Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

Mapigano ya kugombea ardhi yaua Tegeta

vyovyote vile iwe halali au siyo wana tegeta walilinda mali zao kikamilifu na wamenifurahisha sana.
 
A little piece of good demonstration if the dead ones are the so called bouncer
 
vyovyote vile iwe halali au siyo wana tegeta walilinda mali zao kikamilifu na wamenifurahisha sana.

Marytina una hasira kweli. Ndo maana hata kwenye ile thread nyingine jamaa kadai wewe si "ke"
 
Jamani huku tuendako siko kabisa. Kwanini mtu avamie eneo la mtu mpaka anajenga viongozi na mwenye shamba wakae kimya? Hakika huu ni mwanzo mbaya sana. Mungu tuepushe na hali hii.
 
Mwenyekiti wa Serikali za mitaa Bw Deogratius Kamugisha amesima ofisi yake iliwasiliana na jesho la polisi hawakupata Msaada.
Wakampigia Said Mwema, Said Mwema akaambia wampigie Kova, Kova akasema analeta polisi.
Wananchi wakaona haitoshi, wakamtuma mtu (Ali Mgulu) aende polisi moja kwa moja kuomba msaada Ali akajibiwa na polisi "ngoja wakaune alafu huyo wamwisho atakaye pona aje atoe taarifa" na Diwani aliingia wakati polisi wanatoa hayo matamko.

SOURCE ITV news YouTube - Habari via ITV -Watu watano wapigwa mapanga mpaka kufa- Jeshi la polisi liko wapi?

Ila serikali isipuuzie, Rwanda walianza hivi hivi, maana kwa sasa inavyoonekana Tanzania ni kama bomu lililotegwa muda wowote kama hatatokea kulitegua basi linaweza kulipuka anytime, cheki Hapa Rwanda ilivyokuwa,......
 
Last edited by a moderator:
Mwema ndiye wa kwanza anayepaswa ajiuzuru, haiwezekani wewe kama bosi wa polisi unapigiwa unasema mpigie kova, si umpigie wewe mwenyewe. kama gongolamboto mkuu wa majeshi anawataka wananchi waende mbali sijui km ngapi, mibasi ya jeshi imewekwa tu makambini, sasa si wangewapelekea usafiri wa kuwapeleka huo umbali anaoutaka, hili nchi watu wanapeana kazi tu

Ni kweli kabisa, haiwezekani kiongozi wa wadhifa wake atoe tamko kama hilo wakati hali imefikia pabaya namna hiyo.ndio maana hata huyo kijana wao polisi akaishia kutoa tamko la mzaha mzaha. Mimi naonda umefika wakati Said Mwema na huyo polisi alie toa RUKSA wawajibishwe na wizara husika, lasivyo waziri wa mambo ya ndani apaki vilago.
 
Hatuna serikali kama ni hivi....... limebaki jina tu.
 
Kwani video hujaona? Mwananchi anaongea kwa maneno yake. Kama polisi hawata kanusha matamko hayo tutaendelea kuichukua kama ilivyo, hasa ukizingatia jinsi jeshi la polisi linavyopenda kuwahi kujikosha kwenye matukio kama haya.
Mkuu naunga mkono maoni yako,sambamaba na hilo tujiulize panapotekea matukio kama hayo nani anapaswa kuwa wakwanza fika sehemu ya tukio waandishi wa habari au polisi?.Kama hakutakuwa na maelezo ya kutosha juu ya tuhuma hizi ni wazi kutegemea polisi kama walinzi wa usalama wa raia itakuwa haina maana!
 
now you attack me. shame on me. sawa.

media (hasa ya Tanzania) haiwezi kuwa uthibitisho wa mwisho. magazeti, redio na hata baadhi ya TV zimeripoti waliuliwa watu watano; gazeti la serikali yenu, Habari Leo limeripoti walikufa wawili.

shame on who? me or you?

kabla ya kumshambulia mtu inabidi ujiulize kwanza 'umejiandaa-andaaje' kabla ya kuweka post yako hapa jamvini.

Na hakuna haja ya kumshambulia mtu hapa faza, dont entertain that. Hapa tuzigonganishe hoja tu, na hatufahamiani by the way...
 
jimbo la chadema hilo......!

Join Date : 27th January 2008
Location : manzese
Posts : 1,908
Thanks1,222Rep Power : 26
kumbe mauaji ya morogoro kati ya wafugaji na wakulima, ajali za mabasi na ukimwi hapo nyuma yako uwanja wa fisi manzese ni majimbo ya chadema.
 
Inatisha,ila wacha na hili liwe fundisho kwa serikali,kampuni za udalali,wananchi na wote. Kama ushawai kuvunjiwa nyumba ndio utajua hili lililofanyika, mimi hata kwa imagination zangu tu naona siku mtu akija kuvunja ninapoishi ndio utakuwa mwisho wake ama wangu.

