Mapinduzi yawe ni ya kilimo....

Mapinduzi yawe ni ya kilimo....

Wrong .. It's vice versa.
Viwanda vya tumbaku ndivo vilivyoanzisha uhitaji wa mashamba ya tumbaku na kutafuta makoloni.
Ulimaji wa tumbaku bila viwanda ni sawa na kuwa na shamba la miarobaini.
OK you're right

 
Lengo ni kuwaondoa hao wananchi wanaotegemea kilimo, wategemee viwanda (manufacturing).
Tuna watu wengi wanaolima, na hilo ni tatizo kubwa.
Watu wengi wanalima lakini hawalimi kilimo cha biashaza. Wengi kilimo chao ninkwa ajili ya chakula.

Hata kilimo hicho hakitoshelezi mahitaji ya watu wote. Ndo mana mvua isiponyesha kidogo tu, unasikia kelele za njaaa!!

Hivyo wengi wanalima lkn kilimo mfuu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujaelewa.
Hizo mali ghafi hazihitaji watu milioni 20 au 30 walime. Tatizo mnataka kilimo kitoe ajira, na huo ni uongo. Ni saa na kuingia baa ina mabaamedi 60 wateja wanne.
Kwa uwezo na uduni wa technolojia tulionao ni lazima wengi walime ili malighafi ipatikane

Hao wakulima wachache wa kuzalisha kwaajili ya viwanda vingi wako wapi?
Uwezo wao ukoje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wengi wanalima lakini hawalimi kilimo cha biashaza. Wengi kilimo chao ninkwa ajili ya chakula.

Hata kilimo hicho hakitoshelezi mahitaji ya watu wote. Ndo mana mvua isiponyesha kidogo tu, unasikia kelele za njaaa!!

Hivyo wengi wanalima lkn kilimo mfuu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kilimo cha biashara hakihitaji watu wengi. Kwa hiyo, kwa vyovyote vile lazima tuwe na lengo la kuwaondoa wananchi wengi kutoka kwenye kilimo. Ondoa kabisa! Tupa kule!
 
Kwa uwezo na uduni wa technolojia tulionao ni lazima wengi walime ili malighafi ipatikane

Hao wakulima wachache wa kuzalisha kwaajili ya viwanda vingi wako wapi?
Uwezo wao ukoje?

Sent using Jamii Forums mobile app
Utarudi kwenye siasa za Mugabe.
Skiza .... Kilimo siyo jambo la kufanywa na watu wengi. Mbona mbishi?
Huwezi kuwa na peasants wengi wadogowadogo, wazalishe mali ghafi za viwanda. Hivyo viwanda havitakuwepo Tanzania, mtakuwa mna -export mazao na kurudi kulekule.
 
Kilimo cha biashara hakihitaji watu wengi. Kwa hiyo, kwa vyovyote vile lazima tuwe na lengo la kuwaondoa wananchi wengi kutoka kwenye kilimo. Ondoa kabisa! Tupa kule!
Sasa una waondoaje?
Upeleke kwenye viwanda?.

Viwanda havipo, na huko tuendako viwanda havihitaji tena binadam

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Actually kilimo hufanywa na watu wachache na manufacturing hufanywa na watu wengi. Unapoanzisha viwanda, unachochea migration ya wakulima na unachochea ukuaji wa miji midogo kuwa mikubwa au vijiji kuwa miji.

Pia kuna vitu kama REA. Huu mradi kama hautakuwa coupled na industrialization drive, faida yake aitakuwa kubwa, watu watalima mahindi na mihogo na watashindwa hata kulipia gharama za huo umeme.

Ukichochea uzalishaji wa kilimo tu, utakuwa na surplus for export, na hii haitakufikisha popote pale bali kukubakisha kuwa taifa linalolima na kuuza mazao nje na kununua manufactured products.

