Manji na Gwajima wamelala mahabusu ipi?

Manji na Gwajima wamelala mahabusu ipi?

Kuna wakati nilikuwa humu JF kwa ID nyingine, ilikuwa ninadhani 2009, kuna bwana alileta uzi mzuri sana hapa, si mkumbuki jina. Alisema Tanzania ya leo si ile ya Nyerere ya ujamaa na kujitegemea, kila mtu ni ndugu na watoto wote wanasoma pamoja, anaefaulu anakwenda secondary, hata kama mzazi wake hana pesa, atapata barua ya balozi wa nyumba kumi, na katibu kata mpaka wilayani atakapo chukua warrant ya kusafiria kwa train kwenda shule.

Tanzania ya leo tumegawanywa, watoto wa vigogo wanasoma Braenburn, IST, Fedha boys ect, watoto wetu wanasoma shule za kata. Matokeo ya shule za kata wanaopata div four wamefaulu angalao wanaondoka na cheti, yaani wenzao wana wapongeza, wakati wale wa Braenburn wanatoka na div I na II, anaepata III walimu wenyewe wanambeleza mzazi motto arudie mitihani kwa gharama yao, wakimuonea huruma pesa alizolipa.

Watoto wao wakimaliza shule wanakwenda kusoma nje ya nchi, wakirudi wanakuwa wameandaliwa nafasi za kugombea katika chama na taasisi nyingine, watoto wetu wanaishia kuwa wapiga kura kuwapigia kura watoto wao.

Watoto wao wakipata matatizo wazazi wao wanapiga simu na yanamalizwa, yakikwa magumu sana ndiyo inabidi waitwe polisi, wakifika polisi mahojiano yanfanyika katika ofisi ya mkuu wa kituo, na kama itabidi alale ndani, mkuu wa kituo mwenyewe anakwenda kumchukulia soda na mishikaki, na analazwa ofisini kwa mkuu wa kituo.

Watoto wetu sisi wakikutwa na kosa wanakaa mahabusu miezi sita, waka kesi haijasikilizwa.

Baada ya kuagana na ujamaa tumebaki na tabaka la wapiga kura na wapigiwa kura.
 
Sijawahi ona mtuhumiwa anapewa kiti akae na kukunja nne,Jana Manji walimpa kiti akae. Halafu badae wanakuja kutwambia wamemlaza mahabusu .
Mtu anatimba na wanasheria nane, na sio wanasheria tu ila ni vichwa vya wanasheria 8. Unategemea watamueka ndani ili baadae akishinda kesi washtakiwe wao? Si watamlipa mpaka pesa za kuchukua wanasheria.
 
Jana baada ya mwenyekiti wa club ya Yanga na mfanyabiashara mkubwa Yusuph Manji, na mchungaji Gwajima kuwasili polisi central, tulishuhudia badae wakiondolewa kituoni kwa gari nyeupe. Leo mchana kamanda Siro ametoa taarifa kuwa bado wanashikiliwa kwa mahojiano. Binafsi sijaelewa imekuwaje hawa wakapelekwa mahabusu kimya kimya? Na wapo mahabusu ipi?
Acha move iendelee
 
Siyo lazima achanganywe na mahabusu wa kawaida lakini mahabusu hata kama ni Kilimanjaro kempinski ile kuwa chini ya ulinzi na kunyimwa uhuru.
Hivi kaka wewe unaamini kabisa serikali yetu inaweza ikamueka chini ya Ulinzi mtu kama Manji mwenye pesa zake? Unadhani wakimsumbua sana Manji, baada ya kesi Manji atawaacha hivihivi? Kama Lissu tu anawasumbua na kuwachezea wanasheria wa Serikali atakavyo, unasemaje juu ya mtu kama Manji ambae jan tu kaenda na wanasheria 8. Ingekuwa ni nchi za wenzetu walau ningeamini kwamba Manji ataweza kunyooshwa ila sio nchi hii.
 
Hawa walikuwa wawili tu na alikosekana mheshimiwa Mbowe tu pale, wale vijana wenu walikuwa wengi, waliingizwa kwenye defender tena nyuma kule mnasimama na kushika bomba.
Unasemaje ya Manji kuhojiwa na Kamanda Siro mwenyewe tofauti na hawa vijana wengine?
 
Hivi kaka wewe unaamini kabisa serikali yetu inaweza ikamueka chini ya Ulinzi mtu kama Manji mwenye pesa zake? Unadhani wakimsumbua sana Manji, baada ya kesi Manji atawaacha hivihivi? Kama Lissu tu anawasumbua na kuwachezea wanasheria wa Serikali atakavyo, unasemaje juu ya mtu kama Manji ambae jan tu kaenda na wanasheria 8. Ingekuwa ni nchi za wenzetu walau ningeamini kwamba Manji ataweza kunyooshwa ila sio nchi hii.
Mkuu hakuna kinachoshindikana, sema akitoka hatakaa tena Tz ndiyo anahama.
 
Hawa jamaa hawapendagi ujinga sio watu wa mchezo mchezo huenda hata walienda kulala white house hawa
 
Mkuu hakuna kinachoshindikana, sema akitoka hatakaa tena Tz ndiyo anahama.
Sijajua Mkuu umri wako na ufatiliaji wako wa mambo ya siasa nchini.

Hivi kwa akili zako unaamini kabisa Wamasheria wa serikali watamzidi kesi Manji mpaka Manji afike hatua ya kuhama nchi baada ya kesi?

Kama unafikiria hivyo basi unahitaji msaada Mkuu ili kuweka fahamu zako sawa.
 
Iwe mahabusu au la lakini usiku wa jana walikuwa chini ya ulinzi tena mbali na wake zao.
wake zao hata wasipokua karibu nao wanaridhika wasipokuwepo pesa ipo karibu yao je ww labda uwe karibu na kunguni
 
Hata Mimi ninashangaaa, kuna sitofahamu.
Kumbuka, akina TID na wenzake walitolewa central police kwa defender hawa watu wawili walibebwa na Land cruiser (Shangingi) tena wakiwa na wana sheria wao.
Walilala mahabusu ipi?? Gwajima atajibu ibada ya jumapili
Bora ata hao mumewaona, je Majizo ameonekana popote
 
Back
Top Bottom