Marafiki wa Nape: Kwanini Nape hakutulia?

Marafiki wa Nape: Kwanini Nape hakutulia?

Hoja nzuri kaka, lakini ukimsoma Nape kwa makini ni kana kwamba alikuwa anawasilisha malalamiko ya Baraza la Mawaziri, ni kama inaonyesha Mawaziri wengi hawako happy na jinsi Raisi anavyoendesha nchi, sio kwa issue ya Makonda pekee bali pia kwenye maamuzi mbalimbali, yaani Mawaziri wanakosa ile hali ya kujiamini, issue ya Makonda kuendesha zoezi la Madawa ya kulevya bila kumshirikisha Waziri mwenye dhamana ni tatizo kubwa
Nape amekuwa kama Kondoo wa kafara na sababu kubwa ni kuwa Nnape sio mwoga hivyo aliamua kupambana na Magufuli kupitia vituko vya Makonda
Shida kubwa iko kwa mawaziri wenzie, je watamuunga mkono nao wajihudhuru? Ili kuonyesha hawakubaliani na jinsi Raisi anavyoendesha nchi
Stereotype reasoning, look for the big picture of things, education can help you increase your vision , but can not give you sight
 
"Waberoya, post: 20318452, member: 11515"]Kwa nini hakutulia??? au kulikuwa na ulazima wa yeye kusema kitu?
Taharuki na kuondolewa kwake ilikuwa ni fedheha iliyopelekea taharuki na kupoteza sehemu ya hekima.
what if kama Magufuli alikuwa anataka ampe nafasi ingine ya serikalini?
Mazingira aliyomuondoa hayampi heshima. Kuliko kupewa 'pipi' ni afadhali aendelee na majukumu yake ya ubunge.
Nyuma ya pazia kuna nini ambacho Nape anahisi kachukiwa sana wakati kitu alichofanya is obvious ilikuwa lazima ajiuzulu yeye , bila hata kuondolewa.
Alitambua anachokifanya ni kumsaidia mh kama kiongozi mwenye dhamanaHakutambua alipogusa sipo
Hakukuwa na haja ya Kamati wakati mwisho wa matokeo ya kamati ni kupeleka report kwa Rais ambaye aliishaamua na kusema pale ubungo
Rais alizungumza baada ya kamati kuundwa si kabla. Nape hakutambua Rais hapendezwi na kitendo!
Naamini rais sio malaika, wala sio kuwa Nape hana namba ya simu ya Magu kiasi ambacho wangeongea kuhusu hili swala na kupata baraka zake, kufanya jambo kama lile au kuendelea nalo likiwa linakinzana na bosi wako lina maana gani?? (tuache mihemko wengi tuna mabosi hapa)
Bosi hakuwahi kutoa kauli yoyote kuhusu RC wiki nzima na hata ilipotokea. Nape alichukua nafasi kama msaidizi wa Rais ambaye si lazima apate maagizo kama tarishi. Alijua kama kuna masahihisho ni mbele ya safari
Namna ya kudeal na lile swala ilikuwa lazima kuwe na kamati? au angebadili methodology? what was the mission behind? tuwaze nje ya box
Ni utamaduni uliokuwepo na Nape alikuwa anakwenda na 'blue print'
Lakini nani angemchunguza RC ambaye alisimama na kusema kamishna huenda anachukua milioni za wauza unga? Nani anamchunguza ikiwa alitoa ruhusa ya watu kupigwa na hakuna aliyeshtuka? Nani atamgusa ikiwa aliweka watu ndani kwa tuhuma tu hata bila ya ushahidi?
1. Rais awe kwenye wakati mgumu wa maamuzi
2. au Nape aondoke yeye
Kwanini kwa RC kuwe na maamuzi magumu ikiwa alichukua maamuzi mahumu kwa waziri wa mambo ya ndani na swahiba yake Kitwanga?
Imani yangu na msimamo wangu, Makonda ataondoka kupitia mahakama kwa sasa, kuvamia clouds was the best opportunity ya kumuweka kwenye majengo ya mahakama....ingemlazimisha rais kumuondoa
Sina uhakika ikiwa media zimekemewa leo, sasa huko mahakamani nani angeweza? Kuna jambo gumu katika mfumo wet hilo lazima tukubali.
 
