Mapinduzi yawe ni ya kilimo....

Mapinduzi yawe ni ya kilimo....

Hata sielewi mnachobishana lol

Mie bado naamini katika kilimo

Just because watu wengine walifeli walivyotegemea kilimo..it doesn’t mean na sisi tutafeli

Solution ni kuidentify the GAP ama makosa waliyofanywa wenzetu ..ndio tujipange ki stratergy

Pia tunahitaji mazao kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na mengine kuuza,then kilimo lazima kuwe na UZALISHAJI at maximum..

Hatuwezi kuwa na viwanda, kama kilimo hakijazalisha to this level..

Sasa utajenga viwanda,utatoa wapi malighafi ?

So,viwanda vinategemea kilimo,,,,

Kudismiss role ya kilimo kwenye uchumi,ni kua kwenye denial
 
Sehemu kubwa ya uchumi? Hilo pia halipo. Ukimwambia Mmarekani aachane na Soy beans, mahindi na ngano hawezi kabisa kukuelewa. Kilimo ni sehemu kubwa kabisa ya uchumi wa Marekani.

Kwa nini Tanzania iachane na kilimo kama sehemu muhimu ya uchumi wake wakati ina potential ya kulisha Africa Mashariki nzima?
Hivyo viwanda vitajengwa vizalishe vitu gani katika miaka 10, 15, hadi ishirini ijayo, vitakavyoweza kuhudumia sehemu kubwa ya uchumi wake?
Kilimo kinatakiwa kuboreshwa, si kidogo, ila sana tena kwa haraka zaidi kutuwezesha kuinua uchumi wetu haraka wakati viwanda vinaanzishwa. Kwa maana hiyo, kilimo kitaendelea kuwa muhimu sana kama ajira kwa waTanzania, na ndio maana kinatakiwa kiboreshwe haraka ili hawa watu wengi wainue maisha yao. Hatuwezi kuwa na viwanda kuajiri watu hao uliowasema, na wala hatuwezi kusubiri ndipo mabadiliko yapatikane katika maisha yao.
And you know what that 1% GDP means for the US!
Unalazimisha kutoelewa, 1% of GDP means 1% and nothing else. Inamaanisha katika kila pesa 100 ya pato la US pesa moja inatokana na kilimo. Kwa Tanzania ni karibia mara ishirini na Tano ya hiyo.
Not good.
 
Hata sielewi mnachobishana lol

Mie bado naamini katika kilimo

Just because watu wengine walifeli walivyotegemea kilimo..it doesn’t mean na sisi tutafeli

Solution ni kuidentify the GAP ama makosa waliyofanywa wenzetu ..ndio tujipange ki stratergy

Pia tunahitaji mazao kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na mengine kuuza,then kilimo lazima kuwe na UZALISHAJI at maximum..

Hatuwezi kuwa na viwanda, kama kilimo hakijazalisha to this level..

Sasa utajenga viwanda,utatoa wapi malighafi ?

So,viwanda vinategemea kilimo,,,,

Kudismiss role ya kilimo kwenye uchumi,ni kua kwenye denial
Unachochanya ni kuwa, kwa mfano umesema tunahitaji mazao kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kuuza. Hilo ni sawa, hakuna anayekataa, ila halihitaji watu wawili kati ya kila watatu washiriki kilimo.

Kuondoa hilo, itabidi uanzishe viwanda. Viwanda then, vitachochea kilimo and not vice versa.
 
Unachochanya ni kuwa, kwa mfano umesema tunahitaji mazao kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kuuza. Hilo ni sawa, hakuna anayekataa, ila halihitaji watu wawili kati ya kila watatu washiriki kilimo.

Kuondoa hilo, itabidi uanzishe viwanda. Viwanda then, vitachochea kilimo and not vice versa.

mie I believe opposite mkuu,

hao wa tatu wote each watalima nusu kwa ajili yao,

na nusu watapeleka kiwandani,

na wote tufanye hivyo,amen. LOLS.

..kuna kitu hujakielewa watu hawapingi kuwa na viwanda ,i

la position yake ni second after uzalishaji,

ukiwa na viwanda yes utavutia watu walime,lakini kama hela yako yote umeweka kwenye maviwanda,utapata wapi hela ya kilimo??

najua ni utoto kudhania hivyo lakini ni kweli kuzalisha kwanza,then upate malighafi na hela ya production
 
dhana ya 'competative advantage' mh ameshindwa kuitumia. kilimo ndio mkombozi wa nchi hii. mengine baadae. japo alikuwepo, amesahau viwanda enzi ya mwl.
 
Unalazimisha kutoelewa, 1% of GDP means 1% and nothing else. Inamaanisha katika kila pesa 100 ya pato la US pesa moja inatokana na kilimo. Kwa Tanzania ni karibia mara ishirini na Tano ya hiyo.
Not good.

