Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Tatizo CCM kila baya kwao ni fursa kutia fitna Invisible polisi imetoa ripoti yake,familia imesema ukweli na madaktari pia wamesema marehemu aliumia,JE,si sahihi kuacha jukwaa kuwa sehemu ya fitna namna hii.mnaruhusu uzushi ambao umepatiwa majibu?
 
Last edited by a moderator:
Jamani tufike Mahala tuache vyombo husika vitoe majibu ya nini kilichotokea kwenye ajali hii kuliko kuanza kutengeneza majibu yasiyo na ushahidi na yenye lengo la kuleta uchonganishi wa kijamiii. Haya angalieni sasa majibu ya Dakitari na Polisi wenye taaluma zao.
hao wote wametoa majibu kuwa rasmi kitaalam.nashangaa Invisible ameacha jukwaa linatumika vibaya
 
Last edited by a moderator:
Historia ipo ili watu wajifunze kwayo, kila tukio linalotekea ni funzo kwa mwenye akili…

Mwaka 1985 tarehe 7 April, Afisa mstaafu, Mwanasheria na Mwanaharakati maarufu nchini Uingereza mwenye asili ya usikochi Willie MacRae ambaye alikuwa Makamu mwenyekiti wa SNP, aliyekuwa akipambana na Unyonyaji wa waskochi masikini na makundi ya mafia yenye kumiliki makampuni makubwa nchini humo alipata ajali ya gari na kufariki katika milima ya Scot.

Ajali yake ilizua mjadala mkubwa kuwahi kutokea nchini humo kutokana na mambo yafuatayo;

1.Wajihi wa Willie na vita yake dhidi ya MAFISADI.
2.Utata wa Ajali yake.
3.Ripoti ya Polisi.

WAJIHI WA WILLIE NA VITA YA UFISADI.
Willie kama walivyo wanaharakati wengi duniani alikuwa ni sauti ya wasio na sauti, wanyonge wa nchi ambae alitangaza wazi wazi vita dhidi ya Wanyonyaji na Mafisadi nchini mwake, akiwa kama Mpinzani ambaye aliweza kuwashambulia na hata kufungua kesi mara kadhaa mahakamani kupinga operation za makampuni makubwa ya Nuclear yanayomilikiwa na Mafia wenye mikono mirefu Serikalini ambao walinunua vyama vya siasa na wanasiasa kuwatetea.

Willie akiwa mstari wa mbele kupinga Kitendo cha Kampuni ya Dounrey Nuclear Power Development kumwaga takataka baharini, alifungua kesi na kuandaa vidhibiti vya kisheria kuthibitisha kuwa jambo hilo lina athari kubwa kwa wananchi, na kutokana na vitisho na sensitivity ya vidhibiti hivyo ilimbidi awe anatembea navyo kila wakati na kila anapokwenda hakuwahi kuziacha sehemu hata ofisini kwake ingawa baada ya kifo chake haikujulikana Document hizo zilipotelea wapi.

UTATA WA AJALI.
Watalii wawili watalii wa Ki-australia waliona gari aina ya Volvo katika bonde la Glenmoriston, na watalii wale walisogelea na kukuta mwili wa mtu kwenye gari hiyo ukiwa umejaa damu kuanzia kichwani na mwili mzima, mikono ikiwa imeshika usukani wa gari, kichwa kimelalia bega moja na hakuwa amevaa mkanda wa gari (seatbelt)
Wakasogea barabarani na kusimamisha gari ambayo ndani yake kulikuwa na Diwani wa Chama Cha SNP ambaye alimtambua WILLIE na kutambua pia kuwa alikuwa HAJAFA bado, wakamuwaisha Hospitali Aberdeen Royal infirmary ambapo alifariki na hospitali hapo iligundulika alipigwa risasi kichwani, kabla ya gari yake kutumbukia kwenye korongo hilo.


RIPOTI ZA POLISI
Ilikuwa kitendawili kikubwa kwa kuwa ripoti ya kwanza ilisema kuwa alitumbukia bondeni kwa kukosa kulimiliki gari kutokana na spidi, lakini ripoti ya hospitali inasema alipigwa risasi ya kichwa kabla ya kutumbukia kwenye korongo na kwa kuwa kioo cha gari hiyo hakikuwa na tundu la risasi ikabainika kuwa mpigaji wa risasi hiyo alikuwa ndani ya Gari hiyo kisha akashuka na kulisukuma gari kwenye Korongo.
Uchunguzi pia ulibaini kuwa bastola aina ya Wesson 45 Calibre ilipatikana mita chache kutoka ilipookotwa gari ya Willie, lakini hakukuwa na alama zozote za vidole kwenye bastola hiyo jambo lililofanya isitumike kama ushahidi katika upelelezi wa kesi hiyo.

