China atasubiri sana kwasababu
1. China teknolojia yake ni copy na paste. Hawana ubunifu kbsa. Software karibia zote tunatumia za Marekani. Hiyo simu unayotumia inatoka China ila Operating system ni ya Marekani.
2. China inaongozwa na watu wenye akili za kichina lkn Marekani inaongozwa na watu waliotoka katika mataifa mbalimbali. Kuna viongozi wenye asili ya tanzania, china, japani, india, israel, uingereza, iraq n.k wote wapo Marekani wanafanya kazi
3. Mashirika makubwa dunia kama UN, FAO, IMF n.k yapo Marekani.
4. Nguvu ya USD. Ukitaka kununua kitu chochote lazima utumie dola ya marekani. Ushawahi kununua kitu kwa Yuan mtandaoni?
5. Misaada ya kifedha na dawa. Marekani anatoa sana misaada ya kifedha na wakati mwingine anasamehe mikopo.
6. Entertaiment
Mieleka, muziki, Kikapu, kampuni kubwa za filamu zipo Marekani tena zinatumia teknolojia kubwa. Hollywood. Wanamuziki wakubwa duniani wapo Marekani wote hao wanakusanya pesa kutoka kwenye nchi mbalimbali wanapeleka kwao. Hata Wacheza filamu wakubwa wa China wapo Marekani kwa sasa.
Umejiunga Tiktok?