Pamoja na maelezo yako marefu, hebu tusaidie majibu ya maswali haya machache:Very 'interesting' observation...'interesting' indeed....
Kwanza nisahihishe neno moja ....wajihudhuru.......>>>>>>>>>>>>wajiuzulu
Ikiwa mtu unataka kufanya analysis kwa jambo ni vema uwe sober na objective....usitangulize hisia zako mbele kwani hisia hizo zitakupofusha katika uchambuzi wako...Hilo la kusema eti 'mawaziri wanakosa ile hali ya kujiamini' ni hisia zako wewe.....Aidha kwamba eti Nape 'anawasilisha malalamiko ya Braza la Mawaziri' ni hisia na pia matamanio yako ukiombea hali iwe hivyo...
Ukweli ni kuwa ukitaka kuchambua suala la Mhe. Nape ni kuangalia taratibu, kanuni na utendaji wa Baraza la Mawaziri ...ukifanya hivyo utagundua kuwa Mhe. Nape alitenda kosa la insubordination (au dharau mbaya) kwa bosi wake ambaye ni Rais...
Kama Rais ametamka kuwa wewe 'Makonda chapa kazi', Nape hakuwa na sababu tena ya kuendelea na kamati ile 'uchwara'...natumia neon 'uchwara' kwa kuwa kamati ile in the first place haikustahili iwepo...
Kamati ile imeteuliwa na Waziri kuchunguza issue ya Mkuu wa mkoa....utaona kabisa kuwa kuna walakini hapa....Ninavyoelewa mimi mabosi wa wakuu wa mikoa ni Rais na Waziri Mkuu na siyo mtu mwingine....Kwa maoni yangu hao ndio wanaopaswa kuunda kamati...Halafu wajumbe wa kamati ni lazima wawe na nyadhifa nzito wakiwemo majaji na hata makamishna wa polisi na wengineo wazito na siyo waandishi wa habari wenye 'maslahi' na suala lenyewe....kamati ni lazima iwe huru.
Kamati 'uchwara' ya Nape ilihusisha wengi wa waandisi wa habari wa print media, je wakati suala lenyewe linahusu televisheni....hii ni kasoro nyingine ya kamati hiyo 'uchwara'...
Jambo jingine Mhe. Nape hata hiyo kamati 'uchwara' haijatoa taarifa yeye alishasema kuwa Mhe. Makonda amenajisi tasnia ya habari...maana yake ni kuwa tayari ameingilia kazi za kamati hiyo aliyoiunda mwenyewe...
Jambo jingine ni namna waandishi wa habari wenyewe walivyokosa weledi kwa kutanguliza kuwa mhe. Makonda 'alivamia' Clouds bila hata ripoti ya kamati haijatolewa...
Aidha hakukuwa na sababu yoyote kutoa taarifa ya upande mmoja bila kumhoji mtuhumiwa ambaye ni Mhe. Makonda....
Kwamba Mhe. Makonda 'hakuhojiwa' na kamati hiyo 'uchwara' ni jambo lililotarajiwa na wajuzi wa mambo...Mhe. Makonda asingeweza kukubali 'kuhojiwa' na kamati hiyo isiyo na kichwa wala miguu.
Suala hili la Mhe. Makonda na Clouds limejaa ushabiki zaidi kuliko uhalisia...uko ushabiki wa kisiasa, ushabiki wa chuki kutoka makundi mbalimbali na pia njama...
Mtu hahitaji kuwa mjuzi wa mambo kutambua kuwa yapo makundi mbalimbali yenye njama dhidi ya Mhe. Makonda....namna suala hili lilivyochukuliwa inadhihirisha kuwepo kwa njama hizo...
Makonda anaweza kuwa ana makosa kwenda clouds na kuingia studio, lakini namna wabaya wake walivyolishupalia jambo hili wamekosa 'weledi' wa kuandaa njama....
Kinachojitokeza ni kuwa makundi ambayo ni wabaya wa Mhe. Makonda wanafanya shinikizo kwa Rais ili amuondoe Makonda....Kiongozi mzuri hawezi kukubaliana na shinikizo la aina hiyo....
Mhe. Makonda anaweza akaondolewa Dar es Salaam lakini siyo katika kipindi hiki, anaweza kuondolewa 'wakati muafaka' siyo sasa...
