hata sijui mkuu,naona hili wazo liepingwa vikali,
mie I just think tukiwekeza kwenye kilimo,
kutakua hakuna unemployment,
na kama hakuna unemployment then serkali inaweza kudirect resources zake kwingine including kujenga viwanda…
swala la tunahitaji wakulima wachache sioni kama liko sahihi,yaani uwajaze watu viwandani wakufanyie kazi,instead wangelima na kujilisha na mengine ndio wakulete kiwandani.???.hili jambo mmelichukulia too general..labda hatutaona positivity at national level ila uchumi wa mmoja mmoja wetu atainuka …kama tukitilia mkazo
second viwanda vitahitahi skilled labour na machinery sasa hivi uki compare na kilimo kipi chepesi na achievable?
Again,UZALSHAJI lazima uwe maximum ndio twende viwandani,sasa kama wakizalisha/lima kidogo utafanyia nini hizo machine???uzalishaji lazima uwe at Maximum sad it means kilimo ndio kianze kwanza...kikishafika maximum or optimum level ndio viwanda vijengwe....
Rebeca83, iko hivi: hata huko ulaya kwenye mashamba makubwa ya wakulima wachache, palikuwepo pia wakulima wadogo hapo zamani, hata kama hawakuwa wa kilimo cha jembe la mkono tunalolijua sisi. Rudi tu miaka hamsini nyuma, hata hapo Marekani walikuwepo, na pale China wakulima hao bado wapo, hata ukiangalia movie zao utawaona wakipandikiza mpunga, tena kwa mikono. Hivyo hivyo hata Korea ya kusini. Uingereza, wadogo kabisa walikwisha siku nyingi zaidi, lakini hata leo wapo wa kati (sio wadogo sana na wala sio wakubwa).
Kilichotokea, ni kwamba kadri ya maisha ya watu yalivyozidi kuwa mazuri, na watoto wengi wakawa wanapata elimu, wengi hawakurudi tena kwenye familia zao kuendelea na kazi za kilimo. Wengi wakawa ni wafanya kazi mbali mbali mijini. Hizo kazi hazikuwa kwenye viwanda tu, lakini unajua sehemu nyingi watu wenye ujuzi wao wanakoajiriwa, ikiwa of course hata kwenye viwanda.
Hawa wazee waliobaki mashambani, siku zao zilipofika, au kwa kuishiwa nguvu kutokana na uzee, kazi zao za kilimo zilikoma. Watoto hawakurithi majukumuhayo. Sasa kama kilikuwa ni kishamba chenye tija, wanunuzi walinunua na ku-consolidate kwenye mashamba mengine na kuwa biashara kubwa ya kilimo.
Jameni, kwani hata sisi hapa yanayotokea tayari hamyaoni? Utanisamehe Rebeca83, lakini nakuona kama vile umekwishaonja maisha ya mjini na kunogewa. Sidhani kama unao mpango wowote wa kurudi kijijini kwenu kuendeleza kilimo kile alipoishia babu na bibi. Na kama utabahatika kupewa urithi ule, nina uhakika zaidi ya 50%, kishamba kile utakipiga bei. Tungekuwa tumekwishafikia hatua ya 'consolidation', nina hakika ungefuatwa haraka sana na wanunuzi wanaopanua sehemu zao za kilimo.
Lakini pamoja na hayo yote, kwa mawazo yangu binafsi, Tanzania bado tutaendelea kuwa na wakulima wadogo wadogo kwa muda mrefu kidogo. Hawa hawatatoweka miaka 10 au ishirini ijayo. Kwa sababu watu wetu wengi bado maisha yao yako vijijini.
Kwa hiyo basi, ili hawa watu tuweze kuwasaidia kwa bidii zao nyingi wanazozifanya, serikali haina budi kuweka kilimo kiwe kipaumbele cha kudumu, kikiungana na Elimu.
Maana yangu hapa ni kwamba wakulima hawa wawe na uwezo wa kilimo cha kuzalisha mazao mengi zaidi katika hivyo vishamba vya ekari 5, 10, hata 50, maradufu ya mazao wanayopata sasa hivi. Hili litakisaidia kizazi hiki cha wakulima kujipatia kipato zaidi, nyumba nzuri, watoto shule, afya, n.k..
Hiki kizazi kitaendelea kupungua mwaka hadi mwaka, na Tanzania itapata maendeleo kwa kasi zaidi (I hope haitakuwa Haiti) na kuwa na viwanda inavyotaka kuwa navyo. Na hawa vijana waliotoka vijijini wasiopenda kwenda huko tena, watakuwa na elimu ya kutosha kufanya kazi viwandani, na kwingineko. Hawarudi tena kwenda kuendeleza kishamba cha babu.
Sitaki uchoke kusoma. As for "kutakuwa hakuna unemployment" - hata tukiagiza wafanya kazi wa shambani kutoka Kenya, as for Mexico to USA- bado unemployment to some people will always be a fact of life. I hope you understand what I mean. Hivi Saudi kuna 'unemployment?