Maoni na Ushauri kwa Joshua Nassari

Maoni na Ushauri kwa Joshua Nassari

Jpm ananunua wapinzani kwa mamilioni huku mtaani tunalazimishwa vitambusho vyake kilazima kwa 20 elfu
 
Mm huwa mrengo wangu wa kisiasa ni uoinzani but huyu jamaa mm wala simsupport wala kumuonea huruma! Yaan vikao vi3 ushindwe kutokea hata kimoja? Sheria unaijua na hata kama una mgonjwa wewe suyo dr, kwan alishindwa kuja kuhudhuria for one week halafu akaondoka? Unakaaje muda huo? Play the system! Hudhuria hata 2 days sepa! What a fool

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iyo sheria ya kujieleza CDM wamegeuza yaani hawa jamaa ujanja mwingi mbele kiza mkuu.

Je uhisi kuna usaliti kutoka CDM katika hili mkuu? wabunge wote wa CDM pamoja na yule Mrema walikuwa awajui sheria,taratibu na kanuni za Bunge?

Sent using Jamii Forums mobile app
Nachoelewa Viongoz wa chadema wamefanikiwa kuwageuza misukule wanafuasi wao.Wafuasi wa chadema wanaamini viongoz wao ni MALAIKA, kila kosa watakalo fanya lazima watafute pa kuwaficha waonekane hawana ttz.Mikutano mitatu ni mingi sana,inamaana hata ule mkutano wa bunge la bajeti ambao ni miezi mitatu hakuhudhuria. Inamaana muda wote huo ilikua ngumu kwa yeye kuomba ruhusa au kupata mda kidogo na kumuona speaker direct kuwa nina shida hii na hii.

Ingekua hajahudhuria kikao kimoja tungesema kweli ilikua emergency, sasa mikutano mitatu, maana yake vikao zaidi ya 50 kama sikosei. Huyu mtu hata siku moja hakuwahi pata nafasi kuja kuomba ruhusa. Mara yuko masomoni, yuko kutafuta misaada kwa ajili ya wananchi na baada ya kutumbuliwa anakuambia alikua anauguza mke. Hivi huko Ufipa hamna hata mmoja mwenye akili timamu kufanya analysis ya hizi kauli na kujua ukweli ni upi?

Speaker kamlima barua iliyojaa vifungu vya sheria na hakuna hata kifungu kimoja kinasema mbunge ataitwa kamati ya maadili au sehem yyt ajieleze. Hawa bavicha utetezi wa speaker kumhoji Nasari wanatumia vifungu gani?Wanataka kuingiza vifungu vya huruma mara hekima, Huu ndio utaratibu?Mbona maamuzi mengine mfano Jpm hela za uhuru kujenga barabara ni uamuzi wa hekima na busara lkn walikua wanapinga kuwa hadi bunge lijadili?Au hizi sheria zina macho kwamba kuna sehemu zione na sehem zisione?

Inawezekanaje Nasari kutohudhuria mikutano mitatu Mbowe, Mashinji, Lema na wabunge wote wasijue?Hiki ni chama Au genge la WAHUNI?Au walikua wanajua na saiz wanawahadaa wananchi?

Naamini Chadema na Nasari wanajua nini wanafanya na mtaji mkubwa ni wafuasi wao wenye AKILI za kizombie.

The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
 
Mm huwa mrengo wangu wa kisiasa ni uoinzani but huyu jamaa mm wala simsupport wala kumuonea huruma! Yaan vikao vi3 ushindwe kutokea hata kimoja? Sheria unaijua na hata kama una mgonjwa wewe suyo dr, kwan alishindwa kuja kuhudhuria for one week halafu akaondoka? Unakaaje muda huo? Play the system! Hudhuria hata 2 days sepa! What a fool
kwanza ruhusa alipewa na nani maana kuuliza swali siyo kupata jibu, jibu ndiyo linakuhalalisha wewe ulichokiuliza hana hata barua ya ruhusa utasema kaonewa na sheria inasemaje
 
Nadhani cha kufanya ni yeye ajipange kugombea tena ubunge tu. Kwenye kampeni kama wapiga kura wataelewa hoja zake haitakuwa tabu kushinda
Ushauri wako siyo sahihi, huyu dogo hahudhurii bungeni sasa agombee kufanya nini? Kwa mwaka bunge lina mikutano minne, yeye hajahudhuria mikutano mitatu mfululizo halafu eti agombee tena? Nitashangaa watakaomchagua.
 
