Light saber
JF-Expert Member
- Nov 3, 2017
- 4,129
- 7,447
Jaji ameingia Mahakamani.
Kesi Na. 16 ya mwaka 2021 inatajwa
Kesi namba 16 ya 2021, jamhuri dhidi ya Khalfan Bwire, Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe
Jaji anamuita Wakili wa Serikali...
Wakili wa Serikali anatambulisha Jopo lake
Mawakili upande wa Utetezi wanatambulishwa
Mawakili wa mshtakiwa wa kwanza ni Jeremiah Mtobesya na Nashon Nkungu.
Mshtakiwa wa tatu atawakilishwa na Dickson Matata na Fredrick Kihwelo
Mshtakiwa wa pili atawakilishwa na John Mallya
Mawakili wengine wote watamwakilisha mshtakiwa wa nne
Jaji anauliza kama mawakili wa serikali wanalolote Juu ya ingizo Jipya la wakili Fredrick Kihwelo kama kuna mgongano wa maslahi.
Wakili wa Serikali anasema hakuna tatizo kwa sababu tangu kesi ianze hajaonekana kwenye Column yoyote.
Jaji: hiyo wakili Fredrick Kihwelo anamshikia mikoba wakili Dickson Matata au atakuwa moja kwa moja kwa mshtakiwa watatu?
Kibatala: kuanzia leo mshtakiwa watatu atawakilishwa na wakili Fredrick Kihwelo na kusaidiana na Dickson Matata ambaye leo hayupo mahakamani
Wakili wa Serikali anahoji mshtakiwa mwenyewe anasemaje baada ya kumsikiliza Kibatala
Jaji: hilo tayari nimeshaliongelea kuwa baada ya utambulisho wa Kibatala nitamuhoji Mshtakiwa
Jaji: Ling'wenya bila shaka umesikia?
Ling'wenya: Nimesikia Mh. nakubaliana na Wakili Kibatala
Jaji: Kuna taarifa gani kuhusiana na Wakili Dickson Matata kutokwepo mahakamani?
Kibatala: Ana appear mbele ya Jaji mwingine wa mahakama Kuu ambaye ni Jaji Senior
Jaji: Kama hakuna session inayoendelea huko mahakamani anaweza kuomba udhuru huko, Otherwise ni mahakama ya Rufaa na pia kama kuna kesi inaendelea huko Seniority inatake place.
Jaji: Ila ni vizuri tukawa tunajua na mjue katika kesi, kesi za Jinai zinapewa kipaumbele kuliko kesi za madai, ni vizuri tujue ni kesi gani aliyopo huko.
Kibatala: Sina Details sana ila ukiniruhusu naweza kumuuliza ili ujaze.
Jaji: Je, mawakili wa serikali kuna jambo lolote la kuongezea?
Wakili wa Serikali: Hatuna mheshimiwa
Jaji: Sawa, upande wa Serikali mpo tayari?
Wakili wa serikali: Nadhani tulikuja kwa ajili ya kesi ndogo na kuna shahidi alihitajika kuendelea, shahidi yupo tayari kuendelea
Jaji: Mawakili wa utetezi, mpo tayari kuendelea?
Kibatala: Ndiyo mheshimiwa.
Jaji: Shahidi aliyebakiza ushahidi wake apande kizimbani tuendeleee
Jaji: siku ya Ijumaa tulikuapisha, Nakukumbusha kuwa kiapo chako kinaendelea
Shahidi: Sawa Mheshimiwa
Kibatala: Unakumbuka mara ya mwisho wakati unatoa ushahidi ulisema mkiwa maeneo ya Boma Ng'ombe washtakiwa walikula Chakula. Je, unakumbuka walikula chakula gani?
Shahidi: Ndizi, Nyamachoma na MO Energy
Kibatala: Wakati shauri limehairishwa tulituma mtu huko Boma Ng'omba na Siha kutokana na unyeti wa Kesi, Je unakumbuka Jina la Muhudumu?
Shahidi: Hapana sikumbuki.
Kibatala: Je, unakumbuka jinsia yake aliyewahudumia?
Shahidi: Hapana, tulikuwa kwenye gari, Chakula afande Kingai ndiye aliyeleta
Kibatala: Je, ni mara ngapi umekuwa na watuhumiwa na kuwapatia chakula?
Shahidi: Ni jambo la kawaida mkiwa kwenye operesheni kumpatia mtu chakula
Kibatala: unafahamu PGO imetaja utaratibu wa kupatia chakula watuhumiwa?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: unafahamu kuwa PGO ndiyo ina maelekezo ya pekee juu ya utaratibu wa kumpatia chakula Mtuhumiwa?
Shahidi: na sheria mbalimbali siyo tu PGO
Kibatala: Zitaje
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu kwa Mujibu wa taratibu za Tanzania na kimataifa kuna hotuba inayotambua kuwa na vikosi maalum vya ugaidi Tanzania.. Je unamfahamu?
Shahidi: Ungemfuata aliyesema umuulize
Jaji: Shahidi anakuuliza wewe!
Kibatala: Je, kuna sehemu yoyote umejitambulisha wewe ni mmoja ya kikosi Maalum cha kupambana na magaidi Tanzania?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je, inaruhusiwa wakati wa kumuhoji mtuhumiwa kumchoma choma na bisibisi?
Shahidi: Hapana hairusiwi
Kibatala: Je inaruhusiwa kumchoma choma mtuhumiwa na bisibisi na kumwambia tutakufanya kama tulichokufanya Moshi?
Shahidi: Hairuhusiwi
Kibatala: Je, inaruhusiwa kumfunga mtu pingu miguuni na mikononi na kumining'iza na kumpiga na marungu kwenye unyayopaka hawezi kutembea?
Shahidi: Hairuhusiwi
Kibatala: Je, Tazara ni kituo Class A au B?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Ulizungumzia kuwa ulimtoa mtuhumiwa kutoka Central kwenda Mbweni?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Central ulipomtoa mtuhumiwa ni Class A au B?
Shahidi: Class A
Kibatala: Kwa hiyo ulimtoa kituo Class A kwenda class A?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, unafahamu kuwa taratibu za kumsafirisha mtuhumiwa kwenda popote zimewekwa kwenye PGO?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: PGO inasema kuwa wakati wa kumhamisha mtuhumiwa kutoka Point moja kwenda kwenye point nyingine inatakiwa kuandikwa Detention Register.?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Wewe ulikuwa Arresting Officer.?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jaji akimaliza kuandika mwambie kuwa ni kwa PGO ya ngapi
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Unafanya kazi kwa kutumia PGO au mazoea?
Shahidi: kwa taratibu mbalimbali
Kibatala: ikiwepo PGO
Shahidi: NDIYO
Kibatala: Je, unafahamu lolote kuhusu Moses Lijenje na umezungumzia hapa hatima ya Moses Lijenje?
Shahidi: Sikuzungumzia
Kibatala: Je, unafahamu lolote kuhusu utaratibu wa kumtangaza mtuhumiwa kwa kutumia tangazo?
Shahidi: Hapana
Kibatala: umezungumzia kuhusu KUMFUNGA Pingu mshtakiwa, Je kuna sehemu yoyote umezungumzia KUMFUNGUA pingu mshtakiwa ?
Shahidi: Kwenye maelezo yangu siku zungumzia.
Kibatala: Wakati wakili John Mallya anakuhoji kuhusu chakula alikuhoji kuhusu kiwango cha chakula mtuhumiwa alipewa, unafahamu PGO imezungumzia kiwango, kiasi na aina gani ya chakula ambacho mtuhumiwa anapaswa kupewa akiwa chini ya Ulinzi? je Unafahamu?
Shahidi: Hapana, sifahamu
Kibatala: Umezungumzia kupewa chakula watuhumiwa wakiwa Boma Ng'ombe na Himo, je umezungumzia kuhusu watuhumiwa kupewa chakula wakiwa kituo cha polisi Moshi?
Shahidi: Hapana sikuzungumzia
Kibatala: Je, umezungumzia kuhusu kuwapekua watuhumiwa mauongoni ulipowakuta, Je kwa mujibu wa PGO inaruhusiwa kumfanyia mtu Upekuzi maungoni mbele za Watu?
Shaidi: Ndiyo inaruhusiwa
Kibatala: PGO ipi?
Shahidi: sifahamu
Kibatala: nakusomea PGO 272(5) inayozungumzia kumpekua mtu mauongoni, PGO inasema kwa Kuanzia Kichwani, Kushuka chini... hapa mwisho inasema nobody search in Public view.
Shahidi: mheshimiwa inaruhusiwa Kwa mujibu wa PGO
Kibatala: Je, PGO inaruhusu kumpekua mtu maungoni hadharani?
Shahidi: inaruhusu
Kibatala: Nikikupa PGO utaonyesha ni wapi?
Shahidi: ndiyo..
Peter Kibatala anamkabidhi shahidi PGO
Shahidi: PGO inaruhusu isipokuwa kama utamvua mtu nguo, kuchuchumaa inakatazwa.
Jaji: ungesoma kama wakili Kibatala anavyosoma au ungependa kuelezea?
Shahidi: Ningependa kuelezea tu..
Kibatala: Je, UNASOMA PGO au HUSOMI?
Shahidi: SISOMI Mheshimiwa JAJI
Kibatala: Ahsante, sasa ngoja Jaji aaandike umekataa kusoma PGO kwa unachokisema.
Kibatala: Unafahamu Diary ya Afisa wa Polisi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wewe ni Gazetted au siyo Gazetted Officer?
Shahidi: Siyo Gazetted Officer
Kibatala: Unafahamu PGO inazungumzia Afisa wa Polisi wa cheo kama cha kwako anapotoka eneo la kazi?
Shahidi: Siyo Gazetted Officer
Kibatala: Je unafahamu RPC anatakiwa kukupa wewe ruhusa?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je unafahamu RPC anatakiwa kukupa wewe ruhusa?
Shahidi: Siyo RPC pekee yake
Kibatala: Je nani mwingine?
Shahidi: RPC, RCO na Staff Officer
Kibatala: Je Ruhusa ya kipolisi inatolewa kwa maandishi au kwa mdomo?
Shahidi: maandishi
Kibatala: Je umetoa nyaraka (Movement Order) Mahakamani.?
Shahidi: PGO inasema Officer ambaye ni Gazetted haitaji Movement Order na kwa cheo changu Movement yangu ilikuwa inabeba Wengine.
Kibatala: Tuokoe muda, Sijakuuliza hicho
Shahidi: Muda tunao Mheshimiwa
Jaji: Jibu kuwa ulikuwa na kibali au hukuwa na kibali
Shahidi: Ndiyo nilikuwa namjibu
Kibatala: Wakati unatoa ushahidi wako hapa na ulionyesha hiyo Movement Order?
Shahidi: Ukimaloza inarudishwa ofisini
Kibatala: Ulitoa mahakamani au hukutoa?
Shahidi: Haikuhitajika, sikuulizwa lakini ipo..
Kibatala: Ulitoa au hukutoa?
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Je, unafahamu hata RCO kama afande kingai anasehemu anatakiwa kuripoti?
Shahidi: Siwezi kumuongelea Afande wangu.
Kibatala: Ongelea concept unaifahamu au huifahamu, kwa sababu hata mimi nafahamu juu ya mawakili Senior taratibu zao zikoje.
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umezungumzia mtuhumiwa kuwa na Jacket
Shahidi: ndiyo
Kibatala: Je, unafahamu kuwa hilo Jacket ndilo lililotumika kumfungia machoni asione mtuhumiwa?
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Je, unafahamu anayetakiwa kufanya upekuzi ni afisa wa Polisi mkamataji
Shahidi: Yeyote anaweza kufanya upekuzi
Kibatala: Je nikikupa PGO unaweza kunionyesha popote ambapo polisi yeyote anaweza kufanya upekuzi?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati wote wa kazi yako ulishawahi kufuata PGO ukawa nayo karibu na kuitumia?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mh. Jaji ni hayo tu, sina swali lingine
Jaji: Ahsante, kila siku naona mtuhumiwa mmoja tu ndiyo anakunywa maji, mmewapa wengine? wapeni Maji wanywe,Askari Magereza Myakague ni haya tunayokunywa wote
Jaji: Mawakili wa Serikali kuna lolote kwa ajili ya Re: examination?
Wakili wa serikali: Tupo tayari
Wakili wa Serikali: Nitakuhoji kwa ufafanuzi. Je, Ijumaa wakati Kibatala anakuhoji ulisema anachanganya PGO ulikuwa una maana gani?
Shahidi: Wakati wakili Kibatala ananihoji alitaka PGO ya 272 leo nashukuru kafanya Research kidogo kwa sababu alikuwa anaongela kuhusu kuchukua Maelezo, Leo ndiyo kanihoji kwa usahihi kuhusu ukamataji.
Wakili wa Serikali: Hiyo PGO inayozungumzia kuhusu maelezo eleza ni kwa namna gani?
Shahidi: wakati unamchukulia maelezo ndiyo unamuhoji kwa kumuonya kama utatumia mahakamani Kama ushahidi
Wakili wa Serikali: Wakati Kibatala anakuhoji kuhusu kumtoboa na bisibisi kila kitu ulikuwa unasema hairuhusiwi
Shahidi: Hairuhusiwi kwa mujibu wa katiba zetu, kama torture na vinginevyo.
Wakili wa Serikali: Fafanua kuhusiana kumfunga na mtu kwa Jacket
Shahidi: Kama nilivyomuuliza wakili Kibatala hairuhusiwi na hakuna haja ya kufanya hivyo
Wakili wa Serikali: Hakuna sehemu uliomba ruhusa kufuata Notebook yako hapa Mahakamani, kwanini ulifanya hivyo?
Shahidi: Sikuhitaji kwa sababu yote niliyoyaeleza nilikuwa nayakaumbuka
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuwa hukuandika katika maelezo yako kama mliwapatia chakula Adam kasekwa mkiwa Boma Ng'ombe na Himo
Shahidi: Sikuandika katika maelezo yangu kwa sababu nili' focus katika mambo ya ukamataji
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa pia kuhusiana na uhitaji wa movement Order kutoka kituo chako cha kazi, Kwanini hukuileta hapa mahakamani?
Shahidi: Kwa mujibu wa taratibu, Polisi ukimaliza kuitumia Movement Order umarudisha ofisini, nikaendelea na kazi.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mimi ni hayo hatuna kingine..
Jaji: Shahidi tunashukuru umemaliza ushahidi wako unaweza kwenda sasa..
Shahidi anatoka kizimbani.
Jaji: Upande wa Serikali.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa tunaomba kuendelea na shahidi wa tatu..
Jaji: sawa Mleteni Shahidi wa 3 Mahakama ipo kimya.
---
Shahidi wa tatu amefika
Jaji: Shahidi jitambulishe
Shahidi: Naitwa Askari namba H2343, afande Msemwa
Jaji: Apa
Shahidi: Mimi Afande H2343 naapa Ninachosema kitakuwa kweli, Eeh! Mwenyezi Mungu nisaidie
Jaji: Anayehoji nani upande wa serikali?
Wakili wa Serikali: MIMI NASSORO KATUGA
Wakili wa Serikali: Shahidi ungependa kusimama au kukaa?