Wako wanaosema kuwa Nape ni shujaa...binafsi sioni hivyo....Mhe. Nape alifanya insubordination kwa Rais kwa hiyo kutumbuliwa kwake ni halali....huwezi kwenda kinyume na Rais halafu ukaachwa...
Na katika historia ya nchi hii hakuna Waziri ambaye ameondolewa madarakani aliyewahi kujaribu kuitisha mkutano wa waandishi wa habari kuelezea kuondolewa kwake kwenye Baraza la Mawaziri kama alivyofanya Mhe. Nape....Hili nalo ni tukio la aina yake, na inaonesha kwamba Mhe. Nape bado hajaiva sawasawa kiutendaji na kisiasa.
1. Nape ni mara ya kwanza ameteuliwa kuwa waziri. Amekuwa na uzoefu wa mwaka na ushee kabla ya kufikwa na kilichomfika. Kama kulikuwa na tatizo (kiutendaji) katika ku handle suala la Makonda kulikuwa na ulazima wa Rais kumwondoa wakati msimamo wake Rais katika suala hilo aliuonyesha wakati tayari Nape ameishaunda hiyo kamati na iko field?
2. Katika mazingira haya, ni nani alipaswa kumpigia simu mwenzake katika hili; mkuu wa nchi au Nape?
3. Pamoja na kwamba haijathibitishwa kimahakama, lakini watu wengi wanakichukulia kile kitendo cha Makonda aka Bashite kuvamia Clouds kwa mujibu wa sheria ya matangazo ya kielektroniki kuwa ni kosa la jinai. Kwa kuzingatia kuwa kitendo hicho cha Bashite kilikuwa kimeongeza kosa jingine la kijinai kudaiwa kutendwa na mteule huyo wa Rais, hatua zilizochukuliwa na Nape zilikuwa na faida au athari gani kwa serikali inayotokana na watu? Je, haiwezi kuwa kwamba motive behind kwa Nape ilikuwa ni kuihami serikali dhidi ya mtazamo hasi kutoka kwa wananchi?
4.Nape alipofika Clouds ni kweli alitamka kuwa kama kweli kile kitendo kimefanyika kama ilivyoelezwa na Ruge basi itakuwa ni kunajisi uhuru wa habari. Swali linaweza kuwa kama kauli hii ya Nape ni mbaya mno kustahili kuondolewa katika nafasi ya uwaziri, unamaanisha mtazamo wa mteule wake ni kinyume cha kauli hiyo ya Nape? Na kama ni ndiyo wewe pia unakubaliana hivyo kwamba kuvamia na mabunduki studio kwa lengo la kushinikiza kurushwa kwa habari yako ya kuchafua mtu sio kunajisi uhuru wa habari?
5. Unadai ile kamati ilikuwa ni "uchwara" kwa kuwa ilihusisha wajumbe wengi ambao wako katika "print media". Hoja hii nimeona imeletwa pia na msemaji wa Yanga. Labda utusaidie, mtu anayesoma shahada ya kwanza, hata stashahada ya uandishi wa habari hasomi "broadcasting"? Kwa mujibu wa "hadidu" rejea kuu ya kamati iliyoundwa na Nape, kamati ilitakiwa kupata maelezo ya upande wa pili; hapa unataka kutuaminisha wahariri wa aina ya Balile, Jesse Kwayu na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo wasingeweza kutimiza hilo kwa uweledi?
6. Swali hili liwe la mwisho japo yako mengi. Ni swali la mwisho lakini lina uzito wa kipekee kwa kuwa naona hoja iliyo katika swali hili mmekuwa mkii expose sana. Umedai kuwa kuna watu wabaya wa Makonda aka Bashite wanafanya shinikizo ili Rais amwondoe. Na unadai kuwa watu hao "wabaya" wanatumia makosa yaliyofanywa na Makonda (ni bahati nzuri wewe mwenyewe unakiri kuwa ni makosa) kumshinikiza Rais amtumbue lakini unasema huu sio wakati mwafaka.
Je, ni kwanini unadhani sasa pamoja na kelele hizi zinazopigwa kiasi cha kuharibu kabisa image ya Rais na taasisi yenyewe ya urais, sio wakati mwafaka kwa Rais kuchukua hatua ili kulinda heshima yake mwenyewe, taasisi ya urais pamoja na thamani ya kura ambazo watu walimpigia?