Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Sishangai kama ni ukweli. Nanitaamini kuwa ni kweli hata ikiweje. Si tunawafahamu majibu yao.
Je kunatofauti gani na viongozi wakuu kama JK na Makinda kuhusisha kila wasichokipenda kusikia kikisemwa na dini, au CDM? hata maoni ya wanachi kuhusu mswada mbovu wa katiba, kila anayepinga ni CDM. Hawa nisawa na hao mapolisi hakuna tofauti

Wanashangaa maana hawakuzoea haya. Kwa sababu kupinga kwao ni kazi ya upinzani (Samahani kwa kutoka nje ya mada ya mauaji ya tegeta)
 
ITV ndivyo walivyomrekodi raia mmoja wa Tegeta. Sasa sijuhi kama polisi watakubali kuwa walisema hivyo. Kazi kweli kweli. Haya mambo ya kuvunjia watu nyumba ni mabaya sana na ni kinyume cha haki za binadamu. Watu wamekata tamaa wameamua kuuwa. Embu nambie mtu aje avunje nyumba uliyojenga kwa kudunduliza for more than 10 years. Eti eneo la muwekezaji ambaye kwake yeye ela si tatizo, he/she just got a loan from the Bank. Sishangai hawa wananchi kuchukua sheria mkononi aisee.

Huwezi kumiliki heka 30 hapa mjini wakati watu wanatafuta mahali pa kujihifadhi
 
hatuna serikali ndio maana yote haya yanatokea mchana kweupeee..

Siwezi kuwalaumu wananchi hata chembe, kwani hata mimi mtu akitokea kuvunja ninapoishi atakiona palepale..simsubiri.

Huu uhuni wakuliana mark-time wakati nyumba ni maisha ya mtu lazima ukome, pumba* zao.
 
polisi wamepewa jukumu na mamlaka kisheria kufanya kazi ya kulinda watu pamoja na mali zao. Polisi ni chombo serikali inatumia kuhakikisha wananchi na malizao wanalindwa. Matamko na matendo ya polisi yanaonyesha Msimamo wa serikali iliopo madarakani. Hii inakua si kweli pale serikali imapotoa tamko la kukemea na kuwawajibisha wote walioshindwa kufanya kazi yao kwa niaba ya serikali.
 
inauma sana na ishara tosha kuwa hii serikali inayoendeshwa na watu mbumbumbu wenye mawazo mgando (CCM). Wanafikiri watanzania wa enzi zile za naapa naaamini mbele ya chama....mapinduzi nitaiiilinda mpaka kufa....bado wapo?
 
Kwa hiyo chadema ndio waliwaambia raia wafanye mauaji?
duh nchi hii sasa noma.If CDM waliwaambia raia wafanye mauwaji basi dereva aliyeuwa wanamziki 13 bagamoya aliambiwa aulie jimbo la ccm.
 
hapa kuna mambo mengi yanachangai- kama vile uzembe wa serikali (polisi), rushwa, mahakama, wizara ya ardhi, hali ngumu ya maisha, watu kukosa utu, tamaa ya mali za duniani na kiburi cha kutosikia.
 
Poleni WaTz. Ni ishara mbaya kuwa Serikali ya Kikwete sasa imeifikisha nchi mahali hapo.
Nasikia alisema ktk mahojiano wakati wa uchaguzi wa 2010 ataka akumbukwe kuwa na nakuu "..niliitoa Tz hapa nikaifikisha hapa.." mwisho wa kunukuu. Labda ni kujiuliza kama ameifikisha Tz hapo mahala! Bila shaka ni pabaya hapana hata jina
 
Kuna kundi la wavamizi wa ardhi maeneo ya mbezi beach, mikocheni, tegeta na wameanza kuingia salasala kwa kushirikiana na watu wa ardhi wanaiba faili zima ardhi na wanabadili documents na kuweka zao halafu wanaenda kuvamia kiwanja ukienda kulalamika wanawaita wanawaomba documents wakiangalia unakuta zako hazipo hiyo ndio unakua umeachia kiwanja hata ukienda mahakamani

i can see transformation ya ufisadi, na serikali iliyoshindwa kuwahudumia wananchi kwa haki. if this is true, basi kila raia awajibike kulinda mali na maisha yake mwenyewe. na sisi tusio na uwezo ndo imekula kwetu for good
 
Zaidi ya watu 5 wamekufa ktk mapigano ya kugombea ardhi kati ya wananchi na mabaunsa wa kampuni ya udalali ya Mwangata huko Mivumoni Tegeta. RADIO1 STEREO

TUSISAHAU KUWA SERA YA ARDHI ALIIANDIKA ISSA SHIVJI KWA STAILI ILE ILE ANAYOTAKA KATIBA MPYA IANDIKWE. MATOKEO YAKE NI MIGOGORO YA ARDHI ISIYOISHA NA WAGENI KUJA KUWANYANGANYA WANANCHI ARDHI YAO. MIFANO IKO MINGI, TEGETA NDIO WA LEO TU. TUKIMSIKILIZA SHIVJI TENA LEO KATIKA MASWALA YA KATIBA MATOKEO YAKE TUTACHINJANA KAMA KUKU.


Grabbed_Frame_1.jpg

Grabbed_Frame_2.jpg

Grabbed_Frame_4.jpg

02+%25281%2529.JPG


 
Last edited by a moderator:
TUSISAHAU KUWA SERA YA ARDHI ALIIANDIKA ISSA SHIVJI KWA STAILI ILE ILE ANAYOTAKA KATIBA MPYA IANDIKWE. MATOKEO YAKE NI MIGOGORO YA ARDHI ISIYOISHA NA WAGENI KUJA KUWANYANGANYA WANANCHI ARDHI YAO. MIFANO IKO MINGI, TEGETA NDIO WA LEO TU. TUKIMSIKILIZA SHIVJI TENA LEO KATIKA MASWALA YA KATIBA MATOKEO YAKE TUTACHINJANA KAMA KUKU.