Sijapata nafasi ya kumuangalia ila kuanzia mwanzo wa sinema hii tayari tumeshaujua mwisho wake utakua ni nini! Inaelekea director wa hizi movie hana uzoefu wa kutosha na kazi zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jimbo walipoteza wapinzani wakalichukua tena kwa siku za karibuni? Na umewasikikiza wazee wa kimeru walichokisema?
Hicho kitu hakipo, kwa kifupi tu
wazee wa kimeru wapi babu? mimi niko meru na wale uliowaona ni wazee wa ccm walioandaliwa kukusanyika chini ya mti wa kimila wakajifanya ni kuwa hawamtaki ila ukweli ni kuwa Joshua alikuwa anakubalika sana huku! hayo unayoona ni muvi kama za jiwe mzee. ila all in all simuamini Joshua na huenda kaunga juhudi kwa njia nyingine mpya!
 
Siasa za tz kwa sasa ni unbelievable, Japo namkubali sana Nassari ila kwa hili moyo wangu umekuwa mzito kukubaliana nae. naona analeta hoja za madeko zaidi badala ya kujikita kisheria na sio kifamilia.
NB: ujinga wa kutojua sheria hauzuii sheria kukuadhibu.


na kweli mkuu analeta deko ngoja afunzwe tu kwakwel...mie pia simwqmin kbs
 
Ninachojua tu na nina uhakika nacho ni kwamba Spika Ndugai ' hajakurupuka ' katika hili na kwamba Vigezo vyote na Masharti yote vilizingatiwa katika ' Kumpoka ' Jimbo Mbunge ' Mpokwaji ' Joshua Nassari. Sheria ni Msumeno na si kila akifanyacho Spika Job Ndugai ni Kibaya kwakuwa tu kuna Watu wana Chuki nae ambazo nyingi zimetawaliwa na kuchochewa na Siasa na Itikadi zetu. Binafsi nimeshawahi Kuanzisha ' Threads ' kadhaa hapa za ' Kumchana / Kumnanga / Kumsiliba / Kumsema ' Spika Ndugai kwa baadhi ya mambo katika ' Utendaji ' wake ila kwa hili naungana nae tena kwa 100% na hata huyo Mbunge ' Mpokwaji ' sina uhakika kwamba hata akienda / akikimbilia huko Mahakamani kuna atakachokipata kwani Watu walishachungulia mbali kwa marefu na mapana yake hadi ndiyo wakaamua Kumla Mtu Kichwa tena mapema ( asubuhi ) tu.
Vipi kuhus Bunge kumuita kumhoji Nasari kabla ya kumfuta kazi??
 
Dogo msanii, kifupi kapiga hela kwa staili ambayo lazima ilete mkanganyiko na mwisho wa siku blah blah zitapigwa litaisha dogo atatulia na mkwanja akijifanya bado CDM, ila ajue wameshamblackmail tayari ataendelea kuwa kondom akiwa CDM labda CDM wastuke wamfukuze.. Nina mashaka Lema analijua hili na ndiye mwalimu wa dogo kwenye hili, this is business bwana..

CDM timueni haraka huyu dogo, Mwambieni Lema aache usanii.
 
Ni hivi, Nassari kachukua pesa ya ccm muda mrefu, tena alichelewa kuondoka maana alikuwa anajiuliza ataungaje mkono juhudi. Hawa wakina Nassari ndio wanatupa muda mgumu kuutetea upinzani.
 
