Mapinduzi yawe ni ya kilimo....

Mapinduzi yawe ni ya kilimo....

hello JF,

Mie naona kwa vile taifa letu 80% wanategemea kilimo

Then serikali inge invest huko
Tuishaurini serikali iielekeze nguvu kwenye kilimo na kukomboa uchumi wa mtu mmoja mmoja….

1.Ningependa kuona courses za kilimo kwenye vyuo vikuu ziko nyingi na tofauti,FEES kwa hizo course ziwe ALMOST FREE,itawaencourage watu kujiunga na kusoma mambo ya kilimo,kuajiri au kuajiriwa skills ziwe part ya hizi courses pia......​
2.Kuwe na workshops ndogo ndogo zinazo run throughout the year,zinazofundisha mambo ya kilimo,kwa mfano nimeona huko jukwaa la kilimo watu wanauliza nataka kujiajiri kwenye kilimo ila sijui nianzie wapi au mtaji nitenge shilingi ngapi?,au nilime nini? naamini kungekua na hizi workshop majibu yao yangepatiwa ufumbuzi na kuwapa confidence...kufanya wanayotaka….​
Dada Rebeca, hapa umesema kweli, yeyoye atakayekubishia, anabisha tuu.

Japo asilimia ya wanaotegemea kilimo imeshuka. Wakati wa Nyerere ndio tulikuwa asilimia 80%, sasa watu wamekimbilia mijini, wanaotegemea kilimo, wamebaki asilimia 67% ambayo bado ni nyingi.

Hivyo kwa taifa linalotogemea kilimo, kutengeneza Tanzania ya viwanda ya ukweli, ni Tanzania ya Agro Processing Industries. Ili hili lifanyike, tulipaswa kuanza na Mapinduzi ya Kilimo ili kizalishe malighafi ya viwanda vya bidhaa za chakula. Ni aibu Tanzania tunaagiza mchele!, sukari, mafuta ya kupikia. Ngano yote ya viwanda vyote vya unga ni imported!. Hata hizi juices za Azam, 80% ya pulp is imported, wakati machungwa yanaozea mitini pale Lushoto, na maembe ya Unyanyembe ni chakula cha popo!.

Tanzania ndio nchi ya tatu kwa mifugo mingi barani Africa Kusini mwa Jangwa la Sahara, lakini kwenye meat export hatupo, export ya hides and skins tuko nyuma, tunaagiza ngozi, maziwa, siagi, jibini!.

Tanzania ndio nchi inayoongoza barani Africa kwa kuwa na vyanzo vingi vya maji!. Bahari ipo na imejaa samaki wa bure, lakini huwezi amini, tuna import vibua kutoka China!.

Ni mengi siwezi kuyamaliza.

Je, Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu au Vitu?- Wachumi Tusaidieni, Magufuli Analisaidia Taifa au Ataliangamiza?. - JamiiForums

Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!. - JamiiForums


Priorities Zetu Nini?. Dola Milioni 300 Zinatosha Kununua Smelter, Jee Tununue Au Tuzitumie Kwa Mahitaji Muhimu Zaidi? - JamiiForums

P.
 