Unapochochea manufacturing unachochea population inayofanya kazi za viwandani ambayo itataka kula na itakuwa tayari kununua vyakula vinavyolimwa na watu wachache than before factories were established. Wakulima wachache, wenye soko kubwa la ndani watalima efficiently through mechanization,genetic engineering etc na kuchochea biashara na service industry.

Viwanda pia vinaleta technological transfer. naamini hata tu kwa mfano mdogo sana wa waajiriwa wa Tazara overpass, kuna watu wamejifunza welding, ujenzi, kuendesha bulldozers etc.. au angalau kuchochewa kujifunza hayo.

So, industrialization itoe focus kwenye investment of capital in manufacuring either from private sector or PPP. Na itanguliwe au iende sambamba na uendelezaji wa infrastructure.

Umesema vizuri mkuu

Ila sidhani kama umetizama kwa kina nchi yetu jinsi ilivyo sidhani kwa kweli japo umetoa vivid examples

Kuna forward and backward linkage katika hii mada ila kilimo ni muhimu sana kwa sasa kuliko viwanda japo viwanda vinaumuhimu wake
 
mawazo yako ni mazuri ingawaje umeyatoa kwa mfumo wa kutokubali kile kinachofanywa na serikali ya awamu hii ya 5 kitu kilichosababisha usione uhalisia wa kinachofanyika ila kwa kuwa umetoa nafasi ya kuongeza naeza nikaeleza kulingana na uwelewa wangu..
moja naeza kusema kiwanda na kilimo ni sector mbili tofautu zinazofanya kazi kwa ushirikiano..na ukiangalia sera mazubuti ya serikali hii ni viwanda kitu kinachoopelekea mkulima kupata sokoo la kile ancholima kwa kuwa kiwanda kinategemea raw material kutoka kwa mkulima kwa naeza nikasema sera ya viwanda inaeza ikakuza uchumi kupitia viwanda huku inaipa tija kilimoo kwa kuongeza wigo wa soko kwa hiyo kilimo akijaachwa nyumaa...pili naeza nikasema serikali haijasahau kilimo kamo unavyosema ingeelekeza nguvu kwa ninicho kiona kuna nguvu kubwa tuuh imeelekweza huko ukiangalia mfumo wa kodi ulivorahisihwa kwa wakulima kwa awamu hii..ukitazama kweny mbolea na baadhi ya madawa yameekewa rdhuku ya kutosha kitu kinachowezesha mkulima kupta pmbjeo kwa bei rahisii kwa kweli mi ninacho ona ni ujapendezwa na bombadier tuuh so ukaamua kutoa duku duku lako...

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu umeeleza jinsi sector hizi mbili zinavyo fanya kazi ila ujaeleza kiundani haswa kinachotokea katka sector hizi mbili

Kwa taarifa almost more than 50% and above ya watanzania wanategemea kilimo kama shughuli yao kuu so ukigusa kilimo umegusa walio wengi

Though kuna umuhimu wa kuwa na viwanda ila viwanda vitatoa wapi raw materials kama kilimo ni duni mambo ya msamaha wa kodi na uwepo wa rudhuku katka baadhi ya bidhaa sio relevant sana mkuu
 
Watu wengi wanalima lakini hawalimi kilimo cha biashaza. Wengi kilimo chao ninkwa ajili ya chakula.

Hata kilimo hicho hakitoshelezi mahitaji ya watu wote. Ndo mana mvua isiponyesha kidogo tu, unasikia kelele za njaaa!!

Hivyo wengi wanalima lkn kilimo mfuu!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndo mana kuna haja ya serekali kuwekeza katika kilimo ili kuondoa ili tatizo

60% ya mazoa yanayo vunwa huwaribika kabla ya kumfikia mlaji hii inadhihirisha elimu ya post harvesting management ni zero kwa wakulima wetu
 
Huelewi concept.
Mtu mmoja alime korosho Mtwara nzima, mwingine Pwani nzima halafu kuwe na viwanda vya mafuta ya korosho, kubangua na kupakia korosho, na kutengeneza pombe za ulaka au juice ya mabibo.
Pia mbolea, mashine za mashamba yake, repair, banks na huduma za wafanyakazi wa shamba hilo kubwa na viwanda vinavyozunguka, mahoteli, etc .. ndiyo vitachochea ukuaji wa uchumi wa Mtwara au Pwani.

Haya mambo ya heka tatu na vyama vya ushirika mtakaa miaka mia mbili hamuendi popote.

Hiyo concept ninaielewa sana, kwa sababu sio kitu kipya au cha ajabu.
.
Kwa bahati mbaya wewe ndio hiyo hiyo tu uliyofundishwa na unaendelea kuing'ang'ania kana kwamba hakuwezi kuwa na dhana tofauti na hiyo na bado wakulima wetu wakafaidika na juhudi zao za kilimo katika mazingira tofauti na hayo inakotumika na kufanikiwa.

Hilo la kumpa mkulima mmoja Mtwara nzima, na mwingine Morogoro nzima unajua dhahiri kwamba halitatokea Tanzanaia. Lakini hatuwezi kuacha kutafuta njia mbadala, na ambazo zimekwisha hakikiwa kuwa zinafaa katika kuwainua wakulima wadogo wadogo, kwa kuwasaidia waongeze uzalishaji wa mazao yao hata katika hivyo vishamba vyao vidogo. Kama mkulima wetu anaweza kupata gunia 15 za mahindi katika eka moja badala ya gunia tano, hayo si mafanikio? Na hayo yote uliyoyataja ya mafuta nakadhalika, kwa nini yasiwepo kama watumiaji wapo katika wingi wao.
Kulima au kufuga kwa mkataba sio jambo geni, hata ukiachilia hilo la ushirika unalolidharau wewe.

Tatizo ni kuwa wewe unachukulia mifano iliyo 'fail'; kama ya kulima kwa jembe la mkono, au ushirika uliowadhurumu wanachama wake, ndio unautolea mfano na nadhaeia hiyo ya wakulima wakubwa.na kuendelea kuamini tu kwamba ushirika hauwezi kufanikiwa. Kwa nini usifanikiwe kama unaendeshwa vizuri. Mbona kuna ushirika hata katika nchi nyingi zilizoendelea na unafanya kazi vizuri, na sio katika kilimo tu?
 
Umesema vizuri mkuu

Ila sidhani kama umetizama kwa kina nchi yetu jinsi ilivyo sidhani kwa kweli japo umetoa vivid examples

Kuna forward and backward linkage katika hii mada ila kilimo ni muhimu sana kwa sasa kuliko viwanda japo viwanda vinaumuhimu wake
This is the time! La sivyo sisi tutakuwa peasants na backward.
 
Hiyo concept ninaielewa sana, kwa sababu sio kitu kipya au cha ajabu.
.
Kwa bahati mbaya wewe ndio hiyo hiyo tu uliyofundishwa na unaendelea kuing'ang'ania kana kwamba hakuwezi kuwa na dhana tofauti na hiyo na bado wakulima wetu wakafaidika na juhudi zao za kilimo katika mazingira tofauti na hayo inakotumika na kufanikiwa.

Hilo la kumpa mkulima mmoja Mtwara nzima, na mwingine Morogoro nzima unajua dhahiri kwamba halitatokea Tanzanaia. Lakini hatuwezi kuacha kutafuta njia mbadala, na ambazo zimekwisha hakikiwa kuwa zinafaa katika kuwainua wakulima wadogo wadogo, kwa kuwasaidia waongeze uzalishaji wa mazao yao hata katika hivyo vishamba vyao vidogo. Kama mkulima wetu anaweza kupata gunia 15 za mahindi katika eka moja badala ya gunia tano, hayo si mafanikio? Na hayo yote uliyoyataja ya mafuta nakadhalika, kwa nini yasiwepo kama watumiaji wapo katika wingi wao.
Kulima au kufuga kwa mkataba sio jambo geni, hata ukiachilia hilo la ushirika unalolidharau wewe.

