Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

maneno mazito hayo mkuu. natamani uweke uthibitisho, au unyamaze tu tuendelee kuomboleza.

Sishangai kama ni ukweli. Nanitaamini kuwa ni kweli hata ikiweje. Si tunawafahamu majibu yao.
Je kunatofauti gani na viongozi wakuu kama JK na Makinda kuhusisha kila wasichokipenda kusikia kikisemwa na dini, au CDM? hata maoni ya wanachi kuhusu mswada mbovu wa katiba, kila anayepinga ni CDM. Hawa nisawa na hao mapolisi hakuna tofauti
 
Mungu atusaidie tuishi salama maana niionavyo nchi hii inapoelekea,siku moja nasi hatutoshangaa kujikuta tunaingia katika vita kama nchi za wenzetu,mambo kama haya huanza taratibu na kujenga chuki na siku ikilipuka hakuna atakayekuwa salama.
 
Kwa kauli hiyo ya POLISI ni kwamba hawajali wananchi wanyonge wao wanawajali Mafisadi tu, kama wangepigiwa simu wakaambiwa kuna maandamano ya CHADEMA wangetoka mbio kama mbwa mwizi
 
maneno mazito hayo mkuu. natamani uweke uthibitisho, au unyamaze tu tuendelee kuomboleza.
Nilimsikia mtangazaji wa ITV akitamka hayo wakati anatangaza 'live' tukio hilo, na baadae kutoka kwa mtu alyepiga simu polisi na kuambiwa hayo, alipohojiwa tena na waandishi wa habari wa ITV jana kwenye taarifa ya habari ya saa 2 usiku.
 
Mwenyekiti wa Serikali za mitaa Bw Deogratius Kamugisha amesima ofisi yake iliwasiliana na jesho la polisi hawakupata Msaada.
Wakampigia Said Mwema, Said Mwema akaambia wampigie Kova, Kova akasema analeta polisi.
Wananchi wakaona haitoshi, wakamtuma mtu (Ali Mgulu) aende polisi moja kwa moja kuomba msaada Ali akajibiwa na polisi "ngoja wakaune alafu huyo wamwisho atakaye pona aje atoe taarifa" na Diwani aliingia wakati polisi wanatoa hayo matamko.

SOURCE ITV news YouTube - Habari via ITV -Watu watano wapigwa mapanga mpaka kufa- Jeshi la polisi liko wapi?
 
maneno mazito hayo mkuu. natamani uweke uthibitisho, au unyamaze tu tuendelee kuomboleza.
Kulingana na maelezo ya waliotoa taarifa ndio walijibiwa hivyo............kama sijakosea ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa ule kulikotokea mauaji.
 
Matukio ya namna hii ni matokeo ya kuwa na serikali isiyojali wananchi wake, hasa wa kipato cha chini. Hili linanifanya nihoji mambo kadhaa,

(a) Kama kweli kampuni ya mwangata ilipewa kibali halali cha kubomoa hizo nyumba, ilifwata utaratibu wa kuwa taarifu watu ambao wangebomolewa mapema ili wajipange na kutafuta makazi mengine?? narejea maneno ya JK kuhusu ubomoaji wa MAGUFULI , kwamba ikibidi mtu apewe hata miaka miwili ili ajipange na kupata makazi mengine.

(b) Hilo eneo lingekuwa limevamiwa na mafisadi na kujengwa manyumba ya kifahari, kungetokea hali kama hiyo?? au kwasababu wale waliojenga ni wanyonge ndio maana wakatendewa hayo???

(c) Msimamo mzima wa utendaji wa jeshi la polisi unabagua?? je ingekuwa wamepigiwa simu wakaambiwa CDM wanaandamana wange react on the same way?? na je jeshi la polisi ndio mwanzo wa machafuko Tanzania?? (1) CDM arusha, walipambana na raia wakawauwa (2) Mivumoni tegeta, wamepewa taarifa, wakazipotezea, watu watano wakafa......hii inaashiria nini??

