Uongozi wa Simba umekurupuka, Yusuph Manji alipotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya Uongozi wa Yanga ulikaa kimya

Nature

JF-Expert Member
Nov 5, 2014
758
2,027
Binafsi nimeshangazwa sana na uongozi wa Klabu ya Simba SC kukurupuka kumkana Kocha wa Makipa, Muharami Said Mohamed kutokana na tuhuma za Kukutwa na madawa ya kulevya kwa kusema kwamba Klabu ya Simba haikuwa na mkataba naye bali alipewa mwezi mmoja wakati Simba inatafuta Kocha Rasmi wa Makipa,
Cha ajabu zaidi ni kwamba imemtangaza kocha mpya masaa matatu baadaye.

Ni vyema Uongozi wa Klabu ya Simba na Mashabiki wa Soka kwa ujumla kukumbuka kwamba, Miaka kadhaa iloyopita Aliyekuwa Mwenyekiti na Mdhamini wa klabu ya Yanga Bwana Yusuph Manji aliwekwa mahabusu kwa Zaidi ya Miezi mitatu kwa tuhuma za Makosa tofauti tofauti ikiwemo kutumia madawa ya kulevya. Na mahakamani ukaketwa ushahidi wa Kitabibu baada ya kupimwa mkojo kuwa amethibitika kitumia madawa ya kulevya (japo ilitiliwa shaka)

Katika kipindi chote cha Kesi ya Manji uongozi wa Klabu ya Yanga haukutoa Kauli yoyote kumhusu mpaka mahakama ilipotoa maamuzi ya mwisho..pamoja na kwamba Serikali ya wakati ule ilitisha haswaa na kulikuwa na kila sababu ya Yanga kama klabu kuogopa na kumkana Manji lakini Yanga haikusema neno liwe jema au baya.

Pia ni vyema tukakumbuka Kwamba haya mambo siyo mara ya kwanza kutokea katika michezo...

Mlinzi wa Klabu ya Manjester City Benjamin Mendy Alishtakiwa kwa makosa ya ubakaji, utekaji na unyanyasaji wa kingono na mpaka sasa yuko Gerezani lakini Haikuiathiri Klabu kwa namna yoyote ile..

Pia Tumeona kwa wachezaji Kama Mason Greenwood nk wote hawa Klabu zao zilitoa kauli ya kukemea vitendo vyao lakini siyo kuwakana

Katika hili Uongozi wa Kalbu ya Simba ni lazima ukubali kuwa umekurupuka kwa maana tuhuma zinazomkabili Mharami hazijathibitishwa na mahakama ....hakukuwa na ulazima wa Klabu kutoa Statement ya haraka haraka kumkana kocha na kutoa maelezo ya kitoto kabisa Eti aliombwa afundisha kwa Muda wa Mwezi mmoja

Swali ni Je kama Tuhuma hizi zisingekuwepo, leo hii Simba wangemtangaza Kocha mpya wa makipa...?
Huo mwezi mmoja ulikuwa unisha leo?

Kwa kweli Statement ya Klabu inaonekana imeandikwa kwa Hofu na Mashaka makubwa na inaacha maswali mengi zaidi..ni afadhali wangekaa kimya na kupata muda mzuri wa kutafakari kauli ipi ya kusema.
images%20(20).jpg
 
Simba kama club washatoa maelezo. Sisi mashabiki wa Simba tumesimama na club.
Huu upepo utaisha kesho tu baada ya CAF kumaliza kutangaza timu zitakazochuana group stage.
 
Nadhani ni kutokuwa na uzoefu katika mambo haya. Kwanza kulinganisha Manji wa Yanga na Muharami wa Simba ni tofauti. Manji alikuwa kiongozi mkuu sasa nani atoe statement? Pia Manji alikuwa mfadhili wa Yanga. Sasa huyu Muharami alikuwa Dayworket pale Simba. Kuna utofauti mkubwa sana.

Pamoja na hayo Simba wamekurupuka. Wanadai Muharami hakuwa mwajiriwa hivyo Simba wasihusishwe. Je angekuwa ameajiriwa na ana mkataba halali ingekuwa sawa Simba kuhusishwa? Lisingekuwa kosa binafsi la mwajiriwa au angekuwa ametumwa na Simba kuuza hayo madawa kwa vile ni mwajiriwa? SSC wamekurupuka hiyo ni wazi na statement yao inaacha maswali kuliko majibu
 
We utakuwa muhutu yaani enzi zile ubishane na john pompeo aliyemkamata,si utatekwa na maiti yako kuokotwa baharini.manji alikamatwa na magu kwa chuki binafsi
 
Nadhani ni kutokuwa na uzoefu katika mambo haya. Kwanza kulinganisha Manji wa Yanga na Muharami wa Simba ni tofauti. Manji alikuwa kiongozi mkuu sasa nani atoe statement? Pia Manji alikuwa mfadhili wa Yanga. Sasa huyu Muharami alikuwa Dayworket pale Simba. Kuna utofauti mkubwa sana.

Pamoja na hayo Simba wamekurupuka. Wanadai Muharami hakuwa mwajiriwa hivyo Simba wasihusishwe. Je angekuwa ameajiriwa na ana mkataba halali ingekuwa sawa Simba kuhusishwa? Lisingekuwa kosa binafsi la mwajiriwa au angekuwa ametumwa na Simba kuuza hayo madawa kwa vile ni mwajiriwa? SSC wamekurupuka hiyo ni wazi na statement yao inaacha maswali kuliko majibu
Tofauti kubwa ya masakata haya ni kuwa, Manji alishtumiwa kutumia hayo (yeye kama yeye) madawa ila Mwarami kakamatwa na shehena.Tofauti hii inasababisha Mwarami kuhojiwa kwa kina ili kujua washirika wake katika biashara.
 
Binafsi nimeshangazwa sana na uongozi wa Klabu ya Simba SC kukurupuka kumkana Kocha wa Makipa, Muharami Said Mohamed kutokana na tuhuma za Kukutwa na madawa ya kulevya kwa kusema kwamba Klabu ya Simba haikuwa na mkataba naye bali alipewa mwezi mmoja wakati Simba inatafuta Kocha Rasmi wa Makipa,
Cha ajabu zaidi ni kwamba imemtangaza kocha mpya masaa matatu baadaye.

Ni vyema Uongozi wa Klabu ya Simba na Mashabiki wa Soka kwa ujumla kukumbuka kwamba, Miaka kadhaa iloyopita Aliyekuwa Mwenyekiti na Mdhamini wa klabu ya Yanga Bwana Yusuph Manji aliwekwa mahabusu kwa Zaidi ya Miezi mitatu kwa tuhuma za Makosa tofauti tofauti ikiwemo kutumia madawa ya kulevya. Na mahakamani ukaketwa ushahidi wa Kitabibu baada ya kupimwa mkojo kuwa amethibitika kitumia madawa ya kulevya (japo ilitiliwa shaka)

Katika kipindi chote cha Kesi ya Manji uongozi wa Klabu ya Yanga haukutoa Kauli yoyote kumhusu mpaka mahakama ilipotoa maamuzi ya mwisho..pamoja na kwamba Serikali ya wakati ule ilitisha haswaa na kulikuwa na kila sababu ya Yanga kama klabu kuogopa na kumkana Manji lakini Yanga haikusema neno liwe jema au baya.

Pia ni vyema tukakumbuka Kwamba haya mambo siyo mara ya kwanza kutokea katika michezo...

Mlinzi wa Klabu ya Manjester City Benjamin Mendy Alishtakiwa kwa makosa ya ubakaji, utekaji na unyanyasaji wa kingono na mpaka sasa yuko Gerezani lakini Haikuiathiri Klabu kwa namna yoyote ile..

Pia Tumeona kwa wachezaji Kama Mason Greenwood nk wote hawa Klabu zao zilitoa kauli ya kukemea vitendo vyao lakini siyo kuwakana

Katika hili Uongozi wa Kalbu ya Simba ni lazima ukubali kuwa umekurupuka kwa maana tuhuma zinazomkabili Mharami hazijathibitishwa na mahakama ....hakukuwa na ulazima wa Klabu kutoa Statement ya haraka haraka kumkana kocha na kutoa maelezo ya kitoto kabisa Eti aliombwa afundisha kwa Muda wa Mwezi mmoja

Swali ni Je kama Tuhuma hizi zisingekuwepo, leo hii Simba wangemtangaza Kocha mpya wa makipa...?
Huo mwezi mmoja ulikuwa unisha leo?

Kwa kweli Statement ya Klabu inaonekana imeandikwa kwa Hofu na Mashaka makubwa na inaacha maswali mengi zaidi..ni afadhali wangekaa kimya na kupata muda mzuri wa kutafakari kauli ipi ya kusema.View attachment 2418039
Yanga walikaa kimya kwa sababu Manji alikuwa mfadhili wao mkuu,unawezaje kuukata mkono unaokulisha?Think big!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom