Marekani imelitungua puto la kichina

Marekani imelitungua puto la kichina

USA ni mfano halisi namna binadamu kutoka sehemu mbalimbali za dunia wanavyoweza kuishi pamoja kwa amani bila ubaguzi wala chuki baina yao.
U.S.A hakuna chuki na ubaguzi ? Duuuh!
 
Ungefuatilia huo utaalamu wa kuunda hizo electronics kautolea wapi, na usishangae kwenye kiwanda ukamkuta top ni mzungu toka US., nikupe hadithi moja

Rafki yangu alipoenda china kufanya masters fulani alipoingia darasani alimkuta mmarekani ndio lecture akashangaa sana hivi china wanakwama wapi ata elimu ya vyuo vikuu wanakodi walimu toka US?

US hawana mkwara jana wameshatungua puto huko ingekuwa china ingekuwa wanakimbizana tu vipi tulipige au tuliache, tukifyatua itakuwaje, US halazi damu
Unavyo ielezea China ni kwa namna ya kufurahisha kwa kweli 😀
 
Too late. Wachina washasave info. Ila Wachina nao bwana. Wamechemsha, walitakiwa waliset ili lisionekane.
Walifanya makusudi na ni fedheha na aibu kwa US kwamba walishindwa kuliona mapema?
 
Ndio mkuu, ndio mana lile Puto halikuchukua muda limepasuliwa pasuliwa ili kama kuna mchina aje juu alete ngebe zake aone
Ndio maana wewe sio Rais wala kiongozi yoyote yule wa taifa kubwa especially China, hauna ufahamu wowote kuhusu masuala ya uongozi haujui madhara ya maamuzi mabaya kwa taifa na dunia kwa ujumla.

Kuongoza nchi sio kuji ongoza mwenyewe kutokana na hisia zako zinavyo kusukuma.
 
Unajuaje wakat wanauingilia mambo yalikuaje !!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo ni taarifa ya maafisa wa wizara ya ulinzi (DOD). Kulingana na taarifa, USAF iliingilia mfumo wa mawasiliano uliobebwa na hilo puto ili kuzuia ukusanywaji wa taarifa nyeti.

Ndege za kiintelijensia zimeonekana mara kadhaa zikichunguza na kukusanya taarifa karibu kabisa na hilo puto kabla ya utunguaji.
 
Hakika ni "The land of opportunity"
USA ni nchi ya kipekee sana. Watu kutoka nchi mbalimbali wameshika nafasi kubwa na wanatambulika kama raia wa Marekani.
Unaweza ukamkuta mhindi kutoka india lkn ni mkuu wa polisi jimbo fulani.
 
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha BCC wamarekani walikuwa wakingojea lifike eneo la bahari ili kuepusha madhara wa waliko chini ikibukwe puto hilo lilikuwa juu ya eneo la nuclear plant hivyo mabaki yake (debris) yangeweza kuleta madhara.

USSR View attachment 2506511View attachment 2506512
US ndio bure kabisa yaani Balloon ambalo halina sihala za kujilinda unatuma ndege unayoisifia ndio bora kabisa F22 kwenda kuliangusha, wakati angetuma hata helicopter tu ingetosha 🤣🤣🤣🤣
 
"Wenye nchi" Marekani ni kina nani??
Hiyo huwa ni danganya Toto tu,wenye nchi huwa tayari wameweka agenda mezani,so hao huwa wanatakiwa kupita humohumo sio kuja na agenda zao,na ukijifanya mjuaji utake kuwasahihisha Basi fasta wanaku r.i.p. Hivyo kwa marekani hata mwendawazimu inimradi ajue kuongea ,kusoma na ku saini mikataba Basi!,kwa sbb kila kitu unakikuta mezani ww ni kusaini tu .
 
US ndio bure kabisa yaani Balloon ambalo halina sihala za kujilinda unatuma ndege unayoisifia ndio bora kabisa F22 kwenda kuliangusha, wakati angetuma hata helicopter tu ingetosha 🤣🤣🤣🤣
Unatakiwa utumie kifaa ambacho hata adui yako akiona anaona hauna utani. Kitu kinatakiwa kiwe jivu kbsa. Siku nyingine hata akituma ndege anajua itabaki kuwa majivu
 
Nchi gani yenye utu?
  • Russia inaipiga Ukraine sasa hivi.
  • Mwanamke hajafunika kichwa wamemyonga.
  • China anataka kuipa Taiwan
  • Tanzania, watu walikuwa wanapotea, wengine wanateka na kuawawa na watu wasiojulikana.
  • Nchi za kiarabu wadada wa kazi za ndani wanauliwa kila kukicha.
  • Sudan, watu wamegawana nchi na ni waislam 100%
  • Somalia Alshabab hao
  • Nigeria unakutana na boko Haram
Wapi ni salama waende wakaishi?
Brunei
 
Unatakiwa utumie kifaa ambacho hata adui yako akiona anaona hauna utani. Kitu kinatakiwa kiwe jivu kbsa. Siku nyingine hata akituma ndege anajua itabaki kuwa majivu
Puto lipo nchini kwako halina ulinzi wowote unatumiaje f22🤣🤣🤣 lingekuwa na ulinzi si ndo wangechanganyikiwa kabisa? Hala wana kuja na a lame excuse eti lilikuwa juu ya nuclear facility 🤣🤣🤣 ni mjinga tu ndio ataamini hii, US kwa masatelaiti hakuliona toka awali na wanasema limekuwapo US kwa.muda wa.kutosha? Kama limetokea China hadi kufika US koooote huko hawakuliona?.

Usiwe maandazi tumia akili kidoooogo
 
Mchina ndio future ya hii dunia. Atakuja kalia kiti cha marekani soon baada ya hii vita.
China atasubiri sana kwasababu
1. China teknolojia yake ni copy na paste. Hawana ubunifu kbsa. Software karibia zote tunatumia za Marekani. Hiyo simu unayotumia inatoka China ila Operating system ni ya Marekani.
2. China inaongozwa na watu wenye akili za kichina lkn Marekani inaongozwa na watu waliotoka katika mataifa mbalimbali. Kuna viongozi wenye asili ya tanzania, china, japani, india, israel, uingereza, iraq n.k wote wapo Marekani wanafanya kazi
3. Mashirika makubwa dunia kama UN, FAO, IMF n.k yapo Marekani.
4. Nguvu ya USD. Ukitaka kununua kitu chochote lazima utumie dola ya marekani. Ushawahi kununua kitu kwa Yuan mtandaoni?
5. Misaada ya kifedha na dawa. Marekani anatoa sana misaada ya kifedha na wakati mwingine anasamehe mikopo.
6. Entertaiment
Mieleka, muziki, Kikapu, kampuni kubwa za filamu zipo Marekani tena zinatumia teknolojia kubwa. Hollywood. Wanamuziki wakubwa duniani wapo Marekani wote hao wanakusanya pesa kutoka kwenye nchi mbalimbali wanapeleka kwao. Hata Wacheza filamu wakubwa wa China wapo Marekani kwa sasa.
Umejiunga Tiktok?
 
Back
Top Bottom