(D) Mabaunsa kulipwa 50,000 na kukubali kujitoa mhanga na wengine kupoteza maisha kunaashiria nini?? Hali ngumu ya ajira?? kuwepo kwa vijana wengi wasiokuwa na ajira, na kwamba wako tayari kujitoa maisha yao kwa kipato kidogo?? watu hao ukiwapa 100,000 ukawaambia wakamtoe mtu roho watakataa??

(e) Je serikali yetu legelege itayafumbia macho matukio haya mpaka lini??
-Mbarali
-Karatu
-UDSM
-UDOM
-CDM Arusha
-Mivumoni
Na list inaendelea kubwa tu!


EE MUNGU TUSIKIE MAOMBI YETU NA UIEPUSHE NCHI YETU NA MAJANGA KAMA HAYA!
 
Nimesikiliza Clouds FM wakimuhoji mjumbe wa nyumba Kumi wa eneo hilo
anasema walikuta vichaka wakafyeka na kujenga na hawajui ardhi ni mali ya nani
je ni halali kufanya hivyo bila utaratibu? kwa sentensi hiyo ni wavamizi?
serikali inatakiwa kuwahoji wananchi wa eneo hilo ili kupata ufafanuzi zaidi
pia kujua waliokwenda kubomoa majengo walitumwa na nani?

Ukiishi mahala fulani kwa mda fulani, tayari unakuwa mmiliki halali. Hata JK ka mwambia Magufuli, juzi juzi. Wananchi walikuwa hawana njia mbadala zaidi ya hiyo. Si kwamba mauaji ya aina yoyote ni dhambi, na hata hivyo Mungu awarehemu waliopoteza maisha.
 
Kwa kweli ukitazama tukio hilo linasikitisha sana namna watu wanavyocharangwa na mapanga....
Kingine ambacho sijaelewa ni namna mtu anavyovuja damu badala ya kupewa huduma anahojiwa.......kwa kweli hali hii inatisha na MUNGU apishie mbali hali hii...
 
Kwa kweli ukitazama tukio hilo linasikitisha sana namna watu wanavyocharangwa na mapanga....
Kingine ambacho sijaelewa ni namna mtu anavyovuja damu badala ya kupewa huduma anahojiwa.......kwa kweli hali hii inatisha na MUNGU apishie mbali hali hii...

itabidi mfumo wa kuendesha hii nchi ubadilike mapema, watu wapewe elimu yenye manufaa kwa jamii. kuanzia polisi mpaka raia. kama serikali inashindwa kuingilia kati na kutatua matatizo kama haya lazima iwe tayari kwa lolote maana hata PAKA na upole wake wote ukimbana kwenye kona lazima atoe makucha.
 
maneno mazito hayo mkuu. natamani uweke uthibitisho, au unyamaze tu tuendelee kuomboleza.

uthibitisho upi? it means hukuangalia taarifa ya habari ya jana ITV!! kama upo nje ya tanzania,may be ok lakini kama upo bongo, shame on you!!!
 
Hebu tujuze zaidi kuhusu hayo mauaji ya Tegeta, waliokufa ni waliokodiwa kubomoa au wananchi waliovamiwa na hao wapuuzi?
waliokufa ni mabaunsa ambao wameenda kuvunja nyumba za wanyonge kwakukodiwa namwenye vijipesa,wananchi wakawapa kipigo chambwa mwizi nazaid ya 10 wameuwawa.
 
uthibitisho upi? it means hukuangalia taarifa ya habari ya jana ITV!! kama upo nje ya tanzania,may be ok lakini kama upo bongo, shame on you!!!


now you attack me. shame on me. sawa.

media (hasa ya Tanzania) haiwezi kuwa uthibitisho wa mwisho. magazeti, redio na hata baadhi ya TV zimeripoti waliuliwa watu watano; gazeti la serikali yenu, Habari Leo limeripoti walikufa wawili.

shame on who? me or you?

