Mara ya mwisho uliona lini ......!!!?

Ndivyo nilivyofanya mimi. Hapa ana ujumbe kuwa Umati huu ni kwa kuwa fulani ni maarufu sana, anapendwa sana, anafaa sana n.k.

Kwa hiyo una admit kwamba wewe na serikali yako mliyojiweka madarakani hamna hizo sifa ndio maana katika mikutano yenu yoyote ile watu hawawezi kuja bila:-
1. kukodiwa magari ya kuwaleta uwanjani
2. kupewa tshirt, kanga, vitambaa,
3. kupewa elfu 5,000 - 10,000?
 
Wingi wa watu kuhudhuria mikutano sio lazima wawe wote wanakukubali. Hapo wapo mchanganyiko wengine ni wasikilizaji tu, wengine wa vyama vingine. Na NOTE kuwa hali ngumu ya maisha inawavuta watu wengi kuja kusikiliza kama kuna jipya la kuwaboreshea maisha na sio kwamba wataamini kila unalosema. Wanapima, wanachuja. Hivyo wingi wa mahudhuria si hoja.

wakati nipo primary kuna msemo nilifundishwa mpinga wengiiiii................................................. nyingine ni hii sauti ya wengi................... mtamalizia
 
Dah! Nimeungana nawe Utamaduni......Juu ya yote uliyoeleza na chuki dhidi ya huyu Kiumbe, bila shaka mtanzania yeyote reasonable ataelewa pasi kuhoji. I salute you mkuu.
 
Mhh kwa hiyo nyomi hawa jamaa wa Chechemee wanayo kila sababu ya kulia lia....
 
Ukiulizwa swali, angalia hilo swali limebeba ujumbe gani, usiangalie tu unaulizwa nini. Ndivyo nilivyofanya mimi. Hapa ana ujumbe kuwa Umati huu ni kwa kuwa fulani ni maarufu sana, anapendwa sana, anafaa sana n.k. Kama nimesoma au sikusoma usijali, angalia hoja tu. Ni katika kuchangia na kupeana facts na kuelimishana. Usipoelimika wewe, wapo watakaoambulia chochote katika mchango huu. Ahsante.

The truth is you expected mkuu wa nchi kuwa na mvuto wa namna hii. The TRUTH and FACT ni kuwa hana hata chembe ya mvuto pasipo wahudhuriaji ama kukodiwa, kupelekewa usafiri, kupewa tshirts, kanga, kofia etc au wahudhuriaji kuwa watoto wa shule za msingi wanaokwenda kuwaona wana muziki wa bongo flava. Lakini kwa sasa ni vyama vya upinzani vyenye mvuto mbele ya umma, anayepinga ukweli na uhalisia huu lazima ni mwendawazimu. Chama tawala kimepoteza mvuto, viongozi wa upinzani wana mvuto sana kwa wananchi kwa sababu hotuba zao zinagusa maisha ya watu. Kwa bara, Dr Slaa anaongoza akifuatiwa na Professor Lipumba na kwa visiwani ni Maalim Seif. Unaweza kukataa kwa sababu ni haki yako ya kimaumbile lakini huo ndiyo ukweli.

Ili CCM ipate wahudhuriaji lazima mkutano upigwe pampu na bongo flava na zawadi za bure kibao, tofauti na CHADEMA au CUF. Too shame!!!
 
Go to HELL. Huna shukrani. Hata kama kuna kasoro za kimaendeleo, nchi gani isiyokuwa na kasoro? unaangalia makosa tu huangalii mafanikio. Au ulinyimwa cheo.

Ka noma na iwe noma tu

wewe ni ms...e huyo mkwele wako kafanya nini ana mafanikio gani?

Ana nini cha kujivunia katika uongozi wake mpaka sasa?
 
umati kama huu ndo unawatia jambajamba wa-thithiemu,ngoja walale wala sie hatuwahamshi ,na muda si muda tunaenda kujipanga kusini ,hadi mwaka huu wataelewa kwanini nyoka hana kiuno.
 