Nape akiwa Waziri wenye dhamana ameitendea Haki nafasi hio.

Wakulaumiwa moja kwa moja sasa sio NAPE ni RAIS MAGUFULI anayemlinda BASHITE MAKONDA kwa gharama zote.
Anayoyatenda RC WA DAR PAUL MAKONDA sasa ni zaidi ya BANYAMLENGE, Na hao wawili DINGI NA MWANAE Wakiachwa bila kukosolewa WATALINGIZA TAIFA LETU KWENYE MATATIZO MAKUBWA.
 
Tumemsikia rais kasema nini

move ya Nape nchi zingine ashazua vita!!
 
Hlafu ujue jambo moja. Nape alifanya uchunguzi na kujua ni nini hasa kilichotekea ndipo akatoa maamuzi. Yeye Magufuli alitoa maamuzi bila kufanya uchunguzi na kujua undani wa scandal yenyewe ulikuwaje! Hivyo Nape alitumia nafasi yake kama waziri kumsaidia rais kutekeleza majukumu yake!

Nape hawezi kumpigia simu rais? kwa nini wako mbali hivyo?
 
Taharuki na kuondolewa kwake ilikuwa ni fedheha iliyopelekea taharuki na kupoteza sehemu ya hekima.Mazingira aliyomuondoa hayampi heshima. Kuliko kupewa 'pipi' ni afadhali aendelee na majukumu yake ya ubunge.Alitambua anachokifanya ni kumsaidia mh kama kiongozi mwenye dhamanaHakutambua alipogusa sipoRais alizungumza baada ya kamati kuundwa si kabla. Nape hakutambua Rais hapendezwi na kitendo!Bosi hakuwahi kutoa kauli yoyote kuhusu RC wiki nzima na hata ilipotokea. Nape alichukua nafasi kama msaidizi wa Rais ambaye si lazima apate maagizo kama tarishi. Alijua kama kuna masahihisho ni mbele ya safari
Ni utamaduni uliokuwepo na Nape alikuwa anakwenda na 'blue print'
Lakini nani angemchunguza RC ambaye alisimama na kusema kamishna huenda anachukua milioni za wauza unga? Nani anamchunguza ikiwa alitoa ruhusa ya watu kupigwa na hakuna aliyeshtuka? Nani atamgusa ikiwa aliweka watu ndani kwa tuhuma tu hata bila ya ushahidi? Kwanini kwa RC kuwe na maamuzi magumu ikiwa alichukua maamuzi mahumu kwa waziri wa mambo ya ndani na swahiba yake Kitwanga?
Sina uhakika ikiwa media zimekemewa leo, sasa huko mahakamani nani angeweza? Kuna jambo gumu katika mfumo wet hilo lazima tukubali.

Mkuu, mtei alipotofautiana na Nyerere aliondoka asubuhi!!

nape alichelewa sana, hakutakiwa kusubiri kufukuzwa....
 
Hoja nzuri kaka, lakini ukimsoma Nape kwa makini ni kana kwamba alikuwa anawasilisha malalamiko ya Baraza la Mawaziri, ni kama inaonyesha Mawaziri wengi hawako happy na jinsi Raisi anavyoendesha nchi, sio kwa issue ya Makonda pekee bali pia kwenye maamuzi mbalimbali, yaani Mawaziri wanakosa ile hali ya kujiamini, issue ya Makonda kuendesha zoezi la Madawa ya kulevya bila kumshirikisha Waziri mwenye dhamana ni tatizo kubwa
Nape amekuwa kama Kondoo wa kafara na sababu kubwa ni kuwa Nnape sio mwoga hivyo aliamua kupambana na Magufuli kupitia vituko vya Makonda
Shida kubwa iko kwa mawaziri wenzie, je watamuunga mkono nao wajihudhuru? Ili kuonyesha hawakubaliani na jinsi Raisi anavyoendesha nchi
Rais anaendesha nchi bombaa kabisa na wala mawazir hawana shida kama unavyodai.
 
Hii hoja ipeleke lumumba pale ndo itakuwa na maana ya kudeal na masrahi ya chama c taifa
 
So mtoa mada ulitaka akae kimya kama taasisi au wizara nyingine zilizo kaa kimya juu ya swala hilo na mengine kabla ya hili? Ishu ya bashite kufoji cheti wizara gani au taasisi gani haijasikia na wahusika wamenyuti kama wamemwagiwa maji ya kwenye refrigerator. Je kunyuti kwao mpaka sasa kuna tija yoyote kwa Taifa? Bora hata huyu hajawa mnafiki kaamua kusema kweli na kweli itamlinda
 
mtoa mada inaonekana bado una yale mawazo ya zidumu fikra as mwenyekiti ambayo ni very nonsense
4 ur info nape did wat was really supposed to do.
and infact it's a message to u guys mnaoshi maisha ya kinafiki na ya kuigiza kumpendeza boss wako
pia usidhan hakujua nini kitamtokea isipokua hakua tayar kua mnafiki kisa uwaziri
historia itmhufadhia pazuri heshima yake.
I wish wote tue kama nape kwene utata kama huu
 
HARAKA YOTE ILIKUWA YA NINI HASA KUNA MTU ALIUAWA PALE AU KUNA MALI ILIPOTEA MPAKA KAMATI IPEWE SAA 24 KWA LIPI HASA?
TUSIPELEKWE NA MIHEMUKO NA JAZBA TUKASAHAU UKWELI NI KWAMBA NAPE ALIKUWA NA CHUKI NA MAKONDA KUANZIA KWENYE SUALA LA MADAWA ALIANZA KUMLAUMU HADHARANI KWAMBA ANAFANYA MAKOSA JAMBO AMBALO KIUTENDAJI SERIKALINI HALITAKIWI, LAKINI BADO NAPE ALITHIBITISHA PASIPO SHAKA KWAMBA ANATAKA MAKONDA AHARIBIKIWE KAMA ANGELIKUWA NA NIA KWELI YA KUTETEA WAAANDISHI WA HABARI KAMA ALIVYOJINADI ANGEANZA NA YULE DC ALIYEMUWEKA MAHABUSU MWANDISHI WA HABARI WA ITV IWEJE LEO MAKONDA KWENDA STUDIO IMEKUWA NONGWA MPAKA AUNDIWE TUME YA KUFANYA KAZI MASAA 24 IWE IMETOA REPORT??? HAPO MWENYE AKILI NA AELEWE HUU WEMA WA NAPE KWA WAANDISHI WA HABARI UMEANZA LINI WAKATI NI YEYE HUYOHUYO AMESIMAMIA MAGAZETI KADHAA KUFUNGIWA NA BUNGE LIVE KUONDOLEWA ?? UKWELI NI KWAMBA WAUZA MADAWA WALIMTUMIA NAPE VILIVYO NA AKATAKA KUTUHADAA KWAMBA ANATETEA WAANDISHI WA HABARI NI UWONGO WA WAZI AKADANGANYE WAJINGA WENZIE. MAKONDA NI KWELI HAKUWA SAHIHI LAKINI NGUVU KUBWA ILIYOTUMIWA NA WAZIRI INADHIHIRISHA WAZI KABISA NAPE HAKUWA NA NIA NJEMA KWA MAKONDA SASA KIBAO KIMEMGEUKIA YEYE MWENYEWE NA ANAVUNA ALICHOPANDA.

Yani maandishi yako tu nmekuona kama vile gongoti hata nmeshindwa kusoma, lakini nahisi umeandika pumba tupu. Nahisi pia hata mwanao akiona hii kitu lazima ajiulize maswali mengi juu yako. Mwenye akili atakuwa ameshajua wewe ni mtu wa aina gani. CCM OYEEEE OYEEE
 
Hebu jaribu tena kumsoma Mtoa mada!

Busara ni pamoja na kukubali lile usilolielewa na kusubiri,There after unarudi na tafakuri za kina juu ya suala husika.Ni ukweli mtupu kuwa hatupaswi kutetea makosa, Lakini ni kwanini Nnape asingesubiri kwa muda fulani ndipo alizungumzie hili lililotokea kwa mapana yake?.Au ilikuwa ni LAZIMA tu alizungumzie jana?.I think hiyo ndiyo dhana nzima ya thread na mengine baadhi.