TUKIO SIKU YA KIFO CHA WILLIE
Siku ya Kifo cha Willie ambacho kilikuwa ni gumzo kilifuatiwa na tukio la Wanasiasa wawili maarufu na wabunge wa Chama Cha Ulster Unionist kujiuzulu, Ulster ni Chama ambacho kilikuwa kinapingana na harakati za WILLIE. Kitendo hicho kilitafsiriwa kuwa ni Decoy..,kuwaondoa wananchi katika mjadala wa kifo cha WILLIE.

‘’NCHI zingine Duniani Serikali zina Mafia lakini TANZANIA mafia wana Serikali..” Dr Slaa Nov,2009 on response to Richmond Scandal’s.

R.I.P Mtanganyika Rev. Christopher Mtikila…Hivyo ndivyo ulivyo mwisho wa wanaharakati wa kweli duniani.
Asante sana mkuu
 
Uchunguzi uliofanywa kwa kukagua tukio na kuwahoji majeruhi walionusurika (katika eneo hilo hakuna watu wengine walioshuhudia tukio hilo kwa kuwa si eneo la makazi ya watu, ni mbuga). Ajali hii imeonyesha kuwa imesababishwa na sababu zifuatazo:


  1. Mwendo kasi, dereva mwenyewe anakubali kwamba alikuwa mwendo kasi licha ya kuwepo kwa alama zinazooonyesha kwenda mwendo wa Km 50 kwa saa. Aidha baada ya kuacha barabara kuu, gari hilo lilikwenda umbali wa mita 125 kabla ya kupinduka hali inayoashiria kuwa lilikuwa kwenye mwendo kasi.
  2. Uchovu wa dereva kutokana na safari ndefu kwa kuendesha gari mchana na usiku kucha kabla ya kuanza safari walikuwa wakishughulikia matengenezo ya gari hilo ambapo hakupata muda wa kupumzika.
  3. Kutofunga mkanda ya usalama. Katika uchunguzi inaonyesha marehemu hakufunga mkanda kwa kuwa alirushwa nje kupitia kioo cha mbele (wind screen).
  4. Ubovu wa gari. Gari hilo lilipata ajali tarehe 03/10/2015 na moja ya sehemu muhimu iliyoharibika ni mfumo wa usukana (steering system) yawezekana halikupata matengenezo kikamilifu na hivyo kuchangia kutokea kwa ajali hiyo.

Hivyo nitumie fursa hii kuwaomba wananchi kuwafichua maderva wanaokwenda mwendo kasi kupitia namba 08007575 ama 0715 009953 au 0658 376012. Aidha niwatake madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani na kwa wale watakao kaidi Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani hatutasita kuwachukulia hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wengi.

Asanteni kwa kunisikiliza.
Imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani


Kamishina Msaidizi Jafari Ibrahim.
 
Wajinga kama we uliyetoa ndo mnakua na mawazo finyu yenye mipaka,kuna sababu zaidi ya 10 inayoweza kusababisha. acha kufikiri usawa wa pua yako
 
Mtu karishwa nje ya gari kupitia wind screen lakini hajapata hata michirizi ya michubuko,zaidi zaidi wind screen ilimvua viatu tu marehemu.....daah
 
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limetoa ripoti ya kile kilichoelezwa kuwa ni sababu zilizopelekea ajali iliyopelekea kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa DP, Mch. Christopher Mtikila na kuainisha sababu hizo kuwa ni pamoja na:

1. Ubovu wa gari kwa kuwa lilipata ajali oktoba 3, moja ya sehemu muhimu zilizoharibika ni mfumo wa usukani, hivyo inawezekana halikupata matengenezo kikamilifu na hivyo kuchangia ajali hiyo ya pili.

2. Mtikila kutovaa mkanda wa usalama na hivyo kusababishwa arushwe nje kupitia kioo cha mbele.

3. Uchovu wa dereva kutokana na safari ndefu ya kuendesha gari mchana na usiku na kabla ya safari kurudi alikuwa akishughulikia matengenezo ya gari hivyo hakupata muda wa kumpumzika.

4. Mwendo kasi.

maswali tata baada ya ripoti ya Polisi

1. Kutofunga Mkanda na hivyo kurushwa nje kupitia kioo cha mbele ni sababu ya ajali au ni yatokanayo na ajali hiyo?

2. Mwili wa Mch. Mtikila haukua na jeraha sehemu yoyote ya mwili, unaweza kurushwa nje kupitia kioo cha mbele hata usichubuke? Ripoti ya Daktari inasema marehemu alivunjika mbavu nane, unaweza kuvunjika mbavu 8 bila kujibamiza popote? Na kama alijibamiza, unaweza kujibamiza na jeraha lisionekane?

3. Mtikila amesafiri kutoka Dar es Salaam mpaka Njombe na kurudi kuja kupata ajali Mkoani Pwani. Mbona ripori ya ya kifo chake imetolewa Mapema sana isivyozoeleka?

4. Daktari aliyechunguza safari za kifo chake ni wa Hospitali ya Tumbi alikopelekwa mara ya kwanza au wa Muhimbili alikohamishiwa?

