Mashine 6 za kuzalisha umeme Kituo cha Ubungo 1 zapata hitilafu, Naibu Waziri atoa maelekezo kwa TANESCO

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Naibu Waziri Nishati, Judith Salvio Kapinga ametembelea vituo vya Kuzalisha Umeme, Ubungo 1 na Ubungo 2 ili kuona hali ya uzalishaji wa umeme katika vituo hivi kwa maelekezo ya Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko.
IMG-20230929-WA0017.jpg

Naibu Waziri anazungumza
Kwenye Kituo cha Ubungo 2, mashine zipo tatu na kila moja inaweza kuzalisha Megawati 43, kati ya hizo moja haifanyi kazi na ipo kwenye matengenezo.
IMG-20230929-WA0016.jpg

Kituo cha Ubungo 1 kuna mashine 12, zinazofanya kazi ni 6 ambazi kila mashine inazalisha Megawats 42 hadi 43, nyingine zipo kwenye matengenezo, hivyo nimewalekeza TANESCO kuhakikisha wanakuwa na mpango wa marekebisho ya muda mfupi, wa kati na mrefu.

Matengenezo ya muda mfupi yafanyike kwa wakati ili huduma ya umeme iweze kupatikana kwa wakati, hivyohivyo kwa mipango ya marekebisho ya muda wa kati na mrefu.

Kitendo cha kuwa na mashine moja nje ya huduma ni kupoteza umeme mwingi.
IMG-20230929-WA0019.jpg

Leo pia kwa bahati mbaya Kituo cha Ubungo 1 kimezimika umeme kuanzia usiku hadi muda huu (mchana wa Septemba 29, 2023), mitambo sita ambayo inatakiwa kuzalisha umeme nayo haizalishi.

Wataalam wapo ‘site’ wanahakikisha umeme unarejea, nimewaambia TANESCO kuwa ndani ya saa mbili kituo kiwe kimerejea kufanya kazi na ikishindikana watafute mbadala ya kuhakikisha ndani ya saa sita zijazo uzalishaji wa umeme uwe umerejea kama kawaida ili upatikanaji umeme uimarike.
 
Yaani kati ya machini 15, 7 hazifanyi kazi. Hii ni karibu nusu ya uwezo wa ufuaji umeme haupo.
Hapa kuna uzembe mkubwa kama sio tatizo la bajeti ya maintenance yaani Tanesco haikupata pesa za kigeni kuagiza spea za maintenance.
 
Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amelipa Shirika la Umeme (TANESCO) saa mbili kurudisha uzalishaji wa umeme kwenye kituo cha kuzalisha umeme cha Ubungo I ambacho kimezimika umeme kuanzia usiku mpaka sasa hivi na mitambo sita inayotakiwa kuzalisha umeme kwa sasa hivi haizalishi na hivyo kupelekea baadhi ya Wananchi kukosa umeme.

Kapinga amesema hayo leo September 29,2023 alipotembelea Makao Makuu ya TANESCO, Ubungo Jijini Dar es salaam “Tumefika hapa na leo kwa bahati mbaya pia kituo cha Ubungo I kimezimika umeme kuanzia usiku mpaka sasa hivi na mitambo sita inayotakiwa kuzalisha umeme kwa sasa hivi haizalishi lakini Wataalamu wako saiti wanahakikisha inawaka”

"Nimewaelekeza TANESCO kuhakikisha ndani ya masaa mawili kituo kile kinarudi katika uzalishaji na kama hakitorudi kwenye uzalishaji watafute njia mbadala ya kuhakikisha ndani ya masaa sita yajayo kituo hiki kinarudi kwenye uzalishaji ili hali ya upatikanaji umeme iweze kuimarika”

“Mashine zile sita zinazalisha kati ya megawati 42 hadi 43 lakini kwasababu zimepata hitilafu hizo megawati ziko nje, nimewaagiza warudishe kituo kwenye uzalishaji na umeme upatikane kwa Wananchi”
 
Ukiona nchi bado inahangaika na zimwi la umeme/nishati kwa miaka zaidi ya 60 basi ujue nchi hiyo hata kiuchumi haiko imara. Mengine yanabaki ni unafiki wa data za wanaojiita wasomi wa uchumi ila uhalisia ni hsli mbaya.
 
Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amelipa Shirika la Umeme (TANESCO) saa mbili kurudisha uzalishaji wa umeme kwenye kituo cha kuzalisha umeme cha Ubungo I ambacho kimezimika umeme kuanzia usiku mpaka sasa hivi na mitambo sita inayotakiwa kuzalisha umeme kwa sasa hivi haizalishi na hivyo kupelekea baadhi ya Wananchi kukosa umeme.

Kapinga amesema hayo leo September 29,2023 alipotembelea Makao Makuu ya TANESCO, Ubungo Jijini Dar es salaam “Tumefika hapa na leo kwa bahati mbaya pia kituo cha Ubungo I kimezimika umeme kuanzia usiku mpaka sasa hivi na mitambo sita inayotakiwa kuzalisha umeme kwa sasa hivi haizalishi lakini Wataalamu wako saiti wanahakikisha inawaka”

"Nimewaelekeza TANESCO kuhakikisha ndani ya masaa mawili kituo kile kinarudi katika uzalishaji na kama hakitorudi kwenye uzalishaji watafute njia mbadala ya kuhakikisha ndani ya masaa sita yajayo kituo hiki kinarudi kwenye uzalishaji ili hali ya upatikanaji umeme iweze kuimarika”

“Mashine zile sita zinazalisha kati ya megawati 42 hadi 43 lakini kwasababu zimepata hitilafu hizo megawati ziko nje, nimewaagiza warudishe kituo kwenye uzalishaji na umeme upatikane kwa Wananchi”
Umeme hamna.
Mnatoa ajira kwa connection.
Alafu mnataka vijana wajiajiri.

Mungu atete na Serikali ya CCM.
Kuna muda wananchi watachoka na kitanuka, maandamani hayataisha, Serikali shughulikieni hili swala haraka.
 
Naibu Waziri Nishati, Judith Salvio Kapinga ametembelea vituo vya Kuzalisha Umeme, Ubungo 1 na Ubungo 2 ili kuona hali ya uzalishaji wa umeme katika vituo hivi kwa maelekezo ya Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko.

Naibu Waziri anazungumza
Kwenye Kituo cha Ubungo 2, mashine zipo tatu na kila moja inaweza kuzalisha Megawati 43, kati ya hizo moja haifanyi kazi na ipo kwenye matengenezo.

Kituo cha Ubungo 1 kuna mashine 12, zinazofanya kazi ni 6 ambazi kila mashine inazalisha Megawats 42 hadi 43, nyingine zipo kwenye matengenezo, hivyo nimewalekeza TANESCO kuhakikisha wanakuwa na mpango wa marekebisho ya muda mfupi, wa kati na mrefu.

Matengenezo ya muda mfupi yafanyike kwa wakati ili huduma ya umeme iweze kupatikana kwa wakati, hivyohivyo kwa mipango ya marekebisho ya muda wa kati na mrefu.

Kitendo cha kuwa na mashine moja nje ya huduma ni kupoteza umeme mwingi.

Leo pia kwa bahati mbaya Kituo cha Ubungo 1 kimezimika umeme kuanzia usiku hadi muda huu (mchana wa Septemba 29, 2023), mitambo sita ambayo inatakiwa kuzalisha umeme nayo haizalishi.

Wataalam wapo ‘site’ wanahakikisha umeme unarejea, nimewaambia TANESCO kuwa ndani ya saa mbili kituo kiwe kimerejea kufanya kazi na ikishindikana watafute mbadala ya kuhakikisha ndani ya saa sita zijazo uzalishaji wa umeme uwe umerejea kama kawaida ili upatikanaji umeme uimarike.
Mshaambiwa mitambo imechakaa inatakiwa mipya mkasema wakati wa Magufuli ilikuwa haikatiki ndio Sasa life span yake imefika mwisho.

Hakuna Cha maelekezo kinachotakiwa ni pesa ikanunuliwe mipya.
 
Hivi January yale marekebisho aliyosema anafanya ni yapi?

Iweje tupoteze mashine 10+ kituo 1?

Contingency ni ipi?

Je ikitokea tunapigwa kama Ukraine tutaweza washa umeme kweli?
Alidai Trilioni 4 mkasema atazipiga haya kawasheni mitambo chakavu maana alipewa bil.500 tuu
 
Back
Top Bottom