Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Master PLan ya Mji mpya wa Singapore

Nimekuwa na chuki sana dhidi ya serikali hii hasa wiki hii. Nitarudi kucomment kwenye hili ntakapokuwa sawasawa.
 
Nakubaliana na wewe mwalimu wangu Anna kuhusu upangaji wa miji, lakini kitu hapa cha msigi ni kuanza kwa awamu kwa mfano katika maeneo mengi hapa nchini bado watu wanaendelea na ujenzi holela bila initiative yoyote ya serikali kuu ama serikali za mitaa kuzuia kwanza ujenzi holela huu, mimi napendekeza ufumuaji wa awamu kwa mfano tukianza na Dar es salaam tuzuie ujenzi huo na tufumue maeneo yaliyojengwa bila mpango, serikali iwe na fund maalumu itakayowajengea hao wakazi nyumba nzuri kama fidia na nyumba zitakazojengwa kwenye maeneo yaliyobomolewa itakuwa investment ya serikali kwa utaratibu wowote kwani wataalamu tunao wengi tuu hatuhitaji watu kutoka nje, jambo lingine la msingi ni transparency katika ufanyaji kazi wa serikali utafanya wananchi waamini itachotaka kufanya kwa mfano wakati serikali inasema kwenye mradi wa Kigamboni wananchi walishirikishwa mwakilishi wa wananchi yaani Mbunge anasema wananchi wake hawakushirikishwa hii inawachanganya sana wananchi tuweke kando siasa tufanye kazi Anna then tutafanikiwa. Hii itatufanya tuwe na uwezo mkubwa wa ukusanyaji kodi katika nyumba kwani kodi nyingi haikusanywi kutokana na nyumba hizi kuwa hazijulikani.
 
Mojo wa Dar es salaam Unatia aibi kwa uholela wake. Wiki iliyopita nilikuwa na wageni Wangu toka marekani. Dereva wetu akaamua kutumia short cut toka mnazi mmoja kwenda mlimani mwenge kwenye soko la cultural souvenirs ilikuwa aibu na mmoja akaamua kusema hapa ili muweze kuwa na mji mzuri " you have to bomb Dar es salaam and rebuild a new city.
 
Profesa shida ya nchi yetu ni kutokutii sheria zilizopo na kutojali mipango tuliyojiwekea. Inasikitisha kuona miji mingi nchini ikikua kwa kasi-holela...kila mtu anajenga anavyotaka na hakuna mamlaka inayojishughulisha kuzuia hali hiyo.

Kama ulivyosema kupanga ni kuchagua. Nyie mliopewa nafasi ya kusimamia miji yetu ndiyo mnapaswa kuhakikisha sheria zilizopo zinafuatwa na kila raia. Pia wizara yako na halmashauri au manispaa zijitahidi kupima, kuuza na kusimamia uuzaji ardhi hasa za mijini kwa wananchi kuliko kuachia kila mtu auze kiholela hali inayopelekea ujenzi holela kuendelea kuwa tatizo kwenye miji yetu.

Asante sana Ehud umesema ambayo yanatakiwa kufanywa na mamlaka husika kwa mfano wakati Waziri Magufuri anasema nyumba zilizojengwa ndani ya hifadhi ya barabara zibomolewe mwajili wake Rais pamoja na Waziri Mkuu wanasema awe na huruma, sheria haina huruma kama umeivunja lazima ikuadabishe bila kubagua na hapo ndipo watu wote watafuata sheria.
 
Mimi binafsi nachelea kusema mbona mnahangaika na Dar tu nendeni Arusha Mwanza mbeya na Moshi Ili mjenge miji ya kisasa isije ikawa kama Dar na kuanza kuplan upya wakati mji ukiwa umejaa.
 