Uuuwii!

Natamani ningeruhusiwa kisheria nivue nguo nitembee uchi hadharani kwa uongo unaomsingizia Issa Shivji.

Maoni ya Shivji ambayo yalilenga kuepusha migogoro ya ardhi hayakuzingatiwa na serikali, baadaye Shivji aliandika kitabu na alitumia muda wake mwingi kufanya presentations kufafanua madhara ya sheria hii. Kuna nchi ya Afrika walichukua mapendekezo ya Shivji na kuyatumia kwa kiasi kikubwa kama yalivyo bahati mbaya sikumbuki jina lake sasa hivi.

Tafadhali usimchafue babu wa watu hana akili finyu kama nyie
 
That's very true. Huyu jamaa ahache kupotosha umma ama kwa makusudi au kwa kukurupuka. Serikali yetu haishauriki! Sera ya Ardhi ilichangiwa na wana harakati wengi lakini serikali ilitupilia mbali hoja zao!

TUSISAHAU KUWA SERA YA ARDHI ALIIANDIKA ISSA SHIVJI KWA STAILI ILE ILE ANAYOTAKA KATIBA MPYA IANDIKWE. MATOKEO YAKE NI MIGOGORO YA ARDHI ISIYOISHA NA WAGENI KUJA KUWANYANGANYA WANANCHI ARDHI YAO. MIFANO IKO MINGI, TEGETA NDIO WA LEO TU. TUKIMSIKILIZA SHIVJI TENA LEO KATIKA MASWALA YA KATIBA MATOKEO YAKE TUTACHINJANA KAMA KUKU.


Uuuwii!

Natamani ningeruhusiwa kisheria nivue nguo nitembee uchi hadharani kwa uongo unaomsingizia Issa Shivji.

Maoni ya Shivji ambayo yalilenga kuepusha migogoro ya ardhi hayakuzingatiwa na serikali, baadaye Shivji aliandika kitabu na alitumia muda wake mwingi kufanya presentations kufafanua madhara ya sheria hii. Kuna nchi ya Afrika walichukua mapendekezo ya Shivji na kuyatumia kwa kiasi kikubwa kama yalivyo bahati mbaya sikumbuki jina lake sasa hivi.

Tafadhali usimchafue babu wa watu hana akili finyu kama nyie
 
Haya sasa sebene linaanza, kamanda wapoli mkoa wa Kinondoni amekanusha madai kwamba polisi walipewa taarifa wakachelewa kufika.
Source: BBC Swahili

Maoni yangu:
The Mighty is always right!
 
Haya sasa sebene linaanza, kamanda wapoli mkoa wa Kinondoni amekanusha madai kwamba polisi walipewa taarifa wakachelewa kufika.
Source: BBC Swahili

Maoni yangu:
The Mighty is always right!
Haya sasa, nani mkweli nani muongo? Wananchi wa JMT vs Jeshi la Polisi.
 
watu wanapoteza muda na wimbo wa AMANI, tengenezeni justice system inayofanya kazi, mtu akienda kinyume na sheria ANASHUGULIKIWA.
sasa hivi hakuna sheria TANZANIA, kama huna "connection" au hela hupati kitu, hata kilicho chako unanyang'anywa. Na wananchi wengi wanalijua hili.

Mnataka hawa wananchi wa Tegeta wafanye nini? mtu anaishi na familia yake kwenye nyumba yake , alioijenga kwa jasho lake, unataka kuja siku mmoja umtoe, alafu familia akailaze wapi? tena zaidi ya hapo wamepiga simu polisi lakini polisi wamekataa kwenda. Serikali haijali kama fujo hazitishiii utawala wake. Pale UDSM wanafunzi hata nje ya compound hawakutoka, FFU wakaanza kuwapiga na kuzuia maandamano yao. Sasa unataka huyu mwananchi wa Tegeta anyanyaswe kiasi gani na wananchi wenzake, polisi na mahakama hadi achukue hatua.

Tu focus effort yetu kuhakikisha haki inapatikana, mtu akileta fujo tunatumia sheria iliopo na kutoa hakumu kwa HAKI. Watu wataona hata aibu kufanya haya mambo.

Kama katiba inaruhusu marais waliotangulia kugombea tena, ningeshauri Mkapa agombee urais. Alikua serious sana. Nchi imeyumba sana. Amani inazidi kutoweka
 
Kama katiba inaruhusu marais waliotangulia kugombea tena, ningeshauri Mkapa agombee urais. Alikua serious sana. Nchi imeyumba sana. Amani inazidi kutoweka

hapana , nikuhakikisha nguvu ya kuchagua RAIS inrudishwa kwa wananchi. Kwa hali iliopo sasa, rais anachaguliwa na wenye pesa ndani ya CCM, kisha wananchi wanapitisha chochote kile CCM inachoweka mezani...CCM ikijua kwamba wananchi wanachagua RAIS wa JMT kwa vigezo vinavyoeleweka, basi itawalazimu kumteua mgombea ambaye atakua anajibu maswali na matatizo ya wananchi, haya mambo ya kurudisha watawala wa zamani ndio mambo yakutengeneza madikteta na kusababisha maafa ya vita miaka ya mbele, kwani hakuna dikteta anayetoka hivi hivi.
 
Back
Top Bottom