Kifo cha Mtikila kimekuja baada ya Serikali ya Rwanda inayoongozwa na rais Paul Kagame, rais anayetajwa kuwa na mawasiliano ya karibu na mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa kushutumu Mtikila kumpa hifadhi kiongozi wa jeshi la waasi la FDLRnchini humo, Brigedia Jenerali GRATIEN KABILIGI(EXCLUSIVE: Tanzania hosts more meetings for FDLR with ICTR convicts News Of Rwanda – Rwanda News)

Aidha, tangu kuanza kwa mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia CCM ambapo Lowassa naye alikuwa kwenye kinyang'anyiro na hata alipohamia Ukawa, Mtikila amempinga waziwazi kuwa hana sifa za kwenda ikulu kwa sababu ya ufisadi na afya yake. Mtikila alitoa waraka unaosomeka"MTIKILA ATOA WARAKA MKALI KUMHUSU LOWASSA, ADAI NI BALAA"(#Urais 2015: Mtikila atoa waraka mkali sana kuhusu Lowassa, adai ni balaa kwa taifa ~ Kulikoni Ughaibuni)

Mambo hayo mwili yanahusishwa na kifo cha Mch. Mtikila hususan kupitia mitandao ya kijamii. Watu wamekwenda mbali na kusema namna ambavyo mwili wa Marehemu Mtikila ulivyokuwa umelazwa ndivyo hulazwa maiti za watu waliyouwawa kwa sababu ya kuikosoa serikali ya Kagame.
 
Tupe Ushahidi wa tuhuma zako? Usilete porojo kwenye kifo bwana!
 
acha kuweweseka weweeee!!! acheni kitengo husika kifanye kazi yake!
Wee ni nani hadi uanze kutoa ripoti ya kifo cha Rev. late ????
Tata madiba, acha kujaribu kuingilia mamlaka ya uchunguzi otherwise, tunakuomba
u declare kwamba nawe ni mchunguzi na kama sivyo,
acha kupotosha umma. Vyombo husika vitatoa majibu sahihi na si vinginevyo.Period!
 
Sasa tuambie wewe, ulitaka Polisi waseme nini kuhusu kifo chake Mchungaji?
Sema tu maana unapo ongea kitu najua una ushahidi na unacho kizungumza, kwa nilivyoelewa mada yako, inaonyesha kauwawa sio, Hapa umetaja Rwanda na Lowassa, tuambie nani kahusika na Kifo.
 
Hakuna kifo kisichokuwa na sababu ila tukubali Mtikila amekufa kwenye ajali angekuwa amekufa mwana Ukawa hizi Conspirency zote zisingekuwepo ila kwa vile amekufa aliyekuwa anampinga Mzee mnaona kama kauwawa.
Rest In Piece
 
Mkuu usipoteshe umma kwa maslai yako binafsi. ajali ya Mtikila ni ajali kama ajali nyingine, sio kila anayepata ajali hata kama atatupwa dirishani atapata michubuko utakayo iona. Marehemu Mtikila hakufunga mkanda na ndio maaa akatupwa nje na kwasababu gari ilikuwa kwenye mwendo kasi na derve akashindwa kulimudu gari ni jambo la kawaida kwa mwendo kama huo. Marehemu alivyorushwa nje yawezekana aligonga kichwa akaanza kupata internal bleeding na kawaida damu ikivujia ndani kwa ndani haitoki nje inakimbilia kwenye ubongo so ubongo utakosa hewa ndani ya dk unapoteza maisha. TAFUTA WATAALAMU WA MAMBO YA AFYA WATAKUJUZA KIUNDANI ZAIDI
 
Inaonekana Intelejensia ya TataMadiba ni Kali kuliko ile ya Jeshi la Polisi Tanzania. Itabidi Lowassa akiingia madarakani tuanze na kuliboresha jeshi la Polisi. linashindwa mpaka na Tata Madiba?
 
Last edited by a moderator:
Watu wengine bwana, yani wanataka kulazimisha njano kuwa nyekundu kwa lazima!
 
Nyongeza ya swali la 3 eneo la ajali liko mita chache kutoka kituo cha Mafuta cha Msolwa, ni ngumu kidogo.

Eneo lile hakuna makazi ya watu. Sikiliza maelezo ya mchungaji majeruhi. Dereva alikwepa Gari jingine ambalo liliovateki Lori lililopaki pembeni ili wasigongane USO kwa USO, huko alipochochora alitumbukia kwenye kakorongo ndo ikapinduka. Kwa sababu marehemu hakufunga mkanda, alirushwa nje na Gari ikamlalia.
 
alitokea kioo cha mbele kisha akaanguka chini pwaaaa! akavunjika mbavu nane hii ripoti ya potmotam imejitosheleza ila muandishi wa hii mada ana kiweri weri eitha anapandisha jina ao anatafuta kick ili kuokoa lichama lake lilochokwa na watanzania
 
Back
Top Bottom