Tatizo ni kuwa wewe unachukulia mifano iliyo 'fail'; kama ya kulima kwa jembe la mkono, au ushirika uliowadhurumu wanachama wake, ndio unautolea mfano na nadhaeia hiyo ya wakulima wakubwa.na kuendelea kuamini tu kwamba ushirika hauwezi kufanikiwa. Kwa nini usifanikiwe kama unaendeshwa vizuri. Mbona kuna ushirika hata katika nchi nyingi zilizoendelea na unafanya kazi vizuri, na sio katika kilimo tu?
Hakuna duniani nchi iliyoendelea kwa kutumia asilimia 50 ya watu wake kuwa wakulima wadogowadogo. Pia, model ya ushirika wetu ni medievel.
Ushirika ni kuwa na ma-combine harvesters, research centers etc.. siyo kulima pamba na kubeba magunia au kahawa na kuipeleka chama. Hiyo hata mpee pembejeo bure, hamtafika mahali na mtakuwa mnapangiwa bei na manufacturers of usable products.
Mimi nina mifano hai iliyopo duniani ya economic models mbalimbali. Unforunately, your approach has been tried and failed. I's like a cat chasing it's own tail.
 
Hakuna duniani nchi iliyoendelea kwa kutumia asilimia 50 ya watu wake kuwa wakulima wadogowadogo. Pia, model ya ushirika wetu ni medievel.
Ushirika ni kuwa na ma-combine harvesters, research centers etc.. siyo kulima pamba na kubeba magunia au kahawa na kuipeleka chama. Hiyo hata mpee pembejeo bure, hamtafika mahali na mtakuwa mnapangiwa bei na manufacturers of usable products.
Mimi nina mifano hai iliyopo duniani ya economic models mbalimbali. Unforunately, your approach has been tried and failed. I's like a cat chasing it's own tail.

Hiyo asili mia hamsini imetoka wapi?
Hivi hakuna service sctotors kama afya n.k, financial services, nk. Kwa nini iwe viwanda tu na kilimo?
Si hapo ndipo ninapokwambia tunabishana kwa kupishana? Wewe unazungumzia 'ushirika medieval, mimi nazungumzia modern ushirika, modern agriculture. Hizo 'research centres' si ndio zitakuwepo kabisa, kuwahudumia wakulima. Sijui ni kitu gani kitazuia wakulima wasihudumiwe na kusafirisha mazao yao. Hapa sikuelewi kabisa. Kwani si ni biashara? Wafanya biashara watakataa kusafirisha kwa kuwa ni mazao ya wakulima wadogo wadogo?
Haya unayoyaingiza sasa ya kupangiwa bei yantuondoa katika mjadala wa kilimo cha kumnufaisha mkulima kwa kuongeza uzalishaji wake. Lakini hata hayo yana majibu yake tukitaka kwenda huko.
 
u

Arbitrary number. Watanzania wanaojihusisha na kilimo ni 67%. Ndiyo maana maendeleo yanakuwa tabu.

Ilikuwa 80, ikaendelea kushuka hadi 75, kwa hiyo sasa hivi ni 67?
Na obviously unajua haitakaa static 67 milele. Kwa hali hiyo basi tunaendelea ingawaje ni taratibu mno.
Hao watakaokuwa wamebakia kwenye kilimo, ndio tunaowatakia mafanikio katika kazi yao hiyo.
Na isije ikaeleweka kwamba kilimo hicho cha wadogo ni exclusive. Patakuwepo na wakubwa pia. Hivyo hivyo hata katika nyanja nyingine zinazofanana na kilimo, kama ufugaji na uvuvi.
 
