Inasikitisha sana leo baadhi ya watanzania wanafurahia kifo cha Mtikila kisa amerudia kuponda ufisadi wa Lowasa,
Hivi kama Mtikila angefariki siku chache tu baada ya kutoka list of shame pale muembe yanga mngefurahia kifo
chake?
Naam,kumbe tatizo ni muda tu,
Kusema Lowasa fisadi wakati ule ni sawa ila leo ni mwiko kwani ukisema utakufa.
Kuna wapumbavu wanaenda mbali zaidi wakiamini kwamba ukiponda Ufisadi wa Lowasa utakufa,
Kwanini Slaa,Lisu,Msigwa,Mbowe,Sugu,Lema na wengineo wapo hai mpaka leo wakati hawa ndio walikua waasisi wakumponda waziwazi Lowasa kwamba ni mwizi na fisadi mkubwa nchini?
Tujiulize kwapamoja kwanini watu hawa hawakufa wapo hai mpaka leo?
Hivi kama kweli ukimponda lowasa kwamba ni fisadi utakufa hivi tanzania ingebaki na nani hai kwani ni dhahiri zaidi ya 80% walitamka sana ufisadi wa mh huyu.
Watanzania kama haya ndio mabadiliko tunayoyataka basi muheshimiwa Msigwa alikua sahihi,"wanaomshabikia lowasa wakapimwe akili".
Msigwa ukaanze na wewe mwenyewe kupata vipimo ili uwe mfano kwa mashabiki wengine.
Pumzika kwa amani mtanganyika tutakukumbuka kwa harakati zako na misimamo yako daima,Amina!