Shahidi: Kusimama
Wakili wa Serikali: Kituo chako cha Polisi ni wapi?
Shahidi: Kituo cha Polisi Oysterbay
Wakili wa Serikali: upo tangu lini?
Shahidi: Mwaka huu January/February
Mawakili wa Serikali: Umeajiriwa mwaka gani? Shahidi: 2013 Wakili wa Serikali: Ulianzia kituo gani?
Shahidi: Nilianzia Polisi Ilala na baadae nikahamia Central Polisi
Wakili wa Serikali: Central ulikuwa mpaka lini?
Shahidi: 2014 Mwanzoni Mpaka Mwaka jana mwishoni kuanzia January 2021 nikaenda Oysterbay
Wakili wa Serikali: Oyesterbay upo kitengo gani?
Shahidi: Upelelezi
Wakili wa Serikali: Ukiwa Central Polisi Ilala ulikuwa unafanya kazi gani?
Shahidi: Nilikuwa General Duty sisi ambao tunavaa uniform kawaida tofauti na wale wa kofia nyekundu FFU
Wakili wa Serikali: Ulikuwa na Jukumu gani?
Shahidi: Nilikuwa nalinda raia na mali zao.
Shahidi: Doria na ukaaji wa point pamoja na kuwa chumba cha mashtaka
Wakili wa Serikali: Umezungumzia chumba cha mashtaka ni nini?
Shahidi: Ni pale wanapokaa Askari (CRO) kwa ajili ya kupokea taarifa mbalimbali na ufunguaji wa kesi na kupokea watuhumiwa wanaoletwa
Wakili wa Serikali: Watuhumiwa wanaoletwa kutoka wapi?
Shahidi: Sehemu mbalimbali
Wakili wa Serikali: Unasema ulikuwa kwenye chumba cha mashitaka, ufanyaji kazi unakuwa ni Vipi?
Shahidi: Kwanza lazima kiwe na CRO incharge kazi utakazofanya ni zile utazopewa na CRO incharge
Jaji: naona Joto ni kali, naomba madirisha yafunguliwe.
Wakili wa Serikali: Naweza kukumbushwa alipoishia?
Jaji: CRO panakuwa na Incharge
Wakili wa Serikali: Enheee Endelea...
Shahidi: Unakuwa unafanya majukumu unayopewa na Incharge.
Wakili wa Serikali: Iambie mahakama sasa kwa ufupi sana mnapokuwa mnapokea watuhumiwa nini kinafanyika?
Shahidi: Mnapopolea watuhumiwa kuna taratibu zake ukiwa CRO kinakamilishwa na kitu kinaitwa DR (Detention Register)
Wakili wa Serikali: Iambie mahakama ni kitu gani
Shahidi: Ni kitabu kinachotunza kumbukumbu za kituo cha Polisi
Wakili wa Serikali: Kwa namna gani!?
Shahidi: Kuna taratibu zake za kumpokea mtuhumiwa na askari anayekuwa chumba cha mashtaka uzifahamu.
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ni taratibu gani..
Shahidi: Kwanza wakati unamuhoji ni Kumpekua ili wakati unampekua unakuwa mpo nae salama
Wakili wa Serikali: Wakati mnampekua mnafanya utaratibu gani?
Shahidi: Chochote kinaweza kuanza kuhojiwa na kumpekua
Shahidi: Kiuhalisia nilichofundishwa CCP kuwa mtu anapokuwa amekamatwa anakuwa na Mawazo yeye mwenyewe
Wakili wa Serikali: Mimi sitaki mawazo yako, sasa wewe unafanya kitu gani?
Shahidi: kuhakikisha haingii na kitu chenye madhara Mahabusu..
Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Kumuingiza kitabu cha mahabusu (Detention Register)
Wakili wa Serikali: Unampekuaje?
Shahidi: Unampekua kwa kumwambia nyoosha mikono Juu, kwa kugeukia ukuta na kuushika, na mwisho wa kumpekua ni kumwambia kaa chini
Wakili wa Serikali: unamhoji kwa namna gani
Shahidi: Kama Mtuhumiwa analetwa kwa kesi ambayo imeshafunguliwa anatakiwa awe na Case reference namba yake
Wakili wa Serikali: Kesi inayokuwa imefunguliwa wapi?
Shahidi: Popote pale ndani ya Tanzania
Wakili wa Serikali: Hiyo Reference inahusisha vitu gani?
Shahidi: Reference ndiyo kitu kinafahamila sana Mtaani RB, mfano kesi za Oysterbay zinakuwa na neno Kifupisho OB kwa maana Oysterbay Mkwaju, RB kwa maana imeripotiwa
Wakili wa Serikali: Hiyo ya Oysterbay je ya Central?
Shahidi: Cental ni neno CD na reference namba kesi ilianza kupelelezwa inakuwa na IR badala ya RB
Wakili wa Serikali: Baada ya namba nini kingine analeta?
Shahidi: na Jina la kosa analokuwa ametenda
Wakili wa Serikali: Vitu gani Vingine?
Shahidi: Unapata Particulars kwa aliyemleta mtuhumiwa na zingine kwa mtuhumiwa mwenyewe.
Wakili wa Serikali: zipi hizo?
Shahidi: Majina, Miaka yake, Jinsia yake..
Wakili wa Serikali: Jinsia ukimaanisha?
Shahidi: Kama ni mwanamke au mwanaume
Jaji: Wewe unajuaje?
Shahidi: Namkagua pia kuthibitisha
Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Hali yake ya Ki afya
Wakili wa Serikali: Akikujibu wewe unafanyaje?
Shahidi: Lazima ujiridhishe kama mgongoni unaweza kumkagua
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama kwenye ukaguzi wa jinsia mnafanya kitu gani?
Shahidi: Ni kujihakikishia physically
Jaji: Ina maana mwanamke unamkagua wewe?
Wakili wa Serikali: Ndiyo nilichotaka ila niliogopa nisije kuonekana namuongoza
Shahidi: CRO panakuwa na Askari wa kike kwa Ukaguzi wa Mwanamke. Akiletwa mwanamke ukaguzi utafanywa na Askari wa Kike
Wakili wa Serikali: Tarehe 7 Mwezi wa 8 2020 Ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa bado sijahamia Oysterbay nilikwa bado mkoa wa kipolisi Ilala, Central
Wakili wa Serikali: Unakumbuka nini siku hiyo?
Shahidi: Niliiingia kazini, nilikuwa na zamu ya CRO shifti
Wakili wa Serikali: Unaposema CRO shift unamaana gani?
Shahidi: Pale CRO panakuwa na Shift sababu tunafanya kazi masaa 24 kwa hiyo tunafanya kazi kwa zamu
Wakili wa Serikali: Ulipoingia kazini ulifanya nini?
Shahidi: Niliingia kazini Alfajiri na askari wengine watano
Wakili wa Serikali: Unaweza kuwataja kama unawakumbuka Shahidi: WP fatuma,Aziz na wengine
Wakili wa Serikali: Mliingia kazini Saa ngapi?
Shahidi: 12 Alfajiri
Wakili wa Serikali: Siku hiyo CRO Incharge alikuwa ni nani?
Shahidi: Palikuwa na Inspector msaidizi wa Polisi
Wakili wa Serikali: Siku hiyo wewe ulikuwa na jukumu gani
Shahidi: nilikuwa ni mtunza mahabusu, mahabusu wa kiume ni mimi, na wakike wata dili na WP SEMENI
Wakili wa Serikali: Unakumbuka Jukumu la Kufungua kesi.?
Shahidi: Nakumbuka Afande Emmanuel na Afande Samuel
Wakili wa Serikali: Ulikuwa na majukumu gani
Shahidi: ilikuwa saa 12 kasoro nilifika na kupangiwa majukumu na wengine
Wakili wa Serikali: Kitu gani ulifanya
Shahidi: Baada ya kukabidhiwa mahabusu naenda kuhakiki kule mahabusu chini kwa kutaja jina mojamoja
Wakili wa Serikali: Nini Unakumbuka kikafuata?
Shahidi: Siku hiyo ilikuwa tofauti kidogo baada ya kukagua mahabusu nikamuona Afande Kingai akiwa anaingia na Mahabusu
Wakili wa Serikali: Mahakama ingependa kujua ulikuwa unamfahamu kabla?
Shahidi: Ndiyo nilikuwa namfahamu
Wakili wa Serikali: alikuwa na nani?
Shahidi: Afande Jumanne
Wakili wa Serikali: ulikuwa unamfahamu Jumanne?
Shahidi: ndiyo, alikuwa makao Makuu ya polisi kabla
Wakili wa Serikali: nini kilifuata?
Shahidi: Akaniambia ni watuhumiwa kesi yao imefunguliwa hapa
Wakili wa Serikali: Unakumbuka RB yao?
Shahidi: Sikumbuli RB ila kosa nakumbuka
Wakili wa Serikali: Unakumbuka kosa gani Shahidi Kula njama za kutenda makosa ya ugaidi
Jaji: Naona tunge' break kidogo... Tutarudi saa saba na nusu kuendelea...
Wakili wa Serikali: Ikupemdeze Mheshimiwa jaji column yetu ya kwanza ipo vilevile tupo tayari kuendelea.
Kibatala: Tupo tayari kuendelea.
Jaji: Wakili aliyekuwa anamuongoza shahidi aendelee.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa naomba kukumbushwa na mahakama tuliishia wapi.
Jaji: Wakati wa kuandika RB na IR namba
Wakili wa Serikali: Unazikumbuka?
Shahidi: Hapana lakini zile namba CD za Central haziwezi kujirudia na kufanana
Wakili wa Serikali: Baada ya kupokea hizo reference kiliendelea nini?
Shahidi: Afande kingai na Afande Jumanne walitoka
Wakili wa Serikali: Kiliendelea nini baada ya kupokea hizo reference?
Shahidi: Taratibu zingine zilifuatwa baada ya kuwa na watuhumiwa
Wakili wa Serikali: Eleza mahakama nini kilifuata
Shahidi: Nilianza kumpekua mmoja mmoja, namwambia nyoosha mikono juu, kaa chini anakaa.
Wakili wa Serikali: Iambie mahakama baada ya Afande Jumanne kuwaleta watuhumiwa wakiwa na pingu nini kilifuatia kuhusu pingu?
Shahidi: Baada ya kufungua pingu kila mmoja na pingu yake, alisema akituachia pingu zitapotea
Wakili wa Serikali: Hujasema nani alifungua pingu
Shahidi: Mimi nilifungua siyo lazima nitumie pingu za afande Jumanne kwa sababu funguo za pingu zinaingiliana
Jaji: Unaposema koti unamaanisha nini?
Shahidi: Namaanisha Jacket
Jaji: Naamini wakina Kibatala mnaelewa!?
Kibatala: Ndiyo Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Baada ya kuwapekua nini kilifuata?
Shahidi: Nilianza kuchukua taarifa zao
Wakili wa Serikali: Kama zipi?
Shahidi: Kama Jina, Miaka, Jinsia na Dini
Wakili wa Serikali: unaweza kukumbuka majiina yake
Shahidi: Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali: Wakati huo unaandika wapi?
Shahidi: Kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: Ulimuuliza nini kingine?
Shahidi: Alijibu ki Afya yupo vizuri
Wakili wa Serikali: Akakuambiaje kuhusu Afya?
Shahidi: Mzima
Wakili wa Serikali: Ulijiridhishaje?
Shahidi: Tunajiridhisha kwa vitu kama majeraha, vitu kama Malaria ngumu sana
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea baada ya kujiridhisha?
Shahidi: Nikaendelea na mtuhumiwa wa pili
Wakili wa Serikali: Unakumbuka majina yake?
Shahidi: Alinitajia matatu lakini nakumbuka moja
Wakili wa Serikali: Lipi ?
Shahidi: Adam kasekwa
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifuata?
Shahidi: nilichukua majina yake na taarifa zingine
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo?
Shahidi: watuhumiwa wote wawili niliwapeleka mahabusu
Wakili wa Serikali: Unakumbuka muda?
Shahidi: Ilikuwa saa 12 na nusu Wakili wa
Serikali: Kilifuatia nini?
Shahidi: Baada ya muda Afande Kingai alirudi tena
Wakili wa Serikali: Alisemaje?
Shahidi: Nitoleee mtuhumiwa, nikamuhoji Nimamuuliza yupi? akaniambia Adam
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Niliandika maelezo na kuandika kuwa Mtuhumiwa ametoka mahabusu, nikamwambia afande kwakuwa nimtoa huyu mtu inabidi usaini isije kuonekana ametoroka
Wakili wa Serikali: alikutaka umpelekee wapi?
Shahidi: Nilimkuta palepale Counter, akasema nimwachie aende na mtuhumiwa
Shahidi: Afande SEMENI akaniambia niongozane nae
Wakili wa Serikali: Mlienda wapi?
Shahidi: Ofisi ya RCO floor ya kwanza
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea?
Shahidi: Nilirudi kuendelea na majukumu yangu
Wakili wa Serikali: Baada ya kurudi huyo Afande kingai ikawaje?
Shahidi: Alikaa naye kama masaa mawili akamrudisha. Nilimuhoji majina yake akaniambia, nikamuhoji Jinsia yake, hali yake ya Kiafya yupo vizuri na kumpekua kuhakikisha aingii na chochote mahabusu
Wakili wa Serikali: Baada ya kujaza taarifa zake?
Shahidi: Nilimrudisha mahabusu
Wakili wa Serikali: Ukiwaona unaweza kuwakumbuka?
Shahidi: Nawakumbuka nikiwaona
Wakili wa Serikali: Kitu gani kitakufanya uwakumbuke?
Shahidi: Upekee wa siku hiyo, tangu nizaliwe nilikuwa sijawahi kuona Magaidi, ikabidi niwaangalie vizuri.
Wakili wa Serikali: Hapa mahakamani unaweza kuwatambua?
Shahidi: Ndiyo nikiwaona naweza kuwatambua.
Wakili wa Serikali: Kwa idhini ya mahakama unaweza kwenda kuwagusa na kuwatambua?
Jaji: Nenda sasa au UNAWAOGOPA?
Shahidi: Hapana naweza kwenda.
Shahidi: Ni hawa wawili
Wakili wa Serikali: Unaweza kusema huyu ni nani na huyu ni nani?
Shahidi: Labda wavue barakoa.
Jaji: Sasa Barakoa ni kifaa cha mtu cha Afya, sioni shida kama amewagusa wawili otherwise awaguse na kuwataja majina.
Wakili wa Serikali: Mahakama Imeonyesha kuwavua kifaa cha Afya si sawa, tuendelee
Jaji: Mimi kama mimi nimeelewa watu aliofanya nao kazi siyo Mshtakiwa nne wala wa kwanza
Wakili wa Serikali: Baada ya kuwapokea mtuhumiwa afande Kingai ukamrudisha mahabusu nini kingine kilitokea?
Shahidi: Hakuna kitu kingine kilichotokea, nilipopeleka chakula cha mchana nilimuona
Wakili wa Serikali: Huyu ulimpelekea chakula kutoka wapi?
Shahidi: Kuna vyakula vya mahabusu na vingine kutola kwa ndugu zao
Wakili wa Serikali: Mimi nauliza specific kwa huyu wa Kingai
Shahidi: Chakula cha mahabusu
Jaji: ulipeleka chakula saa ngapi?
Shahidi: saa nane na nusu
Jaji: uliposema ulimuona mara ya mwisho wakati wa chakula unamaana gani?
Shahidi: Narudia tena kuwa alipeleka chakula cha mchana na kumuona mara ya mwisho, lakini ilikuwa tayari Jioni
Jaji: Hebu rudia vizuri hapo, RELAX!
Shahidi: Mchana Jukumu langu ni kupeleka chakula, Mchana tena napeleka chakula, jioni kwa wanaoingia jioni ndiyo wanapeleka chakula cha jioni
Wakili wa Serikali: Unasema ikawa mara ya mwisho kuona, kwanini unasema mara yako ya mwisho?
Shahidi: Baada ya kutoka siku ile, siku inayofuata sikuwakuta
Wakili wa Serikali: Kwanini hukuwakuta?
Shahidi: Kwa sababu siku inayofuata niliingia shift ya 3
Wakili wa Serikali: Hiyo Detention Register ulioona mahakamani unaweza kuikumbuka?
Shahidi: unajua.
Shahidi: unajuaaaa.....
Jaji: Shahidi jibu swali unaweza kuikumbuka au lah
Shahidi: Naweza Kuikumbuka
Wakili wa Serikali: Kitu gani kitakufanya ukumbuke?
Shahidi: Ni taarifa ya pale juu ya kitabu Imeandikwa Detention Register na Ministry of Home Affair,tuliandika kwa Makapeni
Wakili wa Serikali: Shahidi hebu shika hiki kitu, ukipata wasaa kiangalie..
Shahidi: Anakikagua na kuanza kufungua ndani
Shahidi: Tayari
Wakili wa Serikali: umekitambua
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kwa kuona nini?
Shahidi: kuona mwandiko wangu
Wakili wa Serikali: Kwa nje imeandikwa nini?
Shahidi: Ministry of Home affair
Wakili wa Serikali: Muonyeshe Jaji kwa kunyanyua
Shahidi: Mheshimiwa hii ndiyo DR na mbele inaandikwa kwa mwaka fulani
Jaji: Wewe elezea yanayokuhusu tu, sababu mwanzo hukuongelea mambo ya DR ukasema huyakumbuki.
Shahidi: Ndiyo Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Unataka mahakama ifanye nini kuhusu kitabu hiko?
Shahidi: Naomba mahakama ikubali kukitumia kama kielelezo.
Jaji: Sasa Mawakili wa Serikali mnataka nini?
Wakili wa Serikali: Tunaomba kiiingie kama kielelezo cha ushahidi
Jaji: Mawakili wa Utetezi?
Wakili Mtobesya: Kwa niaba ya mshtakiwa wa kwanza sina kipingamizi
Wakili Kihwelo: Kwa naiaba ya mshtakiwa wa pili sina kipingamizi
Wakili John Mallya: Kwa niaba ya mshtakiwa wa tatu sina kipingamizi
Wakili Peter Kibatala: Kwa niaba ya mshtakiwa wa nne sina kipingamizi.
Jaji: Sawa
Jaji: Detention Register imepokelewa kama kielelezo namba 1 kwa upande wa Jamhuri kwenye kesi ndogo..
Wakili wa Serikali: Kama wataitumia naomba watumie page husika
Jaji: Upande wa utetezi Mawakili wote wa utetezi hawana pingamizi.
Wakili wa Serikali: Kama kuna Jambo lolote ungependa kulielezea shahidi, karibu
Shahidi: Mtuhumiwa wa kwanza kumpokea alikuwa na entry namba 392 lakini RB yake ni CD/RB 3093/2020 Mohammed Abdilahi Ling'wemya kosa lilikuwa kula njama za kutenda makosa ya ugaidi IR ni CD/IR 2097/2020
Aliingia tarehe 07.8.2020 Saa 12 na dakika 7 asubuhi na baadae ni saa 2 na dakika 10 aliyemtoa nje ni ASP Jumanne, Sababu za kumtoa nje ni upelelezi.
Shahidi: Mtuhumiwa wa pili Entry namba 393 na Column ya report Book palikuwa na CD/RB 3093/202 Majina ni Adam kasekwa IR /CD/ IR 2097/2020. Aliingia tarehe 07.8.2020 aliingia Saa 12 na dakika 9 na siku anatoka alitolewa na ASP KINGAI. Nikawapokea tena watuhumiwa.
Shahidi: Mtuhumiwa wa kwanza alikuwa Adam Kasekwa akiwa RB /CD/RB/ 3093/2020 Miaka yake aliniambia ni ileile 31 Condition ni Good na IR no CD/IR/2097/2020 nilimpokea Saa 3 dakika 5, anaitwa Adam Hassan Kasekwa, na baadae anaonekana alitolewa 08.8.2020 na alitolewa saa 4 na dakika 5 asubuhi, Mtu aliyemtoa anaitwa Inspector Mahita, sababu za kumtoa ni nje kwa upelelezi.
Shahidi: Mtuhumiwa mwingine nilimpokea tarehe hiyo hiyo Mohammed Abdilah CD Ling'wenya, Miaka 34 na jinsia ni mwanaume na Physical Condition aliniambia yupo Good IR /CD/2097/2020. Mtu huyu tarehe 08.8.2020 Saa 4 na dakika 5 alitolewa nje na aliyemtoa ni Inspector Mahita na Sababu za kumtoa ni nje kwa Upelelezi.
Jaji: Sawa, mawakili wa Serikali...
Wakili wa Serikali: Unasema kuwa ulimuona Mtuhumiwa muda wa mwisho fafanua
Shahidi: Kwenye Detention Register kama unawapa chakula unatiki kwenye Column, na nilitiki kuwa Uji alipata na baadae waliporudi na kuwaingiza upya ilionyesha walipata chakula cha asubuhi, mchana na Jioni
Wakili wa Serikali: Una kitu kingine ungependa kuongeza
Shahidi: Sina cha kuongeza
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji sisi ni hayo tu kwa sasa..
Jaji: Wakili Mtobesya kama kuna lolote.
Mtobesya: Nitaanza na maswali machache kama nitakuwa nimecha Wakili Nashon atamalizia
Mtobesya: Shahidi unafahamu kitu kinaitwa Station Diary?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Mtobesya: Kazi yake ni nini
Shahidi: Wakati wa ukaguzi na masuala yoyote ya watuhumiwa wakiwa kituoni
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema siku hiyo wewe ni charge Room Officer?
Shahidi: Siyo Sahihi
Mtobesya: Ieleze mahakama nani alikuwa charge room officer
Shahidi: Charge Room Officer ni Mkuu wa kituo
Mtobesya: Kama wewe hukuwa charge room Officer ulikuwa unashughulika na watuhumiwa kama nani?
Shahidi: Charge room officer anatupangia sisi tufanye kazi yake
Mtobesya: Kwa hiyo wewe ulikuwa unafanya kazi za Charge room Officer
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwa hiyo ni sahihi nikisema ulikuwa unafanya kazi za Charge room officer
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwa hiyo mambo mengine kama watuhumiwa kutembelewa ulikuwa unashughulika nayo?
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Ni sahihi nikisema wa kuwa yote hayo yalitakiwa kuandikwa kwenye station Diary?
Shahidi: Sina uhakika
Mtobesya: Mtuhumiwa hatakiwi kutolewa mahabusu bila idhini yake.
Shahidi: Hauko sahihi
Mtobesya: Ni sahihi kwako kuwa mtuhumiwa anaweza kutolewa wakati wowote bila idhini yake?
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema charge room officer anatakiwa kuidhinisha movement ya mtuhumiwa?
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Eleza idhini hiyo inatolewaje
Shahidi: Inatolewa kwa maandishi na mdomo
Mtobesya: Kwenye kitu gani?
Shahidi: Naomba urudie
Mtobesya: Wewe ulipewa hiyo idhini kwa mdomo mkuu wa kituo ambaye ni Afande Mwita.
Mtobesya: Tusaidie, nitakuwa sahihi nikisema kuwa mtuhumiwa akifika station ya Polisi CRO akapokelewa na baada ya yeye kufika anatakiwa apelekwe kwa medical officer under esccort.
Shahidi: Sio sahihi
Shahidi: Anatakiwa umpeleke endapo ataainisha anaumwa, unamtaarifu Afande kuwa Mahabusu anaumwa na atafanya utaratibu wa matibabu.
Mtobesya: Unafahamu kitu kinaitwa PGO
Shahidi: Nafahamu ni nyenzo muhimu katika kufanya kazi
Mtobesya: unaifahamu PGO namba 353 inayoshughulikia watuhumiwa wakiwa chini yenu?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Mtobesya: Unaweza kusema siyo matakwa ya PGO 353 kwamba mtuhumiwa kabla ya kuwekwa mahabusu alitakiwa akaonane na medical Officer?
Jaji: Umeelewa Swali lake? Kama unafahamu chochote katika PGO hiyo?
Shahidi: 353 sikumbuki inasemaje
Mtobesya: Kwa hiyo unaweza kuiambia Mahakama kwamba mtuhumiwa kabla ya kuingia mahabusu anatakiwa aende kwa daktari.
Jaji: Shahidi kashasema hakumbuki
Mtobesya: Labda nimpatie asome
Mtobesya: Ungependa nikupatie Usome au nisome mimi mwenyewe?
Mtobesya anaisoma PGO 353(2)(b)
Shahidi: Anasema kwa uelewa wake yupo sahihi hata baada ya kusomwa
Jaji anauliza kama Mtobesya anaona tafsiri yake inatosha...
Mtobesya: Inasema pia kuhusu charge room Officer hatomtoa mahabusu pasipokuwa idhini yake
Mtobesya: Je unasisitiza siyo takwa la Kisheria la mtuhumiwa kutotoka mahabusu bila idhini yake?
Jaji anaomba wakili mwingine asome
Jaji: Sasa tupo pamoja, tunaweza kuendelea hapo
Mtobesya: Naomba tusome na kifungu (c)
Wakili wa Serikali: Naomba Mtobesya aulize swali badala ya kujielekeza kwenye tafsiri, suala la tafsiri iachiwe mahakama
Jaji: Suala la tafsiri niachiwe mimi, kwa sababu shahidi ameshasema anachokielewa.
Mtobesya: Anamuuliza shahidi kifungu A na C kinaongelea mtu mmoja.?
Jaji: Unataka maoni ya shahidi? maana yeye hajatunga PGO
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji shahidi ni mtu anayeshughulika na CRO ni taratibu zake za kila siku
Jaji: Je, akishasema ndiyo au hapana?
Mtobesya: Inayofuata ni kazi yako kutafsiri
Jaji: Tayari nimesha note hiyo
Mtobesya: Ni sahihi Officer kutembelea mahubusu kila baada ya muda fulani
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Wewe uliwatembelea mara ngapi ulivyo waweka?
Shahidi: Wakati wa uji, chakula cha mchana
Mtobesya: Ieleze mahakama ni interval ya masaa mangapi mangapi?
Mtobesya: Mtuhumiwa inatakiwa arekodiwe akitoka nje ya KITUO au kutoka mahabusu?
Shahidi: Detention Register inathibitisha akitoka nje ya mahabusu.
Mtobesya: Ni Entry ipi inarekodiwa mtuhumiwa anapotoka nje ya mahabusu na ipi inarekodiwa anapotoka nje ya kituo?
Shahidi: Anapotoka mahabusu ndiyo tunamuweka kwenye Detention Register tu bila kujua kama alitoka kwenda Mahakamani au kwenye Jambo lingine
Mtobesya: Naomba nipewe kielelezo namba 1 (Q One)
Jaji: Tafadhali apatiwe kielelezo.
Mtobesya anasoma Kielelezo ( Detention Register)
Mtobesya: Nisaidie ni wapi ulisoma tarehe 08 walitoka mahabusu
Jaji: Ukishamaliza na sisi tusikie
Shahidi: Ametoka tarehe 07.8.2020
Mtobesya: Nilikuwa naeleza entry ya tarehe 8
Shahidi: Katika entry inaonyesha aliyemtoa ni Inspector Mahita na sababu ya kumtoa ni Upelelezi
Mtobesya: Sasa ilipita muda gani wakina Kingai walikuachia watuhumiwa na wakarudi tena?
Shahidi: Haikuchukua muda ilikuwa kama saa 1
Mtobesya: Charge room Officer ndiye aliyetakiwa aidhinishe?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Tunaiona wapi?
Shahidi: Inaweza kuwa maandishi au ya mdomo
Jaji: Kielelezo kipo wapi?
Mallya: Tulikuwa tunakiomba kwa ajili ya kukisoma na sisi
Jaji: Mtakiomba kwa sasa ni mali ya Mahakama
Jaji: Karibu sasa wakili Nashoni
Wakili Nashoni: Sina la kuongeza mheshimiwa Jaji
Jaji: karibu sana Wakili Mallya sasa na kama utahitaji Kielelezo
Wakili Mallya: Shahidi umesema wewe ni mzoefu kwa miaka 6 Central!?
Shahidi: Ndiyo kwa miaka 6
Mallya: Kwa miaka yako 6 ushawahi kusikia mahabusu ametoroka?
Shahidi: Hapana
Mallya: Kuna wakati mnawakamata watuhumiwa ambao ni wanajeshi wanatenda jinai, huwa mnawahifadhi central?
Shahidi: Ndiyo tunawahifadhi Central
Mallya: Kuna mahabusu ngapi Central?
Shahidi: Moja iliyogawanyika kwa KE na ME
Mallya: Kwa wanaume kuna mahabusu ngapi?
Shahidi: Zaidi ya 2
Mallya: Kwenye DR afande Mahita alikuwa anawachukua watuhumiwa anawapeleka kwenye Upelelezi, Je ulipata kujua alikuwa anawapeleka wapi?
Shahidi: Siwezi kujua anawapeleka wapi
Mallya: Siku unaingia kazini ulikuta mahabusu ina mahabusu wangapi?
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Lakini mahabusu ilijaa sana?
Shahidi: Siyo sana!
Mallya: Palikuwa na watoto wadogo?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Watuhumiwa wa Mauaji?
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Watuhumiwa wa unyang'anyi wa kutumia silaha?
Shahidi: Siwezi kukumbuka
Mallya: Ulipowapeleka mahabusu watuhumiwa wa ugaidi kama ulivyosema, Je uliwawekaje?
Shahidi: Niliwatenganisha
Mallya: Ulivyowatenga magaidi unafikiri wangeweza Kufanya kikao cha kutoroka?
Shahidi: Walikuwa hawawezi kutoroka, kukutana, hawawezi kufanya lolote
Mallya: Akitokea mtu akisema mule hapakuwa salama wangeweza kupora silaha atakuwa anasema kweli?
Shahidi: Atakuwa anasema tu mambo yake
Mallya: Twende kwenye muda, siku hiyo ulifika muda gani?
Shahidi: Natakiwa kisheria kufika robo saa kabla na nilifika robo saa kabla
Mallya: Ulipofika ulifanya nini?
Shahidi: Tulianza kukabidhiana kazi
Mallya: Kati ya kukabadhiana watuhumiwa mahabusu na kukabidhiana mali ?
Shahidi: Vyote vilienda kwa pamoja
Mallya: Kwa muda gani mlikabidhiana?
Shahidi: dakika 15
Mallya: Ni wakati gani wewe ulishuka mahabusu?
Shahidi: Ni muda huohuo kwa sababu CRO tupo wengi
Mallya: Kwa hiyo ulitumia dakika ngapi kule chini mahabusu?
Shahidi: Dakika 15
Mallya: Ulisema afande Kingai alipomchukua Mtuhumiwa, afande FATUMA alikuelekeza umsindikize, Je ni lazima?
Shahidi: Ni nidhamu ya kipolisi
Mallya: Wakati Kingai anashuka kuja kumfuata Mtuhumiwa ulieleza mahakama alikuwa ameongozana na nani?
Shahidi: Hapana sikueleza
Mallya: Wakati Afande Kingai anawaleta watuhumiwa umesema walikuwa wamefungwa pingu?
Mallya: Siku hizi umesema unafanya kazi Oysterbay
Shahidi: ndiyo
Mallya: Ukiwa unatokea Moshi kituo cha kwanza kukutana nacho ni kipi?
Shahidi: Inategemea njia uliyopita
Mallya: Ukiwa unatokea Bagamoyo Msata, Mbweni, Oysterbay na Central kipi kituo cha kwanza kukutana nacho?
Mallya: Shahidi sasa hivi wewe ni Detective Constable?
Shahidi: ni sahihi
Mallya: Upelelezi unajumuisha nini?
Shahidi: Ni mchakato, process na kisha Kupeleka mahakamani
Mallya: Kuhoji watuhumiwa ni sehemu ya upelelezi?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwenye DR umezungumza muda mrefu sana, ni sahihi unatakiwa kuandika taarifa za ukweli tu?
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Nakupa DR msomee Mheshimiwa Jaji alipokuja Inspector Mahita alisema anaenda kufanya nao nini?
Shahidi anapekua DR (Detention Register)
Shahidi: Mheshimiwa Jaji afande wangu alimtoa mtuhumiwa nje kwa UPELELEZI
Mallya: Akitokea mtu akisema Mahita hakuwa anafanya nao upelelezi atakuwa ni muongo?
Shahidi: Mimi nazungumzia kilichoandikwa humu, Mahita aliwachukua kwa upelelezi
Mallya: Ndiyo nasema akitokea mtu akasema kuwa Mahita hakwenda kufanya nao upelelezi atakuwa muongo?
Shahidi: Nimeeleza Ukweli
Mallya: Kutunza mahabusu ni kazi mpelelezi?
Shahidi: Mtu ambaye ni General Duty na masuala ya kiupelelezi isipokuwa kipindi atakapohitajika
Mallya: Mpelelezi Kama Mahita masuala ya mahabusu Central ni Kazi yake? siku ya tarehe 08.8.2020 ulikuwa wajibu wa Mahita?
Shahidi: Ulikuwa ni wajibu wangu mimi
Mallya: Mheshimiwa Jaji hi hayo tu.
Wakili Fredrick Kihwelo anasimama na kuanza kumuhoji shahidi wa Jamhuri.
Wakili Kihwelo: Wakati shahidi unarekodi vitu anavyoingia navyo, Je alikuwa na simu?
Shahidi: Hapana
Kiwhelo: Je Bastola.?
Shahidi: Hapana
Kiwhelo: Je, Madawa ya kulevya?
Shahidi: Hapana
Kihwelo: Je, wewe ni mtabiri kama SHEIKH YAHAYA?
Shahidi: Hapana siyo MTABIRI
Kihwelo: Wewe ni mtabibu (Physician)?
Shahidi: Ndiyo mimi MTU wa MAZOEZI
Kihwelo: Siyo MAZOEZI nakuuliza AFYA
Shahidi: HAPANA...
Kiwhelo: Je, ulisema ulifika saa 12:30, sasa hivi na mwanzo lipi kweli?
Jaji: Saa ngapi? ni kweli alisema hivyo?
Kihwelo: Natoa swali langu
Jaji: NDIYO. Tuseme vitu kwa usahihi najua humu watu wengi wanarekodi mazungumzo
Kihwelo: Je, watuhumiwa walipumzika?
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Mtuhumiwa namba tatu, alipochukuliwa na afande Jumanne alirudishwa saa ngapi?
Shahidi: Sikumbuki
Kihwelo: ni hayo tu
Wakili Fredrick Kihwelo anakwenda kuketi.
Sasa anasimama wakili Peter Kibatala
Kibatala: Tukitaka kuthibitisha wewe ni Afisa wa Polisi na siyo Usalama wa Taifa nafanyeje?
Shahidi: Kwa kutumia Force Number niliyotaja mwanzoni
Kibatala: Nathibitishaje
Shahidi: Kwa kutumia kitambulisho
Kibatala: Unafahamu kuwa unakuja kwenye zoezi muhimu la kesi ndogo?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umejuaje
Shahidi: Nimeambiwa na Inspector Swila
Kibatala: Mwambie Jaji kuwa Inspector Swila anahusika vipi na mshtakiwa wa 2 na 3
Shahidi: Hakuna sehemu yoyote kwenye Maelezo nimemtaja Inspector Swila au kuja kituoni kushughulika na watuhumiwa
Kibatala: Mueleze Mh Jaji kuwa wewe hujui lolote kuhusu Inspector Swila na hujui anahusika vipi na kesi, kwa sababu siku nikiwa central Kingai alikuja na Askari Wengine huenda Swila alikuwepo
Shahidi: Sikuwa namfahamu Inspector Swila
Kibatala: Iambie Mahakama kama ulitoa angalizo la kiulinzi kwa watuhumiwa hawa wawili
Shahidi: Niulize tena vizuri sijaelewa.
Kibatala: Leo umezungumzia lolote kuhusu Watuhumiwa watolewe kituoni wapelekwe eneo lingine?
Shahidi: Hapana hakuna sehemu niliyo zungumza.
Kibatala: Unakumbuka kurekodi kitu chochote katika station Diary kuwa maoni yako kuwa eneo lile si salama kwa washtakiwa kukaa pale?
Wakili wa Serikali: OBJECTION, nafikiri aulize maswali siyo maoni kwa shahidi
Shahidi: Huwa kwenye station Diary tunarekodi matukio kama mhusika amekabidhiwa gari yake na siyo Maoni, kwenye Station Diary Tunaainisha mali zote za kituo cha polisi siyo maoni
Kibatala: Nimesikia unasema Askari kukabidhiana kituoni, mwambie Jaji kama leo umetoa ushahidi wako wa station Diary kama ulikuwa zamu
Shahidi: Naomba kueleza kuwa station Diary haiwasilishwi
Kibatala: Occurence Book ndiyo nini.?
Shahidi: Ndiyo Station Diary
Kibatala: Ndiyo ambayo hujaitoa leo.?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tukiangalia kwenye Detention Register tutaona kuwa siku hiyo ulikuwa zamu
Shahidi: Huwezi kuona hakuna hiyo column
Kibatala: Tukitaka kuthibitisha kuwa ulikuwa kazini tutaangalia nini? Shahidi: mpaka nikalete documents.
Kibatala: Umetoa ombi kwa jaji kuwa unaomba kuleta uthibitisho kuwa siku hiyo ulikuwa kazini
Shahidi: Hapana sikuomba
Kibatala: Je, uliwahi kufahamu kuwa watuhumiwa walikwenda wapi?
Shahidi: Sikuwahi kufahamu
Kibatala: Je kuna mahala popote wewe uliwapa binafsi washtakiwa wa tatu na wa pili Uji?
Shahidi: Katika maswali unapaswa kunielekezea mimi ni yale tu yanayonihusu, Haiwezekani niulizwe mimi kuwapa mahabusu UJI au SIJAKUELEWA VIZURI.
Kibatala: Nauliza wewe binafsi kwa macho yako ulishuhudia mshtakiwa wa pili na watatu wakipata Uji?
Shahidi: Ndiyo Ndugu Kibatala Nilishuhudia wakipata Uji
Kibatala: Je, unafahamu zoezi la ugawaji kwa Mtuhumiwa ni zoezi lililotungiwa kanuni kwenye PGO?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je, unafahamu kuwa kuanzia chombo cha kumpa mahabusu chakula kimeainishwa na PGO?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu aina za chakula na resheni za chakula ambavyo watuhumiwa wakiwa rumande wanapewa mpaka na kiasi wakiwa rumande?
Shahidi: Nijuze kwanza kwenye PGO ngapi
Kibatala: Wewe jibu unafahamu au hufahamu?
Shahidi: Nijuze tu ndugu Kibatala
Kibatala: Jaji naomba anijibu
Jaji: Sijui kwanini mnaona kila swali ni MTEGO, Wewe jibu kama utakosea Mawakili wa Serikali watakuongoza
Shahidi: Sawa mh Jaji
Kibatala: Kuwa chakula aina za chakula na vyombo vya kutumia mahabusu vimetajwa kwenye PGO?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Uliwahi kufahamu kuwa watu wote waliofika na afande Kingai wametoka Moshi?
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo uliwapokea washtakiwa ukiwa hufahamu wanatoka wapi?
Shahidi: Nilijulishwa walikuwa wamekamatiwa Moshi, Sikujua kama siku hiyo ndiyo walitokea Moshi
Kibatala: Washitakiwa wanasema kabla hawajaja kwako Central walipitishwa kwanza Tazara na Mbweni kwa ajili ya kuteswa, Je tukitaka tujue kama kweli au si Kweli
Wakili wa Serikali: OBJECTION. Wakili Kibatala anamuuliza shahidi maoni yake, amuulize kama anajua waliteswa au hajui
Jaji: Naona ajibu yeye SHAHIDI, siyo LAZIMA kila kitu uelewe wewe, kama unaona kuna swali unataka aulizwe utaulizwa wakati wako ukifika.
Wakili Kibatala: Kwa kutumia DR tunawezaje kujua kuwa waliteswa au hawakuteswa?
Shahidi: DR inaonyesha kama wazima ki Afya au lah!
Kibatala: Kwenye DR kuna sehemu inaonyesha?
Shahidi: Ukinipa muda utaelewa
Jaji: Labda wakili ungempa muda wa majibu shahidi
Jaji: Shahidi UNGEKUNYWA MAJI KWANZA.
Shahidi: Ninayo mheshimiwa Jaji.
Kibatala: Kwa kuangalia DR tunaweza kujua kuwa washtakiwa wanatoka wapi? mfano Mbeya na kwingineko
Shahidi: Kwenye DR hakuna sehemu hiyo
Kibatala: Unakijua Kituo cha Polisi Tazara
Shahidi: Unajua Kwamba ni Class A.. Ni sehemu zozote anazokaa RPC
Kibatala: Unamfahamu Mahita kabla siku ya Tarehe 08?
Shahidi: Sikuwa namfahamu
Kibatala: Mwambie mheshimiwa Jaji, Afisa wa Polisi anayekaa Duty kwenye CRO PGO 288(3)(b) muda wa wa kazi wa Polisi aliyepo CRO ni Masaa 8 Unafahamu?
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Mwanzo ulisema siku ya duty yako ulikaa masaa 12, Je umemwambia Jaji Siku hiyo kuna masaa yaliongezeka kwa sababu fulani?
Shahidi: Duty ni masaa 8 lakini nilitolea muda ukaongezeka hakuna tatizo
Kibatala: Nauliza tena umemwambia mheshimiwa Jaji kwamba kwanini ulivuka muda wa kisheria wa masaa 8 siku ya Duty yako?
Jaji: Jamani Leo tuongeza muda kidogo
Wakili Kibatala anaomba dakika 10 na wengine wote wanaridhia ikiwemo magereza.
Wakili Kibatala: Msingi wa swali langu ulikuwa unatoa ushahidi Asubuhi, ulitoa ufafanuzi kwa mheshimiwa Jaji kwamba masaa ya kazi ya kipolisi CRO ni masaa 8 lakini mimi nilikaa masaa 12.
Shahidi: Hapana
Wakili Kibatala: Kwa mujibu PGO 288(6) MUDA wa kawaida wa kazi kwa Afisa wa RANKING file kwa masaa nane, Muda wa kwanza unaanza saa 7 usiku , mwingine Saa mbili Asubuhi na mwingine Saa 10 Jioni.. wewe ulisema shifti yako umeingia saa ngapi?
Shahidi: Nakukumbusha wakili mimi ni Afisa wa Polisi natakiwa kuwa popote nitakapohitajika.
Wakili Kibatala: Sijakuuliza hilo nataka kujua wewe katika maelezo yako umesema uliingia saa ngapi?
Shahidi: Saa 12 Asubuhi
Wakili Kibatala: Muda wa kwanza saa 7 usiku, saa 12 Asubuhi na muda wa tatu ni saa 10 Jioni, Je muda wako wa shifti uliosema hapa saa 12 imetajwa hapa?
Shahidi: Hapana saa 12 haujatajwa...
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Sana kuhusu Mahita, Wakati anawachukua hawa tarehe 08 ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuta watuhumiwa wametolewa,Mimi sikuwa Kazini
Wakili wa Serikali: Umeulizwa kuhusu occurence Book,ukasema inaonyesha uingiaji wako kazini na Je Vitu gani Vingine Vinaweza kuonyesha?
Shahidi: Station Diary inayoandikwa na Inspector
Wakili wa Serikali: Umebanwa sana na kuonyeshwa sana PGO ukaulizwa kwenye ushahidi wako hukupata muda wa kuelekeza kwanini ulikaa Masaa 12?
Wakili Kibatala: OBJECTION. Labda afanye rephrase siyo kutaka kuongelea masaa manne
Wakili wa Serikali: Naomba niishie hapa tu, na ni hayo tu.
Jaji: Kuna wakili mwingine wa Serikali anataka kumuongoza?
Mawakili wa Serikali: HAPANA
Jaji: AHSANTE shahidi, umemeliza ushahidi wako unaweza kwenda.
Jaji: Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Naomba hairisho mpaka 24.9.2021 kwa sababu shahidi tuliyemtarajia aanze kwanza amepata dharula ya ugonjwa alipata ajali, Jumamosi, wakati tunasubiria akipata muda wa ku'recover tunaomba kumaliza siku ya tarehe 24 mwezi wa 9 siku ya Ijumaa.
Wakili Kibatala: Kwa niaba ya wenzangu hatuna pingamizi.
Jaji: anaandika.
Jaji: Niwashukuru tena kwa mara nyingine kwa uvumilivu wemu wakati tunaendelea na shauri hili
Jaji: Kwa sababu ambazo zimetolewa na upande wa mashtaka na kukubaliwa na upande wa Utetezi, Nalazimika kuahirisha shauri hili mpaka siku ya Ijumaa tutakapoendelea kusikiliza shauri hili, mahabusu wataendelea kuwa mahabusu.
Asanteni sana
MWISHO
Kesi Na. 16 ya mwaka 2021 inatajwa
Kesi namba 16 ya 2021, jamhuri dhidi ya Khalfan Bwire, Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe
Jaji anamuita Wakili wa Serikali...
Wakili wa Serikali anatambulisha Jopo lake
- Robert Kidando
- Nassoro Katuga
- Ignas Mwanuka
- Esther Martin
- Tulumanywa Majigo
Mawakili upande wa Utetezi wanatambulishwa
- Peter Kibatala
- Jeremiah Mtobesya
- Fred Kihwelo
- John Malya
- Gaston Garubindi
- Seleman Mtauka
- Michael Mwangasa
- Evaresta Kisanga
- Khadija Aron
- Maria Mushi
- Deogratius Mahinyila
- Nashon Nkungu
- Jebra Kambole
Mawakili wa mshtakiwa wa kwanza ni Jeremiah Mtobesya na Nashon Nkungu.
Mshtakiwa wa tatu atawakilishwa na Dickson Matata na Fredrick Kihwelo
Mshtakiwa wa pili atawakilishwa na John Mallya
Mawakili wengine wote watamwakilisha mshtakiwa wa nne
Jaji anauliza kama mawakili wa serikali wanalolote Juu ya ingizo Jipya la wakili Fredrick Kihwelo kama kuna mgongano wa maslahi.
Wakili wa Serikali anasema hakuna tatizo kwa sababu tangu kesi ianze hajaonekana kwenye Column yoyote.
Jaji: hiyo wakili Fredrick Kihwelo anamshikia mikoba wakili Dickson Matata au atakuwa moja kwa moja kwa mshtakiwa watatu?
Kibatala: kuanzia leo mshtakiwa watatu atawakilishwa na wakili Fredrick Kihwelo na kusaidiana na Dickson Matata ambaye leo hayupo mahakamani
Wakili wa Serikali anahoji mshtakiwa mwenyewe anasemaje baada ya kumsikiliza Kibatala
Jaji: hilo tayari nimeshaliongelea kuwa baada ya utambulisho wa Kibatala nitamuhoji Mshtakiwa
Jaji: Ling'wenya bila shaka umesikia?
Ling'wenya: Nimesikia Mh. nakubaliana na Wakili Kibatala
Jaji: Kuna taarifa gani kuhusiana na Wakili Dickson Matata kutokwepo mahakamani?
Kibatala: Ana appear mbele ya Jaji mwingine wa mahakama Kuu ambaye ni Jaji Senior
Jaji: Kama hakuna session inayoendelea huko mahakamani anaweza kuomba udhuru huko, Otherwise ni mahakama ya Rufaa na pia kama kuna kesi inaendelea huko Seniority inatake place.
Jaji: Ila ni vizuri tukawa tunajua na mjue katika kesi, kesi za Jinai zinapewa kipaumbele kuliko kesi za madai, ni vizuri tujue ni kesi gani aliyopo huko.
Kibatala: Sina Details sana ila ukiniruhusu naweza kumuuliza ili ujaze.
Jaji: Je, mawakili wa serikali kuna jambo lolote la kuongezea?
Wakili wa Serikali: Hatuna mheshimiwa
Jaji: Sawa, upande wa Serikali mpo tayari?
Wakili wa serikali: Nadhani tulikuja kwa ajili ya kesi ndogo na kuna shahidi alihitajika kuendelea, shahidi yupo tayari kuendelea
Jaji: Mawakili wa utetezi, mpo tayari kuendelea?
Kibatala: Ndiyo mheshimiwa.
Jaji: Shahidi aliyebakiza ushahidi wake apande kizimbani tuendeleee
Jaji: siku ya Ijumaa tulikuapisha, Nakukumbusha kuwa kiapo chako kinaendelea
Shahidi: Sawa Mheshimiwa
Kibatala: Unakumbuka mara ya mwisho wakati unatoa ushahidi ulisema mkiwa maeneo ya Boma Ng'ombe washtakiwa walikula Chakula. Je, unakumbuka walikula chakula gani?
Shahidi: Ndizi, Nyamachoma na MO Energy
Kibatala: Wakati shauri limehairishwa tulituma mtu huko Boma Ng'omba na Siha kutokana na unyeti wa Kesi, Je unakumbuka Jina la Muhudumu?
Shahidi: Hapana sikumbuki.
Kibatala: Je, unakumbuka jinsia yake aliyewahudumia?
Shahidi: Hapana, tulikuwa kwenye gari, Chakula afande Kingai ndiye aliyeleta
Kibatala: Je, ni mara ngapi umekuwa na watuhumiwa na kuwapatia chakula?
Shahidi: Ni jambo la kawaida mkiwa kwenye operesheni kumpatia mtu chakula
Kibatala: unafahamu PGO imetaja utaratibu wa kupatia chakula watuhumiwa?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: unafahamu kuwa PGO ndiyo ina maelekezo ya pekee juu ya utaratibu wa kumpatia chakula Mtuhumiwa?
Shahidi: na sheria mbalimbali siyo tu PGO
Kibatala: Zitaje
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu kwa Mujibu wa taratibu za Tanzania na kimataifa kuna hotuba inayotambua kuwa na vikosi maalum vya ugaidi Tanzania.. Je unamfahamu?
Shahidi: Ungemfuata aliyesema umuulize
Jaji: Shahidi anakuuliza wewe!
Kibatala: Je, kuna sehemu yoyote umejitambulisha wewe ni mmoja ya kikosi Maalum cha kupambana na magaidi Tanzania?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je, inaruhusiwa wakati wa kumuhoji mtuhumiwa kumchoma choma na bisibisi?
Shahidi: Hapana hairusiwi
Kibatala: Je inaruhusiwa kumchoma choma mtuhumiwa na bisibisi na kumwambia tutakufanya kama tulichokufanya Moshi?
Shahidi: Hairuhusiwi
Kibatala: Je, inaruhusiwa kumfunga mtu pingu miguuni na mikononi na kumining'iza na kumpiga na marungu kwenye unyayopaka hawezi kutembea?
Shahidi: Hairuhusiwi
Kibatala: Je, Tazara ni kituo Class A au B?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Ulizungumzia kuwa ulimtoa mtuhumiwa kutoka Central kwenda Mbweni?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Central ulipomtoa mtuhumiwa ni Class A au B?
Shahidi: Class A
Kibatala: Kwa hiyo ulimtoa kituo Class A kwenda class A?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, unafahamu kuwa taratibu za kumsafirisha mtuhumiwa kwenda popote zimewekwa kwenye PGO?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: PGO inasema kuwa wakati wa kumhamisha mtuhumiwa kutoka Point moja kwenda kwenye point nyingine inatakiwa kuandikwa Detention Register.?
Shahidi: Hilo sifahamu
Kibatala: Wewe ulikuwa Arresting Officer.?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jaji akimaliza kuandika mwambie kuwa ni kwa PGO ya ngapi
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Unafanya kazi kwa kutumia PGO au mazoea?
Shahidi: kwa taratibu mbalimbali
Kibatala: ikiwepo PGO
Shahidi: NDIYO
Kibatala: Je, unafahamu lolote kuhusu Moses Lijenje na umezungumzia hapa hatima ya Moses Lijenje?
Shahidi: Sikuzungumzia
Kibatala: Je, unafahamu lolote kuhusu utaratibu wa kumtangaza mtuhumiwa kwa kutumia tangazo?
Shahidi: Hapana
Kibatala: umezungumzia kuhusu KUMFUNGA Pingu mshtakiwa, Je kuna sehemu yoyote umezungumzia KUMFUNGUA pingu mshtakiwa ?
Shahidi: Kwenye maelezo yangu siku zungumzia.
Kibatala: Wakati wakili John Mallya anakuhoji kuhusu chakula alikuhoji kuhusu kiwango cha chakula mtuhumiwa alipewa, unafahamu PGO imezungumzia kiwango, kiasi na aina gani ya chakula ambacho mtuhumiwa anapaswa kupewa akiwa chini ya Ulinzi? je Unafahamu?
Shahidi: Hapana, sifahamu
Kibatala: Umezungumzia kupewa chakula watuhumiwa wakiwa Boma Ng'ombe na Himo, je umezungumzia kuhusu watuhumiwa kupewa chakula wakiwa kituo cha polisi Moshi?
Shahidi: Hapana sikuzungumzia
Kibatala: Je, umezungumzia kuhusu kuwapekua watuhumiwa mauongoni ulipowakuta, Je kwa mujibu wa PGO inaruhusiwa kumfanyia mtu Upekuzi maungoni mbele za Watu?
Shaidi: Ndiyo inaruhusiwa
Kibatala: PGO ipi?
Shahidi: sifahamu
Kibatala: nakusomea PGO 272(5) inayozungumzia kumpekua mtu mauongoni, PGO inasema kwa Kuanzia Kichwani, Kushuka chini... hapa mwisho inasema nobody search in Public view.
Shahidi: mheshimiwa inaruhusiwa Kwa mujibu wa PGO
Kibatala: Je, PGO inaruhusu kumpekua mtu maungoni hadharani?
Shahidi: inaruhusu
Kibatala: Nikikupa PGO utaonyesha ni wapi?
Shahidi: ndiyo..
Peter Kibatala anamkabidhi shahidi PGO
Shahidi: PGO inaruhusu isipokuwa kama utamvua mtu nguo, kuchuchumaa inakatazwa.
Jaji: ungesoma kama wakili Kibatala anavyosoma au ungependa kuelezea?
Shahidi: Ningependa kuelezea tu..
Kibatala: Je, UNASOMA PGO au HUSOMI?
Shahidi: SISOMI Mheshimiwa JAJI
Kibatala: Ahsante, sasa ngoja Jaji aaandike umekataa kusoma PGO kwa unachokisema.
Kibatala: Unafahamu Diary ya Afisa wa Polisi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wewe ni Gazetted au siyo Gazetted Officer?
Shahidi: Siyo Gazetted Officer
Kibatala: Unafahamu PGO inazungumzia Afisa wa Polisi wa cheo kama cha kwako anapotoka eneo la kazi?
Shahidi: Siyo Gazetted Officer
Kibatala: Je unafahamu RPC anatakiwa kukupa wewe ruhusa?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je unafahamu RPC anatakiwa kukupa wewe ruhusa?
Shahidi: Siyo RPC pekee yake
Kibatala: Je nani mwingine?
Shahidi: RPC, RCO na Staff Officer
Kibatala: Je Ruhusa ya kipolisi inatolewa kwa maandishi au kwa mdomo?
Shahidi: maandishi
Kibatala: Je umetoa nyaraka (Movement Order) Mahakamani.?
Shahidi: PGO inasema Officer ambaye ni Gazetted haitaji Movement Order na kwa cheo changu Movement yangu ilikuwa inabeba Wengine.
Kibatala: Tuokoe muda, Sijakuuliza hicho
Shahidi: Muda tunao Mheshimiwa
Jaji: Jibu kuwa ulikuwa na kibali au hukuwa na kibali
Shahidi: Ndiyo nilikuwa namjibu
Kibatala: Wakati unatoa ushahidi wako hapa na ulionyesha hiyo Movement Order?
Shahidi: Ukimaloza inarudishwa ofisini
Kibatala: Ulitoa mahakamani au hukutoa?
Shahidi: Haikuhitajika, sikuulizwa lakini ipo..
Kibatala: Ulitoa au hukutoa?
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Je, unafahamu hata RCO kama afande kingai anasehemu anatakiwa kuripoti?
Shahidi: Siwezi kumuongelea Afande wangu.
Kibatala: Ongelea concept unaifahamu au huifahamu, kwa sababu hata mimi nafahamu juu ya mawakili Senior taratibu zao zikoje.
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umezungumzia mtuhumiwa kuwa na Jacket
Shahidi: ndiyo
Kibatala: Je, unafahamu kuwa hilo Jacket ndilo lililotumika kumfungia machoni asione mtuhumiwa?
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Je, unafahamu anayetakiwa kufanya upekuzi ni afisa wa Polisi mkamataji
Shahidi: Yeyote anaweza kufanya upekuzi
Kibatala: Je nikikupa PGO unaweza kunionyesha popote ambapo polisi yeyote anaweza kufanya upekuzi?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati wote wa kazi yako ulishawahi kufuata PGO ukawa nayo karibu na kuitumia?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mh. Jaji ni hayo tu, sina swali lingine
Jaji: Ahsante, kila siku naona mtuhumiwa mmoja tu ndiyo anakunywa maji, mmewapa wengine? wapeni Maji wanywe,Askari Magereza Myakague ni haya tunayokunywa wote
Jaji: Mawakili wa Serikali kuna lolote kwa ajili ya Re: examination?
Wakili wa serikali: Tupo tayari
Wakili wa Serikali: Nitakuhoji kwa ufafanuzi. Je, Ijumaa wakati Kibatala anakuhoji ulisema anachanganya PGO ulikuwa una maana gani?
Shahidi: Wakati wakili Kibatala ananihoji alitaka PGO ya 272 leo nashukuru kafanya Research kidogo kwa sababu alikuwa anaongela kuhusu kuchukua Maelezo, Leo ndiyo kanihoji kwa usahihi kuhusu ukamataji.
Wakili wa Serikali: Hiyo PGO inayozungumzia kuhusu maelezo eleza ni kwa namna gani?
Shahidi: wakati unamchukulia maelezo ndiyo unamuhoji kwa kumuonya kama utatumia mahakamani Kama ushahidi
Wakili wa Serikali: Wakati Kibatala anakuhoji kuhusu kumtoboa na bisibisi kila kitu ulikuwa unasema hairuhusiwi
Shahidi: Hairuhusiwi kwa mujibu wa katiba zetu, kama torture na vinginevyo.
Wakili wa Serikali: Fafanua kuhusiana kumfunga na mtu kwa Jacket
Shahidi: Kama nilivyomuuliza wakili Kibatala hairuhusiwi na hakuna haja ya kufanya hivyo
Wakili wa Serikali: Hakuna sehemu uliomba ruhusa kufuata Notebook yako hapa Mahakamani, kwanini ulifanya hivyo?
Shahidi: Sikuhitaji kwa sababu yote niliyoyaeleza nilikuwa nayakaumbuka
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuwa hukuandika katika maelezo yako kama mliwapatia chakula Adam kasekwa mkiwa Boma Ng'ombe na Himo
Shahidi: Sikuandika katika maelezo yangu kwa sababu nili' focus katika mambo ya ukamataji
Wakili wa Serikali: Uliulizwa hapa pia kuhusiana na uhitaji wa movement Order kutoka kituo chako cha kazi, Kwanini hukuileta hapa mahakamani?
Shahidi: Kwa mujibu wa taratibu, Polisi ukimaliza kuitumia Movement Order umarudisha ofisini, nikaendelea na kazi.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Mimi ni hayo hatuna kingine..
Jaji: Shahidi tunashukuru umemaliza ushahidi wako unaweza kwenda sasa..
Shahidi anatoka kizimbani.
Jaji: Upande wa Serikali.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa tunaomba kuendelea na shahidi wa tatu..
Jaji: sawa Mleteni Shahidi wa 3 Mahakama ipo kimya.
---
Shahidi wa tatu amefika
Jaji: Shahidi jitambulishe
Shahidi: Naitwa Askari namba H2343, afande Msemwa
Jaji: Apa
Shahidi: Mimi Afande H2343 naapa Ninachosema kitakuwa kweli, Eeh! Mwenyezi Mungu nisaidie
Jaji: Anayehoji nani upande wa serikali?
Wakili wa Serikali: MIMI NASSORO KATUGA
Wakili wa Serikali: Shahidi ungependa kusimama au kukaa?
Shahidi: Kusimama
Wakili wa Serikali: Kituo chako cha Polisi ni wapi?
Shahidi: Kituo cha Polisi Oysterbay
Wakili wa Serikali: upo tangu lini?
Shahidi: Mwaka huu January/February
Mawakili wa Serikali: Umeajiriwa mwaka gani? Shahidi: 2013 Wakili wa Serikali: Ulianzia kituo gani?
Shahidi: Nilianzia Polisi Ilala na baadae nikahamia Central Polisi
Wakili wa Serikali: Central ulikuwa mpaka lini?
Shahidi: 2014 Mwanzoni Mpaka Mwaka jana mwishoni kuanzia January 2021 nikaenda Oysterbay
Wakili wa Serikali: Oyesterbay upo kitengo gani?
Shahidi: Upelelezi
Wakili wa Serikali: Ukiwa Central Polisi Ilala ulikuwa unafanya kazi gani?
Shahidi: Nilikuwa General Duty sisi ambao tunavaa uniform kawaida tofauti na wale wa kofia nyekundu FFU
Wakili wa Serikali: Ulikuwa na Jukumu gani?
Shahidi: Nilikuwa nalinda raia na mali zao.
Shahidi: Doria na ukaaji wa point pamoja na kuwa chumba cha mashtaka
Wakili wa Serikali: Umezungumzia chumba cha mashtaka ni nini?
Shahidi: Ni pale wanapokaa Askari (CRO) kwa ajili ya kupokea taarifa mbalimbali na ufunguaji wa kesi na kupokea watuhumiwa wanaoletwa
Wakili wa Serikali: Watuhumiwa wanaoletwa kutoka wapi?
Shahidi: Sehemu mbalimbali
Wakili wa Serikali: Unasema ulikuwa kwenye chumba cha mashitaka, ufanyaji kazi unakuwa ni Vipi?
Shahidi: Kwanza lazima kiwe na CRO incharge kazi utakazofanya ni zile utazopewa na CRO incharge
Jaji: naona Joto ni kali, naomba madirisha yafunguliwe.
Wakili wa Serikali: Naweza kukumbushwa alipoishia?
Jaji: CRO panakuwa na Incharge
Wakili wa Serikali: Enheee Endelea...
Shahidi: Unakuwa unafanya majukumu unayopewa na Incharge.
Wakili wa Serikali: Iambie mahakama sasa kwa ufupi sana mnapokuwa mnapokea watuhumiwa nini kinafanyika?
Shahidi: Mnapopolea watuhumiwa kuna taratibu zake ukiwa CRO kinakamilishwa na kitu kinaitwa DR (Detention Register)
Wakili wa Serikali: Iambie mahakama ni kitu gani
Shahidi: Ni kitabu kinachotunza kumbukumbu za kituo cha Polisi
Wakili wa Serikali: Kwa namna gani!?
Shahidi: Kuna taratibu zake za kumpokea mtuhumiwa na askari anayekuwa chumba cha mashtaka uzifahamu.
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ni taratibu gani..
Shahidi: Kwanza wakati unamuhoji ni Kumpekua ili wakati unampekua unakuwa mpo nae salama
Wakili wa Serikali: Wakati mnampekua mnafanya utaratibu gani?
Shahidi: Chochote kinaweza kuanza kuhojiwa na kumpekua
Shahidi: Kiuhalisia nilichofundishwa CCP kuwa mtu anapokuwa amekamatwa anakuwa na Mawazo yeye mwenyewe
Wakili wa Serikali: Mimi sitaki mawazo yako, sasa wewe unafanya kitu gani?
Shahidi: kuhakikisha haingii na kitu chenye madhara Mahabusu..
Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Kumuingiza kitabu cha mahabusu (Detention Register)
Wakili wa Serikali: Unampekuaje?
Shahidi: Unampekua kwa kumwambia nyoosha mikono Juu, kwa kugeukia ukuta na kuushika, na mwisho wa kumpekua ni kumwambia kaa chini
Wakili wa Serikali: unamhoji kwa namna gani
Shahidi: Kama Mtuhumiwa analetwa kwa kesi ambayo imeshafunguliwa anatakiwa awe na Case reference namba yake
Wakili wa Serikali: Kesi inayokuwa imefunguliwa wapi?
Shahidi: Popote pale ndani ya Tanzania
Wakili wa Serikali: Hiyo Reference inahusisha vitu gani?
Shahidi: Reference ndiyo kitu kinafahamila sana Mtaani RB, mfano kesi za Oysterbay zinakuwa na neno Kifupisho OB kwa maana Oysterbay Mkwaju, RB kwa maana imeripotiwa
Wakili wa Serikali: Hiyo ya Oysterbay je ya Central?
Shahidi: Cental ni neno CD na reference namba kesi ilianza kupelelezwa inakuwa na IR badala ya RB
Wakili wa Serikali: Baada ya namba nini kingine analeta?
Shahidi: na Jina la kosa analokuwa ametenda
Wakili wa Serikali: Vitu gani Vingine?
Shahidi: Unapata Particulars kwa aliyemleta mtuhumiwa na zingine kwa mtuhumiwa mwenyewe.
Wakili wa Serikali: zipi hizo?
Shahidi: Majina, Miaka yake, Jinsia yake..
Wakili wa Serikali: Jinsia ukimaanisha?
Shahidi: Kama ni mwanamke au mwanaume
Jaji: Wewe unajuaje?
Shahidi: Namkagua pia kuthibitisha
Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Hali yake ya Ki afya
Wakili wa Serikali: Akikujibu wewe unafanyaje?
Shahidi: Lazima ujiridhishe kama mgongoni unaweza kumkagua
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama kwenye ukaguzi wa jinsia mnafanya kitu gani?
Shahidi: Ni kujihakikishia physically
Jaji: Ina maana mwanamke unamkagua wewe?
Wakili wa Serikali: Ndiyo nilichotaka ila niliogopa nisije kuonekana namuongoza
Shahidi: CRO panakuwa na Askari wa kike kwa Ukaguzi wa Mwanamke. Akiletwa mwanamke ukaguzi utafanywa na Askari wa Kike
Wakili wa Serikali: Tarehe 7 Mwezi wa 8 2020 Ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa bado sijahamia Oysterbay nilikwa bado mkoa wa kipolisi Ilala, Central
Wakili wa Serikali: Unakumbuka nini siku hiyo?
Shahidi: Niliiingia kazini, nilikuwa na zamu ya CRO shifti
Wakili wa Serikali: Unaposema CRO shift unamaana gani?
Shahidi: Pale CRO panakuwa na Shift sababu tunafanya kazi masaa 24 kwa hiyo tunafanya kazi kwa zamu
Wakili wa Serikali: Ulipoingia kazini ulifanya nini?
Shahidi: Niliingia kazini Alfajiri na askari wengine watano
Wakili wa Serikali: Unaweza kuwataja kama unawakumbuka Shahidi: WP fatuma,Aziz na wengine
Wakili wa Serikali: Mliingia kazini Saa ngapi?
Shahidi: 12 Alfajiri
Wakili wa Serikali: Siku hiyo CRO Incharge alikuwa ni nani?
Shahidi: Palikuwa na Inspector msaidizi wa Polisi
Wakili wa Serikali: Siku hiyo wewe ulikuwa na jukumu gani
Shahidi: nilikuwa ni mtunza mahabusu, mahabusu wa kiume ni mimi, na wakike wata dili na WP SEMENI
Wakili wa Serikali: Unakumbuka Jukumu la Kufungua kesi.?
Shahidi: Nakumbuka Afande Emmanuel na Afande Samuel
Wakili wa Serikali: Ulikuwa na majukumu gani
Shahidi: ilikuwa saa 12 kasoro nilifika na kupangiwa majukumu na wengine
Wakili wa Serikali: Kitu gani ulifanya
Shahidi: Baada ya kukabidhiwa mahabusu naenda kuhakiki kule mahabusu chini kwa kutaja jina mojamoja
Wakili wa Serikali: Nini Unakumbuka kikafuata?
Shahidi: Siku hiyo ilikuwa tofauti kidogo baada ya kukagua mahabusu nikamuona Afande Kingai akiwa anaingia na Mahabusu
Wakili wa Serikali: Mahakama ingependa kujua ulikuwa unamfahamu kabla?
Shahidi: Ndiyo nilikuwa namfahamu
Wakili wa Serikali: alikuwa na nani?
Shahidi: Afande Jumanne
Wakili wa Serikali: ulikuwa unamfahamu Jumanne?
Shahidi: ndiyo, alikuwa makao Makuu ya polisi kabla
Wakili wa Serikali: nini kilifuata?
Shahidi: Akaniambia ni watuhumiwa kesi yao imefunguliwa hapa
Wakili wa Serikali: Unakumbuka RB yao?
Shahidi: Sikumbuli RB ila kosa nakumbuka
Wakili wa Serikali: Unakumbuka kosa gani Shahidi Kula njama za kutenda makosa ya ugaidi
Jaji: Naona tunge' break kidogo... Tutarudi saa saba na nusu kuendelea...
TUENDELEE BAADA YA BREAK FUPI
Wakili wa Serikali: Ikupemdeze Mheshimiwa jaji column yetu ya kwanza ipo vilevile tupo tayari kuendelea.
Kibatala: Tupo tayari kuendelea.
Jaji: Wakili aliyekuwa anamuongoza shahidi aendelee.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa naomba kukumbushwa na mahakama tuliishia wapi.
Jaji: Wakati wa kuandika RB na IR namba
Wakili wa Serikali: Unazikumbuka?
Shahidi: Hapana lakini zile namba CD za Central haziwezi kujirudia na kufanana
Wakili wa Serikali: Baada ya kupokea hizo reference kiliendelea nini?
Shahidi: Afande kingai na Afande Jumanne walitoka
Wakili wa Serikali: Kiliendelea nini baada ya kupokea hizo reference?
Shahidi: Taratibu zingine zilifuatwa baada ya kuwa na watuhumiwa
Wakili wa Serikali: Eleza mahakama nini kilifuata
Shahidi: Nilianza kumpekua mmoja mmoja, namwambia nyoosha mikono juu, kaa chini anakaa.
Wakili wa Serikali: Iambie mahakama baada ya Afande Jumanne kuwaleta watuhumiwa wakiwa na pingu nini kilifuatia kuhusu pingu?
Shahidi: Baada ya kufungua pingu kila mmoja na pingu yake, alisema akituachia pingu zitapotea
Wakili wa Serikali: Hujasema nani alifungua pingu
Shahidi: Mimi nilifungua siyo lazima nitumie pingu za afande Jumanne kwa sababu funguo za pingu zinaingiliana
Jaji: Unaposema koti unamaanisha nini?
Shahidi: Namaanisha Jacket
Jaji: Naamini wakina Kibatala mnaelewa!?
Kibatala: Ndiyo Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Baada ya kuwapekua nini kilifuata?
Shahidi: Nilianza kuchukua taarifa zao
Wakili wa Serikali: Kama zipi?
Shahidi: Kama Jina, Miaka, Jinsia na Dini
Wakili wa Serikali: unaweza kukumbuka majiina yake
Shahidi: Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali: Wakati huo unaandika wapi?
Shahidi: Kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: Ulimuuliza nini kingine?
Shahidi: Alijibu ki Afya yupo vizuri
Wakili wa Serikali: Akakuambiaje kuhusu Afya?
Shahidi: Mzima
Wakili wa Serikali: Ulijiridhishaje?
Shahidi: Tunajiridhisha kwa vitu kama majeraha, vitu kama Malaria ngumu sana
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea baada ya kujiridhisha?
Shahidi: Nikaendelea na mtuhumiwa wa pili
Wakili wa Serikali: Unakumbuka majina yake?
Shahidi: Alinitajia matatu lakini nakumbuka moja
Wakili wa Serikali: Lipi ?
Shahidi: Adam kasekwa
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifuata?
Shahidi: nilichukua majina yake na taarifa zingine
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo?
Shahidi: watuhumiwa wote wawili niliwapeleka mahabusu
Wakili wa Serikali: Unakumbuka muda?
Shahidi: Ilikuwa saa 12 na nusu Wakili wa
Serikali: Kilifuatia nini?
Shahidi: Baada ya muda Afande Kingai alirudi tena
Wakili wa Serikali: Alisemaje?
Shahidi: Nitoleee mtuhumiwa, nikamuhoji Nimamuuliza yupi? akaniambia Adam
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Niliandika maelezo na kuandika kuwa Mtuhumiwa ametoka mahabusu, nikamwambia afande kwakuwa nimtoa huyu mtu inabidi usaini isije kuonekana ametoroka
Wakili wa Serikali: alikutaka umpelekee wapi?
Shahidi: Nilimkuta palepale Counter, akasema nimwachie aende na mtuhumiwa
Shahidi: Afande SEMENI akaniambia niongozane nae
Wakili wa Serikali: Mlienda wapi?
Shahidi: Ofisi ya RCO floor ya kwanza
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea?
Shahidi: Nilirudi kuendelea na majukumu yangu
Wakili wa Serikali: Baada ya kurudi huyo Afande kingai ikawaje?
Shahidi: Alikaa naye kama masaa mawili akamrudisha. Nilimuhoji majina yake akaniambia, nikamuhoji Jinsia yake, hali yake ya Kiafya yupo vizuri na kumpekua kuhakikisha aingii na chochote mahabusu
Wakili wa Serikali: Baada ya kujaza taarifa zake?
Shahidi: Nilimrudisha mahabusu
Wakili wa Serikali: Ukiwaona unaweza kuwakumbuka?
Shahidi: Nawakumbuka nikiwaona
Wakili wa Serikali: Kitu gani kitakufanya uwakumbuke?
Shahidi: Upekee wa siku hiyo, tangu nizaliwe nilikuwa sijawahi kuona Magaidi, ikabidi niwaangalie vizuri.
Wakili wa Serikali: Hapa mahakamani unaweza kuwatambua?
Shahidi: Ndiyo nikiwaona naweza kuwatambua.
Wakili wa Serikali: Kwa idhini ya mahakama unaweza kwenda kuwagusa na kuwatambua?
Jaji: Nenda sasa au UNAWAOGOPA?
Shahidi: Hapana naweza kwenda.
Shahidi: Ni hawa wawili
Wakili wa Serikali: Unaweza kusema huyu ni nani na huyu ni nani?
Shahidi: Labda wavue barakoa.
Jaji: Sasa Barakoa ni kifaa cha mtu cha Afya, sioni shida kama amewagusa wawili otherwise awaguse na kuwataja majina.
Wakili wa Serikali: Mahakama Imeonyesha kuwavua kifaa cha Afya si sawa, tuendelee
Jaji: Mimi kama mimi nimeelewa watu aliofanya nao kazi siyo Mshtakiwa nne wala wa kwanza
Wakili wa Serikali: Baada ya kuwapokea mtuhumiwa afande Kingai ukamrudisha mahabusu nini kingine kilitokea?
Shahidi: Hakuna kitu kingine kilichotokea, nilipopeleka chakula cha mchana nilimuona
Wakili wa Serikali: Huyu ulimpelekea chakula kutoka wapi?
Shahidi: Kuna vyakula vya mahabusu na vingine kutola kwa ndugu zao
Wakili wa Serikali: Mimi nauliza specific kwa huyu wa Kingai
Shahidi: Chakula cha mahabusu
Jaji: ulipeleka chakula saa ngapi?
Shahidi: saa nane na nusu
Jaji: uliposema ulimuona mara ya mwisho wakati wa chakula unamaana gani?
Shahidi: Narudia tena kuwa alipeleka chakula cha mchana na kumuona mara ya mwisho, lakini ilikuwa tayari Jioni
Jaji: Hebu rudia vizuri hapo, RELAX!
Shahidi: Mchana Jukumu langu ni kupeleka chakula, Mchana tena napeleka chakula, jioni kwa wanaoingia jioni ndiyo wanapeleka chakula cha jioni
Wakili wa Serikali: Unasema ikawa mara ya mwisho kuona, kwanini unasema mara yako ya mwisho?
Shahidi: Baada ya kutoka siku ile, siku inayofuata sikuwakuta
Wakili wa Serikali: Kwanini hukuwakuta?
Shahidi: Kwa sababu siku inayofuata niliingia shift ya 3
Wakili wa Serikali: Hiyo Detention Register ulioona mahakamani unaweza kuikumbuka?
Shahidi: unajua.
Shahidi: unajuaaaa.....
Jaji: Shahidi jibu swali unaweza kuikumbuka au lah
Shahidi: Naweza Kuikumbuka
Wakili wa Serikali: Kitu gani kitakufanya ukumbuke?
Shahidi: Ni taarifa ya pale juu ya kitabu Imeandikwa Detention Register na Ministry of Home Affair,tuliandika kwa Makapeni
Wakili wa Serikali: Shahidi hebu shika hiki kitu, ukipata wasaa kiangalie..
Shahidi: Anakikagua na kuanza kufungua ndani
Shahidi: Tayari
Wakili wa Serikali: umekitambua
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kwa kuona nini?
Shahidi: kuona mwandiko wangu
Wakili wa Serikali: Kwa nje imeandikwa nini?
Shahidi: Ministry of Home affair
Wakili wa Serikali: Muonyeshe Jaji kwa kunyanyua
Shahidi: Mheshimiwa hii ndiyo DR na mbele inaandikwa kwa mwaka fulani
Jaji: Wewe elezea yanayokuhusu tu, sababu mwanzo hukuongelea mambo ya DR ukasema huyakumbuki.
Shahidi: Ndiyo Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Unataka mahakama ifanye nini kuhusu kitabu hiko?
Shahidi: Naomba mahakama ikubali kukitumia kama kielelezo.
Jaji: Sasa Mawakili wa Serikali mnataka nini?
Wakili wa Serikali: Tunaomba kiiingie kama kielelezo cha ushahidi
Jaji: Mawakili wa Utetezi?
Wakili Mtobesya: Kwa niaba ya mshtakiwa wa kwanza sina kipingamizi
Wakili Kihwelo: Kwa naiaba ya mshtakiwa wa pili sina kipingamizi
Wakili John Mallya: Kwa niaba ya mshtakiwa wa tatu sina kipingamizi
Wakili Peter Kibatala: Kwa niaba ya mshtakiwa wa nne sina kipingamizi.
Jaji: Sawa
Jaji: Detention Register imepokelewa kama kielelezo namba 1 kwa upande wa Jamhuri kwenye kesi ndogo..
Wakili wa Serikali: Kama wataitumia naomba watumie page husika
Jaji: Upande wa utetezi Mawakili wote wa utetezi hawana pingamizi.
Wakili wa Serikali: Kama kuna Jambo lolote ungependa kulielezea shahidi, karibu
Shahidi: Mtuhumiwa wa kwanza kumpokea alikuwa na entry namba 392 lakini RB yake ni CD/RB 3093/2020 Mohammed Abdilahi Ling'wemya kosa lilikuwa kula njama za kutenda makosa ya ugaidi IR ni CD/IR 2097/2020
Aliingia tarehe 07.8.2020 Saa 12 na dakika 7 asubuhi na baadae ni saa 2 na dakika 10 aliyemtoa nje ni ASP Jumanne, Sababu za kumtoa nje ni upelelezi.
Shahidi: Mtuhumiwa wa pili Entry namba 393 na Column ya report Book palikuwa na CD/RB 3093/202 Majina ni Adam kasekwa IR /CD/ IR 2097/2020. Aliingia tarehe 07.8.2020 aliingia Saa 12 na dakika 9 na siku anatoka alitolewa na ASP KINGAI. Nikawapokea tena watuhumiwa.
Shahidi: Mtuhumiwa wa kwanza alikuwa Adam Kasekwa akiwa RB /CD/RB/ 3093/2020 Miaka yake aliniambia ni ileile 31 Condition ni Good na IR no CD/IR/2097/2020 nilimpokea Saa 3 dakika 5, anaitwa Adam Hassan Kasekwa, na baadae anaonekana alitolewa 08.8.2020 na alitolewa saa 4 na dakika 5 asubuhi, Mtu aliyemtoa anaitwa Inspector Mahita, sababu za kumtoa ni nje kwa upelelezi.
Shahidi: Mtuhumiwa mwingine nilimpokea tarehe hiyo hiyo Mohammed Abdilah CD Ling'wenya, Miaka 34 na jinsia ni mwanaume na Physical Condition aliniambia yupo Good IR /CD/2097/2020. Mtu huyu tarehe 08.8.2020 Saa 4 na dakika 5 alitolewa nje na aliyemtoa ni Inspector Mahita na Sababu za kumtoa ni nje kwa Upelelezi.
Jaji: Sawa, mawakili wa Serikali...
Wakili wa Serikali: Unasema kuwa ulimuona Mtuhumiwa muda wa mwisho fafanua
Shahidi: Kwenye Detention Register kama unawapa chakula unatiki kwenye Column, na nilitiki kuwa Uji alipata na baadae waliporudi na kuwaingiza upya ilionyesha walipata chakula cha asubuhi, mchana na Jioni
Wakili wa Serikali: Una kitu kingine ungependa kuongeza
Shahidi: Sina cha kuongeza
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji sisi ni hayo tu kwa sasa..
Jaji: Wakili Mtobesya kama kuna lolote.
Mtobesya: Nitaanza na maswali machache kama nitakuwa nimecha Wakili Nashon atamalizia
Mtobesya: Shahidi unafahamu kitu kinaitwa Station Diary?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Mtobesya: Kazi yake ni nini
Shahidi: Wakati wa ukaguzi na masuala yoyote ya watuhumiwa wakiwa kituoni
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema siku hiyo wewe ni charge Room Officer?
Shahidi: Siyo Sahihi
Mtobesya: Ieleze mahakama nani alikuwa charge room officer
Shahidi: Charge Room Officer ni Mkuu wa kituo
Mtobesya: Kama wewe hukuwa charge room Officer ulikuwa unashughulika na watuhumiwa kama nani?
Shahidi: Charge room officer anatupangia sisi tufanye kazi yake
Mtobesya: Kwa hiyo wewe ulikuwa unafanya kazi za Charge room Officer
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwa hiyo ni sahihi nikisema ulikuwa unafanya kazi za Charge room officer
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwa hiyo mambo mengine kama watuhumiwa kutembelewa ulikuwa unashughulika nayo?
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Ni sahihi nikisema wa kuwa yote hayo yalitakiwa kuandikwa kwenye station Diary?
Shahidi: Sina uhakika
Mtobesya: Mtuhumiwa hatakiwi kutolewa mahabusu bila idhini yake.
Shahidi: Hauko sahihi
Mtobesya: Ni sahihi kwako kuwa mtuhumiwa anaweza kutolewa wakati wowote bila idhini yake?
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema charge room officer anatakiwa kuidhinisha movement ya mtuhumiwa?
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Eleza idhini hiyo inatolewaje
Shahidi: Inatolewa kwa maandishi na mdomo
Mtobesya: Kwenye kitu gani?
Shahidi: Naomba urudie
Mtobesya: Wewe ulipewa hiyo idhini kwa mdomo mkuu wa kituo ambaye ni Afande Mwita.
Mtobesya: Tusaidie, nitakuwa sahihi nikisema kuwa mtuhumiwa akifika station ya Polisi CRO akapokelewa na baada ya yeye kufika anatakiwa apelekwe kwa medical officer under esccort.
Shahidi: Sio sahihi
Shahidi: Anatakiwa umpeleke endapo ataainisha anaumwa, unamtaarifu Afande kuwa Mahabusu anaumwa na atafanya utaratibu wa matibabu.
Mtobesya: Unafahamu kitu kinaitwa PGO
Shahidi: Nafahamu ni nyenzo muhimu katika kufanya kazi
Mtobesya: unaifahamu PGO namba 353 inayoshughulikia watuhumiwa wakiwa chini yenu?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Mtobesya: Unaweza kusema siyo matakwa ya PGO 353 kwamba mtuhumiwa kabla ya kuwekwa mahabusu alitakiwa akaonane na medical Officer?
Jaji: Umeelewa Swali lake? Kama unafahamu chochote katika PGO hiyo?
Shahidi: 353 sikumbuki inasemaje
Mtobesya: Kwa hiyo unaweza kuiambia Mahakama kwamba mtuhumiwa kabla ya kuingia mahabusu anatakiwa aende kwa daktari.
Jaji: Shahidi kashasema hakumbuki
Mtobesya: Labda nimpatie asome
Mtobesya: Ungependa nikupatie Usome au nisome mimi mwenyewe?
Mtobesya anaisoma PGO 353(2)(b)
Shahidi: Anasema kwa uelewa wake yupo sahihi hata baada ya kusomwa
Jaji anauliza kama Mtobesya anaona tafsiri yake inatosha...
Mtobesya: Inasema pia kuhusu charge room Officer hatomtoa mahabusu pasipokuwa idhini yake
Mtobesya: Je unasisitiza siyo takwa la Kisheria la mtuhumiwa kutotoka mahabusu bila idhini yake?
Jaji anaomba wakili mwingine asome
Jaji: Sasa tupo pamoja, tunaweza kuendelea hapo
Mtobesya: Naomba tusome na kifungu (c)
Wakili wa Serikali: Naomba Mtobesya aulize swali badala ya kujielekeza kwenye tafsiri, suala la tafsiri iachiwe mahakama
Jaji: Suala la tafsiri niachiwe mimi, kwa sababu shahidi ameshasema anachokielewa.
Mtobesya: Anamuuliza shahidi kifungu A na C kinaongelea mtu mmoja.?
Jaji: Unataka maoni ya shahidi? maana yeye hajatunga PGO
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji shahidi ni mtu anayeshughulika na CRO ni taratibu zake za kila siku
Jaji: Je, akishasema ndiyo au hapana?
Mtobesya: Inayofuata ni kazi yako kutafsiri
Jaji: Tayari nimesha note hiyo
Mtobesya: Ni sahihi Officer kutembelea mahubusu kila baada ya muda fulani
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Wewe uliwatembelea mara ngapi ulivyo waweka?
Shahidi: Wakati wa uji, chakula cha mchana
Mtobesya: Ieleze mahakama ni interval ya masaa mangapi mangapi?
Mtobesya: Mtuhumiwa inatakiwa arekodiwe akitoka nje ya KITUO au kutoka mahabusu?
Shahidi: Detention Register inathibitisha akitoka nje ya mahabusu.
Mtobesya: Ni Entry ipi inarekodiwa mtuhumiwa anapotoka nje ya mahabusu na ipi inarekodiwa anapotoka nje ya kituo?
Shahidi: Anapotoka mahabusu ndiyo tunamuweka kwenye Detention Register tu bila kujua kama alitoka kwenda Mahakamani au kwenye Jambo lingine
Mtobesya: Naomba nipewe kielelezo namba 1 (Q One)
Jaji: Tafadhali apatiwe kielelezo.
Mtobesya anasoma Kielelezo ( Detention Register)
Mtobesya: Nisaidie ni wapi ulisoma tarehe 08 walitoka mahabusu
Jaji: Ukishamaliza na sisi tusikie
Shahidi: Ametoka tarehe 07.8.2020
Mtobesya: Nilikuwa naeleza entry ya tarehe 8
Shahidi: Katika entry inaonyesha aliyemtoa ni Inspector Mahita na sababu ya kumtoa ni Upelelezi
Mtobesya: Sasa ilipita muda gani wakina Kingai walikuachia watuhumiwa na wakarudi tena?
Shahidi: Haikuchukua muda ilikuwa kama saa 1
Mtobesya: Charge room Officer ndiye aliyetakiwa aidhinishe?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Tunaiona wapi?
Shahidi: Inaweza kuwa maandishi au ya mdomo
Jaji: Kielelezo kipo wapi?
Mallya: Tulikuwa tunakiomba kwa ajili ya kukisoma na sisi
Jaji: Mtakiomba kwa sasa ni mali ya Mahakama
Jaji: Karibu sasa wakili Nashoni
Wakili Nashoni: Sina la kuongeza mheshimiwa Jaji
Jaji: karibu sana Wakili Mallya sasa na kama utahitaji Kielelezo
Wakili Mallya: Shahidi umesema wewe ni mzoefu kwa miaka 6 Central!?
Shahidi: Ndiyo kwa miaka 6
Mallya: Kwa miaka yako 6 ushawahi kusikia mahabusu ametoroka?
Shahidi: Hapana
Mallya: Kuna wakati mnawakamata watuhumiwa ambao ni wanajeshi wanatenda jinai, huwa mnawahifadhi central?
Shahidi: Ndiyo tunawahifadhi Central
Mallya: Kuna mahabusu ngapi Central?
Shahidi: Moja iliyogawanyika kwa KE na ME
Mallya: Kwa wanaume kuna mahabusu ngapi?
Shahidi: Zaidi ya 2
Mallya: Kwenye DR afande Mahita alikuwa anawachukua watuhumiwa anawapeleka kwenye Upelelezi, Je ulipata kujua alikuwa anawapeleka wapi?
Shahidi: Siwezi kujua anawapeleka wapi
Mallya: Siku unaingia kazini ulikuta mahabusu ina mahabusu wangapi?
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Lakini mahabusu ilijaa sana?
Shahidi: Siyo sana!
Mallya: Palikuwa na watoto wadogo?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Watuhumiwa wa Mauaji?
Shahidi: Sikumbuki
Mallya: Watuhumiwa wa unyang'anyi wa kutumia silaha?
Shahidi: Siwezi kukumbuka
Mallya: Ulipowapeleka mahabusu watuhumiwa wa ugaidi kama ulivyosema, Je uliwawekaje?
Shahidi: Niliwatenganisha
Mallya: Ulivyowatenga magaidi unafikiri wangeweza Kufanya kikao cha kutoroka?
Shahidi: Walikuwa hawawezi kutoroka, kukutana, hawawezi kufanya lolote
Mallya: Akitokea mtu akisema mule hapakuwa salama wangeweza kupora silaha atakuwa anasema kweli?
Shahidi: Atakuwa anasema tu mambo yake
Mallya: Twende kwenye muda, siku hiyo ulifika muda gani?
Shahidi: Natakiwa kisheria kufika robo saa kabla na nilifika robo saa kabla
Mallya: Ulipofika ulifanya nini?
Shahidi: Tulianza kukabidhiana kazi
Mallya: Kati ya kukabadhiana watuhumiwa mahabusu na kukabidhiana mali ?
Shahidi: Vyote vilienda kwa pamoja
Mallya: Kwa muda gani mlikabidhiana?
Shahidi: dakika 15
Mallya: Ni wakati gani wewe ulishuka mahabusu?
Shahidi: Ni muda huohuo kwa sababu CRO tupo wengi
Mallya: Kwa hiyo ulitumia dakika ngapi kule chini mahabusu?
Shahidi: Dakika 15
Mallya: Ulisema afande Kingai alipomchukua Mtuhumiwa, afande FATUMA alikuelekeza umsindikize, Je ni lazima?
Shahidi: Ni nidhamu ya kipolisi
Mallya: Wakati Kingai anashuka kuja kumfuata Mtuhumiwa ulieleza mahakama alikuwa ameongozana na nani?
Shahidi: Hapana sikueleza
Mallya: Wakati Afande Kingai anawaleta watuhumiwa umesema walikuwa wamefungwa pingu?
Mallya: Siku hizi umesema unafanya kazi Oysterbay
Shahidi: ndiyo
Mallya: Ukiwa unatokea Moshi kituo cha kwanza kukutana nacho ni kipi?
Shahidi: Inategemea njia uliyopita
Mallya: Ukiwa unatokea Bagamoyo Msata, Mbweni, Oysterbay na Central kipi kituo cha kwanza kukutana nacho?
Mallya: Shahidi sasa hivi wewe ni Detective Constable?
Shahidi: ni sahihi
Mallya: Upelelezi unajumuisha nini?
Shahidi: Ni mchakato, process na kisha Kupeleka mahakamani
Mallya: Kuhoji watuhumiwa ni sehemu ya upelelezi?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwenye DR umezungumza muda mrefu sana, ni sahihi unatakiwa kuandika taarifa za ukweli tu?
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Nakupa DR msomee Mheshimiwa Jaji alipokuja Inspector Mahita alisema anaenda kufanya nao nini?
Shahidi anapekua DR (Detention Register)
Shahidi: Mheshimiwa Jaji afande wangu alimtoa mtuhumiwa nje kwa UPELELEZI
Mallya: Akitokea mtu akisema Mahita hakuwa anafanya nao upelelezi atakuwa ni muongo?
Shahidi: Mimi nazungumzia kilichoandikwa humu, Mahita aliwachukua kwa upelelezi
Mallya: Ndiyo nasema akitokea mtu akasema kuwa Mahita hakwenda kufanya nao upelelezi atakuwa muongo?
Shahidi: Nimeeleza Ukweli
Mallya: Kutunza mahabusu ni kazi mpelelezi?
Shahidi: Mtu ambaye ni General Duty na masuala ya kiupelelezi isipokuwa kipindi atakapohitajika
Mallya: Mpelelezi Kama Mahita masuala ya mahabusu Central ni Kazi yake? siku ya tarehe 08.8.2020 ulikuwa wajibu wa Mahita?
Shahidi: Ulikuwa ni wajibu wangu mimi
Mallya: Mheshimiwa Jaji hi hayo tu.
Wakili Fredrick Kihwelo anasimama na kuanza kumuhoji shahidi wa Jamhuri.
Wakili Kihwelo: Wakati shahidi unarekodi vitu anavyoingia navyo, Je alikuwa na simu?
Shahidi: Hapana
Kiwhelo: Je Bastola.?
Shahidi: Hapana
Kiwhelo: Je, Madawa ya kulevya?
Shahidi: Hapana
Kihwelo: Je, wewe ni mtabiri kama SHEIKH YAHAYA?
Shahidi: Hapana siyo MTABIRI
Kihwelo: Wewe ni mtabibu (Physician)?
Shahidi: Ndiyo mimi MTU wa MAZOEZI
Kihwelo: Siyo MAZOEZI nakuuliza AFYA
Shahidi: HAPANA...
Kiwhelo: Je, ulisema ulifika saa 12:30, sasa hivi na mwanzo lipi kweli?
Jaji: Saa ngapi? ni kweli alisema hivyo?
Kihwelo: Natoa swali langu
Jaji: NDIYO. Tuseme vitu kwa usahihi najua humu watu wengi wanarekodi mazungumzo
Kihwelo: Je, watuhumiwa walipumzika?
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Mtuhumiwa namba tatu, alipochukuliwa na afande Jumanne alirudishwa saa ngapi?
Shahidi: Sikumbuki
Kihwelo: ni hayo tu
Wakili Fredrick Kihwelo anakwenda kuketi.
Sasa anasimama wakili Peter Kibatala
Kibatala: Tukitaka kuthibitisha wewe ni Afisa wa Polisi na siyo Usalama wa Taifa nafanyeje?
Shahidi: Kwa kutumia Force Number niliyotaja mwanzoni
Kibatala: Nathibitishaje
Shahidi: Kwa kutumia kitambulisho
Kibatala: Unafahamu kuwa unakuja kwenye zoezi muhimu la kesi ndogo?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umejuaje
Shahidi: Nimeambiwa na Inspector Swila
Kibatala: Mwambie Jaji kuwa Inspector Swila anahusika vipi na mshtakiwa wa 2 na 3
Shahidi: Hakuna sehemu yoyote kwenye Maelezo nimemtaja Inspector Swila au kuja kituoni kushughulika na watuhumiwa
Kibatala: Mueleze Mh Jaji kuwa wewe hujui lolote kuhusu Inspector Swila na hujui anahusika vipi na kesi, kwa sababu siku nikiwa central Kingai alikuja na Askari Wengine huenda Swila alikuwepo
Shahidi: Sikuwa namfahamu Inspector Swila
Kibatala: Iambie Mahakama kama ulitoa angalizo la kiulinzi kwa watuhumiwa hawa wawili
Shahidi: Niulize tena vizuri sijaelewa.
Kibatala: Leo umezungumzia lolote kuhusu Watuhumiwa watolewe kituoni wapelekwe eneo lingine?
Shahidi: Hapana hakuna sehemu niliyo zungumza.
Kibatala: Unakumbuka kurekodi kitu chochote katika station Diary kuwa maoni yako kuwa eneo lile si salama kwa washtakiwa kukaa pale?
Wakili wa Serikali: OBJECTION, nafikiri aulize maswali siyo maoni kwa shahidi
Shahidi: Huwa kwenye station Diary tunarekodi matukio kama mhusika amekabidhiwa gari yake na siyo Maoni, kwenye Station Diary Tunaainisha mali zote za kituo cha polisi siyo maoni
Kibatala: Nimesikia unasema Askari kukabidhiana kituoni, mwambie Jaji kama leo umetoa ushahidi wako wa station Diary kama ulikuwa zamu
Shahidi: Naomba kueleza kuwa station Diary haiwasilishwi
Kibatala: Occurence Book ndiyo nini.?
Shahidi: Ndiyo Station Diary
Kibatala: Ndiyo ambayo hujaitoa leo.?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Tukiangalia kwenye Detention Register tutaona kuwa siku hiyo ulikuwa zamu
Shahidi: Huwezi kuona hakuna hiyo column
Kibatala: Tukitaka kuthibitisha kuwa ulikuwa kazini tutaangalia nini? Shahidi: mpaka nikalete documents.
Kibatala: Umetoa ombi kwa jaji kuwa unaomba kuleta uthibitisho kuwa siku hiyo ulikuwa kazini
Shahidi: Hapana sikuomba
Kibatala: Je, uliwahi kufahamu kuwa watuhumiwa walikwenda wapi?
Shahidi: Sikuwahi kufahamu
Kibatala: Je kuna mahala popote wewe uliwapa binafsi washtakiwa wa tatu na wa pili Uji?
Shahidi: Katika maswali unapaswa kunielekezea mimi ni yale tu yanayonihusu, Haiwezekani niulizwe mimi kuwapa mahabusu UJI au SIJAKUELEWA VIZURI.
Kibatala: Nauliza wewe binafsi kwa macho yako ulishuhudia mshtakiwa wa pili na watatu wakipata Uji?
Shahidi: Ndiyo Ndugu Kibatala Nilishuhudia wakipata Uji
Kibatala: Je, unafahamu zoezi la ugawaji kwa Mtuhumiwa ni zoezi lililotungiwa kanuni kwenye PGO?
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je, unafahamu kuwa kuanzia chombo cha kumpa mahabusu chakula kimeainishwa na PGO?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu aina za chakula na resheni za chakula ambavyo watuhumiwa wakiwa rumande wanapewa mpaka na kiasi wakiwa rumande?
Shahidi: Nijuze kwanza kwenye PGO ngapi
Kibatala: Wewe jibu unafahamu au hufahamu?
Shahidi: Nijuze tu ndugu Kibatala
Kibatala: Jaji naomba anijibu
Jaji: Sijui kwanini mnaona kila swali ni MTEGO, Wewe jibu kama utakosea Mawakili wa Serikali watakuongoza
Shahidi: Sawa mh Jaji
Kibatala: Kuwa chakula aina za chakula na vyombo vya kutumia mahabusu vimetajwa kwenye PGO?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Uliwahi kufahamu kuwa watu wote waliofika na afande Kingai wametoka Moshi?
Shahidi: Hapana sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo uliwapokea washtakiwa ukiwa hufahamu wanatoka wapi?
Shahidi: Nilijulishwa walikuwa wamekamatiwa Moshi, Sikujua kama siku hiyo ndiyo walitokea Moshi
Kibatala: Washitakiwa wanasema kabla hawajaja kwako Central walipitishwa kwanza Tazara na Mbweni kwa ajili ya kuteswa, Je tukitaka tujue kama kweli au si Kweli
Wakili wa Serikali: OBJECTION. Wakili Kibatala anamuuliza shahidi maoni yake, amuulize kama anajua waliteswa au hajui
Jaji: Naona ajibu yeye SHAHIDI, siyo LAZIMA kila kitu uelewe wewe, kama unaona kuna swali unataka aulizwe utaulizwa wakati wako ukifika.
Wakili Kibatala: Kwa kutumia DR tunawezaje kujua kuwa waliteswa au hawakuteswa?
Shahidi: DR inaonyesha kama wazima ki Afya au lah!
Kibatala: Kwenye DR kuna sehemu inaonyesha?
Shahidi: Ukinipa muda utaelewa
Jaji: Labda wakili ungempa muda wa majibu shahidi
Jaji: Shahidi UNGEKUNYWA MAJI KWANZA.
Shahidi: Ninayo mheshimiwa Jaji.
Kibatala: Kwa kuangalia DR tunaweza kujua kuwa washtakiwa wanatoka wapi? mfano Mbeya na kwingineko
Shahidi: Kwenye DR hakuna sehemu hiyo
Kibatala: Unakijua Kituo cha Polisi Tazara
Shahidi: Unajua Kwamba ni Class A.. Ni sehemu zozote anazokaa RPC
Kibatala: Unamfahamu Mahita kabla siku ya Tarehe 08?
Shahidi: Sikuwa namfahamu
Kibatala: Mwambie mheshimiwa Jaji, Afisa wa Polisi anayekaa Duty kwenye CRO PGO 288(3)(b) muda wa wa kazi wa Polisi aliyepo CRO ni Masaa 8 Unafahamu?
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Mwanzo ulisema siku ya duty yako ulikaa masaa 12, Je umemwambia Jaji Siku hiyo kuna masaa yaliongezeka kwa sababu fulani?
Shahidi: Duty ni masaa 8 lakini nilitolea muda ukaongezeka hakuna tatizo
Kibatala: Nauliza tena umemwambia mheshimiwa Jaji kwamba kwanini ulivuka muda wa kisheria wa masaa 8 siku ya Duty yako?
Jaji: Jamani Leo tuongeza muda kidogo
Wakili Kibatala anaomba dakika 10 na wengine wote wanaridhia ikiwemo magereza.
Wakili Kibatala: Msingi wa swali langu ulikuwa unatoa ushahidi Asubuhi, ulitoa ufafanuzi kwa mheshimiwa Jaji kwamba masaa ya kazi ya kipolisi CRO ni masaa 8 lakini mimi nilikaa masaa 12.
Shahidi: Hapana
Wakili Kibatala: Kwa mujibu PGO 288(6) MUDA wa kawaida wa kazi kwa Afisa wa RANKING file kwa masaa nane, Muda wa kwanza unaanza saa 7 usiku , mwingine Saa mbili Asubuhi na mwingine Saa 10 Jioni.. wewe ulisema shifti yako umeingia saa ngapi?
Shahidi: Nakukumbusha wakili mimi ni Afisa wa Polisi natakiwa kuwa popote nitakapohitajika.
Wakili Kibatala: Sijakuuliza hilo nataka kujua wewe katika maelezo yako umesema uliingia saa ngapi?
Shahidi: Saa 12 Asubuhi
Wakili Kibatala: Muda wa kwanza saa 7 usiku, saa 12 Asubuhi na muda wa tatu ni saa 10 Jioni, Je muda wako wa shifti uliosema hapa saa 12 imetajwa hapa?
Shahidi: Hapana saa 12 haujatajwa...
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Sana kuhusu Mahita, Wakati anawachukua hawa tarehe 08 ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuta watuhumiwa wametolewa,Mimi sikuwa Kazini
Wakili wa Serikali: Umeulizwa kuhusu occurence Book,ukasema inaonyesha uingiaji wako kazini na Je Vitu gani Vingine Vinaweza kuonyesha?
Shahidi: Station Diary inayoandikwa na Inspector
Wakili wa Serikali: Umebanwa sana na kuonyeshwa sana PGO ukaulizwa kwenye ushahidi wako hukupata muda wa kuelekeza kwanini ulikaa Masaa 12?
Wakili Kibatala: OBJECTION. Labda afanye rephrase siyo kutaka kuongelea masaa manne
Wakili wa Serikali: Naomba niishie hapa tu, na ni hayo tu.
Jaji: Kuna wakili mwingine wa Serikali anataka kumuongoza?
Mawakili wa Serikali: HAPANA
Jaji: AHSANTE shahidi, umemeliza ushahidi wako unaweza kwenda.
Jaji: Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Naomba hairisho mpaka 24.9.2021 kwa sababu shahidi tuliyemtarajia aanze kwanza amepata dharula ya ugonjwa alipata ajali, Jumamosi, wakati tunasubiria akipata muda wa ku'recover tunaomba kumaliza siku ya tarehe 24 mwezi wa 9 siku ya Ijumaa.
Wakili Kibatala: Kwa niaba ya wenzangu hatuna pingamizi.
Jaji: anaandika.
Jaji: Niwashukuru tena kwa mara nyingine kwa uvumilivu wemu wakati tunaendelea na shauri hili
Jaji: Kwa sababu ambazo zimetolewa na upande wa mashtaka na kukubaliwa na upande wa Utetezi, Nalazimika kuahirisha shauri hili mpaka siku ya Ijumaa tutakapoendelea kusikiliza shauri hili, mahabusu wataendelea kuwa mahabusu.
Asanteni sana
MWISHO