Siku zote ukiwa muongo muongo na msanii ndio unapata umati wa watu kukusikiliza, hakuna cha zaidi.

Mara oooh Dowans ya Kikwete, mara ooohhh Mkuu wa mkoa kafa. Mara ooohhhh, nimeoa mke wa pili!

Duhhh! Hata Nyerere alikuwa akivuta umma mkubwa sana watu, lakini ikifikia kwenye utendaji ni ZERO.


Naona sasa mmeamua kumuunga mkono Rais wenu mkwere kwenye kuponda juhudi za nyerere!
 
Wingi wa watu kuhudhuria mikutano sio lazima wawe wote wanakukubali. Hapo wapo mchanganyiko wengine ni wasikilizaji tu, wengine wa vyama vingine. Na NOTE kuwa hali ngumu ya maisha inawavuta watu wengi kuja kusikiliza kama kuna jipya la kuwaboreshea maisha na sio kwamba wataamini kila unalosema. Wanapima, wanachuja. Hivyo wingi wa mahudhuria si hoja.

Hapo umeshindwa kuniconvice kabisaaaa!!! Ili ujue kuwa unapendwa ni lazima kwanza uangalie wangapi wako tayari kukusikiliza!! Unataka kuniambia kuwa tangu mwaka jana kwenye kampen watanzania hawajajua ipi pumba na upi ni mchele mpaka waendelee kufurika hivyo?? Lazima kuna kitu tofauti wamekiona kwa Slaa!! Kama unabisha wakataze wasihudhurie tuone!!
 
ole ole CHADEMA kama show ya Wacko Jacko jinsi watu walivyojaa... ole ole CHADEMA!!
 
huyo ndio Dr.wa ukweli Slaa
acha mchezo anatisha kila kona na kila angle
 
Siku zote ukiwa muongo muongo na msanii ndio unapata umati wa watu kukusikiliza, hakuna cha zaidi.

Mara oooh Dowans ya Kikwete, mara ooohhh Mkuu wa mkoa kafa. Mara ooohhhh, nimeoa mke wa pili!

Duhhh! Hata Nyerere alikuwa akivuta umma mkubwa sana watu, lakini ikifikia kwenye utendaji ni ZERO.
Hata ukisema wamiliki wa Dowans huwajui, hujui kama bei ya sukari imepanda mpaka uunde tume, unaweza kujaza watu kama hivi.
 
Naona sasa mmeamua kumuunga mkono Rais wenu mkwere kwenye kuponda juhudi za nyerere!

Labda alikuwa na juhudi lakini unaweza kuwa na juhudi kubwa sana ushindwe kufikia matarajio na uharibu kabisa, na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Nyerere, juhudi zake hazikuzaa matunda. Au kama unayajuwa/unayo mafanikio ya Nyerere tuwekee hapa tuyajadili.

Mimi nasema hakuna.
 
Hata ukisema wamiliki wa Dowans huwajui, hujui kama bei ya sukari imepanda mpaka uunde tume, unaweza kujaza watu kama hivi.

Naomba u-google na usome habari za UN kuhusu bei za vyakula duniani. Dunia nzima bei za vyakula zimepanda kwa miezi minane mfululizo.

JK aliliona hilo mapema na ndio akaanzisha kilimo kwanza. Au hujui maana ya kilimo kwanza?
 
Siku zote ukiwa muongo muongo na msanii ndio unapata umati wa watu kukusikiliza, hakuna cha zaidi.

Mara oooh Dowans ya Kikwete, mara ooohhh Mkuu wa mkoa kafa. Mara ooohhhh, nimeoa mke wa pili!

Duhhh! Hata Nyerere alikuwa akivuta umma mkubwa sana watu, lakini ikifikia kwenye utendaji ni ZERO.

Umelogwa vibaya...tafuta mganga akakuague....!
 
Back
Top Bottom