umechelewa sana kwa kukosa faedha.Kanisa paleplale lilijitolea fedha kuipa BAKWATA ili ifanye uchaguzi wake. Halikadhalika Mrema alisaidia kukusanya fedha kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya uchaguzi wa BAKWATA. Mkutano ulifanyika Dodoma tarehe 10th -12th Mei. Badala ya kufanya uchaguzi BAKWATA ilirekebisha katiba yake ili iweze kumpa ruhusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA haki ya kufukuza na kumweka katika uongozi au kumtoa mtu yeyote bila ya kipingamizi.

Mzee kwa hiyo serikari na waislamu walikuwa mstari wa mbele kabisa – Adam Nasibu, Sheikh Kassim Juma na Abdallah Chaurembo– na njama hii ikaungwa mkono na Rashid Kawawa na Abeid Amani Karume, Nakubaliana nawe 100% sasa inakuwaje leo hii waislamu bado wanaiamini serikari kuanzisha mahakama ya kadhi kama BAKWATA ilikuwa pandikizi la serikari kwa waislamu?
 
ya viongozi wa dini tuwaachie wenyewe nadhani wanatumiwa au wamesahau job description zao
 
nikiacha miaka mitano iliyopita ya utawala wa JK..... takribani miezi kadhaa tumeona jinsi vugu vugu la uchaguzi liilvyoacha mengi ya kujifunza , kujiuliza na, kutafakari na kujutia kama sio na kujipongeza pia.... ila kubwa ni hili la DINI kutanza kuchukua kasi katika swala zima la siasa na uongozi/utendaji mzima wa serikali....

Kikubwa ninachotaka kusema hapa ni jinsi gani watu walivyoamua kukaa chini ya kivuli cha udini ilimradi waungwe mkono na watu wa aina flani kwa MSLAHI YAO BINAFSI... kwa heshima kubwa na adabu niliyonayo kwa waislam na kwa kuwa nina wajali na kuwaheshim kama watu wangu ninaoishi katika yao... nasikitika kuwaambia kuwa WAO NDIO WATAKUWA WA KWANZA KUWARUSHIA MAWE VIONGOZI/WANACHAMA WA CCM 2015 bila kujali dini zao. pengine kabla hata ya 2015

ninasema hivi kwasababu CCM wameona kwa kutumia udhaifu (no offence) ya baadhi ya waislam katika kuchanganua mambo ya kijamii na kisiasa na kulowea kwao katika dini yao pasipo kutazama na kuisoma dunia inayowazunguka bac ccm wameamua kuwatumia kama MTI..... wakitatumia watakavyo wakati wa shida zao... wanawatumia kama kivuli cha uovu wao... kwa kuwagombanisha na raia wenzao.. huku wao wakiwa chanzo cha mafarakano yao....

kwanza napenda kuwaambia waislam kuwa Amin Amin nawaambia kuwa yote mliyohaidiwa kama yanahusisha jamii yoyote ambayo sio waislam bac hayatatekelezeka kwa 100% au yasitekelezwe kabisa ikiwa hazikufuatwa njia za haki... kwa kuwa kumbuka hiyo serikali iliyowaahidi au hao viongozi ina watendaji ambao nao ni sehem ya jamii...

ubabe au fitina zozote zinaziofanywa na CCM kwa kuwatumia ninyi kumbuka zitawaathiri pia ninyi kwa mlango wa nyuma kwani wao wanajua kuwa hawana ubavu wa kusimama mbele na kuwanyoshee watu vidole ss wanachofanya wanatumia DINI..

KWA NINI CCM hawawatumii wakristo.(kama kun a wanaotumika ni very few percent)

jibu ni rahisi CCM haiwatumii wakristo katika propaganda na conspiracy zake ni kwasabbau mafundisho ya kikristo yamelenga kumjenga mkristo kiroho na kimwili..... (sifahamu kwa waislam so siwezi kuelezea)

kiroho - ni kwa misingi ya imani na kumjua mungu na sheria zake na kuishi kwa mujibu wa amri zake

kimwili - ni kujua mahitaji yako halali ya kimwili na mazingira yanayokuzunguka.. na kuhakikisha hayaingiliani au hayaharibu maisha yako ya kiroho.. na ili uweze kujua mazingira yanayokuzunguaka inabidi uface tabia zake na vyote vilivyomo.. ss kwa hali hii mkristo analishwa chakula cha roho na pia analishwa chakula cha mwili...