Ilikuwa 80, ikaendelea kushuka hadi 75, kwa hiyo sasa hivi ni 67?
Na obviously unajua haitakaa static 67 milele. Kwa hali hiyo basi tunaendelea ingawaje ni taratibu mno.
Hao watakaokuwa wamebakia kwenye kilimo, ndio tunaowatakia mafanikio katika kazi yao hiyo.
Na isije ikaeleweka kwamba kilimo hicho cha wadogo ni exclusive. Patakuwepo na wakubwa pia. Hivyo hivyo hata katika nyanja nyingine zinazofanana na kilimo, kama ufugaji na uvuvi.
Asilimia 67 ni nyingi na maendeleo yanaenda taratibu.
Tunatakiwa tuwe na less than 10%.
Solution ni viwanda siyo kilimo.
Jw unakubali kwamba lengo liwe ni viwanda? Tuanzie hapo kwanza. Halafu tuone jinsi gani tunafikia hapo kwa haraka. Nataka niondoe fikra kuwa kilimo ndiye mkombozi. Hizo ni fikra duni.
 
Asilimia 67 ni nyingi na maendeleo yanaenda taratibu.
Tunatakiwa tuwe na less than 10%.
Solution ni viwanda siyo kilimo.
Jw unakubali kwamba lengo liwe ni viwanda? Tuanzie hapo kwanza. Halafu tuone jinsi gani tunafikia hapo kwa haraka. Nataka niondoe fikra kuwa kilimo ndiye mkombozi. Hizo ni fikra duni.

Tanzania haiwezi kuachana na kilimo. That is a fact of life, hata tuendelee vipi na kuwa tunaunda ma-rocket yetu wenyewe and other exotic gaggets.
Marekani kwenyewe, China na kwingineko hawajaachana na kilimo na hawana mpango huo wa kuachana na kilimo. Itakuwaje Tanzania hata kuboresha tu hicho kilimo kilichopo bado, iachane na kilimo?
 
Tanzania haiwezi kuachana na kilimo. That is a fact of life, hata tuendelee vipi na kuwa tunaunda ma-rocket yetu wenyewe and other exotic gaggets.
Marekani kwenyewe, China na kwingineko hawajaachana na kilimo na hawana mpango huo wa kuachana na kilimo. Itakuwaje Tanzania hata kuboresha tu hicho kilimo kilichopo bado, iachane na kilimo?
Hujajibu swali. Unanielewa ninaposema tuachane na kilimo. Yaani tusitegemee kilimo kama sehemu kubwa ya uchumi na ajira.
Haya, nijibu swali langu kwanza.
Agric. in US is 1% of GDP
 
Hujajibu swali. Unanielewa ninaposema tuachane na kilimo. Yaani tusitegemee kilimo kama sehemu kubwa ya uchumi na ajira.
Haya, nijibu swali langu kwanza.
Agric. in US is 1% of GDP

Sehemu kubwa ya uchumi? Hilo pia halipo. Ukimwambia Mmarekani aachane na Soy beans, mahindi na ngano hawezi kabisa kukuelewa. Kilimo ni sehemu kubwa kabisa ya uchumi wa Marekani.

Kwa nini Tanzania iachane na kilimo kama sehemu muhimu ya uchumi wake wakati ina potential ya kulisha Africa Mashariki nzima?
Hivyo viwanda vitajengwa vizalishe vitu gani katika miaka 10, 15, hadi ishirini ijayo, vitakavyoweza kuhudumia sehemu kubwa ya uchumi wake?
Kilimo kinatakiwa kuboreshwa, si kidogo, ila sana tena kwa haraka zaidi kutuwezesha kuinua uchumi wetu haraka wakati viwanda vinaanzishwa. Kwa maana hiyo, kilimo kitaendelea kuwa muhimu sana kama ajira kwa waTanzania, na ndio maana kinatakiwa kiboreshwe haraka ili hawa watu wengi wainue maisha yao. Hatuwezi kuwa na viwanda kuajiri watu hao uliowasema, na wala hatuwezi kusubiri ndipo mabadiliko yapatikane katika maisha yao.
And you know what that 1% GDP means for the US!
 
Back
Top Bottom