Ninachojua tu na nina uhakika nacho ni kwamba Spika Ndugai ' hajakurupuka ' katika hili na kwamba Vigezo vyote na Masharti yote vilizingatiwa katika ' Kumpoka ' Jimbo Mbunge ' Mpokwaji ' Joshua Nassari. Sheria ni Msumeno na si kila akifanyacho Spika Job Ndugai ni Kibaya kwakuwa tu kuna Watu wana Chuki nae ambazo nyingi zimetawaliwa na kuchochewa na Siasa na Itikadi zetu. Binafsi nimeshawahi Kuanzisha ' Threads ' kadhaa hapa za ' Kumchana / Kumnanga / Kumsiliba / Kumsema ' Spika Ndugai kwa baadhi ya mambo katika ' Utendaji ' wake ila kwa hili naungana nae tena kwa 100% na hata huyo Mbunge ' Mpokwaji ' sina uhakika kwamba hata akienda / akikimbilia huko Mahakamani kuna atakachokipata kwani Watu walishachungulia mbali kwa marefu na mapana yake hadi ndiyo wakaamua Kumla Mtu Kichwa tena mapema ( asubuhi ) tu.
Mimi siyo mtaalam wa sheria, nataka kujua kama akienda mahakamani kuweka pingamizi la kufutiwa ubunge hata kama upande wa speaker utashinda lkn kutokana na utamaduni wa mahakama zetu kuchelewesha hukumu za kesi, je, hukumu ikitoka baada ya Julai hata kama kashindwa kesi, sihakutakuwa tena na uchaguzi ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ameongea na waandishi wa habari kwakuwa mbowe alimwambia ajitete kwa watu ili atoe yaliyoko moyoni yaani apangue hija za spika kupokwa ubunge lakini hakuwa tayari maana alichokifanya anajua ameunga juhudi za awamu ya tano ndiyo maana hata maswali alikataa alijuwa ataumbuka tuuuu
 
Iko namna, kama ulimuangalia vyema haswa ukikumbuka na enzi zake, kuanzia akiwa bungeni, nje ya bunge, mpaka nyakati za kiflash cha madiwani, tone ya ukakamavu ya kikamanda nq namna wanavyoongeaga kwa msisitizo with solid evidence utagundua iko namna ila muda utasema tu tungoje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio vimemgharim sasa, ila mi naona ni halali tu alivyoliwa kichwa kwsbb kuna wabunge wengi tu wanawake wanajifungua na baada ya muda wanaendelea na majukum yao.
Kuna wabunge wa kiume wengi tu ambao wake zao wamejifungua still haikuathiri kazi zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yule dogo mjinga sana....kwani yeye ni wa kwanza kuoa na mke kujifungua....sisi waajiriwa, wake zetu wanajifungua tunachukua 3 days za paternity leave kisha tunarudi kibaruani mtoto hata 7 bado?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu. ndugai kaisha puuuzwa maana yeye anajulikana anayemtumikia. Shida ni kwa bwana mdogo nassari maelezo yake yanajichanganya mnooo. Labda hivyo vielelezo Vingine alivyotamba kua navyo anasubiri kuvionyesha mahakamani kama kweli ataenda.


Tatizo maelezo yake yalijikita zaidi kuomba huruma ya spika, mara aanze kumkumbusha jinsi alivyokula ndafu.mara a mwambie kua yeye ni mzazi.kweli Joshua ni wa kumwamini spika? .kiasi kwamba akashindwa kabisa kuzuia mianya ya spika kutumia.
Alipokaa kimya inakuwa taabu, akiongea mnamtazama kwa jicho la tatu. Huyo Ndugai mbona amjatazama kwa jicho la ziada nae? Mnadhani alilofanya ni sahihi? Ebu acha kuondoa train kwenye reli bhana

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alipokaa kimya inakuwa taabu, akiongea mnamtazama kwa jicho la tatu. Huyo Ndugai mbona amjatazama kwa jicho la ziada nae? Mnadhani alilofanya ni sahihi? Ebu acha kuondoa train kwenye reli bhana

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli viongozi wa upinzani wanapimwa kwa viwango tofauti kabisa,wakidhulumiwa wataambiwa wazembe,wakionewa wanaambiwa ni watu wa kulalamika,sasa sijui wafanyeje?
 
Back
Top Bottom