Kazakh destroyer
JF-Expert Member
- Nov 16, 2017
- 3,967
- 8,099
Pole akhy creedfx mimi nina mengi ya kukushauri mdogo wangu kwasababu nina historia ndefu kwenye hiyo bahari na nimepata kuumizwa kwa kiwango kisichomithilika, kupenda mahali usipopendwa ni kitu kinauma sana kama utapenda uje PM ntakupa mwongozo na ushauri wangu, ila kwa ufupi mkubwa nikwambie kuwa huyo binti si fungu lako mdhanie Allah kheri na ujifunze kusema maneno haya:-
لعله خير
"huenda hivyo ndio kheri"
Tizama mdogo wangu Allah anajua zaidi kuwa wewe unampenda zaidi huyo binti, na yeye anakuhurumia na kukuonea huruma zaidi kuliko unavyojionea mwenyewe, ila amini kwamba yeye anajua kuwa huyo binti sio stahiki yako ijapokuwa moyo wako umezama kabisa, anakuepusha na huyo binti kwa mapenzi na kukuhurumia si kwa makusudio ya kukuumiza na kukujeruhi, mola wetu subhaanah hufanya mambo yake kwa hekma kubwa.
Ambaye ameandikwa kwaajili yako yupo mahali anakusubiri na anakutafuta wewe pia anasubiri usiku na mchana utafika lini, usilie mdogo wangu mola wako anakupitisha njia ngumu kwa hekma na kukuhurumia, tizama mwanamke anaekujibu hivyo ni wazi hatakuwa na huruma na wewe, na hatokujali maana ana kiburi na anataka kuwa na mamlaka juu yako bali wewe umempenda zaidi na yeye hana haja na wewe, kwa kitu gani uidhalilishe nafsi yako kwa mtu asiyekuhitaji?! jikaze mdogo wangu mbona ni wiki moja tu utamsahau, najua kuna warning signs nyingi tu unazipata kupitia heart whispers kuwa ni yeye kweli!? ni huyu niliyekuwa namsubiri? ila unazipuuza kwasababu ya upofu wa mapenzi, jikaze na uamini moyo wako una thamani sio wa kuumizwa kila siku.
Basi nisiongee sana hapa ila wakati mwingine ukitaka kuoa fuata procedures za uislamu, peleka taarifa kwao wakikukataa achana nao usiwalazimishe na hutoumia sana, ila ukipita mwenyewe kwa njia unazozijua wewe maumivu yake ni fatal.
".......lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu, na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu, na Allah anajua na nyinyi hamjui kitu."
Qu'ran 2:216
لعله خير
"huenda hivyo ndio kheri"
Tizama mdogo wangu Allah anajua zaidi kuwa wewe unampenda zaidi huyo binti, na yeye anakuhurumia na kukuonea huruma zaidi kuliko unavyojionea mwenyewe, ila amini kwamba yeye anajua kuwa huyo binti sio stahiki yako ijapokuwa moyo wako umezama kabisa, anakuepusha na huyo binti kwa mapenzi na kukuhurumia si kwa makusudio ya kukuumiza na kukujeruhi, mola wetu subhaanah hufanya mambo yake kwa hekma kubwa.
Ambaye ameandikwa kwaajili yako yupo mahali anakusubiri na anakutafuta wewe pia anasubiri usiku na mchana utafika lini, usilie mdogo wangu mola wako anakupitisha njia ngumu kwa hekma na kukuhurumia, tizama mwanamke anaekujibu hivyo ni wazi hatakuwa na huruma na wewe, na hatokujali maana ana kiburi na anataka kuwa na mamlaka juu yako bali wewe umempenda zaidi na yeye hana haja na wewe, kwa kitu gani uidhalilishe nafsi yako kwa mtu asiyekuhitaji?! jikaze mdogo wangu mbona ni wiki moja tu utamsahau, najua kuna warning signs nyingi tu unazipata kupitia heart whispers kuwa ni yeye kweli!? ni huyu niliyekuwa namsubiri? ila unazipuuza kwasababu ya upofu wa mapenzi, jikaze na uamini moyo wako una thamani sio wa kuumizwa kila siku.
Basi nisiongee sana hapa ila wakati mwingine ukitaka kuoa fuata procedures za uislamu, peleka taarifa kwao wakikukataa achana nao usiwalazimishe na hutoumia sana, ila ukipita mwenyewe kwa njia unazozijua wewe maumivu yake ni fatal.
".......lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu, na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu, na Allah anajua na nyinyi hamjui kitu."
Qu'ran 2:216
