Masikini Manji, hii ndio Bongo!

Masikini Manji, hii ndio Bongo!

Huko Ndani kavaa KOTI na suti yake kali au kaivua maana kuna joto kali kule au yupo ktk ac?
 
Kenya si Tanzania mkuu, nyumbani ni nyumbani hata kama kichakani. Manji ajifunze kuheshimu dola.alidhani anapambana na makonda yule wa mtandaoni.si vema kubishana na dola na hasa inapokua kwenye operesheni ngumu kama hizi kwa kutegemea ukwasi ulionao
Hivi Dangote bado hajafikaKenya?....
 
Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Kwa akili yako kabisa eti manji yupo ndani. Mnachekesha sana
Hahahaha... Yani wabongo wengine akili zenu asikae ndani yeye nani,
 
Wewe unaongea hujui madhara ya kuondoka matajiri katika nchi, mpaka leo Uganda inabembeleza wafanyabiashara wake waliohama kwenda Uingereza na Canada enzi ya Raisi Iddi Amin lakini wapi, wameondoka na nguo zao lakini kwa sasa wengi wao ni wafanyabiashara wakubwa katika nchi hizo. Wafanyabiashara, wawekezaji na hata wananchi wanapenda nchi salama na inaendeshwa katika misingi ya haki na sheria. Tizama mfano wa nchi iliyo karibu ya zimbabwe wananchi wake wengi wamekuwa wakimbizi Afrika ya kusini.
Ni kweli tunahitaji matajiri lakini wawe ni wale wasiokuwa na hata harufu tu ya kujihusisha na biashara hii haramu!
 
Toweni ujinga kudanganya hapa nani kakwambia yupo ndani? Tumia akili kuwaza na sio tumbo

Ujinga ni pale unapopinga hoja bila vielelezo! km unajua hayumo ndani basi pinga kwa ushahidi otherwise na wewe ni wale wale tu! kwa akili ya kawaida tu angekuwa ametoka tungeshamuona kwenye media, na hv mtumiaji akikoswa ile kitu kwa siku moja anavyokuwa anatepeta sipati picha sasa hv ana hali gani!!!
 
Nasisitiza hekima kuu kutumika ktk michakato inayosimamiwa na wanasiasa kwa maslahi ya taifa sasa na baadae..

Tukilejea njia zilizotumiwa kwenye kinachoitwa primitive accumulations of capital yapo mengi ya kujifunza.

Kuna level ya ufanyabiashara,uwekezaji na ujasiliamali mtu akifanikiwa kufika anapaswa kuheshimiwa,kuhenziwa na kupewa misaada ya kimkakati hasa kwa kuzingatia athari za uwekezaji wake katika uchumi na taifa kwa ujumla.Mfano: Ulipaji wa kodi,Ajira rasmi na zisizo rasmi,Mzunguko wa fedha.
Kwahiyo unaamini kwamba vitu kama hivyo inafaa tufanyiwe sisi malofa lakini mtajiri wao ndo wenye haki kisheria kubembelezwa hata wakipata tuhuma mbaya kama hizi za mihadarat?
 
Nahuo ndo ukweli mbona akna dangote,billgates,caros slim wanaheshimu serikali zao Kwani hawa ni akina Nani? Najua hwawez amin saiv ila baadae wataamin tu.... Halafu mwenyenchi angekuwa kama wanavofikiria wao makonda angeshitakiwa lakini KWA magufuli hahaaaa... WAKAJIANDAEE
Kwani hawezi shitakiwa mahakama za nnje
 
Lakini ajifunze kuheshimi mamlaka. Asubiri siku chadomo wakibahatisha kupata madaraka, mwaka 3035 ndiyo aendeleze dharau zake
Ndo umeandika nini sasa. Kukaa kimya nibusara sana kuliko kuonyesha ujinga wako mbele zawatu.
 
Wewe unaongea hujui madhara ya kuondoka matajiri katika nchi, mpaka leo Uganda inabembeleza wafanyabiashara wake waliohama kwenda Uingereza na Canada enzi ya Raisi Iddi Amin lakini wapi, wameondoka na nguo zao lakini kwa sasa wengi wao ni wafanyabiashara wakubwa katika nchi hizo. Wafanyabiashara, wawekezaji na hata wananchi wanapenda nchi salama na inaendeshwa katika misingi ya haki na sheria. Tizama mfano wa nchi iliyo karibu ya zimbabwe wananchi wake wengi wamekuwa wakimbizi Afrika ya kusini.

Tunapenda matajiri lakini sio wa kutuharibia vijana wenzetu...... km ni hzo hela zao chafu waende nazo huko huko tutabaki na ufukara wetu!
 
Back
Top Bottom