Sasa kama unaona nalazimisha, si acha tu kulazimishwa?
Ukweli ni huo, hata kilimo kingechangia 0.5 ya GDP ya uchumi wa Marekani, hakuna kichaa ambaye angependekeza Marekani kuachana na kilimo. It is simple as that.
Halafu unaleta mlinganisho huo na nchi kama Tanzania yenye viwanda vingapi vile? 3 060 alivisema juzi Rais, na havijulikani viko wapi na wala vinazalisha nini! Huko ni kulinganisha kweli?
 
Huelewi concept.
Mtu mmoja alime korosho Mtwara nzima, mwingine Pwani nzima halafu kuwe na viwanda vya mafuta ya korosho, kubangua na kupakia korosho, na kutengeneza pombe za ulaka au juice ya mabibo.
Pia mbolea, mashine za mashamba yake, repair, banks na huduma za wafanyakazi wa shamba hilo kubwa na viwanda vinavyozunguka, mahoteli, etc .. ndiyo vitachochea ukuaji wa uchumi wa Mtwara au Pwani.

Haya mambo ya heka tatu na vyama vya ushirika mtakaa miaka mia mbili hamuendi popote.
Kuna watu ninawajua wana heka hizo tatu za mikorosho na mafanikio yao najua hata ukae miaka 20 huwezi kuwafikia.


Endelea kuishi kijima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ukiwa na viwanda yes utavutia watu walime,lakini kama hela yako yote umeweka kwenye maviwanda,utapata wapi hela ya kilimo??
Jinsi ulivyoweka maneno hayo hapo juu. Angalia hii issue kitaifa bila serikali kutumia fedha kuanzisha viwanda. Ondoa wazo kuwa serikali itaanzisha viwanda.
Kwa mfano, kuna kiwanda cha sukari kinajengwa na kuna mualiko wa watu kujiunga kuanzisha mashamba ya miwa. Tayari hicho kiwanda kimesisimua sugarcane production.

Katika plantations za miwa kutazuka biofuel production if possible na ndivyo Brazil wanavyofanya. Industry stimulating large scale farming and stimulating other industry.

Haya mambo mbona yanafanyika Pwani as we speak? This is not the time for petty issues, we are lagging behind.
 
Kuna watu ninawajua wana heka hizo tatu za mikorosho na mafanikio yao najua hata ukae miaka 20 huwezi kuwafikia.


Endelea kuishi kijima

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajua mkuu, kuna reality na fantasy. Ekari tatu za korosho zitaweza vipi kukupa mafanikio mara ishirini ya kima cha chini cha mshahara?
Nipe mahesabu siyo kuongea mambo ya kichawi.
Nakupa tani moja kwa ekari moja. Hapo ni sawa na shilingi milioni nne kwa ekari moja au milioni 12 kwa ekari 3.
Mshahara wa kima cha chini ni laki 3 kwa mwezi sawa na milioni nne kwa mwaka. Miaka mitatu nimekufikia.
Sasa nipe mahesabu ya hao wachawi unaowajua wenye eka tatu na income yangu ya miaka 20.

Wee ndio uache ujima.
 
Sasa kama unaona nalazimisha, si acha tu kulazimishwa?
Ukweli ni huo, hata kilimo kingechangia 0.5 ya GDP ya uchumi wa Marekani, hakuna kichaa ambaye angependekeza Marekani kuachana na kilimo. It is simple as that.
Halafu unaleta mlinganisho huo na nchi kama Tanzania yenye viwanda vingapi vile? 3 060 alivisema juzi Rais, na havijulikani viko wapi na wala vinazalisha nini! Huko ni kulinganisha kweli?
Honestly, hatuelewani kwa sababu sielewi unachozungumza.
Tunaongelea ili tuendelee haraka tufanye nini na wewe unaleta issues zisizoeleweka. Marekani walisha divert from agriculture a long time ago.
Hatuongelei kufyeka mashamba na kuunguza kila kitu. Thats weird.
 
Mkuu umeeleza jinsi sector hizi mbili zinavyo fanya kazi ila ujaeleza kiundani haswa kinachotokea katka sector hizi mbili

Kwa taarifa almost more than 50% and above ya watanzania wanategemea kilimo kama shughuli yao kuu so ukigusa kilimo umegusa walio wengi