kabla ya kumshambulia mtu inabidi ujiulize kwanza 'umejiandaa-andaaje' kabla ya kuweka post yako hapa jamvini.
 
wa Tanganyika wenzangu serikali imeshindwa kulinda haki ya raia wake. leo tegeta kesho mbezi na kuendelea serikali imewekwa mfukoni na matajiri uchwara wanafanya wanavyotaka. mungu anisamehe lkn nyumba yangu nikiyojenga kwa jasho langu na ardhi mali yangu ukaja ukabomoa nasema tena mungu nisamehe dar itatikisika na kuzizima. itabaki ktk historia ya nchi hii km yule kijana wa Tunisia. ntaanza na ardhi pale!!!MUNGU NISAMEHE NA EPUSHA MBALI ISITOKEE!! wa TZ jilindeni hamna mtetezi tena!!!
 
Mwema ndiye wa kwanza anayepaswa ajiuzuru, haiwezekani wewe kama bosi wa polisi unapigiwa unasema mpigie kova, si umpigie wewe mwenyewe. kama gongolamboto mkuu wa majeshi anawataka wananchi waende mbali sijui km ngapi, mibasi ya jeshi imewekwa tu makambini, sasa si wangewapelekea usafiri wa kuwapeleka huo umbali anaoutaka, hili nchi watu wanapeana kazi tu
 
now you attack me. shame on me. sawa.

media (hasa ya Tanzania) haiwezi kuwa uthibitisho wa mwisho. magazeti, redio na hata baadhi ya TV zimeripoti waliuliwa watu watano; gazeti la serikali yenu, Habari Leo limeripoti walikufa wawili.

shame on who? me or you?

kabla ya kumshambulia mtu inabidi ujiulize kwanza 'umejiandaa-andaaje' kabla ya kuweka post yako hapa jamvini.

Kwani video hujaona? Mwananchi anaongea kwa maneno yake. Kama polisi hawata kanusha matamko hayo tutaendelea kuichukua kama ilivyo, hasa ukizingatia jinsi jeshi la polisi linavyopenda kuwahi kujikosha kwenye matukio kama haya.
 
Nimesikiliza Clouds FM wakimuhoji mjumbe wa nyumba Kumi wa eneo hilo
anasema walikuta vichaka wakafyeka na kujenga na hawajui ardhi ni mali ya nani
je ni halali kufanya hivyo bila utaratibu? kwa sentensi hiyo ni wavamizi?
serikali inatakiwa kuwahoji wananchi wa eneo hilo ili kupata ufafanuzi zaidi
pia kujua waliokwenda kubomoa majengo walitumwa na nani?

Vilevile si busara kwa mtu mmoja kumiliki eneo kubwa ekari 30 na kuendelea maeneo ya mjini. Hilo ni shamba kabisa wala sio kiwanja. Sasa inakuwaje mtu anaruhusiwa kumiliki shamba mjini huku wananchi wakitafuta maeneo ya kuishi.
 
now you attack me. shame on me. sawa.

media (hasa ya Tanzania) haiwezi kuwa uthibitisho wa mwisho. magazeti, redio na hata baadhi ya TV zimeripoti waliuliwa watu watano; gazeti la serikali yenu, Habari Leo limeripoti walikufa wawili.

shame on who? me or you?

kabla ya kumshambulia mtu inabidi ujiulize kwanza 'umejiandaa-andaaje' kabla ya kuweka post yako hapa jamvini.


Amini hiyo source pse, Ni kweli ITV ilionyesha hayo mahojiano so ni kweli kwani tuliwaona watu na sio taarifa tu bila picha.
 
Waliokwenda kuvunja nyumba walizidiwa nguvu na wananchi.

Sio nguvu na wananchi, Sema nguvu ya Umma.

Walianza taratibu, wakikamata kibaka na kuua wanasema "Wananchi wenye hasira kali". Sasa inakuja nguvu ya Umma kuwashughulikia mafisadi mjiandae.
 
Back
Top Bottom