Rejea concept ya Waberoya hapo juu "what if kama Magufuli alikuwa anataka ampe nafasi ingine ya serikalini ?".

Kwani lipi alilolisema baya mpaka asubiri mwezi upite au mwaka ndipo aseme. Wataka afate nyayo za taasisi na wizara nyingine ambazo mpaka sasa zinajipa mda kuzungumzia swala la bashite kufoji vyeti. Sisi nani katuroga mbona tuko hivi!!!
 
bado nawaza sana

IMGumeeleweka ila mliposhikwa na magu ndio shida
 
Kwani lipi alilolisema baya mpaka asubiri mwezi upite au mwaka ndipo aseme. Wataka afate nyayo za taasisi na wizara nyingine ambazo mpaka sasa zinajipa mda kuzungumzia swala la bashite kufoji vyeti. Sisi nani katuroga mbona tuko hivi!!!
Sijalogwa Mkuu!

Sikusema Nape angesubiri mpaka mwezi upite au mwaka upite,HAPANA!,Kanisome vizuri.Nilishauri kuwa kama angesubiri muda fulani (Unknown) upite ndipo azungumze kungeharibika nini?.

Kwani ilikuwa ni lazima azungumze jana na pengine siyo leo wala kesho?.
 
Nape alishaamua "enough is enough" to hell with Bashite! Alikuwa anatafuta mtaji wa kisiasa na ameupata sana!
 
Nadhani Magu na nape kulishaanza kuwa na ufa hata kabla ya uvamizi wa clouds media,kama umemsikiliza Magu leo alikuwa akimuongelea Nape kama vile kazi ilikuwa imemshinda siku nyingi au hakuwa hakipenda utendaji wake. Na dhahiri Nape alishaliona hilo siku nyingi ,so kila mtu alikuwa anamfanyia mwenzake timing.
 
Sijalogwa Mkuu!

Sikusema Nape angesubiri mpaka mwezi upite au mwaka upite,HAPANA!,Kanisome vizuri.Nilishauri kuwa kama angesubiri muda fulani (Unknown) upite ndipo azungumze kungeharibika nini?.

Kwani ilikuwa ni lazima azungumze jana na pengine siyo leo wala kesho?.

So taasisi kama takukuru na Necta mpaka sasa wanajipa muda juu ya swala la bashite, je kuna mwafaka wowote ? Kwako style hii ndiyo naye angefuata?
 
Sio lazima apate baraka za Rais ila kwa kuwa yeye (Nape) ni sehemu ya serikali na Rais ambae ndio mkubwa wake tayari alishaonyesha / kutoa tamko kuhusu hiyo issue kwamba serikali haiwezi kuzifanyia taarifa kutoka mitandao ya kijamii (maana yake hiyo ndo kauli ya serikali hata kama aliropoka) anapokuja mtu mwingine wa chini yake kuendeleza jambo lile lile wakati na yeye ni sehemu ya serikali huku tayari limetolewa tamko maana yake anapingana na serikali wakati na yeye akiwa ni sehemu yake. (angalia kwa jicho la kiplotokali bali usiangalie kwa kosa alilofanya Makonda ambalo kimsingi lipo wazi)
Protokali za kishenzi na kipuuzi hizo...msitumia hizo protokali kuficha madhaifu...tatizo ni kuishi kwa unafiki.

Ndiyo maana mtu mzima na PhD yake, anaonyeshwa yeye hafai, lakini bado analamba miguu ya mtu aliyem-devalue na kumwonyesha hafai!!

Ati mkubwa wake? Kwani mkubwa hakosei? Yeye ni nani? Mungu? Acheni hizo nyinyi. I never liked Nape, and I will never like him, but, I support what he did. Nape alisimamia kutekeleza majukumu yake. Sema, alikose kitu kimoja, alipaswa ajiuzulu baada tu ya rais kuongea zile pumba pale Ubungo. Hapo ningempa heshima zaidi. Siyo kama alivyofanya, ingawa kapata heshima yangu kiduchu.
 
Nape siyo mnafiki kwa hili. Kafanya kazi yake hawezi kukaa kimya kutetea maovu.
 
Back
Top Bottom