Marekani: Msichana mweusi apigwa risasi

Marekani: Msichana mweusi apigwa risasi

Alichonya askari na alichokuwa anataka kufanya kufanya Dada mwenye hakuna tofauti...huwezi kuokoa maisha ya mtu mmoja kwa kuua mtu mmoja.
Ni bora hata angepiga risasi angani kama onyo,kuliko kumshindilia mi risasi minne.
Nawaza kwa sauti
 
Hata kama aliyeuwawa alikuwa kashika kisu bado sio sababu ya kummiminia risasi nne, hoja ilikuwa kum-neutralise aidha au kwa kushoot not to kill. And one round was good enough to neutralise her.
Kweli tena sema wao wajua kuua tu
 
Ni bora hata angepiga risasi angani kama onyo,kuliko kumshindilia mi risasi minne.
Nawaza kwa sauti
Angalia video mkuu, hakukuwa na namna ya kupiga risasi hewani wala hata risasi ya mguuni isingesaidia, Tusiwe watu wa haraka kutoa opinion wakati hatujafanyia analysisi ya real situation, Kisu kilikuwa umbali wa sentimita 1
 
Angalia video mkuu, hakukuwa na namna ya kupiga risasi hewani wala hata risasi ya mguuni isingesaidia, Tusiwe watu wa haraka kutoa opinion wakati hatujafanyia analysisi ya real situation, Kisu kilikuwa umbali wa sentimita 1
Sawa sawa nishaangalia mkuu
 
Halafu sasa ukute ugomvi ulikuwa kugombania mwanaume!

Hao waamerika weusi hovyo sana,hawataki kuishi kwa kufuata sheria huku wanataka sheria ziwalinde wanalalamika mbona weupe hawafanyiwi hivi wanashindwa kujua hao weupe wana-stick sana kufuata sheria hata kama nao wanavunja sheria siyo kwa kiwango kikubwa kama wao.
Mkuu unasema hivyo labda kwa sababu hayo mambo yanafanyika huko kwengine ila yangekuwa yanatokea huku kwetu pengine ungeeleza kwa vyengine kabisa matukio kama hayo, hata kama hawafuati sheria ila ukiangalia wanayoyafanya polisi huko ni zaidi ya raia kutofuata sheria. Niliona video moja polisi janamume zima limemkalia mwanamke kwa juu na kumbana mikono mbele ya mwanae mdogo analia tu, nilipatwa na hasira sana maana kwanza mwanamke asingeweza kumzidi nguvu yule polisi na pia hakuwa na silaha yeyote hivyo sikuona ulazima wa kufanya unyama ule ndio maana nasema wanachofanya polisi huko ni zaidi ya hilo la kwamba Blacks hawafuati sheria.
 
Wakati naandika ile comment nilikua sijaiangalia video.

Nimeandika tu nikaenda kucheki video.

Caller ameripoti kuna watu wanatishia kuchoma visu watu wengine, askari anashuka tu kwenye gari (hata hakupata muda wa kutoa onyo) kuna binti anakula mweleka mpaka nguo inapanda juu, kisha kuna jamaa anampiga teke huyu binti aliyeanguka.

Video ikawa inaenda kwa slow motion. Na kwa angle iliyochukuliwa inaonyesha huyu jamaa anarusha teke at the same time binti mwenye kisu ndiyo anampelekea kisu mwenzake mwilini. Mhanga wa kisu nyuma yake amezuiwa na gari so kurudi nyuma kusingemsaidia.

Majirani na wakazi wa eneo hilo wanaamini askari ana makosa.
Tukiwa wakweli itatusaidia sana hapa askari yupo sahihi maana alikua hana option nyingine zaidi ya kumpiga risasi

Niwape pongezi jeshi la polisi la marekani kwa kuwawekea camera kwenye sare za jeshi la polisi maana isingekuwepo hii video dunia ingeaminishwa kuwa polisi kauwa mtu mweusi na mambo yangekua magumu sana jeshi la polisi la Tanzania tunaweza kujifunza kitu hapa
 
Tukiwa wakweli itatusaidia sana hapa askari yupo sahihi maana alikua hana option nyingine zaidi ya kumpiga risasi

Niwape pongezi jeshi la polisi la marekani kwa kuwawekea camera kwenye sare za jeshi la polisi maana isingekuwepo hii video dunia ingeaminishwa kuwa polisi kauwa mtu mweusi na mambo yangekua magumu sana jeshi la polisi la Tanzania tunaweza kujifunza kitu hapa
Lengo la huyo polisi nae lilikuwa kuuwa au kuokoa maisha? Maana nashindwa kuelewa ni kipi kilichomfanya akatumia risasi zote hizo?
 
Lengo la huyo polisi nae lilikuwa kuuwa au kuokoa maisha? Maana nashindwa kuelewa ni kipi kilichomfanya akatumia risasi zote hizo?
Yote mawili yalikua malengo maana ukitizama video hakupata muda wa kutoa onyo kwa yule alieshika kisu so akaona apige risasi amjeruhi lakin majeraha yamesababisha afe so jibu alikua na malengo yote mawili
 
Angalia video mkuu, hakukuwa na namna ya kupiga risasi hewani wala hata risasi ya mguuni isingesaidia, Tusiwe watu wa haraka kutoa opinion wakati hatujafanyia analysisi ya real situation, Kisu kilikuwa umbali wa sentimita 1
Wengi wanachonga tu ila ukiwaweka kwenye position ya huyo dada wa Pink kwa sekunde moja ukawatoa hawaandiki tena walichoandika. CNN wamefanya kazi nzuri sana duniani ya brainwashing.
 
Hivi askari waliokuwepo hapo walishindwa kumdhibiti mtoto wa kike mmoja mpaka risasi itumike...?
Ukiangalia video clip utaona kabisa kwamba polisi alikuwa mbali kidogo na huyo attacker alikua keshainua kisu kabisa tayari kushambulia. It was a split-second reaction kutoka kwa polisi otherwise watu wawili wangefariki

Labda swali liwe ni kwanini risasi nne? kwanini hakumtungua mguuni? kwanini afyatue ili kuua na sio warning shot angani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom