Hoja nzuri kaka, lakini ukimsoma Nape kwa makini ni kana kwamba alikuwa anawasilisha malalamiko ya Baraza la Mawaziri, ni kama inaonyesha Mawaziri wengi hawako happy na jinsi Raisi anavyoendesha nchi, sio kwa issue ya Makonda pekee bali pia kwenye maamuzi mbalimbali, yaani Mawaziri wanakosa ile hali ya kujiamini, issue ya Makonda kuendesha zoezi la Madawa ya kulevya bila kumshirikisha Waziri mwenye dhamana ni tatizo kubwa
Nape amekuwa kama Kondoo wa kafara na sababu kubwa ni kuwa Nnape sio mwoga hivyo aliamua kupambana na Magufuli kupitia vituko vya Makonda
Shida kubwa iko kwa mawaziri wenzie, je watamuunga mkono nao wajihudhuru? Ili kuonyesha hawakubaliani na jinsi Raisi anavyoendesha nchi
Very 'interesting' observation...'interesting' indeed....
Kwanza nisahihishe neno moja ....wajihudhuru.......>>>>>>>>>>>>wajiuzulu
Ikiwa mtu unataka kufanya analysis kwa jambo ni vema uwe sober na objective....usitangulize hisia zako mbele kwani hisia hizo zitakupofusha katika uchambuzi wako...Hilo la kusema eti 'mawaziri wanakosa ile hali ya kujiamini' ni hisia zako wewe.....Aidha kwamba eti Nape 'anawasilisha malalamiko ya Braza la Mawaziri' ni hisia na pia matamanio yako ukiombea hali iwe hivyo...
Ukweli ni kuwa ukitaka kuchambua suala la Mhe. Nape ni kuangalia taratibu, kanuni na utendaji wa Baraza la Mawaziri ...ukifanya hivyo utagundua kuwa Mhe. Nape alitenda kosa la insubordination (au dharau mbaya) kwa bosi wake ambaye ni Rais...
Kama Rais ametamka kuwa wewe 'Makonda chapa kazi', Nape hakuwa na sababu tena ya kuendelea na kamati ile 'uchwara'...natumia neon 'uchwara' kwa kuwa kamati ile in the first place haikustahili iwepo...
Kamati ile imeteuliwa na Waziri kuchunguza issue ya Mkuu wa mkoa....utaona kabisa kuwa kuna walakini hapa....Ninavyoelewa mimi mabosi wa wakuu wa mikoa ni Rais na Waziri Mkuu na siyo mtu mwingine....Kwa maoni yangu hao ndio wanaopaswa kuunda kamati...Halafu wajumbe wa kamati ni lazima wawe na nyadhifa nzito wakiwemo majaji na hata makamishna wa polisi na wengineo wazito na siyo waandishi wa habari wenye 'maslahi' na suala lenyewe....kamati ni lazima iwe huru.
Kamati 'uchwara' ya Nape ilihusisha wengi wa waandisi wa habari wa print media, je wakati suala lenyewe linahusu televisheni....hii ni kasoro nyingine ya kamati hiyo 'uchwara'...
Jambo jingine Mhe. Nape hata hiyo kamati 'uchwara' haijatoa taarifa yeye alishasema kuwa Mhe. Makonda amenajisi tasnia ya habari...maana yake ni kuwa tayari ameingilia kazi za kamati hiyo aliyoiunda mwenyewe...
Jambo jingine ni namna waandishi wa habari wenyewe walivyokosa weledi kwa kutanguliza kuwa mhe. Makonda 'alivamia' Clouds bila hata ripoti ya kamati haijatolewa...
Aidha hakukuwa na sababu yoyote kutoa taarifa ya upande mmoja bila kumhoji mtuhumiwa ambaye ni Mhe. Makonda....
Kwamba Mhe. Makonda 'hakuhojiwa' na kamati hiyo 'uchwara' ni jambo lililotarajiwa na wajuzi wa mambo...Mhe. Makonda asingeweza kukubali 'kuhojiwa' na kamati hiyo isiyo na kichwa wala miguu.
Suala hili la Mhe. Makonda na Clouds limejaa ushabiki zaidi kuliko uhalisia...uko ushabiki wa kisiasa, ushabiki wa chuki kutoka makundi mbalimbali na pia njama...
Mtu hahitaji kuwa mjuzi wa mambo kutambua kuwa yapo makundi mbalimbali yenye njama dhidi ya Mhe. Makonda....namna suala hili lilivyochukuliwa inadhihirisha kuwepo kwa njama hizo...
Makonda anaweza kuwa ana makosa kwenda clouds na kuingia studio, lakini namna wabaya wake walivyolishupalia jambo hili wamekosa 'weledi' wa kuandaa njama....
Kinachojitokeza ni kuwa makundi ambayo ni wabaya wa Mhe. Makonda wanafanya shinikizo kwa Rais ili amuondoe Makonda....Kiongozi mzuri hawezi kukubaliana na shinikizo la aina hiyo....
Mhe. Makonda anaweza akaondolewa Dar es Salaam lakini siyo katika kipindi hiki, anaweza kuondolewa 'wakati muafaka' siyo sasa...
Wako wanaosema kuwa Nape ni shujaa...binafsi sioni hivyo....Mhe. Nape alifanya insubordination kwa Rais kwa hiyo kutumbuliwa kwake ni halali....huwezi kwenda kinyume na Rais halafu ukaachwa...
Na katika historia ya nchi hii hakuna Waziri ambaye ameondolewa madarakani aliyewahi kujaribu kuitisha mkutano wa waandishi wa habari kuelezea kuondolewa kwake kwenye Baraza la Mawaziri kama alivyofanya Mhe. Nape....Hili nalo ni tukio la aina yake, na inaonesha kwamba Mhe. Nape bado hajaiva sawasawa kiutendaji na kisiasa.