Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

TUSISAHAU KUWA SERA YA ARDHI ALIIANDIKA ISSA SHIVJI KWA STAILI ILE ILE ANAYOTAKA KATIBA MPYA IANDIKWE. MATOKEO YAKE NI MIGOGORO YA ARDHI ISIYOISHA NA WAGENI KUJA KUWANYANGANYA WANANCHI ARDHI YAO. MIFANO IKO MINGI, TEGETA NDIO WA LEO TU. TUKIMSIKILIZA SHIVJI TENA LEO KATIKA MASWALA YA KATIBA MATOKEO YAKE TUTACHINJANA KAMA KUKU.

Sera ya ardhi inaingiaje hapa? Umiliki wa ardhi na taratibu zake zinafahamika, kwamba raia watz wanashikilia tu lease kwa maximum of 33 years, na sioni ubaya wowote hapa.. ishu hapa ni kwa serikali legelege ambayo pamoja na tz kuwa na eneo kubwa la kutosha bado inakabiliwa na tatizo la makazi holela na migogoro ya ardhi isiyo na kichwa wala miguu kutokana na managament mbovu ya rasilimali hii adhimu.
 
lazima tuanze kujadili kati ya wamiliki wa mashamba makubwa na wananchi na tabia ya kuvamia mashamba ya watu
 
Eneo lenye mgogoro lina ukubwa wa kiasi gani...??


EKARI 104 NI SHAMBA La DANIEL CHACHA mwenye hati miliki ya ardhi hiyo lakini kutokana na madai ya wananchi ya upungufu wa ardhi basi wameamua kuvamia eneo la mtu huyu
 
EKARI 104 NI SHAMBA La DANIEL CHACHA mwenye hati miliki ya ardhi hiyo lakini kutokana na madai ya wananchi ya upungufu wa ardhi basi wameamua kuvamia eneo la mtu huyu

Inasikitisha sana...Wananchi wanapoamua kujichukulia sheria mikononi na kuvamia eneo la mtu analomiliki kisheria.

Uhaba wa Arthi..!!!

Tangu lini Tanzania ikawa na uhaba wa Arthi??!!

Wananchi wameamua kuwa wakorofi sijui ni elimu duni, tamaa au jeuri tu!!!!
 
Inasikitisha sana...Wananchi wanapoamua kujichukulia sheria mikononi na kuvamia eneo la mtu analomiliki kisheria.

Uhaba wa Arthi..!!!

Tangu lini Tanzania ikawa na uhaba wa Arthi??!!

Wananchi wameamua kuwa wakorofi sijui ni elimu duni, tamaa au jeuri tu!!!!

Lakini pia ni tabia mbaya, mtu mmoja kuhodhi hekali 104 kati kati ya makzi ya watu bila kuziendeleza!

Serikali inapaswa kuweka mipango madhubuti ya ukuaji wa mji, pale eneo linapokuwa makazi, basi zile hati za mashamba zifutwe ili zigawiwe ktk viwanja na viendelezwe!
 
EKARI 104 NI SHAMBA La DANIEL CHACHA mwenye hati miliki ya ardhi hiyo lakini kutokana na madai ya wananchi ya upungufu wa ardhi basi wameamua kuvamia eneo la mtu huyu

Ni la baba yake Daniel. Mzee Wilson K Chacha. Huyu mzee ni kabaila sana. Anamiliki maeneo kadha hapa Dar kihalali kabisa. Eneo jingine maarufu analomiliki ni ile NAPOCO ya zamani pale Banana ambalo amepangisha baa na maduka mengi.
 
hayo ndiyo matunda ya kuwa na serikali ya kifisadi, serikali ya watu poa! bado tutarajie makubwa zaidi! kwani sheria zetu zimeonekana kuwa kama KISU badala ya MSUMENO! haki tena hakuna mbele ya pesa!:help:
 
Siungani na walioamua kuvunja nyumba bali ninachotaka ni Tujiulize hii nchi yetu inaelekea wapi?Hivi watu wanaweza kuamua kuvamia kichaka na kuhamia?Hali ikiendelea ivi kuna wakati watu wataamua kuja kuhamia kwenye nyumba yako kwa sababu unazo tatu au nne .
Vile vile watachukua gari lako moja kisa tu wewe una magari zaidi ya mawili na wao wana shida ya usafiri.
 
EKARI 104 NI SHAMBA La DANIEL CHACHA mwenye hati miliki ya ardhi hiyo lakini kutokana na madai ya wananchi ya upungufu wa ardhi basi wameamua kuvamia eneo la mtu huyu

Ninachojua ni kwamba watu wote waliokuwa na mashamba eneo lote hilo la Mivumoni wamenyang'anywa na serikali na kupima viwanja 20,000 jijini. Katika walionyang'anywa hata mimi nilikuwamo niaachiwa kiwanja kimoja tu na kulipwa fidia, mwingine ni Dr Kiwia ambaye aliwahi kuwa Meneja wa kiwanda cha Wazo Hill cha cement. Sasa huyo baba yake Chacha ameachiwa vipi hekari 104 katikati ya zoezi hilo la wizara? Kumbe ina maana zoezi la kunyang'anya mashamba liliendeshwa kibaguzi???
 

Samahan wakuu kwa kukumbushia hii stori 🙏🙏🙏
Leo kwenye pita pita zangu nikakutana na hii stori mmoja wa bausa anasimulia tukio lilivokua
Daaah hatar Sana enzi hizo mie nlkua darasa la saba Leo ndiyo nmejua kumbe Hapa Tanzania kumeshatokea matukio ya kinyama kamahaya aisee
Video ya simulizi ipo youtube
Screenshot_20230225-023146.png
 
Back
Top Bottom