Watanzania tusipende kubembeleza haki zetu, pia tukajifunze kuipigania haki; kwani ukicheka na nyani utavuna mabua.

Lakini kama ikihakikishwa sio haki,na mahakama au misingi ya sheria basi si riziki tukubali pia.
 
maneno mazito hayo mkuu. natamani uweke uthibitisho, au unyamaze tu tuendelee kuomboleza.


ITV ndivyo walivyomrekodi raia mmoja wa Tegeta. Sasa sijuhi kama polisi watakubali kuwa walisema hivyo. Kazi kweli kweli. Haya mambo ya kuvunjia watu nyumba ni mabaya sana na ni kinyume cha haki za binadamu. Watu wamekata tamaa wameamua kuuwa. Embu nambie mtu aje avunje nyumba uliyojenga kwa kudunduliza for more than 10 years. Eti eneo la muwekezaji ambaye kwake yeye ela si tatizo, he/she just got a loan from the Bank. Sishangai hawa wananchi kuchukua sheria mkononi aisee.
 
Mimi kinachoniumiza ni watu kupoteza maisha!!!
Damu iliyomwagika haiendi yenyewe lazima tu damu nyingine itamwagwa hivi karibuni, iwe Tegeta au sehemu nyingine damu ya mtu si kama ya wanyama wengine wanaotolewa kafara.
Damu ya mtu ikimwagika hakika hasara yake ni kubwa.
Serikali ingeweza kuzuia hayo mauaji kwa polisi kuwahi eneo la tukio lakini kwa kuchelewa kwao wamesababisha damu kumwagika.
Serikali na Jeshi lake la polisi wanawajibika kwa njia moja au nyingine kwa haya mauaji ya Tegeta kwani yalikuwa yanazuilika!!!
 
Tatizo la mahakama zetu, huwezi kmshinda mwenye nazo. Ndio maana kina Ditopile waliua lakini hawakuwa na murder case. Yaani mtu nyumba imevunjwa alafu utatoa wapi huo muda na ela za kuhudhuria kesi miaka kumi? Hata mimi aisee nitaua mtu atakayejidai kuvunja nyumba yangu. Serikali imekuwa zembe kwenye kupima viwanja, why should citizens pay for that? Nani anataka kujenga holela? Viwanja vilivyopimwa vinapatikana wapi? Nchi za wenzetu eti serikali inataka jenga barabara watu kuhama ni negotiable wakigoma wamegoma. That's why barabara nyingine zinapita juu na nyingine zinadiverge.

Inatisha,ila wacha na hili liwe fundisho kwa serikali,kampuni za udalali,wananchi na wote. Kama ushawai kuvunjiwa nyumba ndio utajua hili lililofanyika, mimi hata kwa imagination zangu tu naona siku mtu akija kuvunja ninapoishi ndio utakuwa mwisho wake ama wangu.

Watanzania tusipende kubembeleza haki zetu, pia tukajifunze kuipigania haki; kwani ukicheka na nyani utavuna mabua.

Lakini kama ikihakikishwa sio haki,na mahakama au misingi ya sheria basi si riziki tukubali pia.
 
maneno mazito na nadhani yana ukweli sana tu, unless tunataka kumziba mdomo

Hayo maneno yataendelea kuwa ukweli tokana na mazingira ya tukio. Kama hawakusema hivyo kwa nini hawakuwepo eneo la tukio kuzuia madhara? It is obvious they said what the woman quoted
 
semeni polisi sio eti serikali... Being too general haisaidii.. Watanzania tunatabia yakuchukua sheria mkononi na polisi wanatabia yakudharau na kuchelewa katika matukio.
 
And just to remind you, mnakumbuka wananchi walivamia shamba la marehemu governor Balali? FFU wote waliamia eneo la tukio na lilikuwa ni pori tu. Sasa hawa wananchi wanpigana nyumba zao zisivunjwe, polisi wanaleta majibu ya mzaa. I also believe police is there for those who have not have not.

Kwa kauli hiyo ya POLISI ni kwamba hawajali wananchi wanyonge wao wanawajali Mafisadi tu, kama wangepigiwa simu wakaambiwa kuna maandamano ya CHADEMA wangetoka mbio kama mbwa mwizi
 
Ni serikali kwa sababu ili tatizo lina cut accross. Upimaji viwanja ni kazi ya wizara husika. Ulinzi wa raia ni kazi ya wizara husika. Upatikanaji wa haki mahakamani ni kazi ya wizara husika. Hapo kwa haraka haraka ni wizara tatu zinahusika na tukio. Kusema serikali nilikuwa sawa kabisa!

semeni polisi sio eti serikali... Being too general haisaidii.. Watanzania tunatabia yakuchukua sheria mkononi na polisi wanatabia yakudharau na kuchelewa katika matukio.
 
Back
Top Bottom