Though kuna umuhimu wa kuwa na viwanda ila viwanda vitatoa wapi raw materials kama kilimo ni duni mambo ya msamaha wa kodi na uwepo wa rudhuku katka baadhi ya bidhaa sio relevant sana mkuu
unachozungumza ni kweli ila sasa ni wakati wakutoka katika kilimo cha subsitence na kuhamia katika industrialized agricltr mkuu bila kuhimiza viwanda wakulima watashindwa kufny lrge scale kwa sababu bila viwanda walime kwa gharama kubwa na ustadi wa hali ya juu alaf wapeleke wap..? yawaozee ndani? hpna vwanda vikishaonekana vitachochea watu kulima kwa ustadi hta vjna ambao hwana kazi watadhubutu kulima sababu wameona soko la bidhaa...na unaposema kilimo ni duni and then hpo hpo unasema msmaha wa kodi kweny baadhi ya pembejeo na zana zingine za kilimo sii relevant na kilimo duni unamaanisha nn mkuu? kwa sababu ninavoelewa poor farming inasababishwa na na zana mbovu za kikimo,mazao kutoka duni kwa sababu ya ardhi mbovu ilio kosa mbolea na virutubisho sasa serikali ilipotia ruzuku huko ni kuwezesha wakulima waji improve katika hyo sectr au nmekosea mkuu??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Honestly, hatuelewani kwa sababu sielewi unachozungumza.
Tunaongelea ili tuendelee haraka tufanye nini na wewe unaleta issues zisizoeleweka. Marekani walisha divert from agriculture a long time ago.
Hatuongelei kufyeka mashamba na kuunguza kila kitu. Thats weird.

So, kama all along tumekuwa hatuelewani ni kipi tumekuwa tukikizungumzia hadi tukafika hapa, what does that mean? It must be more than being 'weird'! 'insane' is the word that comes to mind.
 
So, kama all along tumekuwa hatuelewani ni kipi tumekuwa tukikizungumzia hadi tukafika hapa, what does that mean? It must be more than being 'weird'! 'insane' is the word that comes to mind.
More like .... Absurd.
 
Hivi "kilimo kwanza" ilikuwa na manufaa gani?
 
Tunahitaji "agricultural and industrial revolution", haya mapinduzi yanaenda sambamba. Huwezi kutaka kuwa na mapinduzi ya kilimo wakati hujajipanga kuwa na processing industries, aidha huwezi kufikiri kuwa na viwanda kama huna plans za kufanya mapinduzi ya kilimo.

Ndio maana serikali inatoa vipaumbele kwa sekta binafsi kuwekeza, wanajua kuwa akija mtu anataka kuanzisha kiwanda cha pamba, obviously atalima pamba, akitaka kiwanda cha sukari atalima miwa, wakati huo huo wale wakulima wanaozunguka viwanda hivyo watapata nafasi ya kulima mazao husika kwa kiwango kinachotakiwa.
 
Haya mambo ya heka tatu na vyama vya ushirika mtakaa miaka mia mbili hamuendi popote.
Kwa jinsi hali ya Tanzania ilivyo tayari sehemu kubwa ya ardhi wanayo wakulima wadogo wadogo (hekari 1-5)

Utatumia mfumo gani kuitoa ardhi kwa wakulima hao wadogo na kuwa mikononi mwa wakulimwa wachache wakubwa (full capitalism)???
 
hello JF,

Mie naona kwa vile taifa letu 80% wanategemea kilimo

Then serikali inge invest huko sio kununua ndege..

Ndege ni maendeleo lakini hio pesa ingewekwa kwenye kilimo,kusingekua na malalamishi ya mtaani kugumu…

Tuishaurini serikali iielekeze nguvu kwenye kilimo na kukomboa uchumi wa mtu mmoja mmoja….

1.Magufuli awe flexible,asikilize ushauri wa mawaziri wake,mie statement yake kuwa anakesha kuangalia ma file iliniambia mkuu anapenda kuchukua au kufanya kazi peke yake sio team player,hivyo kuwafanya mawaziri wake kuwa passive,sababu wanaona hawashirikiswi na kuna uoga wa kum confront rais.Hii atmosphere sio nzuri,ibadilike kama tunataka ku move forward...​
2.Ningependa kuona courses za kilimo kwenye vyuo vikuu ziko nyingi na tofauti,FEES kwa hizo course ziwe ALMOST FREE,itawaencourage watu kujiunga na kusoma mambo ya kilimo,kuajiri au kuajiriwa skills ziwe part ya hizi courses pia......​
3.Kuwe na workshops ndogo ndogo zinazo run throughout the year,zinazofundisha mambo ya kilimo,kwa mfano nimeona huko jukwaa la kilimo watu wanauliza nataka kujiajiri kwenye kilimo ila sijui nianzie wapi au mtaji nitenge shilingi ngapi?,au nilime nini? naamini kungekua na hizi workshop majibu yao yangepatiwa ufumbuzi na kuwapa confidence...kufanya wanayotaka….​
NYINGINE ONGEZEENI...lol​

Ushauri mzuri.Sijuwi ule mpango wa Kilimo Kwanza umeishia wapi.
 
Back
Top Bottom