Kingine mama Tibaijuka nashauri eneo la mji mpya wa Kigamboni lipanuliwe ikiwezekana lifike Mto Rufiji. Hii itasaidia kuwa na mipango endelevu ya kuupanua mji huo kwa miaka mingi ijayo. Inabidi tupange kuwa na mji utakao panuka kwa miaka 100 ijayo bila kumbomolea mtu nyumba yake wala kununua shamba la mtu. Huu mtindo wa kuchora kimji kiduchu utadhani tunajenga miji ya watu binafsi umeshapitwa na wakati. Tuwe na mtazamo wa kujenga "Johannesburg" yetu ya hapa Tanzania. Huu mji mpya wa Kigamboni ulitakiwa kwa uchache ufike maeneo ya mto rufiji na kupita na watu wazuiliwe kuyaendeleza kiholela maeneo hayo kunazia sasa.
 
mama, naona hiyo ni ndoto nyingine unataka kutuaminisha! kama tu mpango wako wa kubomoa majumba yaliyojengwa katika hifadhi ya bahari umeshindwa hiyo ndoto ya Kigamboni itatimizwa kweli??!!!
mimi huwa nakasirika nikitaka kwenda beach kupunga upepo napata taabu kuingia huko. mijumba imejengwa na kuunganishwa na chochoro zote zimezibwa!!! tuambie hivi bahari na beach zetu zimebinafsishwa kwa wenye mapesa???!!!
 
Kuendeleza Bagamoyo na Kigamboni na kuiacha Dar ya katikati ni sawa na kununua shati na viatu vipya wakati suruali ni midabwada!
 
Hata sielewi kilichowavutia ktk master plan ya Singapore kwasababu kwenye dunia ya kwanza hicho ni kitu cha kawaida yaani safari zote mnazochoma pesa za walala hoi kwa kutembea kundi kubwa mmejifunza master plan! Hivi hatuna architecture engineer tanzania? Nafikiri tatizo ni serikali isiyokuwa na mipango, ufisadi na uvivu wa kujituma, nchi inazalisha wasomi kibao kwenye kilimo Lakini watu wanakufa njaa hili nalo tunataka watu waje kutufundisha kulima! Ni kitu gani tunachoweza Kama watanzania? Gossip na ngonjera, tanzania itajengwa na sisi watanzania, Hakuna nchi duniani iliyojengwa na wageni.

Nimewahi kujiuliza maswali mengi sana juu ya viongozi wetu ikafika kipindi nikajiuliza kama wana macho au ni vipofu coz safari zote wanazo kwenda ninadhani hawajawahi kuiga ata kitu kimoja uzalendo tunao sema tunao me huwa ninahisi tuna ujinga na si uzalendo huwezi sema wewe ni mzalendo wakati inchi yko inaibiwa huku unangaa macho tu ala unajidai or nimeona master plan ya fulani hii nikuto kujitambua vimesha pitwa na wakati hiyo ni mitumba ya master plan weona tengeneza chakwako kizuri zaidi ya hicho serakali haina sababu ya kujisumbua nyiye tangenezeni miundo mbinu miziri wekeni plan ya barabara za kupita magari ya miaka 60 ijayo siyo plan ya 1972 iliyo pita.weken plan tu na point kwamba mtu aruhusiwi kugusa ni kitu kidogo sana wala hakihitaji computer kufikiri ,plan za maji kila kitu ambacho ni muhimu katika maisha ya uhai.
mkisha fanya hivyo wapeni wana nchi plan hapa lazima jengo liwe hivi lazima vitafanyika hivyo hivyo kama mtakuwa na macho coz hamnaga macho jengo linajengwa karibu na ofisi zenu mnakuja kusema eti or apo mwisho ni gorafo nane mwisho or kumi mwisho wakati mtu yupo ya kumi na nne yni mnakera adi watu tunatamanigi kuingia ndani ya vichwa venu. Mkisafiri angaliyeni wala msiwambiye nyiye mmefanya vip nyiye semeni hawajama wamekose kitu kimoja sisi tutafanya hivi wezenu wanatamani kubomoa wafanye vizuri zaidi sisi tunataka kutamani matapishi mnakera dah kama vile hatunaga macho na hata wasiyo kuwa na macho wana afadhali.
Hivi mnajuwa mnakera sana mnawafundisha ma bibi afya na mabwana afya lakini pita kariakoo vyakula vipo chini pita kwenye ofisi zenu mjini kuna matangazo usifanye biashara hapa watu wanafanya kama hampo naomba itengwe siku moja kila mtu aombe mungu kwa imani yake na lugha yake labda mta funguka macho .
Na yote haya matatizo yanatokana na watukuwa na matumbo makubwa kama vile mtaishi miaka 3,000
Watoto wapeni elimu inatosha siyo kuwapa pesa za laana hazita wasaidia watakuja kuliangamiza hili taifa. mungu awafunguwe macho na fikra ili muachane na fikra za kuiga vitu ambavyo wezetu wana vikataa. kama hatuna uwezo tujenge ata nyumba za majani ziwe kwenye plan zitapendeza tu kitu kinacho takiwa ni plan tu atutaki ndoto za alinacha au abunuwasi
 