Ukiwa na uzalishaji mwingi mwenye kilimo ndpo utaongeza thamani ya mazao na hapo viwanda huinuka , Ndege zilzokuja inawezekana zitashusha gharama ya usafiri Wa ndani lakini hata kama nauli ikitoka 600000/_ ishuke hadi laki mbili bad9 Mimi mkilima na mfanyakazi Wa kawaida nitasafiri kwa treni toka dar hadi Mwanza kwa 27000/, ndio uwezo wangu. Mabingwa waliobadilisha uchumi Wa nchi zao kama Lee Kuan Yew Wa Korea na Mahaghir Mohamed wa Malaysia tutume wajumbe huko waje na taarifa walitumia mbinu gani? Tuzifuate, Mfano mwngine je ni maamuzi kuacha luzslisha Umeme Wa gesi ambayo tayari IPO na haitumilki kikamilifu halafu tukaanza kuzalisha Umeme Wa Majj kule Sgieglers Gorge. Hii miradi mikubwa itatufanya mzunguko Wa hela usinyae.Halafu jamani hata kama unataka kusifia maamuzi yako mazuri si vizuri kiongozi kutoa taarifa isiyo kweli kuhusu waliokutangulia , juzi kiongozi mkuu amesema kabla ya awamu ya tano wafanyakazi walipata mishahara tarehe 15 ya mwezi unaofuata. Lakini Sahihi ni kuwa awamu ya NNE ya JK mishahara haijazidi tarehe 30 ya mwezi husika . Sasa hakuna viongozi wanaomzunguka awe anaongea taarifa Sahihi Mheshimwa ? Kutoa taarifa isiyo Sahihi imetungiwa sheria MTU atafungwa kwa kutoa takwimu potofu.. Sasa kwa upande Wa viongozi wao wanaruhusiwa kutoa statement zisizo Sahihi for public consumption maana hakuna Wa kuwauliza? Mheshimiwa anaweza kuwa na malengo Sahihi na hakuna haja ya kushakia hilo . lakini je ni kwa nini Mawazo mbadala yanakuwa ni kosa LA jinai? Mfano mwingine kuwa Rais akishapewa uongozi Kule Marekani huwa haingiliwi anaachiwa avurunde shauri yake.. Hill sio kweli maana hata Trump anapambana na vhombo vya habari na kila wakati anajihami kuhusu ubaguzi, na kupromote coal badala ya solar na wind power. Akina Bush na Obama kila Mara wanatoa comments dhidi yake lakini kinachombeba Trump uchumi unapanda na si ajabu akachaguliwa tena.. Mbinu aliyotumia ni kinyume cha huku kwetu. Yeye kashusha kodi halafu makampuni yamepata faida kubwa yakaajiri wafanyakazi wengi na waliopo wamepandishwa mishahara kwa hiyo mzungko Wa hela umeongezeka , Kosa dogo kwa kauli ya rais lina athari kubwa kwa taifa ndiyo maana takwimu zinaandaliwa ili wenye nia mbaya wasipotoshe uma kwa kutumia kauli za kiongozi mkuu Wa nchi na kumpa sifa mbaya.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jinsi ulivyoweka maneno hayo hapo juu. Angalia hii issue kitaifa bila serikali kutumia fedha kuanzisha viwanda. Ondoa wazo kuwa serikali itaanzisha viwanda.
Kwa mfano, kuna kiwanda cha sukari kinajengwa na kuna mualiko wa watu kujiunga kuanzisha mashamba ya miwa. Tayari hicho kiwanda kimesisimua sugarcane production.

Katika plantations za miwa kutazuka biofuel production if possible na ndivyo Brazil wanavyofanya. Industry stimulating large scale farming and stimulating other industry.

Haya mambo mbona yanafanyika Pwani as we speak? This is not the time for petty issues, we are lagging behind.
Na hili ndio lililo wainua wakulima wa katani wa brazil, baada ya kutegemea kuexpoet katani wameanzisha viwanda vya kamba, carpets na sasa ni nchi ya Kwanza Duniani kwa uzalishaji wa katani.
 
The gap between pronouncements and implimentation is very wide in this country mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Pia tume centralized karibia kila kitu.

Matatizo kama mbegu bora, njia bora za kilimo ni rahisi kutatuliwa na kampuni kubwa kupiia R&D tofautisha na sasa hivi. Ambapo kuna wakulima wadogo wadogo wengi ambao wanatupa jicho kwa serikali kuwapa msaada. Lakini serikali hiyo haina msaada sababu kipaumbele chake ni kununua ndege ili kukuza sekta ya utalii.
 
Unaposema value addition, hapo ndipo unapozungumzia manufacturing.
Usitegemee mkulima mwenzako akutengenezee kiwanda cha mazulia au tomato sauce.
Naona kama mko on the same chapter sema terminology mnazotumia zinawafanya mjione mna mawazo tofauti.
Value addition inawezwa kufanywa na mkulima mkubwa pia.(in-sourcing)

Au inawezwa kufanywa na mtu mwingine kabisa ambae sio mkulima (kwako wewe umetumia manufacturing).
Kwa njia zote hizo naona mko sahihi midhali output na quality imeongezeka. Na pia tumetoka from peasantry to farming
 
Hakuna nchi iliyoendelea kwa kutegemea kilimo. Nchi zote hujitoa kwenye kutegemea kilimo ili ziwe na maendelea halisi ambayo ni ya viwanda.
Kuna kila sabau ya kumuunga mkono aliyeleta hii mada muhimu kwa watanzania walio wengi amabo ni wakulima na wafugaji. Sio kweli kua nchi haiwezi kuendelea kwa kutegemea kilimo. Kinachtakiwa ni kua na viwanda vya kuongeza thamani mazao yatokanayzalishwa ili tuuze nje bidhaa zilizoshaongezwa thamani. Investment inayotakiwa kwenye kilimo ni ile ya miondombinu ya umwagiliaji, uanzishwaji wa miradi mikubwa ya umwagiliaji ikiwa ni pamoja kujenga mabwawa ya umwagiliaji kwenye mito mikubwa ili maji yatumike na sio kuishia baharini, kuimarisha utafiti ili kutoa teknolohia bora za kilimo, kuimarisha idara za ugani. Kufufua yale mashamba makubwa ya ngano ambayo leo hii mengine yamekua ni mapori.
Kuboresha sekta ya kilimo ni jambo jema sana, ila nchi haiwezi pata maendeleo kwa kutegemea Kilimo Pekee.
Pamoja na kutoa ruzuku kwenye mbolea, mbegu kwa wakulima na madawa ya mifugo kwa wafugaji. Pesa zitokanazo na madini, gesi na utalii ziwe reinvested kwenye kilimo. Hii ni kwa uchahe. Kilimo kisipoimarishwa maisha bora kwa watanzania itakuani ndoto.
 
Naona kama mko on the same chapter sema terminology mnazotumia zinawafanya mjione mna mawazo tofauti.
Value addition inawezwa kufanywa na mkulima mkubwa pia.(in-sourcing)

Au inawezwa kufanywa na mtu mwingine kabisa ambae sio mkulima (kwako wewe umetumia manufacturing).
Kwa njia zote hizo naona mko sahihi midhali output na quality imeongezeka. Na pia tumetoka from peasantry to farming
Mkulima mdogo ni nadra sana, almost impossible kufanya food processing. Muda na resources ni limited na hata akifanya processing ni kwa ajili ya matumizi yake.
Watake wasitake, kuwa na 67% ya watu kama wakulima is too much. Lengo ni kuwaondoa na kubaki na at most 10% au hata basi 20%. To achieve this, ni lazima viletwe viwanda vitakavyokuwa vinategemea mashamba makubwa kutoka hapa nchini. Maana yake ni kuwaondoa wakulima adogo (peasants) na kuwaweka kwenye manufacturing.
Yeye anazungumzia kuchukua mbegu bora na mbolea kutoka kwa mtendaji, na kutawanywa kwa mabwana shamba. Tutakuwa agrarian society for ever.
 
Mtoa mada
hakuna mapinduzi ya viwanda bila mapinduzi ya kilimo
Marekani unayoisifia walianza na Green revolution then industrial revolution
Ningekuelewa kiasi kama ungeacha kubishana bila hoja na ueleze tunaanzaje kupunguza idadi hiyo ya wakulima na kuongeza viwanda HOW?
Where do we start??

Inaweza ikawa Principle mpya tukaifuata.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom