Hii Vita ukiniambia Israel kashindwa nitakataa, pia ukiniambia Iran kashidwa nitakataa.
Kushindwa au kushinda Vita inategemea na malengo. Je malengo ya Israel yalikua ni yapi na malengo ya Iran yalikua ni yapi?
Israel alikua na malengo ya kuzuia nuclear programs ndani ya Iran(hili kafanikiwa kwa asilimia kubwa sababu ni kweli program imerudi nyuma)
Israel alikua na malengo ya kupiga millitary facilities zote, hili kashindwa sababu bado zipo millitary facilities nyingi hazikuguswa.
Israel alikua na lengo la regime change, hili nalo kafeli sababu bado regime ipo.
Hivyo kwa ujumla Israel hakushinda.
Tukija kwa Iran, lengo lake ni kuizuia Israel isiendelee kuikalia gaza kimabavu, lakini bado Israel anaikalia. Hivyo Iran kashindwa.
Lengo kubwa la Iran ni kuifuta Israel, lakini wameshindwa kufanya hivyo. Kama Iran ingekua imeshinda au inaeelekea kushinda basi wasingekubali ceasefire, sababu wangekua wanaenda kutimiza lengo lao la miaka yote la kuifuta Israel.
Hivyo kiujumla Iran nae hakushinda