Maswali kuhusu elimu ya awali ya Dr. Joseph Magufuli

Maswali kuhusu elimu ya awali ya Dr. Joseph Magufuli

Lakini ujue hata kwenda sekondari ya seminari haikuwa haikuwa rahisi. Mara nyingi waliokuwa wakifauru seminari walifauru pia kwenda sekindari za serikali.

Halafu kuacha seminari siyo sababu ya performnace tu ika wakati mwingine kutofautiana mawazo.
Ningependa kutofautiana kidogo na kukubaliana na wewe sehemu nyingine.
Moja Enzi za zamani Watu wengi walipenda kupeleka watoto Shule za seminari kutokana naweledi na nidhamu za hizo shule, Shule za serikali wakati Huo zilikuwa chache saana hivyo ilikuwa unaweza kuwa hukuchaguliwa lakini ulifaulu hivyo ilikuwa kwa mzazi mwenye kujua umuhimu wa elimu kuanza mchakato wa kupata seminari toka mtoto Yupo darasa la tano au sita kwa kupata recommendation toka kwa parokiani yako na kupewa progress report toka Shule ya primary , Shule zingine ambazo zilikuwa ni nzuri au zilihitaji juhudi binafsi za mwanafunzi ni hizi private school ikiwemo lake kwa mza, buluba shy , mzizima, na zile za Moshi ambazo zingine zilikuwa sub standard in terms ya tabia na zingine zilikuwa nzuri kibohehe, kolila kibo boys etc .
Na kubaliana na wewe kuwa kutoka Shule za semenari kunaweza kutokea kutokana na kuto kubaliana na msimamo wa uongozi wa Shule na mwanafunzi etc kwa sababu waalimu wengi wa seminari hawapendi kuwa challenged nina mfano wa mtoto wa ndugu yangu alikuwa seminari moja lakini alipishana na uongozi wa shule akafukuzwa kisa kuulizia fedha za michezo , hivyo mzazi ilibidi akate rufani jimboni na bahati nzuri alipata seminari nyingine kwa vikwazo vingi ikiwemo kwamba anakoenda performance Yao ni juu , ataiharibu etc lakini baada ya hapo yeye alikuwa anafanya vizuri kuliko hao aliowakuta
 
Issue ya kutoka Seminary na kwenda Lake Secondary iko wazi kabisa kwamba SEMINARY wanautaratibu kuwa mtu ambaye performance yake darasani inakuwa poor huwa hawataki kuendelea naye na humfukuza shule mhusika, the same thing happened to MAGU, Baada ya kuwa ametimuliwa ilibidi MZAZI wake amtafutie nafasi pale LAKE Sec ili aendelee na masomo ya SECONDARY. Kipindi hicho most of private schools zilikuwa zinachukuwa wanafunzi waliokosa nafasi kwenye shule za serikali( failures wa mtihani wa Std 7).Kwa hiyo kipindi kile mtu anayesoma private school ni mtu ambaye alifeli Mtihani wa Darasa la Saba ila kwa sasa hivi imekuwa tofauti sana.
Na hiyo si kweli, Seminary kuna vigezo vingi vya kufukuzwa shule si issue ya darasani tu kama ulivyoandika. seminary kuna vikosa vidogo vidogo unaweza kufukuzwa shule pamoja na kuwa issue ya darasani pia ipo. Suala la darasani kuna pass mark, unatakiwa kuwa na asilimia 50 wastani wa masomo yote kwa muhula. Hii inakua majaribio ya kila mwezi kwa kipindi cha muhula wastani wake unajumlishwa na mtihani wa mwisho wa muhula ukigawa kwa mbili kwa kila somo halafu wastani wa kila somo unajumlishwa kwa pamoja na kupata wastani wa jumla. Ukikutwa unavuta bhangi ama sigara inabidi ukatafuta shule nyingine. Ninachoweza kusema tu kuwa labda alikutwa na vimwana na hilo pia ni kosa kubwa hata wakizifuma barua za wasichana ikiwa bahati yako mbaya unafukuzwa.
 
Wakuu najua humu kuna classmates wake ndugu zake jamaa na Marafiki Kipi kilisababisha Jembe akafukuzwa Katoke Seminari?

Kipi huenda ndo sababu ya Mkemia kufukuzwa?
 
Katika vitu huwa sivielewi ni kwa nini hatupati mwangwi chanya kwa watu waliokuwa na mkemia kwamba alikuwa ni mtu mwema na Rahimu kabla hajawa hivi alivyo? Historia yake ikoje. Aliofanya nao kazi walikuwa wanamchukuliaje, wanafunzi wake walimpa jina gani la utani na wao walikuwa wanamuona ni mwalimu Bora ama walikuwa wanamuonaje. Somo lake lilipendwa na wanafunzi wake na wao waliwaalika wengine wafundishwe naye?
 
Katika vitu huwa sivielewi ni kwa nini hatupati mwangwi chanya kwa watu waliokuwa na mkemia kwamba alikuwa ni mtu mwema na Rahimu kabla hajawa hivi alivyo? Historia yake ikoje. Aliofanya nao kazi walikuwa wanamchukuliaje, wanafunzi wake walimpa jina gani la utani na wao walikuwa wanamuona ni mwalimu Bora ama walikuwa wanamuonaje. Somo lake lilipendwa na wanafunzi wake na wao waliwaalika wengine wafundishwe naye?
Umeeleza Vema sana ni Vigumu sana mtu kufukuzwa Seminari!
 
Back
Top Bottom