Why Kigamboni? Nikiangalia Resources zinazokwenda hapo sipati justification.

La swali la msingi, tunataka kufanya Land Reclamation Tanzania? Kwa nini?
Na kama hatuhitaji, kwa nini mlienda kujifunza?

Kuna case moja ya TZ na mikaratusi Australia nayo ilikuwa hivi hivi

Uvivu wa kusoma na kuelewa, naombeni watanzania tuwe tunasoma kila neno aliloandika mtu halafu unalichambua na ku-comment sio kukurupuka tu kama wewe mada hii ni muhimu sana, unatia aibu.
 
1:Muheshimiwa Prof Anna Tibaijuka vipi kuhusu lile ghorofa la kariakoo uliloahidi kuwa litavunjwa kutokana na kutokukidhi vigezo, mbona kimya kimetanda na jengo bado lipo tu?

2: Serikali inamipango gani makini juu ya upangaji miji kwenye mikoa mingine tofauti na Dar ambayo imeanza kuonyesha dalili za kupanuka kwa haraka kutokana na ongezeko la watu au kutokana na kuongezeka kwa vivutio vya kiuchumi ili kuepuka hapo baadae mikoa hiyo isijekuwa na poor planning kama Dar es salaam?

Kwa hili la GHOROFA, Mafisadi wameiweka serikali pamoja na mama Tibaijuka MFUKONI. Hakuna anayefurukuta. Jengo litaendelea kuwepo tu!
 
Mama Anna Tibaijuka,

Nakushauri kuwa Serikali ijitowe katika huu mradi na iwawachie "real estate developers" wa Kimataifa, wenye uzoefu wa hizi kazi.

Serikali yetu haina uzoefu wa hizi kazi na historia inatuonesha Serikali imeshindwa ku-manage mradi wowote wa maana wa kibiashara. Hata NHC inawashinda ni uozo mtupu, ilhali majumba yalikuwa ya kudhulumiwa watu.

Ikiwa Serikali imeshindwa kuendesha viwanda vya umma, leo itaweza kuendesha project ya "magnitude" ya jiji? Jiulize.

Tusipoteze wakati, tuwawachie wenye utaalaam, na uzoefu wafanye haya mambo, wazo ni zuri, watendaji hatuna, tuna wizi tu Tanzania.

Leo ni zaidi ya miaka 6 tunasikia hii lelemama ikiimbwa tu, hebu ondoeni ukiritimba muwape wenye uwezo, kama hamjui pa kuwapata mnaweza wasiliana na mimi kwa PM.
 
ukitaka watu wafunguke wabeep kwenye suala la ardhi; mama Tibaijuka tunaomba leo ufanye majumuisho ya hoja hizi; maana nyingi zinaitupia lawama serikali kwa kutokuwa na kipaombele cha upimaji wa ardhi; miradi ya ardhi imekuwa ya wakurungezi wa wizara yako; leo hii nikitaka kiwanja nikija hapo nikutane na wakurugenzi wako jioni hi hii nitakuwa nimeshakipata cha msingi ni uchakavu wangu tu mfukoni ; tunasubiri mrejesho Mh Waziri Tafadhali...
 
Hii habari ya mji wa Kigamboni mbona maneno mengi vitendo sifuri? Yaani mpaka sasa ndio tupo kwenye hatua ya kuahidiwa kusaidiwa na watu wa Singapore! Je, ni aina gani ya msaada tunayotaka? What was our plan kabla wasingapore hawajaahidi kutusaidia? What are the timelines of implementation?
 
Mama Anna Tibaijuka,

Nakushauri kuwa Serikali ijitowe katika huu mradi na iwawachie "real estate developers" wa Kimataifa, wenye uzoefu wa hizi kazi.

Serikali yetu haina uzoefu wa hizi kazi na historia inatuonesha Serikali imeshindwa ku-manage mradi wowote wa maana wa kibiashara. Hata NHC inawashinda ni uozo mtupu, ilhali majumba yalikuwa ya kudhulumiwa watu.

Ikiwa Serikali imeshindwa kuendesha viwanda vya umma, leo itaweza kuendesha project ya "magnitude" ya jiji? Jiulize.

Tusipoteze wakati, tuwawachie wenye utaalaam, na uzoefu wafanye haya mambo, wazo ni zuri, watendaji hatuna, tuna wizi tu Tanzania.

Leo ni zaidi ya miaka 6 tunasikia hii lelemama ikiimbwa tu, hebu ondoeni ukiritimba muwape wenye uwezo, kama hamjui pa kuwapata mnaweza wasiliana na mimi kwa PM.
mkuu hapa ndiyo umechoma penyewe; kuna watu ndani ya serikali watafaidika na mradi huu kamwe serikali haitajitoa kwanza wana ugomvi na halmashauri ya wilaya ya Temeke nani asimamie mradi huu. Hii ndiyo Tanzania bwana....
 
Hii habari ya mji wa Kigamboni mbona maneno mengi vitendo sifuri? Yaani mpaka sasa ndio tupo kwenye hatua ya kuahidiwa kusaidiwa na watu wa Singapore! Je, ni aina gani ya msaada tunayotaka? What was our plan kabla wasingapore hawajaahidi kutusaidia? What are the timelines of implementation?
wameshawaahidi wananchi kuwalipa 35,000 kwa 1 sqm ya mraba, nyumba 700,000 kwa 1 Sqm. sasa kumbe bado hata hawajawatafuta wawekezaji. Juzi Jumamosi wafanyakazi wa mama Tibaijuka wametimuliwa na mapanga pale mtaa wa Kifurukwe, wakurya wamewaambia wasiwaone tena maeneo yao ; mama anadanganywa na madiwani kwamba wananchi eti wameshirikishwa. kila mtu ameshakuwa msanii nchi hii.
 
Lakini mh. Kwanini mumeshindwa kuboresha huu mji tulionao sasa hivi na munaanza kutafuta mpya wakati bado hamjachelewa? Tunahitaji tuone mabadiliko hapa tulipo sasa, Hizi sheria ndogondogo za miji zinafanya kazi?

Mtu kuweka maeneo ya mjini vibanda, parking ziko ndani ya barabara ukipita maeneo yote ya mjini sehemu za kupita watu na magari zimepakiwa gari na barabara inakua finyu. Majumba mjini yamekua kama magovu je hakuna sheria ya kuwaagiza wamiliki kuyarekebisha kila kipindi inapofika?
aafu pia kwa nini hawawalipi watu fidia stahiki? tatizo ni kwamba kuna uhuni unaendelea usioshirikisha wananchi wa uuzaji wa ardhi, sisi hatuwezi kukubali kuacha ardhi yetu bila kushirikishwa na kulipwa fidia stahiki. tunapenda kufuata vitu vya nje ila utekelezaji waloufanya hao wenzetu hatuufuati.
 
Back
Top Bottom