kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,685
Hata sielewi kilichowavutia ktk master plan ya Singapore kwasababu kwenye dunia ya kwanza hicho ni kitu cha kawaida yaani safari zote mnazochoma pesa za walala hoi kwa kutembea kundi kubwa mmejifunza master plan! Hivi hatuna architecture engineer tanzania? Nafikiri tatizo ni serikali isiyokuwa na mipango, ufisadi na uvivu wa kujituma, nchi inazalisha wasomi kibao kwenye kilimo Lakini watu wanakufa njaa hili nalo tunataka watu waje kutufundisha kulima! Ni kitu gani tunachoweza Kama watanzania? Gossip na ngonjera, tanzania itajengwa na sisi watanzania, Hakuna nchi duniani iliyojengwa na wageni.
..."yaani safari zote mnazochoma pesa
za walala hoi kwa kutembea kundi kubwa"...mkuu umenena haswa...
...safari za viongozi wa TZ nje ya nchi imekuwa kero kubwa kwa walipa kodi..., na habari za uhakika mwezi huu wa sita mama huyu, atakwenda Uingereza kwa ziara ya kikazi, pia rais JK ATAKUWA NA ZIARA huko huko Uingereza, na kufuatiwa ziara ya Makamu wake G. Bilal, na baadaye WIZIRI MKUU Mizengo Kayanza Peter Pinda !
...huu ni ufujaji wa kodi za wananchi.... "wakirudi wanakuja na Master Plan nyingine ya miji mipya"