Manji na Gwajima wamelala mahabusu ipi?

Manji na Gwajima wamelala mahabusu ipi?

Sijajua Mkuu umri wako na ufatiliaji wako wa mambo ya siasa nchini.

Hivi kwa akili zako unaamini kabisa Wamasheria wa serikali watamzidi kesi Manji mpaka Manji afike hatua ya kuhama nchi baada ya kesi?

Kama unafikiria hivyo basi unahitaji msaada Mkuu ili kuweka fahamu zako sawa.
Fahamu zangu haziko sawa kwa sababu ya Manji kukaa ndani?
 
Jana baada ya mwenyekiti wa club ya Yanga na mfanyabiashara mkubwa Yusuph Manji, na mchungaji Gwajima kuwasili polisi central, tulishuhudia badae wakiondolewa kituoni kwa gari nyeupe. Leo mchana kamanda Siro ametoa taarifa kuwa bado wanashikiliwa kwa mahojiano. Binafsi sijaelewa imekuwaje hawa wakapelekwa mahabusu kimya kimya? Na wapo mahabusu ipi?
Kwani kwa tanzania kuna mahabusu zaidi ya zile za polisi?

Walilala mahabusu ya polisi
 
Bora ata hao mumewaona, je Majizo ameonekana popote
Umeongea point sana.
Majizo hatujasikia hata aliripoti lini??
Yuko ndan kwa mda gan??
Mahakamani anapelekwa lini??
Hatujui kama ni ukwel au uongo kuwa yupo ndani....
Lakin wengne wanatajwa tena kwa sifa..
Looooo
 
Kuna wakati nilikuwa humu JF kwa ID nyingine, ilikuwa ninadhani 2009, kuna bwana alileta uzi mzuri sana hapa, si mkumbuki jina. Alisema Tanzania ya leo si ile ya Nyerere ya ujamaa na kujitegemea, kila mtu ni ndugu na watoto wote wanasoma pamoja, anaefaulu anakwenda secondary, hata kama mzazi wake hana pesa, atapata barua ya balozi wa nyumba kumi, na katibu kata mpaka wilayani atakapo chukua warrant ya kusafiria kwa train kwenda shule.

Tanzania ya leo tumegawanywa, watoto wa vigogo wanasoma Braenburn, IST, Fedha boys ect, watoto wetu wanasoma shule za kata. Matokeo ya shule za kata wanaopata div four wamefaulu angalao wanaondoka na cheti, yaani wenzao wana wapongeza, wakati wale wa Braenburn wanatoka na div I na II, anaepata III walimu wenyewe wanambeleza mzazi motto arudie mitihani kwa gharama yao, wakimuonea huruma pesa alizolipa.

Watoto wao wakimaliza shule wanakwenda kusoma nje ya nchi, wakirudi wanakuwa wameandaliwa nafasi za kugombea katika chama na taasisi nyingine, watoto wetu wanaishia kuwa wapiga kura kuwapigia kura watoto wao.

Watoto wao wakipata matatizo wazazi wao wanapiga simu na yanamalizwa, yakikwa magumu sana ndiyo inabidi waitwe polisi, wakifika polisi mahojiano yanfanyika katika ofisi ya mkuu wa kituo, na kama itabidi alale ndani, mkuu wa kituo mwenyewe anakwenda kumchukulia soda na mishikaki, na analazwa ofisini kwa mkuu wa kituo.

Watoto wetu sisi wakikutwa na kosa wanakaa mahabusu miezi sita, waka kesi haijasikilizwa.

Baada ya kuagana na ujamaa tumebaki na tabaka la wapiga kura na wapigiwa kura.
tatizo ni sisi wenyewe. Mfano halisi wewe kitu gani kilifufanya ubadili ID
 
Jana baada ya mwenyekiti wa club ya Yanga na mfanyabiashara mkubwa Yusuph Manji, na mchungaji Gwajima kuwasili polisi central, tulishuhudia badae wakiondolewa kituoni kwa gari nyeupe. Leo mchana kamanda Siro ametoa taarifa kuwa bado wanashikiliwa kwa mahojiano. Binafsi sijaelewa imekuwaje hawa wakapelekwa mahabusu kimya kimya? Na wapo mahabusu ipi?

Kazi ya police hiyo mkuu!!!!
 
Sijawahi ona mtuhumiwa anapewa kiti akae na kukunja nne,Jana Manji walimpa kiti akae. Halafu badae wanakuja kutwambia wamemlaza mahabusu .
Ile picha ni ya ndani ya uwanja mkuu. Pole sana
 
Jana baada ya mwenyekiti wa club ya Yanga na mfanyabiashara mkubwa Yusuph Manji, na mchungaji Gwajima kuwasili polisi central, tulishuhudia badae wakiondolewa kituoni kwa gari nyeupe. Leo mchana kamanda Siro ametoa taarifa kuwa bado wanashikiliwa kwa mahojiano. Binafsi sijaelewa imekuwaje hawa wakapelekwa mahabusu kimya kimya? Na wapo mahabusu ipi?
Next time watapelekwa kwa matarumbeta
 
Jana baada ya mwenyekiti wa club ya Yanga na mfanyabiashara mkubwa Yusuph Manji, na mchungaji Gwajima kuwasili polisi central, tulishuhudia badae wakiondolewa kituoni kwa gari nyeupe. Leo mchana kamanda Siro ametoa taarifa kuwa bado wanashikiliwa kwa mahojiano. Binafsi sijaelewa imekuwaje hawa wakapelekwa mahabusu kimya kimya? Na wapo mahabusu ipi?


ULITAKA WAPELEKWE NA MATARUMBETA ?
 
Kwa ile statement ya Siro, naamini hakika kuwa wawili hao, walikutwa na si chini ya kilo 3 za coc. haiwezekani wapotezwe kiharamia hivyo, tena wakitetemeka wakasahau kuwa walienda na wanasheria wao wakakubali wawaache ofisini kwa Siro watolewe mlango wa nyuma na kupotezwa fyaaaa ka panga la kukatia fence. Lazima walikutwa na kitu
 
Katika kuweka kumbukumbu sawa. Gwajima n Manji walitolewa kwenda kusiko kusiko julikana na ile land cruiser nyeupe mida ya jioni n walirudishwa mida ya saa 4 usiku walilala hapo hapo central. Kuna wanachama wa Yanga walishinda n baadhi kulala hapo hapo central na mmojawao namfahamu na jana pia walikuwa hapo siku nzima. Manji alilala central. Period
 
Back
Top Bottom