mungu aliumba viumbe vyote akavipa pumzi na (UTASHI) utashi ni zaidi ya ufahamu huitaji kujua vifungu flani vya biblia au quran ili ujue kuwa jambo flani ni jema au baya.. kwa utashi wako tu utajua.. ss unapochanganya maamuzi ambayo yanamuliwa kwa utashi ukayapeleka kiimani, trust me u make things even worse... kwasababu iman its very complicated things na... cc wakristo tunaamini kuwa iman ni kitu chenye effect kubwa ukiweza kumtawala mtu kiiman bac kamwe itakuwa ngumu huyo mtu kukugeuka... ndio maana kibwetere aliweza choma watu moto kwani alishika iman.. na hata yesu alisema ukiwa na iman utaweza kuhamisha mlima alijaribu kuonyesha nguvu ya iman...

sasa CCM wanajua kuwa kuna baahdi ya waislam hawana utashi wa kuweza kuchanganua mambo na kuwa ile hali ya ushabiki aliyoijenga huku yeye akiamini ni iman bac wanakubali na kufanya lolote wakiamini wanafanya kwa ajili ya uislam...

Ndio hao wailsam wako kishabiki... coz kama ni kwa iman huwezi taka kitu flani kifanyike na muilsam ili kiwe halali ikiwa mungu alisema heshimuni mamlaka iliyowekwa na ninyi wenye mkakubali kuwa na serikali isiyo na dini iweje uingize swala la dini kwenye uongozi na kumbuka viongozi wenu hawateuliwi mnawachagua ingekuwa mko kiiman mngesimami misingi inayohakikisha serikali yenu haivunji haki yenu yoyote ya misingi yenu ya dini na pia misingi yenu haiathiri iman zingine kwani tunachangamana...

ila ss CCM itawatumia kwa kivuli chenu kama mti jua likishazama na giza kuingia bac itakata huo mti na kuufanya kuni ya kuokea moto ili ajikinge na baridi la usiku... na hapo ndipo mtakapo kuwa wa kwanza kuwarushia mawe...

NB: atakapo ondoka kikwete amin nawaambia CCM yeyote watakayemsimamisha akiwa muislam nawaahidi hata yafanya yale mnayoyataka ya dini yenu kwasababu hicho chama kiko mikonononi kwa mafisadi na lugha pekee wanayoielewa ni pesa na mali... kama walivyomuweka JK ... Jk anaahidi anayo ahidi hadharani na sirini ila anajua utekelezaji wake inategemea mafisadi wamelipokeaje..

ss aina hiyo ya chama na watu wake itawasaidia vp kwenye dini yenu huku mkizidi kuweka gape na watu mnaoishia nao na kupanga foleni za maji mitaani huku watoto wenu wakisoma chini ya miti na kukaa kwenye udongo ..lakini mmegeuka maadui kwasababu tu wao hawaelekei kwenye nyumba ile mnayoenda ninyi kuabudu bali wanaenda ya kwao... wanakaoimba na kushanbgilia kwa sauti.

tafakari.. sio mzuri wa kuandika Article ila naamini walau nusu ya ujumbe utakuwa umeeleweka

hapo kwenye RED mkuu umenena hizo ndo za CCM
 
Mzee kwa hiyo serikari na waislamu walikuwa mstari wa mbele kabisa – Adam Nasibu, Sheikh Kassim Juma na Abdallah Chaurembo– na njama hii ikaungwa mkono na Rashid Kawawa na Abeid Amani Karume, Nakubaliana nawe 100% sasa inakuwaje leo hii waislamu bado wanaiamini serikari kuanzisha mahakama ya kadhi kama BAKWATA ilikuwa pandikizi la serikari kwa waislamu?

Nimekuuliza unaelewa nini kuhusu dhana ya mahakama ya kadhi? navyoelekea unaelewa ndio maana unawasiwasi naomba nijuze uelewa wako kuhusu mahakama ya kadhi ili niweze kukujibu kwa ufasaha.

Shukran.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom